Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,662
- 20,416
Kule kwa wazenji kwenye blog moja (jina kapuni) nimekutana na post ya jamaa mmoja ambaye anasema ameamua kuachana na JF kwa kile alichoona ina 'post zenye maudhi'. Msome hapa chini:
Jamani punguzeni ukali wa makombora, tunahitaji michango yao humu hao jamaa!
kassem 15/02/2012 kwa 12:34 um ·
Kule Jamii foroum kumenishinda. Kumenishinda kwasababu ya kejeli zao kwa Waislamu na Wa-Zanzibari. Nyuso zao mbaya zimekosa hata kuona aibu kutukana watu wa Zanzibar. Kuendelea kubakia ni kuzidi kujiudhi kwa hiyo nikaamua kuachana nao kwanza sioni faida niipatayo. Juzi CUF walipokwenda Ikulu kukawa na picha ambayo kama nakumbuka vizuri kuna Samiha Suluhu na mfanyakazi wa Ikulu mwengine ambao wote wamevaa Hijab ehee Jamii Forum wamepata nini tena Haya mahijabu ya nini Ikulu mwengine kasema vyake almradi ni kejeli tu.
Jamani punguzeni ukali wa makombora, tunahitaji michango yao humu hao jamaa!