Zipuwawa
JF-Expert Member
- Nov 28, 2010
- 3,051
- 653
Wengi watadhani ninachokiandika hapa ni cha kijinga ila vyombo vya habari vya Tanzania vina tia Aibu. Kazi ya vyombo vya habari ni kupasha habari jamii hasa pale habari zozote muhimu au mbaya zinapotokea. Lakini imekuwa tofauti kwa vyombo vya habari Tanzania yapo kama sasa kuna matukio mengi zanzibar na Tanzania Bara lakini vyombo vinapiga miziki tu bila hata kujua umuhimu wao wao wanasubiri saa 2 usiku ndio watoe habari hizo huku hata habari nyingine kufichwa kabisa huu ni ujinga na aibu.
Angalau ITV hujitahidi kutoa habari za saa lakini nao wamekuwa wakirudia hata za jana ina maana gani? TBC ndio ujinga kabisa sioni hata haja ya kuwa na chombo hichi kwa Taifa , Star TV kama kawaida......Sasa nani kasema vyombo vya habari ni kuwapasha watu habari saa mbili tu usiku na marudio sanne au saa tano.
Kwanini Wananchi hawapati habari za kweli na za uhakika zikiwa za moto? Huu ni ujinga na ugonjwa kwa vyombo vya habari.
Nasema Bora uwe humu jamii Forum utapata kila siku kuliko kusikiliza hizi radio na TV za kibabaishaji.
Wanajamii mimi nakerwa na hili kutokana na matukio mengi kama ya uchomaji wa makanisa na mengine kupata kutoka kwenye mitandao kuliko hivi vyombo vya habari. Nawasilisha hoja yangu wana jamii
Angalau ITV hujitahidi kutoa habari za saa lakini nao wamekuwa wakirudia hata za jana ina maana gani? TBC ndio ujinga kabisa sioni hata haja ya kuwa na chombo hichi kwa Taifa , Star TV kama kawaida......Sasa nani kasema vyombo vya habari ni kuwapasha watu habari saa mbili tu usiku na marudio sanne au saa tano.
Kwanini Wananchi hawapati habari za kweli na za uhakika zikiwa za moto? Huu ni ujinga na ugonjwa kwa vyombo vya habari.
Nasema Bora uwe humu jamii Forum utapata kila siku kuliko kusikiliza hizi radio na TV za kibabaishaji.
Wanajamii mimi nakerwa na hili kutokana na matukio mengi kama ya uchomaji wa makanisa na mengine kupata kutoka kwenye mitandao kuliko hivi vyombo vya habari. Nawasilisha hoja yangu wana jamii