AICC, Arusha: Wakili Fatma A. Karume aangua kilio akiwahutubia Mawakili Wasomi

Basi na kakiingereza kako ka ugoko hako ndio unadhani utaonekana 'msomi'! Duuuh.

Eti "personal inferiority 'belong' to you"!!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Msiuchukulie personal huu mjadala, ni maoni tu, yayoweza kuwasaidia kuongeza ufanisi kwenye kazi zenu kuheshimika zaidi na kuwasaidia wananchi.

Kuna matatizo mengi kesi za kubambikiziwa maskini, watu kukaa mahabusu muda mrefu bila kesi zao kusikilizwa wengine hawana hatia kabisa, makosa madogo kama faini chini ya laki moja kutupwa jela miezi sita, ingewezekana kuwapa Community service.

Mrundikano wa watu magerezani, chakula, watu wenye mental problem kuendelea kuwa gerezani, wakimbizi mfano Waethiopia kuwekwa lupango kwa gharama kubwa sana ya kodi yako si bora wangepigwa faini,

Kesi za nyumba, Mashamba, viwanja, wakulima, wajane, yatima, makini wanavyodhulumiwa, gharama za kupambana na matajiri, Polisi, Usumbufu kwenye mahakama za mwanzo.

Haya mambo yangewapa credibility, relevance kubwa sana kama mngeyasimamia kwa nguvu zote kila siku, kupiga kelele kwa wananchi wengi. Sababu yanawagusa moja kwa moja.

Kwamba hata hapa JF mngeanzisha hata uzi kuwasaidia wananchi na basics abc za sheria, haki zao, kwenye criminal, property, cooperate laws etc.

Kwamba mnaweza kujitolea labda kuchukua kesi fulani moja kwa mwaka kwa wanyonge kuwasimamia bila pesa.

Ni ushauri tu kwa hii taasisi yenu. Msikwazike sana. Nothing personal.
 
Rais anayemaliza muda wake wa Chama cha Mawakili Tanganyika(TLS), Wakili Msomi Fatma Karume ameangua kilio alipokuwa akifungua Mkutano wa Mawakili Wasomi unaofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha(AICC).

Wakili Msomi Karume alikuwa akitoa ripoti ya majukumu na utekelezaji wa majukumu hayo kwa kipindi chake cha Urais wa TLS. Ripoti hiyo imesheheni mafanikio yake yakiwemo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ndani ya TLS na kusimamia utawala wa sheria kwenye nchi hii.

Wakili Msomi Fatma Karume alimaliza hotuba yake kwa kuangua kilio akiwaambia Mawakili Wasomi kuwa wamempa heshima kubwa na nafasi adimu na adhimu kuwaongoza kama Rais wao kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Katika kuonyesha kuwa amewagusa wahusika,Mawakili Wasomi walisimama kwa heshima huku wakimshangilia Wakili Msomi Fatma Karume. Kimsingi,Wakili Msomi Fatma Karume aliwaaga na kuwashukuru wanachama wote wa TLS.

Uchaguzi wa uongozi mpya wa TLS utafanyika kesho hapa Arusha.


Ndugu Petro E. Mselewa

Nadhani kwa kunyambua wakili msoni na mawakili wasomi umemaanisha kuwa kuna mawakili wasiokuwa wasomi. Tafadhali tusaidie kuwajua mawakili wasiokuwa wasomi kusudi tusiwatumie katika shghuli zetu. Mwanzoni nilikuwa najua kuwa mawakili wote lazima wawe namesomea elimu ya sheria angalu kiwango cha diploma a kuthibitishwa na mahakama kuu; kwa marekani lazima awe na digrii ya kwanza ya Arts au Sayansi na baadaye upate JD na kupasi mtihani wa bench. Kuna taaluma nyingi sana kama Uhandishi, udaktari, na uhasibu ambazo kwa taaluma hiyo tu unakuwa unajulikana umeisomea wala huna haja ya kusema msomi daktari, msomi mhandisi au msomi mhasibu, msomi mkaguzi wa mahesabu. Kwa nini uliamua kunyambulisha usomi kwenye uwakili? Je kuna mawakili siyo wasomi?.
 
Ndugu Petro E. Mselewa

Nadhani kwa kunyambua wakili msoni na mawakili wasomi umemaanisha kuwa kuna mawakili wasiokuwa wasomi. Tafadhali tusaidie kuwajua mawakili wasiokuwa wasomi kusudi tusiwatumie katika shghuli zetu. Mwanzoni nilikuwa najua kuwa mawakili wote lazima wawe namesomea elimu ya sheria angalu kiwango cha diploma a kuthibitishwa na mahakama kuu; kwa marekani lazima awe na digrii ya kwanza ya Arts au Sayansi na baadaye upate JD na kupasi mtihani wa bench. Kuna taaluma nyingi sana kama Uhandishi, udaktari, na uhasibu ambazo kwa taaluma hiyo tu unakuwa unajulikana umeisomea wala huna haja ya kusema msomi daktari, msomi mhandisi au msomi mhasibu, msomi mkaguzi wa mahesabu. Kwa nini uliamua kunyambulisha usomi kwenye uwakili? Je kuna mawakili siyo wasomi?.

Soma michango iliyotangulia
 
Achana na mambo wakili msomi, unaonekana ni mjinga, hujasoma, hujaelimika, Mshamba flani.

Ila wapo wamesoma USA, UK, hawatumii maneno hayo.
eti USA UK kwendaaaa kibaraka wahedi, ndo nini kwani. MLIMANI HOYEEEE! NDO SISI HAOOO!
 
eti USA UK kwendaaaa kibaraka wahedi, ndo nini kwani. MLIMANI HOYEEEE! NDO SISI HAOOO!

Point yako ni nini hasa?

Au labda ni kutukana, kama ni hivyo umekamililisha malengo.

Tulia, andika taratibu, ueleweke unataka nini, unaongea nini, unauliza nini? Kama una hoja itajibiwa kwa ukamilifu..
 
Back
Top Bottom