AIYOLA- Riwaya murua

AIYOLA- Riwaya murua

Nduhu tabu

Member
Joined
Jul 21, 2017
Posts
90
Reaction score
99
d9b553be6769987bf06a7438f9eb1401.jpg



AIYOLA
SEHEMU.........01
AUTHOR.......MWL.SADALAH
CONT.....0629306194
WHATSAPP........0768552126

Chini ya mti wa muembe, uliokuwa nje kidogo ya kijiji sofu,kata ya kwala,wilaya ya kisarawe, mkoa wa pwani mashariki mwa nchi ya Tanzania. Alionekana kijana mmoja aliyekuwa amekaa chini ya jiwe lililokuwa kando ya mti huo. Alionekana kuchoshwa na hali ya umasikini na alikuwa kwenye dimbi zito la mawazo. Alikuwa alikuwa amevaa suruali nzito ya jinsi iliyojazia uchafu na kuifanya ionekane nyeusi, shati jeusi lililo chanika, na chini alikua amevaa viatu vya wazi yaani sandals sijui aliziokota wapi. Usingeweza kumtofautisha binadamu huyu mwenye akili zake timamu na vichaa wanaoranda mitaani na kwenye madampo ya uchafu. Alionekana dhaifu sana nadhani shauri ya njaa na ni ndovyo ilivyo kuwa.shingo yake ilikuwa imepinda kidogo na kufanya kichwa chake kitulie vyema kenye magoti yake.
"Oya oya" ilikuwa ni sauti aliyoisikia vyema kutoka nyuma yake na kumfanya ashtuke kidogo kwa unyonge akageuza shingo yake na kumtazama mtu aliye mshtua.
"Vipi ndugu yangu nimekuona hapa muda mrefu na unekana kama hauko sawa"
Akauliza.
Jamaa akasita kidogo kisha akaguna na kumjibu.
"Daaaah!!!! We acha tu bana"
"Kulikoni"
"Maisha kaka"
Baada ya kauli hiyo yule jamaa akahisi kuna kitu kwa huyo jamaa akaainama na kumshhoka bega kisha akamwambia
"Naitwa jamali sijui mwenzangu unaitwa nani vile"
"Mi naitwa paschal matogwa" akajibu kwa kujitambulisha
"Sijawahi kukuona hapa Sofu wewe ni mwenyeji wa wapi bwana paschal"
"Samahani nikuombe kitu"
"Usijali we omba tu hata usiwe na wasiwasi"
"unaweza kuendelea na safari yako tu"
paschal akamwambia jamali, kisha akainama tena alionekana kukereka na maswali mengi aliyokuwa anaulizwa.
Ukimya mdogo ukapita na baadae વjamali akaonekana kama anafikilia kitu kisha કakaanzisha tena mazungumzo
"Usiseme hivyo રndugu yangu mi ni mtu mwema japo sina uwezo ila ninaweza kukusaidia "
"Unataka kunisaidia kweli" akauliza paschal.
"Kama jambo liko ndani ya uwezo wangu naweza kukusaidia kweli. Paschal akamwangalia jamali kwa kumdadisi kisha.
વ"labda kweli anaweza kunisaidia au ndo walewale tu" akawaza paschal "ila ngoja nijaribu tena" akaendelea kuwaza, akakumbuka mateso aliyoyapata kwa miongo miwili sasa, akamkumbuka mpenzi wake pros, picha ya wazazi wake wawili baba na mama take ikapita akilini mwake. Haraka haraka akayakumbuka maisha yake ya nyuma yakamjaza maumivu.
"Vipi wewe...." Sauti ya jamali ikamuamsha tena kutoka alipokuwa ameinama na safari hii uso wake ulikuwa umejaa machozi
"Na...o..mba uni..sa..saidii.ie cha..cha...kula na maji" Akaomba paschal kwa kwikwi na kwa sauti ya chini
Jamali akazidi kuzungukiwa na roho ya huruma. "Mi ni maskini na nina shida ila huyu jamaa anashida sana tena zaidi yangu lazima nimsaidie" akawaza jamali kisha akamshika mkono, akamuomba waongozane kwenda nyumbani kwa jamali. Taratibu akaanza kujikongoja huku akisaidiwa kutembea hakika alikuwa amejichokea sana. Haikuwa mbali sana waliweza kufika nyumbani kwa jamali.
***************
Mwezi desemba Mwaka 1979 mzee juma alirudi kutoka katika mapigano ya vita vya Tanzania na Uganda wengi hupenda kuita vita vya kagera. Alifika Moja kwa Moja kijijini kwao kasulu mkoa wa kigoma na akawakuta ndugu zake, waliomlaki kwa furaha hawakuanini kama Huyo ndugu yao amerudi akiwa mzima maana vita ni kama mnavyojua kufa au kupona. Alifanyiwa sherehe kubwa ya kumkaribisha nyumbani, watu wakala, wakanywa na wakacheza mziki. Watu wengi kutoka kila sehemu walihudhuria sherehe hiyo isipokuwa MTU mmoja, tena mtu wa karibu sana na familia hiyo. Siyo mwingine bali ni mke wa mzee Juma. Aliogopa na hakujua atamweleza nini mume wake. Wakati anaenda kupigana alimuacha mke wake na watoto watatu. Akiwa huko make wake alikosa uvumilivu na akajikuta anachepuka na kupata mimba hatimae mtoto wa nne ambae siyo wa mzee juma. Hakutegemea kama itakua hivyo na ndiyo sababu ilimfanya aende akajifiche katika kijiji cha Runzewe akiwa yeye na mtoto wake mmoja alikuwa anaitwa jamali mtoto huyu alikuwa na umri wa miezi mitatu tu. Huko akawa anajishughurisha na biashara ndogo ndogo ya kuuza ndizi mbivu.
Baada ya kukaa kijijini huku, taarifa ya mke wake kujifungua akawa ameshaambiwa na waongo si unajua tena vijijini. Taarifa hiyo ilimfanya ajenge chuki dhidi ya mke wake akawaza kuja kumfanyia kitu kibaya pindi atakapo mtia machoni. Alikaa kijijini hapo kwa miezi mitatu huku akifanya upererezi, na hatimae alijua sehemu alipo. Siku hiyo hiyi jioni alichukua kisu chake akakieka kiunoni na akaenda stend tayari kwa safari. Kama bahati Siku hiyo alipata basi la kwenda kahama lililokuwa limecherewa akapanda tayari kwa safari.
Alifika Runzewe saa mbili usiku, kwa kuwa alikuwa anaijua mke wake anajishughurisha na uuzaji wa ndizi. Alienda kwenye genge la jioni na alikusudia kuondoa uhai wa mtu leo leo. Kama bahati alimuona kwa mbali na roho ya kinyama pamoja na hasira ikamjaa. Akaamua apoteze muda kwenye kijiwe cha kahawa kilichokuwa jirani na gange hilo. Baada ya kama nusu saa alimuona mama Huyo aliyekuwa make wake akikusanya vitu, akambeba mwanae mgongoni ambae ni Jamali kisha akaanza kuelekea alikokuwa anaishi. Bila kuchelewa juma naye alisimama na kuanza kumfatilia. Alitembea umbali mdogo akaziacha taa na kuingia gizani. Hapa ndipo Mzee Juma naye aliongeza mwendo na akafanikiwa kumpata.


Story unaweza kuipata yote kwa tsh 2500 whsapp au Facebook in box kwa sh. 500 vipande vitatu.

Huu ni mwanzo tu je, ni nini hatma ya Mama huyu, hatma ya paschal na hatma ya Jamali.
Coment
Like
Share
Itaendelea.......
 
Ahsante ila ushauri wa bure kama wengeweza kwenda mbali kidogo na hadhira yenyewe ingevutwa na hadithi yako lakini kwa mistari michache hii sidhani kama wengi watavutika.
 
Mkuu mbona mapema hivyo jaman mambo ya kulipia ebu fanya kama wenzio wanavyofanya wanatuonjesha utamu weeeh ndio wanaanza hizo mambo sasa wewe hata story hatujui ni nzuri au vipii
 
Mkuu mbona mapema hivyo jaman mambo ya kulipia ebu fanya kama wenzio wanavyofanya wanatuonjesha utamu weeeh ndio wanaanza hizo mambo sasa wewe hata story hatujui ni nzuri au vipii
story hii itaendelea mpaka mwisho hapa hapa usijali.
d9b553be6769987bf06a7438f9eb1401.jpg



AIYOLA
SEHEMU.........01
AUTHOR.......MWL.SADALAH
CONT.....0629306194
WHATSAPP........0768552126

Chini ya mti wa muembe, uliokuwa nje kidogo ya kijiji sofu,kata ya kwala,wilaya ya kisarawe, mkoa wa pwani mashariki mwa nchi ya Tanzania. Alionekana kijana mmoja aliyekuwa amekaa chini ya jiwe lililokuwa kando ya mti huo. Alionekana kuchoshwa na hali ya umasikini na alikuwa kwenye dimbi zito la mawazo. Alikuwa alikuwa amevaa suruali nzito ya jinsi iliyojazia uchafu na kuifanya ionekane nyeusi, shati jeusi lililo chanika, na chini alikua amevaa viatu vya wazi yaani sandals sijui aliziokota wapi. Usingeweza kumtofautisha binadamu huyu mwenye akili zake timamu na vichaa wanaoranda mitaani na kwenye madampo ya uchafu. Alionekana dhaifu sana nadhani shauri ya njaa na ni ndovyo ilivyo kuwa.shingo yake ilikuwa imepinda kidogo na kufanya kichwa chake kitulie vyema kenye magoti yake.
"Oya oya" ilikuwa ni sauti aliyoisikia vyema kutoka nyuma yake na kumfanya ashtuke kidogo kwa unyonge akageuza shingo yake na kumtazama mtu aliye mshtua.
"Vipi ndugu yangu nimekuona hapa muda mrefu na unekana kama hauko sawa"
Akauliza.
Jamaa akasita kidogo kisha akaguna na kumjibu.
"Daaaah!!!! We acha tu bana"
"Kulikoni"
"Maisha kaka"
Baada ya kauli hiyo yule jamaa akahisi kuna kitu kwa huyo jamaa akaainama na kumshhoka bega kisha akamwambia
"Naitwa jamali sijui mwenzangu unaitwa nani vile"
"Mi naitwa paschal matogwa" akajibu kwa kujitambulisha
"Sijawahi kukuona hapa Sofu wewe ni mwenyeji wa wapi bwana paschal"
"Samahani nikuombe kitu"
"Usijali we omba tu hata usiwe na wasiwasi"
"unaweza kuendelea na safari yako tu"
paschal akamwambia jamali, kisha akainama tena alionekana kukereka na maswali mengi aliyokuwa anaulizwa.
Ukimya mdogo ukapita na baadae વjamali akaonekana kama anafikilia kitu kisha કakaanzisha tena mazungumzo
"Usiseme hivyo રndugu yangu mi ni mtu mwema japo sina uwezo ila ninaweza kukusaidia "
"Unataka kunisaidia kweli" akauliza paschal.
"Kama jambo liko ndani ya uwezo wangu naweza kukusaidia kweli. Paschal akamwangalia jamali kwa kumdadisi kisha.
વ"labda kweli anaweza kunisaidia au ndo walewale tu" akawaza paschal "ila ngoja nijaribu tena" akaendelea kuwaza, akakumbuka mateso aliyoyapata kwa miongo miwili sasa, akamkumbuka mpenzi wake pros, picha ya wazazi wake wawili baba na mama take ikapita akilini mwake. Haraka haraka akayakumbuka maisha yake ya nyuma yakamjaza maumivu.
"Vipi wewe...." Sauti ya jamali ikamuamsha tena kutoka alipokuwa ameinama na safari hii uso wake ulikuwa umejaa machozi
"Na...o..mba uni..sa..saidii.ie cha..cha...kula na maji" Akaomba paschal kwa kwikwi na kwa sauti ya chini
Jamali akazidi kuzungukiwa na roho ya huruma. "Mi ni maskini na nina shida ila huyu jamaa anashida sana tena zaidi yangu lazima nimsaidie" akawaza jamali kisha akamshika mkono, akamuomba waongozane kwenda nyumbani kwa jamali. Taratibu akaanza kujikongoja huku akisaidiwa kutembea hakika alikuwa amejichokea sana. Haikuwa mbali sana waliweza kufika nyumbani kwa jamali.
***************
Mwezi desemba Mwaka 1979 mzee juma alirudi kutoka katika mapigano ya vita vya Tanzania na Uganda wengi hupenda kuita vita vya kagera. Alifika Moja kwa Moja kijijini kwao kasulu mkoa wa kigoma na akawakuta ndugu zake, waliomlaki kwa furaha hawakuanini kama Huyo ndugu yao amerudi akiwa mzima maana vita ni kama mnavyojua kufa au kupona. Alifanyiwa sherehe kubwa ya kumkaribisha nyumbani, watu wakala, wakanywa na wakacheza mziki. Watu wengi kutoka kila sehemu walihudhuria sherehe hiyo isipokuwa MTU mmoja, tena mtu wa karibu sana na familia hiyo. Siyo mwingine bali ni mke wa mzee Juma. Aliogopa na hakujua atamweleza nini mume wake. Wakati anaenda kupigana alimuacha mke wake na watoto watatu. Akiwa huko make wake alikosa uvumilivu na akajikuta anachepuka na kupata mimba hatimae mtoto wa nne ambae siyo wa mzee juma. Hakutegemea kama itakua hivyo na ndiyo sababu ilimfanya aende akajifiche katika kijiji cha Runzewe akiwa yeye na mtoto wake mmoja alikuwa anaitwa jamali mtoto huyu alikuwa na umri wa miezi mitatu tu. Huko akawa anajishughurisha na biashara ndogo ndogo ya kuuza ndizi mbivu.
Baada ya kukaa kijijini huku, taarifa ya mke wake kujifungua akawa ameshaambiwa na waongo si unajua tena vijijini. Taarifa hiyo ilimfanya ajenge chuki dhidi ya mke wake akawaza kuja kumfanyia kitu kibaya pindi atakapo mtia machoni. Alikaa kijijini hapo kwa miezi mitatu huku akifanya upererezi, na hatimae alijua sehemu alipo. Siku hiyo hiyi jioni alichukua kisu chake akakieka kiunoni na akaenda stend tayari kwa safari. Kama bahati Siku hiyo alipata basi la kwenda kahama lililokuwa limecherewa akapanda tayari kwa safari.
Alifika Runzewe saa mbili usiku, kwa kuwa alikuwa anaijua mke wake anajishughurisha na uuzaji wa ndizi. Alienda kwenye genge la jioni na alikusudia kuondoa uhai wa mtu leo leo. Kama bahati alimuona kwa mbali na roho ya kinyama pamoja na hasira ikamjaa. Akaamua apoteze muda kwenye kijiwe cha kahawa kilichokuwa jirani na gange hilo. Baada ya kama nusu saa alimuona mama Huyo aliyekuwa make wake akikusanya vitu, akambeba mwanae mgongoni ambae ni Jamali kisha akaanza kuelekea alikokuwa anaishi. Bila kuchelewa juma naye alisimama na kuanza kumfatilia. Alitembea umbali mdogo akaziacha taa na kuingia gizani. Hapa ndipo Mzee Juma naye aliongeza mwendo na akafanikiwa kumpata.


Story unaweza kuipata yote kwa tsh 2500 whsapp au Facebook in box kwa sh. 500 vipande vitatu.

Huu ni mwanzo tu je, ni nini hatma ya Mama huyu, hatma ya paschal na hatma ya Jamali.
Coment
Like
Share
Itaendelea.......
 
Mkuu mbona mapema hivyo jaman mambo ya kulipia ebu fanya kama wenzio wanavyofanya wanatuonjesha utamu weeeh ndio wanaanza hizo mambo sasa wewe hata story hatujui ni nzuri au vipii
Mlafi huyu mxiiew
 
Duh umetuonjesha kidogo tuu na malipo mkuu
Yaani kipyenga pyee na malipo? hilo lisingekuwa jema atupeleke peleke kisha atulipishe mfano mzuri Patrick yeye kiasi flan khadithi zake zinavuta na kazi zake nyingi zinajulikana sasa nawe kuwa kiasi kwanza kazi zako zikubalike
 
AIYOLA ...... ..2
AUTHOR................MWL SADALA
CONT..............0629306194
WHATSAPP.............0768552126
ILIPOISHIA
Akambeba mwanaya mgongoni ambae ni Jamali. Kisha akaanza kisha akaanza kuelekea alikokuwa anaishi. Bila kupoteza muda Mzee Juma naye alisimama na kuaanza kumfatilia. Alitembea umbali kidogo akaziacha taa na kuingia gizani. Hapo ndipo Mzee Juma naye na akafanikiwa kumpata.
ENDELEA...
"Mama.... Mussa... we Mama Mussa wewe"
Sauti hiyo ilisikika vyema kutokea nyuma, mwanzo aliipuuza na alijua siyo yeye anayeitwa kwa sababu hapo Runzewe hakuwa anafahamika kwa jina hilo la Mama Massa. Mussa ni mtoto wake wa kwanza aliye muacha Kasulu. Na ndiyo sababu Mzee Juma aliita kwa kurudiarudia.
Baada ya kusikiliza vizuri akaigundua hiyo sauti ni ya mme weke aliyeondoka kwenda kupigana vita miaka mitatu iliyopita. Akashtuka na taa ya hatari ikawaka alimjua vyema Mme wake na ndiyo sababu iliyomfanya akimbie mafichoni. Mwili ulizidi kutetemeka na aliogopa kupita maelezo. Aliendelea kutetemeka hadi sinia la ndizi likadondoka. Hapo hapo akafungua nguo aliyombebea mwanaye akamshusha na kumkalisha chini. Zoezi hilo lilifanyika kwa sekunde chache. Roho mbili zikawa zinakinzana moja ilimwambia asimame ila roho nyingine yenye nguvu iilimwambia akimbie. Basi akaanza kukimbia kukiacha kijiji akawa anaelekea bondeni huku akipiga kelele za kuomba msaada.
Simama we nakuumbia usimame
Aliongea mzee huyu mfupi huku akimkimbiza. Hakuzoea kukimbia ila alijitahidi ili aokoe maisha yake. Alienda kama mita miamoja akakutana na mfereji uliokuwa unapitisha maji siunajua tena bondeni. Alipokanyaga tu akatereza vibaya na akaangukia tumbo. Hapo hapo Mzee Juma akawa amefika sehemu alipo angukia bila kupoteza muda akinama huku akichomoa kisu aina ya CHEFS KNIFE kiunoni. Akamchoma kisu maeneo ya nyuma shingoni, akachomoa akamgeuza akamchoma tena kifuani akawa anachoma na kuchoma kama mara tano hivi. Dah!!!! huyu mzee alikuwa na roho ya kinyama kweli hakika jeshi ilimuacha vibaya. Alipohakikisha amekata roho, akainuka huku akiwa ametapakaa damu mwili hadi nguo. Alishindwa hata aende wapi akawa amepigwa na bumbuwazi. Dah!!! Damu nzito kuliko maji. Wakati akiwa amesimama alisikia sauti za watu wakija sehemu alipo.
********
"We Baba sophia unasikia hiyo sauti"
"Eee dah!!!! sijui kuna nini tena huko "
"Ni kama mtu anaomba msaada "
"Huyo atakuwa Mama Makotwe anapigwa na mme wake"
"Twende basi tukamsaidie ataumizwa"
"Mi sitoki nje bwana hebu lete chakula nile kwanza nimechoka"
Maneno ya wanandoa hao yalisikika vyema kutoka ndani sebuleni baada ya kusikia sauti ya mtu akilia nje. Siyo wao tu hata majirani wa karibu na wao walisikia kelele hizo. Hadi ikambidi Baba Makotwe aende akamuamshe jirani yake Baba Sophia.
"Ngo...ngo...ngooooo hodi"
"Karibu ..... Nani....?"
"Ni mimi jirani"
Alijibu Baba Makotwe akasubiri mlango ufunguliwe.
Baba Sophia alishtuka baada ya kufungua mlango akamkuta jirani yake Baba Makotwe ili hali alijua ile kelele ni yake na mke wake.
"Oooh jirani karibu pita ndani"
"Hata siingii unasikia hizo kelele kule bondeni"
"Ndiyo ni nani huyo"
"Ni mpangaji wa Mzee Abdul"
"Mpangaji gani hapo?? naonaga kuna wapangaji wanne"
"Ni yule anayeuza ndizi gengeni"
"Aaaa yule Muha mwenye mtoto mdogo"
"Huyohuyo"
"Kapatwa na nini?"
"Hata sijui.. Ila nilikuwa naoga humo bafuni kwangu nikasikia vishindo vya mtu anamkimbiza"
"Watakuwa vibaka hao siunajua siku izi machimbo hayatemi"
"Kwa kweli nimekuja kukuamsha tukamsaidie"
"Aya ngoja nivae suruali nisubiri nakuja"
"Sawa wewe vaa nimuamshe na Mwalimu Mashauri hapa"
"Aya"
Baada ya dakika saba watu zaidi ya Thelathini walokuwa wamekuasanyika. Hakika walikuwa wamechoshwa na vibaka katika mtaa huo na ndiyo sababu wengi wao walikuwa wamebeba siraha za hatari kama vile mapanga, marungu, mikuki, na visu na kila ghasia. Walisudia kwenda kumfanyia kitu kibaya mtu aliyekuwa anamkimbiza Mama Jamali.
Kabla hawajaianza safari ya kwenda bondeni, kutoa msaada sauti ya mtoto akilia iliwafanya wabadilishe mawazo, wote wakawa wanamshangaa mtoto huyo aliye kaa chini, nje tena usiku peke yake.
Laiti angelikuwa siyo mtoto pengine wangeliwahi bondeni na kuokoa maisha ya Mama huyo na Mzee Juma asingepata mwanya wa kutimiza adhima yake. Lakini walichelewa.
Baada ya kumusaidia Mtoto huyo na kumkabidhi mikononi mwa wasamalia wema. Ndipo safari ya kwenda bondeni ilianza na hata walipofika walishangaa kumuona Mzee mfupi akiwa ametapakaa damu na pembeni walimona mtu akiwa amelala. Kama ujuavyo watu wenye hasira kali hawakutaka kuuliza hapo hapo wakaanza kumshambuli moja kwa moja walijua huyo ndiye aliye tekeleza mauaji kutokana na mazingira waliyomkuta
STORY HII UNAWEZA KUIPATA YOTE WHATSAPP NA FACEBOOK INBOX KWA SHILINGI 2500 AU VIPANDE VITATU KWA SHILINGI 500 PIA USIACHE KU-COMENT, KU-LIKE NA KU-SHARE ILI UJINYAKULIE ZAWADI
ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom