Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,788
- 218,416
Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Mbeya, Wakili wa Mwabukusi, Mwakilima, amesema kwamba Maudhui yanayosambaa mtandaoni na kudaiwa kwamba ni ya Boniface Mwabukusi yamewekwa na Polisi wenyewe baada ya kudukua akaunti yake ya Instagram baada ya kumnyang'anya simu yake ya mkononi.
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba, ndio maana hakukuwa na taarifa hizo awali, zimeletwa ghafla baada ya udukuzi huo kufanikiwa.
Lengo la jambo hili ni kuudanganya umma ili ijulikane kweli kwamba Mwabukusi na wenzake ni Wahaini.
Ni aibu sana kwa Jeshi letu la Polisi, kugundulika kufanya njama hii ya kijinga, na ni kuidhalilisha nchi nzima kwa manufaa ya DP WORLD na wapambe wake.
Nakala imfikie wakala wa DP WORLD Ritz