Afande Awadhi unachofanya sio sahihi

Afande Awadhi unachofanya sio sahihi

Kwa nini Rajabu Mchechu hujibu maswali yetu, nimeangalia hakuna sehemu hata moja ambayo umejibu nini maana yake?
 
1. Kama ungekuwa mwanaharakati wa haki za binadamu, ungeshuka na kwenda kumuuliza sababu ya kumpiga makofi pasipo hukumu ya mahakama.
2. Jengeni tabia ya kutumia simu zenu kurekodi matukio muhimu kama hayo na kisha kuja kuyaleta sehemu kama hizi ili muweze kupata msahada wa kisheria.
3. Next time chagua kufanya moja kati ya hayo mawili au yote kwa pamoja.
Ni wazo zuri sana kutumia simu kurecord matukio ya kihalifu yanayofanywa na wanausalama.Kuna tukio la rushwa kwa askari usalama barabarani,nalo lilirekodiwa na kupostiwa kwenye mitandao,na yule askari aliadhibiwa.Pia askari wengine wa usalama barabarani waliokuwa wakifanya mapenzi wakiwa na nguo za kazi
 
Uoga ulioje. Ungeshuka na kumfata kuonyesha kitendo alichofanya sio cha kiungwana. Au wewe ni mwanaume wa Kisukuma?
 
Sio haki mkuu ungesaidia mazingira hayo lazima aliendelea na kumnyanyasa zaid
 
dar ni shida mwanamke ananyanyaswa wanaume wanaangalia tuu iyo Arusha au mbeya wasingekubaliana na huo aliofanya tungepata mrejesho mzuri tuu...
 
Dah... isije kuwa watu wanaumiza vichwa kwa fadhaa na huruma kumbe mleta uzi alilambwa elfu 30 kwa kosa la kutanua sasa akaamua kuja kumalizia hasira zake humu. Ni wazo tu[emoji12]
 
Wanaume wa Dar mnatuangusha...Inakuaje binti anakosa msaada tena barabarani?????
 
Picha kwa ushahidi usije kuwa haumpendi tu binafsi, ushahidi ili tufanyie kazi mkuu
 
Majungu tu hayo, halafu huyo mwanamke angesababisha ajali? au watu wasingekufa au kujeruhiwa kwa sababu aliyesababisha ni mwanamke? Kwa bahati mbaya siku hizi kuna baadhi ya member wamegeuza jf kijiwe cha majungu, fitna na kuchafuana.
 
Awadh ni mfalme wa barabara ya Ally Hassan Mwinyi



Road toll officer
 
SP aongoze magari? Au siwajui maSP(warakibu)
 
Hivi kwa ujumla bila kujali kama dereva ni wa jinsia ya kike au kiume ni sahihi kwa askari wa usalama barabarani kumpiga makofi dereva, kumtolea upepo kwenye tairi na pia kumnyang'anya funguo?
Unauliza makofi polisi? Police force-hiyo force unajua maana yake?
 
huyu awadhi daladala zote zinamjua kuna konda na dereva sikumoja walikuwa wanamjadili wakasema walienda kumroga bagamoyo wakakuta huyo mganga ndo pia ni mganga wa awadhi walienda kumuua ila akawaambia wasimuuwe atamwita amuonye mbele yao ... kwahiyo wakawa wanajisifia kuwa awadhi hawafanyi lolote
Unaleta story za kusogeza foleni
 
Hivi kwa ujumla bila kujali kama dereva ni wa jinsia ya kike au kiume ni sahihi kwa askari wa usalama barabarani kumpiga makofi dereva, kumtolea upepo kwenye tairi na pia kumnyang'anya funguo?
Ni sahihi kwa baadhi ya wakati, na hasa kwa nyinyi madereva vijana wenye vigari vya automatic na munaojifanya eti muna haraka sana wakati wa asubuhi.
Utaona mtu anatanua kwenye barabara nyembamba yenye kona kali kama pale Mbagala Mission. Akikumbana na gari zinazokuja kutoka upande wa pili hulazimisha kupenya kwenye foleni. Nilishaona hiyo mjamaa akaparaza gari ya afande akaishia kuchapwa vibao.
 
Huu uzi si kweli! Haiwezekani mdada kupigwa na askari. Askari wengi huwa wanawafavor wanawake kwa sababu nyingi ikiwa pamoja na wengi wao huwa makini katika uendeshaji mi naona ni majungu tu.
 
Back
Top Bottom