Aibu, fedhea ya DART, Jiji, Manispa Dar

Aibu, fedhea ya DART, Jiji, Manispa Dar

Yaani sisi bado sana kwa kweli,utajisaidiaje kwenye kituo cha basi jamani,kabla ya vituo hivyo walikuwa wanajisaidia wapi?ila pia inatakiwa kuwe na wafanya usafi,ila jamani waweke ulinzi ili watu wasijisadie kabisa,yaani sisi watu weusi bila viboko ni sio wastaarabu hata kidogo

Inasemekana vyoo vipo lakini muda wote vimefungwa kwa sababu utaratibu wa kuvisimamia haujaandaliwa!!....lol makubwa haya

Ni sawa na mtu unaanzisha biashara ya nyumba ya kulala wageni, hotel au bar unakuwa huna choo!!
 
Mi nashangaa sana muafrika anataka kuwa na maendeleo kama ya mzungu lakini vikwazo na changamoto anazopitia huzichukulia kama laana kwa mtu mweusi na kumfanya ajione yeye ni binadamu tofauti na alivyo mzungu. Anasahau hata hao wazungu hawakulala na kuamka na kujikuta wamefika hapo walipo,yapo mengi tu ambayo nao wameyapitia.
 
Tatizo kubwa la Watanzania au niseme Waafrika ni akili. Walio wengi "majority" ni finyu kupita kiasi.

Mambo yetu yote ni hovyo kabisa.
Akili tunayo tatizo ni uvivu wa kuzitumia tu.Na pia self dispiline ndio zero kabisa
 
Yani mradi unaanza alafu utaratibu wa matumizi ya vyoo bado haujakamilika.Huu ni uzembe mkubwa.Inamaana kinyesi kinasubiri mchakato?
 
Ccm imeharibu sana watanzania
Hapo ndipo ulipo dhihirisha umbumbumbu wako..... Huna tofauti na hao wanaokojoa kwenye hizo sehemu...

Jikomboe kifikra broo!!! Uchama hata kwenye mambo yasiyo ya kichama unajitukana.... Usipende watu watu wajue sana ulivyo kiakili na kitabia
 
Inasemekana vyoo vipo lakini muda wote vimefungwa kwa sababu utaratibu wa kuvisimamia haujaandaliwa!!....lol makubwa haya

Ni sawa na mtu unaanzisha biashara ya nyumba ya kulala wageni, hotel au bar unakuwa huna choo!!
Hivi vituo vya kawaida havina vyoo pia mbona hawashushi mizigo yao hapo

Sisi watanzania/Afrika ni bure kabisa kwenye mambo mengi usafi moja wapo.

Bila kubadilika hatutafika popote.
 
kuna vituo vingine havijakamilika kama Ubungo,Morocco na Kimara mwisho.

Jana ndio wametoa tangazo la kutafuta wafanya usafi wa vyoo.

Kuna vituo sehem ya kufanyia malipo hayajakamilika,mfano kufunga mashine za kukatia risit amna.
 
Hivi vituo vya kawaida havina vyoo pia mbona hawashushi mizigo yao hapo

Sisi watanzania/Afrika ni bure kabisa kwenye mambo mengi usafi moja wapo.

Bila kubadilika hatutafika popote.

Mimi niko zangu kwetu Shinyanga mkubwa. Haya mambo tunayasoma na kuyaona kupitia media tu

Una maanisha ktk vituo cha mabasi hayo hakuna vyoo kabisa?

Nilitazama taarifa ya habari ITV jana wakionesha jinsi watu wanavyojisaidia hovyo na wengine kwenye chupa za maji poa.

Sina hakika sana iwapo hii ilikuwa ndani ya bus au ktk vituo vya mabasi haya

All in all ni kwamba wahusika walipohojiwa walisema utaratibu wa kutumia hivyo vyoo ulikuwa haujakamilika na kwamba wanaongea na watu wa DAWASCO kwa ajili nadhani kuunganishiwa huduma ya maji ili j3 kesho vyoo hivyo vianze kutumika!!

Sasa nashangaa kusema hapa hakuna vyoo ktk vituo hivyo!!
 
Sasa naona mtapewa vibali maalum vya kuingia jijini Dar-es-salaam....
masikini babu yangu al-watan uliwajengea jiji lenye jina la mbinguni !!!😛😛😛
 
Mradi wa UDART umedhihirisha tabia halisi ya mtanzania (mwafrika). Tukitukanwa tunalalamika, hatuna akili.
 
Mimi niko zangu kwetu Shinyanga mkubwa. Haya mambo tunayasoma na kuyaona kupitia media tu

Una maanisha ktk vituo cha mabasi hayo hakuna vyoo kabisa?

Nilitazama taarifa ya habari ITV jana wakionesha jinsi watu wanavyojisaidia hovyo na wengine kwenye chupa za maji poa.

Sina hakika sana iwapo hii ilikuwa ndani ya bus au ktk vituo vya mabasi haya

All in all ni kwamba wahusika walipohojiwa walisema utaratibu wa kutumia hivyo vyoo ulikuwa haujakamilika na kwamba wanaongea na watu wa DAWASCO kwa ajili nadhani kuunganishiwa huduma ya maji ili j3 kesho vyoo hivyo vianze kutumika!!

Sasa nashangaa kusema hapa hakuna vyoo ktk vituo hivyo!!
Vyoo vipo labda tu havijaanza kutumika lakini hiyo pia sio sababu ndio maana nikasema mbona vile vingine havina vyoo na vingine hata paa au sehemu ya kukaa hamna mbona hawashushi mizigo hapo.

Za Shinyanga lakini, kwema? Karibu Dart bwana.
 
Vyoo vipo labda tu havijaanza kutumika lakini hiyo pia sio sababu ndio maana nikasema mbona vile vingine havina vyoo na vingine hata paa au sehemu ya kukaa hamna mbona hawashushi mizigo hapo.

Za Shinyanga lakini, kwema? Karibu Dart bwana.

Shy ni poa kabisa, hatuna umeme leo bwana sijui kuna nini tu.

Ishu ya umeme huku kwetu ni karibu miezi mitano sasa, kila jumapili tunakuwa hatuna kwa takribani masaa 16 kuanzia saa 12asb hadi wakati mwingine saa 3usiku!

Back to the topic;

Inawezekana mizigo ilikuwa haishushwi kutokana eneo kuwa la wazi tofauti na stend za mabasi ya DART zenye vikona kona na sehemu zingine giza kiasi ambacho mtu aweza kufanya mambo yake tu na kujisitiri!!
 
Shy ni poa kabisa, hatuna umeme leo bwana sijui kuna nini tu.

Ishu ya umeme huku kwetu ni karibu miezi mitano sasa, kila jumapili tunakuwa hatuna kwa takribani masaa 16 kuanzia saa 12asb hadi wakati mwingine saa 3usiku!

Back to the topic;

Inawezekana mizigo ilikuwa haishushwi kutokana eneo kuwa la wazi tofauti na stend za mabasi ya DART zenye vikona kona na sehemu zingine giza kiasi ambacho mtu aweza kufanya mambo yake tu na kujisitiri!!
Poleni sana Nasikia Songas wamegoma kuuza umeme kwa Tanesco, Tuvumilie tu

Back to the Topic,

Sasa kwa nyomi ile pale vituoni na vyoo vimefungwa unajisaidiaje nje? Inahitaji ujasiri wa aina yake.
 
Wakulaumiwa ni watu wanaokijoa na kunya hovyo kabla ya watu wengine. Watu wanalalamikia vituo havina vyoo, zamani kuna kituo gani cha daladala kilikuwa na choo? Unatokaje nyumbani kwenda kituoni na mkojo au haja kubwa kama si tabia mbaya tu? Watanzania wenyewe bado sana kwa kweli. Wanahitaji nguvu kubwa sana kuwabadilisha mawazo yao. Unye na kukojoa wewe ulalamikie wengine? Sio fair
 
Ustaarabu bongo bado nashauri Halmashauri ya Jiji kwa kushirikiana na mamlaka nyingine ziweke by Laws za kuwalazimisha watu wawe wanakaa katika Lines pindi wanapohitaji huduma fulani yenye kuhitaji wengine waliowahi kuipata kwanza. Kiufupi watu wamekuwa kama ming'ombe kukimbilia Seat vituoni, ustaarabu hakuna hata kidogo. Jana nimepanda magari ya DART, milango ya Kupandia na kushukia ni ile ile, basi kuna kusukumana mwanzo mwisho.
 
Wakati mwingine uwa nashindwa kuwaelewa watanzania wengine wanajisadia Garden daah!!
Asa hapo unatudhalilisha tumeshasikia suala la kujisaidia vituoni tunajirekebisha haya mengine yanatoka wapi!
 
Back
Top Bottom