Binafsi ili kombe la afrika nililifuata Kenya 1996,wakanyang'anywa 7bu uwanja wa manispaa jijini Mombasa haukukamilika,wakapewa South Africa na nilibahatika kwenda huku NIgeria ikijiondoa dk za mwisho mambo ya siasa ya Sani Abacha ilipingwa na Umoja wa Mataifa so kundi C wakati ule likabaki timu 3 Gabon,Zaire(DRC) na Liberia,nilishudia mechi zote za Gabon jijini Durban uwanja wa Kings Park(sio wa sasa Moses Mabhida uliojengwa wakati wa world cup ukingoni mwa bahari,ila vipo karibu kama mita 200 hivi)Gabon alimchapa Zaire 2-0 akafungwa na Liberia 2-1 wakapita Gabon na Zaire ktk kundi C,na hata nikirindima mechi za Spain sio naona ktk luninga la,baadhi nimeshashuhudia kwa macho yangu,mimi ni kama Manolo el Del Bombo,hata mechi za TZ niliziangalia sana zamani ila toka nihamie Mkuranga(karibia na Linyola siri yako) ninakuwa mbali na soka la bongo na afrika kwa ujumla ni hayo!mkuu Mphamvu utaonekana wa ajabu mbele za wengi lakini wengi hao hao ndio walio kwenye huo mkumbo so you better stand out of from the Crowd so long as you are correct.
Niliwahi kukutana na mtu wa Scotland na tukawa tunaongelea mambo ya mpira na ndio tukaingilia issues za upenzi wa timu. Mimi nilidhania moja kwa moja kuwa angelikuwa ni shabiki either wa rangers, celtic au basi dundee lakini kwa mshituko ndo akasema anaweza kuhesabu hata mara ngapi alienda kushuhudiia mechi zao maana timu yake ni ndogo sana ambayo ni ya eneo (locality) anapotokea/anapoishi. Sawa ni ushabiki/upenzi lakini hii ilinipa picha kubwa ya ni jinsi gani tulivyo wajinga maana unakuta mtaani kuna tawi la simba/yanga na hata Manchester lakini hawana hata timu ya kuwakilisha wilaya!!! Wabongo kila kitu kujiendea tu kama nyumbu wa serengeti wakivuka mto mara