Aina za wasukuma na kisukuma

Gawiza...!!

Lugha ya kisukuma ina lahaja kuu nne; ginantuzu, ginang'weli, ginangw'agala na gidakama. Vivyo hivyo, Wasukuma wamegawanyika katika misingi ya lahaja za lugha ya kisukuma.

1.Bhadakama. Hawa wanapatikana sehemu za mji wa Shinyanga, sehemu za Gahama na sehemu za Igunga na Nzega. Kwa idadi, hawa ndiyo Wasukuma wachache sana. Ni watu wenye aibu, wakimya mno... wana muingiliano na utamaduni wa Wanyamwezi. Pengine hawa ndiyo Wasukuma masikini kuliko aina yoyote ya Wasukuma!

2. Bhanang'weli.
Hawa ni Wasukuma wenyeji wa mikoa ya Mwanza, Geita, na kusini - Magharibi mwa Mkoa wa SIMIYU. Kiidadi, hawa ndiyo Wasukuma wengi sana... katika ongea yao, wana matumizi mengi ya 'shi' kwa mfano, shikolo, shiliwa. Pia hawatumii 'ng'wadila' katika salamu za jioni. Wao hutumia 'gawiza' au 'dillo gawiza' Kwa sababu wanaishi katika strategic areas, wana muingiliano na watu wa makabila mbalimbali. Au tuseme wamemezwa na watu wa kuja. Ukienda Geita wenyeji hawaonekani, labda kukimbiza daladala za baiskeli. Mwanza ndiyo usiseme kabisa.

3. Bhanang'wagalla.
Hawa ni Wasukuma wenyeji wa Wilaya za Meatu, Kishapu na Maswa na sehemu za Igunga. Ukikutana nao ni rahisi mno kuwasikia wakisema, 'yombaga bhahebhu', ong'wawiya, kaaa, aghayaa... ni nadra sana kuwasikia wakisalimia, 'ng'wadila' Wao hufupisha, 'dilla mayu' au dilla bhabha. Majina ya maeneo mengi huanza na Ng'wa. Kwa mfano, ng'wabagimu, ng'wajidalala, ng'wanhuzi... Utajiri wao uko kwenye mifugo.
Vijana wa huko hulizika mapema. Kwa mfano, kama mavuno ya matobholwa, karanga, alizeti na pamba ni mazuri, vijana wa maeneo haya hushinda kwenye ngoma za jadi. Hawajui kusaka ridhiki nje ya maeneo yao, utafikiri wako kisiwani. Wanaotoka nje ya maeneo yao ni wafugaji tu. Wanawake wa huko hupenda kuvaa shanga kiunoni na shingoni ingawa sio wajuzi wa mambo ya Tanga. Wavulana nao huvaa miguuni. Soko la wasichana liko juu sana. Pengine huu ukanda, hasa Meatu, ndiyo unaongoza kwa kutoa mahari kubwa Tanzania nzima.

4.Bhanantuzu /Wanyantuzu
Hawa ni Wasukuma wenyeji wa Wilaya za Bariadi na Itilima. Hawa ndiyo Wasukuma waliotapakaa kila kona ya nchi hii. Na pengine bila ya hawa kabila la Wasukuma
lisingejulikana kwa namna hii. Kisukuma chao hakina 'shi' bali hutumia 'si' kwa mfano, sikolo, siliwa....Jamaa hawa wanajua kuchakalika kutafuta mali. Hawaogopi kitu, hawaogopi mtu. Jamaa hawa ndiyo Wasukuma pekee wanaothubutu kwenda kupora ng'ombe za Wamasaai. Ni Wasukuma wenye dharau na mikogo mingi. Kama unasikia watu wanaopenda utani na masihara, basi hawa ni kiboko. Si unamjua Danni Makanga? Mambo ya ujanja ujanja na upigaji dili, hapa ndipo penyewe. We mwangalie Chenge tu, au hata Cheyo au hata Mbunge Njaru. Utanipa jibu. Wanaume wa huko hupenda kuoa wake weupe. Kama sio mweupe basi awe na sifa za ziada. Michepuko kwa mwanaume ni kitu cha kawaida.

Swala la ni msukuma yupi anaongoza kwa ushamba na ukilaza, halikuwa lengo la utafiti huu.

Mobheja sana.
Naitwa Masanja Lunyilija Nebelwa.Uchambuzi wako uko sahihi kabisa.Ulimhola nkoyi?
 
Kwenye hizo lahaja za kisukuma, mbona hujawataja wanzilankende mkuu. Ina maana Magufuli sio msukuma coz yy ni mnzilamkende akidai ni msukuma pia. Mkuu hivi hawa wanzilankende hawana asili ya Rwanda kweli?
 
Umejitahidi lakini kuna sehemu kubwa sana hujaweka mambo sawa. Mfano:Ntuzu ni utemi ambao ulikuja kujulikana sana baada ya tarafa ya Ntuzu ambayo mtemi wake Wa Mwisho alikuwa Ndatulu, 1974 Bariad iliyotokana Na jina "Kubalya Dii" ulio karibu Na kanisa katoliki bariadi .
 
Shikolo- bhanang'weli
Sikolo- Wanyantuzu
Jikolo-Bhanangw'agala/bhadakama
Uko vizuri mkuu, kuna kipindi nilikuwa shy kila nikuongea baadhi ya sentensi wananicheka na kunirekebisha
 
Kutokana Na eneo la Somanda kuwa makao makuu ya wilaya,karibia kila MTU Wa eneo Jirani alitamani kuonekana Wa Mjini Na kujiita MTU Wa Ntuzu. Ng'wagala ni utemi mdogo ambao haufiki maeneo uliyotaja. Nadhani lengo lako kuu ilikuwa kuwasifia watu Wa bariadi ili waonekane wako juu.
 
Wasukuma ni watu washamba na waoga sana.

Mwaka wa 2001, niliwahi kuona ugomvi wa panga barabara ya serengeti kuelekea geti la Nabi ambapo Wamasai wawili waliwakatakata wasukuma waliokuwa weengi haswa kwa panga na bado wamasai wakawa wanawafuata wasukuma wakakimbia na kuacha ng'ombe zao.


Wasukuma walikuwa wengi kuzidi Maasai.
 
Asante Ndugu. Vipi kuhusu salamu zao? Kama Engh'washi, Esega, EMiinza, Engolo..nk. Zinazingatia nini?
 
Asante Ndugu. Vipi kuhusu salamu zao? Kama Engh'washi, Esega, EMiinza, Engolo..nk. Zinazingatia nini?
 
Safi sana, kula kudos na tano juu, Wabheja mno, (1.Bhadakama. Hawa wanapatikana sehemu za mji wa Shinyanga, sehemu za Gahama na sehemu za Igunga na Nzega. Kwa idadi, hawa ndiyo Wasukuma wachache sana. Ni watu wenye aibu, wakimya mno... wana muingiliano na utamaduni wa Wanyamwezi. Pengine hawa ndiyo Wasukuma masikini kuliko aina yoyote ya Wasukuma!)
 
Mimi naanzia Bariadi, somanda,oldmaswa, mwakibuga, nyakabindi,Dutwa,igegu, sapiwi. Then kuelelea shinyanga ni Bariadi, Kidulya,luguru, mwamapalala maswa,. Kuelekea magu unatoka bariadi, salunda, ibulyu, mbiti,ngulyati,kasoli alliance gunnery thenu magu. Ukitokea mwamapalala unaenda dasina, gambasingu l,lagangabilili,Ngheaha, logolambogo,shishani na ukirudi unatokea Bumera au nkololo then pldmaswa to Bariadi. Unaweza pia ukatokea nyakabindi, ikungilyabashashi, gamboshi to mbiti ulaamuua kurudi Brd au kwenda Magu hadi mwanza.
 
Wale wasukuma JEMBE ndiyo wapo chato?hata kule bukoba,mara na singida kidogo wasukuma wapo kibao je?hao nao ni wasukuma gani?
Chato wanakaa wasubi, waketewe, wahangaza, wazinza na waha. Wazinza ni kama wasukuma na wakerewe na wasubi ni kama watutsi na asili yao ni Burudi na Rwanda. Nadhani sizonje ni msubi
 
Chato wanakaa wasubi, waketewe, wahangaza, wazinza na waha. Wazinza ni kama wasukuma na wakerewe na wasubi ni kama watutsi na asili yao ni Burudi na Rwanda. Nadhani sizonje ni msubi
Siyo kweli, Wazinza ni jamii za Interlacustrine na hawana uhusiano wowote na Wasukuma labda tu wote kwa kuwa ni Wabantu. Wazinza wana uhusiano wa karibu na Wahaya na Wanyambo, pamoja na Wasubi na siyo Wasukuma "Nkoi"
 
Wanajamii mbona threads za ukabila kwenye JF,zimekua nyingi Sana wakati huu kuliko huko tulikotoka? ni pepo linataka kutuingilia kinyume na maumbile humu ndani?? Ngoja nianze kulikemea kabla hamjaingiliwa nyote humu JF. Shindwa nasema Iegeaaaah hutakieee? Shindwa uwe mbendembende nasema shhhhhndwa.
 
Back
Top Bottom