Watu8
Platinum Member
- Feb 19, 2010
- 76,283
- 108,297
Kwa heshima napenda kumpa ahsante Mbunge wa Chadema Mheshimiwa Halima Mdee kwa haya:
Mheshimiwa Spika, napenda pia kutoa shukrani za dhati kwa CHADEMA kikiwa chini ya Mtendaji wake mkuu (KATIBU MKUU-TAIFA), Mhe. Wilbroad Peter Slaa. Hakika kila Mtanzania anaona kazi unayoifanya ya kuhakikisha chama chetu kina kuwa juu na Watanzania wote wanatuunga mkono. Mungu akupe uhai, naamini ipo siku tutaifikia Nchi ya Ahadi! - Halima Mdee Bungeni 11-07-2012 .
Soma zaidi: "tutaifikia Nchi ya Ahadi".
Mheshimiwa Zomba, elimu yako ya sekondari umesoma Tanzania?
Kama jibu ni ndio, basi katika somo la kiswahili kwa elimu ya sekondari kuna kitu kinaitwa "Tamathali za Semi" mfano Dhihaka, tafsida ,kejeli/shitizai, Sitiari, Tashibiha, Tashihisi, Mubaalagha, Tabaini, Takriri.
Tafadhali rejelea hayo mafundisho, hakika utamuelewa Bi. Mdee