Mzee wa Rula
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 8,171
- 3,346
Ajali mbaya imetokea Arusha leo hii, maeneo ya Burka - Redds na kupelekea takribani watu sita kufa. Chanzo cha ajali inasadikiwa ni poor overtaking baada ya dereva wa Hiace No. T706 BFE alipokuwa anajaribu kuovertake gari nyingine na kukutana uso kwa uso na gari Toyota Hilux T509 ATY na kusababisha ajali hiyo mbaya.
Gari hiyo ilikuwa imetokea Kisongo - Gereza Arusha au Airport kwa mujibu wa mashuhuda walioiona ikitoka eneo hilo, na kwa kuwa leo ni siku ya Jumapili hivyo ni ruksa kuona mahabusu na wafungwa. Wakati ikirudi ndipo ilipobeba baadhi ya watu hao waliotoka kuona ndugu zao na kupata ajali mitaa hiyo.
Hiace inayosadikiwa kusababisha ajali.
Wakuu nilichelewa kupata taarifa na kufika eneo la tukio lakini nilifanya mahojiano na baadhi ya watu walioshuhudia ajali hiyo wanasema ilikuwa ni ajali mbaya sana hasa wale watu waliopakizwa katika Hilux waliruka baada ya kugongana na wengine kudondokea kwenye lami na kuumia vibaya licha ya wanaosadikiwa kufa.
Gari hiyo ilikuwa imetokea Kisongo - Gereza Arusha au Airport kwa mujibu wa mashuhuda walioiona ikitoka eneo hilo, na kwa kuwa leo ni siku ya Jumapili hivyo ni ruksa kuona mahabusu na wafungwa. Wakati ikirudi ndipo ilipobeba baadhi ya watu hao waliotoka kuona ndugu zao na kupata ajali mitaa hiyo.
Hiace inayosadikiwa kusababisha ajali.
Wakuu nilichelewa kupata taarifa na kufika eneo la tukio lakini nilifanya mahojiano na baadhi ya watu walioshuhudia ajali hiyo wanasema ilikuwa ni ajali mbaya sana hasa wale watu waliopakizwa katika Hilux waliruka baada ya kugongana na wengine kudondokea kwenye lami na kuumia vibaya licha ya wanaosadikiwa kufa.