Aibu kubwa nyingine kwa chama tawala - CCM

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Inaweza kuonekana kama si jambo kubwa sana, lakini likawa na maana kubwa sana. Tena linaweza lisionekane kumaanisha kitu lakini likawa na ujumbe mzito uliojificha.

Katikati ya rasimali watu zaidi ya mia mbili, na kuna wengine wamechukuliwa nje ya hao lakini bado wameshindwa kutimia 34 tu aliowakusudia Mh.RAIS! Hivi hilo ni jambo la kawaida kweli!? Labda angetumia wiki moja au mbili kuwatafuta huenda tungesema muda ulikuwa hautoshi. Lakini si hivyo, ametumia zaidi ya siku 32 kuwachuja toka miongoni mwa hao 200+ na nje ya hao lakini ameshindwa kuunda kikosi kazi chenye idadi aliyoikusudia achilia mbali sifa na umakini anaouhitaji kwani binadamu hatuwezi kuwa sawa!

Nionavyo mimi, ndani ya hao 200 na ushee wa CCM amewakosa wenye mawazo na maona ya kizalendo kwa nchi yao TANZANIA! Huenda, narudia tena huenda walio wengi wana uzalendo kwa wao binafsi, kwa chama, familia zao na kwa matapeli na mafisadi wakubwa wa nchi zaidi kuliko uzalendo walio nao kwa Taifa ndio maana RAIS anahangaika kuwamulika kwa tochi ndani na nje ya waliochaguliwa lakini bado hawatimii 34 aliowakusudia kuanza nao!

USHAURI WANGU: Mtakaporudi bungeni, jaribu kuwa wazalendo kwa nchi kuliko chama na watu. Jaribuni kuumizwa na shida za watanzania kuliko kung'ang'ania kupitisha mikataba itakayowanufaisha watu ambao wakiwa huko wana wacheka na kuwadharau! Jaribuni kuheshimu na kuthamini mawazo ya wanaokosoa serikali na kuelekeza nini cha kufanya kwani huo ndo wajibu wenu. HII NI AIBU KWA CHAMA TAWALA KUKOSEKANA KWA MAWAZIRI WENYE SIFA WA KUTOSHA!
 
Most of CCM members are so conservative and corrupt, that is why Mr Jpm has spent alot to try to get at least few from them to cover the positions but has failet. To get a clean man from among ccm members is like trying to find a grain of millet from a shower sand.
 
Kuwa Rais wa nchi si sawa na kuwa Mwenyekiti wa chama. Magufuli anatafuta watu ambao wataendana na kasi yake na ambao watakidhi matarajio ya Watanzania. Kumbuka performance nzuri ya serikali ni ushindi kwa CCM.
 
Most of CCM members are so conservative and corrupt, that is why Mr Jpm has spent alot to try to get at least few from them to cover the positions but has failet. To get a clean man from among ccm members is like trying to find a grain of millet from a shower sand.
Lakini pia ameamua kuwaacha wana CCM wengi ili chama kitimize jykumu lake la kuisimamia serikali badala ya kazi hiyo kufanywa na upinzani
 
Mnaoponda Uteuzi Huu,je Mlitaka Wachaguliwe Malaika?
Tatizo Baadhi Mmejawa Na Chuki Kwa Baadhi Ya Hao Waliochaguliwa Kwa Kuwa Ndo Walikuwa Mwiba Katika Kampeni...Lakini Tukaye Tujue Kampeni Zimekwisha Mmeshindwa,na Miiba Iliyowachoma Ndiyo Inaongoza Serikali,tuache Wafanye Wajibu Wao.
 
Mnaoponda Uteuzi Huu,je Mlitaka Wachaguliwe Malaika?
Tatizo Baadhi Mmejawa Na Chuki Kwa Baadhi Ya Hao Waliochaguliwa Kwa Kuwa Ndo Walikuwa Mwiba Katika Kampeni...Lakini Tukaye Tujue Kampeni Zimekwisha Mmeshindwa,na Miiba Iliyowachoma Ndiyo Inaongoza Serikali,tuache Wafanye Wajibu Wao.

Mkuu Tony, hawa nyumbu ni haki yao kufanya hivyo. Kumbukawamekuwa kimya kwa muda wa mwezi mmoja. Hawakuwa na Kick baada ya msiba wa Mawazo. Na hili litapita tu
 
Tulieni mpingo uwaingie bado mnaweweseka tu? Chama dume,chama kikuu cha upinzani miaka ishirini mmeshindwa kutayarisha viongozi kwa miaka yote hiyo hadi kusubiri makombo,matapishi na fisadi watapikwe Ccm ndio mlambe matapishi? Ni aibu iliyoje hii. Huko Jembe Dr Magufuli anachambua,jambo jema halitaki haraka
 
Kwa Mujibu wa KATIBA YA 1977 MH.RAISI HUTEUA KWA NAMNA APENDAVYO WEWE NI MTU MZIMA UNAELEWA NA ANA UHURU MPANA NA WA KUTOSHA KUMTEUA MTU NA WALA HANA ULAZIMA KUMTEUA MWANA CCM TU ILA ANAETEULIWA AWE MBUNGE HAFUNGWI NA KIPENGELE CHO CHOTE ILA BASI MH.RAISI ANAYAISHI MANENO YAKE KIVITENDO AKIWATANGULIZA WANANCHI MBELE NA MAMA TANZANIA ACHENI KUZOZA
 
Mnaoponda Uteuzi Huu,je Mlitaka Wachaguliwe Malaika?
Tatizo Baadhi Mmejawa Na Chuki Kwa Baadhi Ya Hao Waliochaguliwa Kwa Kuwa Ndo Walikuwa Mwiba Katika Kampeni...Lakini Tukaye Tujue Kampeni Zimekwisha Mmeshindwa,na Miiba Iliyowachoma Ndiyo Inaongoza Serikali,tuache Wafanye Wajibu Wao.

Wewe ndiye mpuuzi mwisho! Hoja hapa siyo wachaguliwe malaika! Rais ametumia zaidi ya mwezi kujaribu kusuka baraza la mawaziri kutoka miongoni mwa wana CCM ameshindwa!!!

1. Je Rais hakujiandaa kuwa kiongozi mkuu wa nchi?!
2. Je wana CCM wote zaidi ya 200 wamekosa sifa ya kuwa mawaziri?!
3. Je Rais amekosa wana CCM wengine nje ya wabunge ambao wanafaa kuwa mawaziri?!

Kama hali ikiendelea hivyo ni vema akalivunja bunge ili uchaguzi mwingine ufanyike huenda wenye sifa wakapatikana!

Mungu apishie mbali, endapo mmoja wa mawaziri wake akifariki itamchukuwa muda gani kupata mbadala (replacement)?!
 
Wewe ndiye mpuuzi mwisho! Hoja hapa siyo wachaguliwe malaika! Rais ametumia zaidi ya mwezi kujaribu kusuka baraza la mawaziri kutoka miongoni mwa wana CCM ameshindwa!!!

1. Je Rais hakujiandaa kuwa kiongozi mkuu wa nchi?!
2. Je wana CCM wote zaidi ya 200 wamekosa sifa ya kuwa mawaziri?!
3. Je Rais amekosa wana CCM wengine nje ya wabunge ambao wanafaa kuwa mawaziri?!

Kama hali ikiendelea hivyo ni vema akalivunja bunge ili uchaguzi mwingine ufanyike huenda wenye sifa wakapatikana!

Mungu apishie mbali, endapo mmoja wa mawaziri wake akifariki itamchukuwa muda gani kupata mbadala (replacement)?!

nashukuru kuona umenielewa, maana naona kuna wengine wanaweweseka na kwende nje ya mada na kuanza kuleta hoja za upinzani na uccm hapa. ishu ni miongoni mwa wabunge 200 na zaidi na wasio wabunge wana ccm, RAIS kakosa anayefaa kuwa waziri wa ELIMU, FEDHA, UTALII NA MIUNDOMBINU ili angalau amalize kazi moja aendelee na mengine? Wana CCM msilikwepe hili, lazima kuna tatizo tu!
 
Kwa Mujibu wa KATIBA YA 1977 MH.RAISI HUTEUA KWA NAMNA APENDAVYO WEWE NI MTU MZIMA UNAELEWA NA ANA UHURU MPANA NA WA KUTOSHA KUMTEUA MTU NA WALA HANA ULAZIMA KUMTEUA MWANA CCM TU ILA ANAETEULIWA AWE MBUNGE HAFUNGWI NA KIPENGELE CHO CHOTE ILA BASI MH.RAISI ANAYAISHI MANENO YAKE KIVITENDO AKIWATANGULIZA WANANCHI MBELE NA MAMA TANZANIA ACHENI KUZOZA

kazi hiyo atake asitake lazima aifanye na mawaziri ambao ndo washauri wake wakuu na ambao bado inaonesha wenye kuiweza kazi hiyo wamekuwa wachache kiasi kwamba hata hao wachache aliowahitaji ameshindwa kuwapata kwa wakati ndani na nje ya wabunge wa ccm
 
Wewe ndiye mpuuzi mwisho! Hoja hapa siyo wachaguliwe malaika! Rais ametumia zaidi ya mwezi kujaribu kusuka baraza la mawaziri kutoka miongoni mwa wana CCM ameshindwa!!!

1. Je Rais hakujiandaa kuwa kiongozi mkuu wa nchi?!
2. Je wana CCM wote zaidi ya 200 wamekosa sifa ya kuwa mawaziri?!
3. Je Rais amekosa wana CCM wengine nje ya wabunge ambao wanafaa kuwa mawaziri?!

Kama hali ikiendelea hivyo ni vema akalivunja bunge ili uchaguzi mwingine ufanyike huenda wenye sifa wakapatikana!

Mungu apishie mbali, endapo mmoja wa mawaziri wake akifariki itamchukuwa muda gani kupata mbadala (replacement)?!

Mtu unatumia mwezi kumfikiria Nape?
Mwigulu?
Mwakyembe?
MUHONGO?
Simbachawanene?
Makamba?
Endelea. . .

Ajabu sana
 
Tulieni mpingo uwaingie bado mnaweweseka tu? Chama dume,chama kikuu cha upinzani miaka ishirini mmeshindwa kutayarisha viongozi kwa miaka yote hiyo hadi kusubiri makombo,matapishi na fisadi watapikwe Ccm ndio mlambe matapishi? Ni aibu iliyoje hii. Huko Jembe Dr Magufuli anachambua,jambo jema halitaki haraka
Ni jambo la kawaida. Kuna chama kilikosa mgombea urais kikasubiri makapi toka Chama dume bado kikaangukia pua
 
Back
Top Bottom