FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,506
- 123,777
Katika hali ya kushangaza sana kisiasa Tanzania, nyimbo imegeuka ghafla.
Wiki mbili nyuma ilikuwa tukiwasikia UKAWA hapa na pale, sasa hivi kila mmoja, awe ni mwana CCM au mpinzani wa chama chochote kile, nyimbo ni CCM, CCM, CCM, CCM. Hakuna cha CHADEMA, CUF, NCCR wala ACT.
Kinachoongelewa kuanzia na washabiki wa mitaani, wana siasa waliobobea, magazeti, wachambuzi wa kisiasa, vijiweni, kwenye ma redio, ma TV, licha ya mtandaoni, bila kuisahau JF ni CCM. Ama kwa hakika, wataiongelea CCM wakitaka wasitake, umewaweza sana na hawana ujanja hata chembe. Halafu wewe kimya, baada ya kuwawachia kizungumkuti, umeingia kwenye basi lako jipya kabisa, huyooooo unakwenda kumwaga sera mikoani.
Kiingereza tunasema hii ni "Political Strategy" ya karne.
Kila nnapopita JF, gumzo ni wagombea nafasi ya kuwania Urais wa CCM, nani wa kubisha hilo? Kila mtu anaamini, awe wa chama chochote kile, kuwa Rais wa Tanzania bado ataendelea kutokea CCM uchaguzi huu na sasa nnaamini hata zijazo, na ulivyowaparaganisha hata ubunge na udiwani wameusahau.
Hii imenikumbusha ile nyimbo ya zamani "nimuokowe nani?".
Kinana ni Kichwa.
Wiki mbili nyuma ilikuwa tukiwasikia UKAWA hapa na pale, sasa hivi kila mmoja, awe ni mwana CCM au mpinzani wa chama chochote kile, nyimbo ni CCM, CCM, CCM, CCM. Hakuna cha CHADEMA, CUF, NCCR wala ACT.
Kinachoongelewa kuanzia na washabiki wa mitaani, wana siasa waliobobea, magazeti, wachambuzi wa kisiasa, vijiweni, kwenye ma redio, ma TV, licha ya mtandaoni, bila kuisahau JF ni CCM. Ama kwa hakika, wataiongelea CCM wakitaka wasitake, umewaweza sana na hawana ujanja hata chembe. Halafu wewe kimya, baada ya kuwawachia kizungumkuti, umeingia kwenye basi lako jipya kabisa, huyooooo unakwenda kumwaga sera mikoani.
Kiingereza tunasema hii ni "Political Strategy" ya karne.
Kila nnapopita JF, gumzo ni wagombea nafasi ya kuwania Urais wa CCM, nani wa kubisha hilo? Kila mtu anaamini, awe wa chama chochote kile, kuwa Rais wa Tanzania bado ataendelea kutokea CCM uchaguzi huu na sasa nnaamini hata zijazo, na ulivyowaparaganisha hata ubunge na udiwani wameusahau.
Hii imenikumbusha ile nyimbo ya zamani "nimuokowe nani?".
Kinana ni Kichwa.