ADVICE: Ninunue gari aina gani?

miss username

Member
Joined
Mar 30, 2013
Posts
78
Reaction score
32
Nina
kiasi cha shilingi 7mil na ninataka kununua usafiri wangu binafsi.
Naombeni wenye uzoefu na magari mnishauri ni aina gani ya gari naweza
kuipata kutoka show room kwa kiasi hicho cha fedha.

Binafsi nilikuwa napendelea toyota mark II ila sasa sijui bei yake
ikoje.

Then naomba kujua gharama za utunzaji gari zikoje kwa mfano inatakiwa
ifanyiwe service mara ngapi kwa mwezi.

Mshara wangu ni lak 3 kwa mwezi sina familia je nitaweza kuzimudu gharama za utunzaji gari?
 
show room hautopata gari kwa bei hiyo, option ni kununua kwa mtu.

nakushauri ununue Toyota corolla AE110 au AE111. au Toyota Starlet model yoyote except Glanza

spear parts ni nafuu, body ni ngumu na fuel economic cz beinya mafuta inatia kichaa

achana na vigari vya kibishoo kama Duet, IST, Nissan March, hizi ni gari laini na sio imara

Mark 2, chaser na cresta ni majini mahaba, utafilisi mfuko wako kununua mafuta
 

Utaweza
 

Asante sana kwa ushauri
 
Nunua Starlet!!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Nunua funcargo ni nzuri sana, ukiwa pale TAZARA station kamata njia ya kwenda k/koo kwa kupitia barabara ya chini ya hyo tazara station...ukifika kw mbele kdogo kuna njia panda ya nyerere road inayoelekea mnazi mmoja....ukitazama kwa mbele tu utaona kuna open space kamezungushiwa ukuwa mfupi wa tofali....utapata gari ya 6.5, 7, 7.5, 8m nk
 
Full maushauri eeh, nunua Duet inatembea hadi Km 14 kwa lita, ndio ninayoitumia ni nzuri sana. Sijasema engine ni mabaya.
 

Mkuu,GLANZA zina nini kwani?, huwa nazipenda zilivyo sana,sasa hapa umenifungua,naomba unipe hasara zaka kaka ili nisije kuingia mkenge
 
Agiza kutoka japan kwahyo amount,toyota passo,sprinter,au mazda demio inatosha sana
 
Tafuta Toyota Carina cc1500 itakusaidia sana!ngumu inadumu na spare zake ziko bei poa!ukishindwa kabisa basi nenda starlet ziko sawa nunua milango 4!
 
Duu kweli vijana kazi tunayo vijana una mshahara wa laki 3 unataka kununua gari? Jijenge kwanza dogo kununua gari la matumizi binafsi ni kujipunguzia speed ya kukua kiuchumi.Zungusha hizo mil 7 zako ili kuja kununua gari ukiwa una raha zako zote na uwezo wa kununua fuel
 

Acha kumkatisha tamaa mwenzio na waswahili wanasema maisha ni mipango. Kuna iliepanga kuanza na gari then nyumba, pia mwingine ndoa then gari, mwingine nyumba kwanza mengine yanafuata.
Pia kumbuka inategemea na kaza pia mizunguko ya mtu anaweza akaona matumizi ya tax, bodaboda au daladala na gharama pia anapoteza muda mwingi kuliko anapokua na usafiri binafsi.
 

Mi nadhani ungefungua buzness ya 5M, baada ya mwaka tunakusahau! ni dalili ya umaskini kuwaza kuongeza matumizi badala ya kuongeza kipato
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…