Aibiwa fedha zote kwenye akaunti kwa NBC MasterCard kupitia ATM

Mzalendo JR

JF-Expert Member
Jun 6, 2012
1,193
515
Wizi wa elektoniki unaonesha kushika kasi jijini baada ya watu wawili kuibiwa fedha zao kwa kutumia MasterCard.

Mmoja wa waandishi waandamizi wa gazeti la HabariLEO, Bantulaki Bilango mwenye akaunti namba 017201056410 iliyofunguliwa katika tawi la NBC Moshi ameibiwa zote zilizokuwemo kwenye akaunti yake kupitia ATM ya tawi la Benki hiyo la Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kutoa taarifa NBC Makao Makuu yaliyopo Mtaa wa Sokoine Drive mapema leo, Bilango alisema baada ya kutoa fedha katika akaunti yake kupitia ATM iliyopo tawi la benki hiyo la Viwandani barabara ya Nyerere jana, leo alikupokwenda ATM zilizopo katika tawi la Corperate, alikuta fedha hizo zimechukuliwa muda mfupi kabla yake.

Taarifa ya benki aliyopewa ilionesha kuwa pesa hizo zilitolewa leo asubuhi katika ATM iliyopo Kinondoni.

Scan sehemu ya statement uonyeshe jinsi gani mwizi huyo alivyoiba.

"Jamani huu wizi ni wa aina yake. Mimi nimechuka Master Card yangu juzi tu leo hii kuna mtu amekomba pesa zangu zote kwenye ATM," alisema .

Hata hivyo alipoomba waangalie kamera zao kwa kuwa kila anayeingia kwenye mashine za ATM humulikwa walidai kuwa hiyo ni hatua ya juu sana inayohusisha polisi, hivyo hawawezi kufanya hivyo kwa wakati ule.

Hata hivyo, Bilango anasema alipata ushirikiano mzuri katika tawi la benki ya Viwandani katika barabara Nyerere alikochukulia fedha jana ambapo msimamizi wa Huduma kwa Wateja na Huduma za Biashara na Nje, Matilda Manumbu kwa kushirikiana na viongozi wengine wa benki hiyi waliahidi kufuatilia kwa karibu ili kuweza kumpata mhusika.

Kulingana na maelezo ya Bilango, kadi iliyokuwa ikitumika kuiba fedha ni ile ile ambayo alikuwa anayo mfukoni. Alisema la kushangaza, wakati yeye akiwa nayo, mtu mwingine alikuwa akiendelea kutoa fedha katika ATM.

Mmoja wa wateja alisema wizi huo unaoweza kufanyika kwa kuwatumia wafanyakazi wa benki lakini wakati mwingine kuna carbon inaachwa kwenye mashine ya ATM ambapo mteja akiweka kadi, taarifa zake zinanaswa kwenye carbon hiyo na baada mwizi kutumia taarifa hizo kuiba fedha hizo katika ATM nyingine.

Alishauri wateja kuacha kutumia njia hiyo na badala yake watumie dirisha kwa kuwa mashine hizo zinatumiwa vibaya.

Wizi huo unaonekana kukithiri hasa katika tawi la Kinondoni ambapo mteja mwingine ambaye hakupenda kutaja jina lake alichukulia fedha zake katika tawi hilo la Viwandani, kisha kuibiwa fedha zake kupitia tawi la Kinondoni wiki iliyopita kwa kutumia kadi yake ya ATM .

"Nami nimelizwa, lakini wamesema wanashughulikia, hivyo naamini fedha zangu zitarudishwa maana walichukua mshahara wangu wote.

Tukio hilo lilimpata tena mkazi mwingine, Fabian Rugaimukamu mwenye akaunti namba 2012401429 katika benki ya NMB tawi la Bank House.


Source: http://ziro99.blogspot.com/2012/10/mwandishi-akombwa-fedha-zote-atm-ya-nbc.html
 
Wizi wa elektoniki unaonesha kushika kasi jijini baada ya watu wawili kuibiwa fedha zao kwa kutumia MasterCard.

Mmoja wa waandishi waandamizi wa gazeti la HabariLEO, Bantulaki Bilango mwenye akaunti namba 017201056410 iliyofunguliwa katika tawi la NBC Moshi ameibiwa zote zilizokuwemo kwenye akaunti yake kupitia ATM ya tawi la Benki hiyo la Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kutoa taarifa NBC Makao Makuu yaliyopo Mtaa wa Sokoine Drive mapema leo, Bilango alisema baada ya kutoa fedha katika akaunti yake kupitia ATM iliyopo tawi la benki hiyo la Viwandani barabara ya Nyerere jana, leo alikupokwenda ATM zilizopo katika tawi la Corperate, alikuta fedha hizo zimechukuliwa muda mfupi kabla yake.

Taarifa ya benki aliyopewa ilionesha kuwa pesa hizo zilitolewa leo asubuhi katika ATM iliyopo Kinondoni.

Scan sehemu ya statement uonyeshe jinsi gani mwizi huyo alivyoiba.

“Jamani huu wizi ni wa aina yake. Mimi nimechuka Master Card yangu juzi tu leo hii kuna mtu amekomba pesa zangu zote kwenye ATM,” alisema .

Hata hivyo alipoomba waangalie kamera zao kwa kuwa kila anayeingia kwenye mashine za ATM humulikwa walidai kuwa hiyo ni hatua ya juu sana inayohusisha polisi, hivyo hawawezi kufanya hivyo kwa wakati ule.

Hata hivyo, Bilango anasema alipata ushirikiano mzuri katika tawi la benki ya Viwandani katika barabara Nyerere alikochukulia fedha jana ambapo msimamizi wa Huduma kwa Wateja na Huduma za Biashara na Nje, Matilda Manumbu kwa kushirikiana na viongozi wengine wa benki hiyi waliahidi kufuatilia kwa karibu ili kuweza kumpata mhusika.

Kulingana na maelezo ya Bilango, kadi iliyokuwa ikitumika kuiba fedha ni ile ile ambayo alikuwa anayo mfukoni. Alisema la kushangaza, wakati yeye akiwa nayo, mtu mwingine alikuwa akiendelea kutoa fedha katika ATM.

Mmoja wa wateja alisema wizi huo unaoweza kufanyika kwa kuwatumia wafanyakazi wa benki lakini wakati mwingine kuna carbon inaachwa kwenye mashine ya ATM ambapo mteja akiweka kadi, taarifa zake zinanaswa kwenye carbon hiyo na baada mwizi kutumia taarifa hizo kuiba fedha hizo katika ATM nyingine.

Alishauri wateja kuacha kutumia njia hiyo na badala yake watumie dirisha kwa kuwa mashine hizo zinatumiwa vibaya.

Wizi huo unaonekana kukithiri hasa katika tawi la Kinondoni ambapo mteja mwingine ambaye hakupenda kutaja jina lake alichukulia fedha zake katika tawi hilo la Viwandani, kisha kuibiwa fedha zake kupitia tawi la Kinondoni wiki iliyopita kwa kutumia kadi yake ya ATM .

“Nami nimelizwa, lakini wamesema wanashughulikia, hivyo naamini fedha zangu zitarudishwa maana walichukua mshahara wangu wote.

Tukio hilo lilimpata tena mkazi mwingine, Fabian Rugaimukamu mwenye akaunti namba 2012401429 katika benki ya NMB tawi la Bank House.


Source: ziro99blog: MWANDISHI AKOMBWA FEDHA ZOTE ATM YA NBC...

wizi huu sasa umeshamiri sana , mdogo wangukaibiwa hivo hivo CRDB ATM pesa nyingi sana, mwizi alikuwa anatoa kila siku ya mungu 1 M mpaka siku mdogo wangu alipokweenda kutoa pesa akakuta anaambiwa hawezi kutoa pesa kwani alishafikia limit ya siku kutoa pesa. Ndo kushituka iweje siku hioanataka pesa anaambiwa kashatoa, ndio haraka kukimbilia CRDB kuripoti na hapo wakamwambia asubiri siku 45 za uchunguzi....verry sad
 
wizi huu sasa umeshamiri sana , mdogo wangukaibiwa hivo hivo CRDB ATM pesa nyingi sana, mwizi alikuwa anatoa kila siku ya mungu 1 M mpaka siku mdogo wangu alipokweenda kutoa pesa akakuta anaambiwa hawezi kutoa pesa kwani alishafikia limit ya siku kutoa pesa. Ndo kushituka iweje siku hioanataka pesa anaambiwa kashatoa, ndio haraka kukimbilia CRDB kuripoti na hapo wakamwambia asubiri siku 45 za uchunguzi....verry sad
 
Hii ni hatari sana. Hizo ndio hasara za teknolojia za kisasa. Inabidi watu wa benki wawe makini sana katika jambo hili, ili kuzuia wizi wa fedha za wateja hauendelei. Wateja tutaogopa kutumia kadi hizi ambazo zinaonekana kuwa tanzi sasa.
 
NBC hawafai...shangazi yangu naye yamemkuta maswahibu hayo hayo. Sishangai yule boss kawekwa kando kupisha uchunguzi. Ethics za wafanyakazi wao pengine ziko very low na ndio hao wanaoiharibu sifa ya bank.
 
Mimi nimeanza utaratibu wa kucheki salio langu kwa siku mara nne, hii inaweza kusaidia kidogo
 
Maxmam ya kutoa pesa nadhani haizidi milioni tatu so ukute kaibuwa hela ya kufungulia acc

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
kamera itakusaidia sana ku truck mtu aliyetoa hizo hela! Mimi nadhani technolojia nzuri ingelikuwa ni ATM kudetect account holder kwa kutumia fingerprint kutolea hela, nadhani hiyo ingekuwa komesha kuliko Password number.
 
yaani haya ndo matatizo ya utandawazi, maana tunaletewa technology kabla ya kuandaliwa jinsi ya kuitumia, kutokana na hali hii ni bora kutochukua hizi master card maana jinsi unavyokuwa na uwezo wa ku access pesa yako zaidi ndo jinsi wizi unavyoongezeka maana unaweza kuibiwa pia kimtandao maana hadi ulaya wanaweza ku access pesa yako
 
kamera itakusaidia sana ku truck mtu aliyetoa hizo hela! Mimi nadhani technolojia nzuri ingelikuwa ni ATM kudetect account holder kwa kutumia fingerprint kutolea hela, nadhani hiyo ingekuwa komesha kuliko Password number.

kama mtu hajaibiwa kadi mara nyingi anayeiba anakuwa ni miongoni mwa watu anaowafahamu. Njia nyuri ni kuacha account open na once kadi hiyo ikiingia kwenye ATM wanadelay searching na immediately wanafanya utaratibu wa kumuhoji anayetoa pesa.
Iwapo mtu anayeiba anatumia kadi ambayo siyo ile aliyepewa mteja, basi hapo mteja hajaibiwa, iliyoibiwa ni bank. Mteja atatakiwa kulipwa na bank kiasi chake kilekile kilicho kwenye account. Eitherway, mteja anatakiwa kutokupoteza pesa kwa either kumtambua mwizi wake au kulipwa na bank.
Kutumia fingerprint ni nzuri, lakini on the other side inalimit mteja. Mtu anaweza kuwa mgonjwa akamtuma mwanae akamchukulie pesa. Wakati mwingine mtu anaweza kusafiri akaiachia familia kadi ili mshahara ukiingia wanacheza nao. Ila ikiwa fungerprint hilo haliwezekani.
 
tatizo la wizi wa mtandaoni, unaweza kuhisi na kung'ang'ana na ATM mashine kumbe wizi uko electronically zaidi na sio kwamba kuna mtu kaenda kusimama kwenye machine, watu wa benk upade wa IT wanajua la kufanya na ndo wanaweza kutoa majibu sahihi
 
kama mtu hajaibiwa kadi mara nyingi anayeiba anakuwa ni miongoni mwa watu anaowafahamu. Njia nyuri ni kuacha account open na once kadi hiyo ikiingia kwenye ATM wanadelay searching na immediately wanafanya utaratibu wa kumuhoji anayetoa pesa.
Iwapo mtu anayeiba anatumia kadi ambayo siyo ile aliyepewa mteja, basi hapo mteja hajaibiwa, iliyoibiwa ni bank. Mteja atatakiwa kulipwa na bank kiasi chake kilekile kilicho kwenye account. Eitherway, mteja anatakiwa kutokupoteza pesa kwa either kumtambua mwizi wake au kulipwa na bank.
Kutumia fingerprint ni nzuri, lakini on the other side inalimit mteja. Mtu anaweza kuwa mgonjwa akamtuma mwanae akamchukulie pesa. Wakati mwingine mtu anaweza kusafiri akaiachia familia kadi ili mshahara ukiingia wanacheza nao. Ila ikiwa fungerprint hilo haliwezekani.

Hapo kwenye red! hayo mahojiano na majibu yake si ni secret information ambazo ni sawasawa na kama ilivyo password? Source ya matatizo ya password, inaanzaga hapo kwenye kumuachia mtu mwingine kadi (familia,rafiki,mke/mume,ndugu) hapo haliwezi kuwa tatizo la benki iwapo password yako itahujumiwa.benki haitahusika.
Fingerprint ndio komesha kabisa, kama unapenda mtu mwingine awe na access na account yako unaposafiri au kuugua, ulipaswa ukamjazishe fomu flani na maelezo kwa permission na committment zako ndani ya benki.Na iwe uwezekano wa kuchukua hizo hela ndani (kwa teller) kwa kitambulisho na document maalum.Suala la ATM liwe lako binafsi.
 
Kwa wateja wa CRDB jengeni utaratibu wa kucheki salio kila siku kupitia simu zenu za mikononi kwa kutumia CRDB Mobile banking
 
Fingerprint ndio komesha kabisa, kama unapenda mtu mwingine awe na access na account yako unaposafiri au kuugua, ulipaswa ukamjazishe fomu flani na maelezo kwa permission na committment zako ndani ya benki.Na iwe uwezekano wa kuchukua hizo hela ndani (kwa teller) kwa kitambulisho na document maalum.Suala la ATM liwe lako binafsi.

ethics zingekuwa zinaniruhusu ningekwambia ni kwanini biological data hazitumiki
 
kamera itakusaidia sana ku truck mtu aliyetoa hizo hela! Mimi nadhani technolojia nzuri ingelikuwa ni ATM kudetect account holder kwa kutumia fingerprint kutolea hela, nadhani hiyo ingekuwa komesha kuliko Password number.

Mkuu hapo kwenye bluu inaonekana hawa benki kama wanasita kuangalia rekodi za kamera kama vile wanafahamu vizuri kinachoendelea hapo (i.e wanafahamiana vizuri katika huu wizi). Hiyo kwenye nyekundu hapo ndo kwenye suluhu ya yote vinginevyo sasa inatia hofu kweli kweli.
 
tatizo la wizi wa mtandaoni, unaweza kuhisi na kung'ang'ana na ATM mashine kumbe wizi uko electronically zaidi na sio kwamba kuna mtu kaenda kusimama kwenye machine, watu wa benk upade wa IT wanajua la kufanya na ndo wanaweza kutoa majibu sahihi

Haswa hili jamani huo wizi mostly wafanyakazi wa ndani wanahusika sana na kesi nyingi sasa hivi ni crdb.halafu me nashangaa tangu wale Wabulgaria wakamatwe na kina nani sijui nilitegemea benk waelekeze wateja kucheki pale kwenye ile catrage wezi wanapodakia data lakini coz they know inside outside game hawawezi fanya hivyo
 
kamera itakusaidia sana ku truck mtu aliyetoa hizo hela! Mimi nadhani technolojia nzuri ingelikuwa ni ATM kudetect account holder kwa kutumia fingerprint kutolea hela, nadhani hiyo ingekuwa komesha kuliko Password number.

Tena biometric ndo mbaya zaidi coz once utakaposign in coclusively itaonyesha we mwenye account ndo umechukua.CRDB me nilitoa pesa zote Na NMB sa hivi ukichukua pesa on the sport unapokea msg kwenye simu kama sio wewe umechukua pesa uwajulishe.sa kama no ya simu ulibadilisha rhat is up to you
 
Tena biometric ndo mbaya zaidi coz once utakaposign in coclusively itaonyesha we mwenye account ndo umechukua.CRDB me nilitoa pesa zote Na NMB sa hivi ukichukua pesa on the sport unapokea msg kwenye simu kama sio wewe umechukua pesa uwajulishe.sa kama no ya simu ulibadilisha rhat is up to you

hapo kwenye red inasaidia sana kwa haraka kujua kama kuna tatizo
! wasiwasi wangu pia ni kama bank itaweza kushughulikia hizo taarifa kwa haraka mara upatapo hiyo sms, iwapo utataka kuwajibu aliyetoa hela kwenye a/c yako sio wewe (ni mwizi).kama hawatakuwa faster kushughulikia itakuwa haina tofauti na mwanzoni.
 
Back
Top Bottom