Adili na Nduguze:- Shaaban Robert

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,870
155,829
MTUNZI: SHAABAN ROBERT.
WACHAPISHAJI : Tanzania Publishing House. Dar es Salaam.

SURA YA 1

Mfalme Rai

Rai, mfalme wa Ughaibu , alikuwa mfalme namna ya peke yake duniani. Alikuwa na tabia iliyohitilafiana kabisa na tabia za watu wengine wa zamani zake. Tabia yake ilijigawa katika theluthi tatu mbalimbali kama rangi ya ngozi ya punda milia. Kwa theluthi ya kwanza alikuwa msuluhifu akapendwa na watu, Kwa theluthi ya pili alifanana na Daud akaheshimiwa kama mtunzaji mkuu wa wanyama, na kwa theluthi ya tatu alikuwa kama Suleiman akatiiwa na majini. Kutawala suluhu na mapenzi ya wanadam, utunzaji wa wanyama, na utii juu ya viumbe wasioonekana kama majini hutaka uwezo mkubwa sana. Kwa hivi, fikiri wewe mwenyewe jinsi Rai alivyojipambanua mwenyewe na wafalme wengine.

Katika miliki ya mfalme huyu kodi ilitozwa juu ya mifugo ya wanyama. Kodi hii ilihalalishwa kwa sababu Ughaibu ilikuwa nchi ya mifugo. Ughaibu ilipokuwa juu ya kilele cha usitawi mifugo yake ilikuwa hailingani kwa ubora na mifugo ya nchi yoyote nyingine ulimwenguni. Fahari yake ya mifugo ilikuwa kubwa kabisa. Fahari hiyo haikuwezekana kukadaika ikatazamwa kwa wivu katika dunia nzima.

Malipo ya kodi hii yalifanywa kwa wanyama waliozaliwa pacha. Kila zizi lilitozwa pacha moja kila mwaka. Mazizi yaliyokuwa hayana wanyama waliozaliwa pacha katika mwaka uliodaiwa kodi yalisamehewa. Zizi lililoshindwa kulipa kodi lilitokea kwa nadra sana kwa sababu mifugo yote ilikuwa mizazi ya ajabu. Zilipatikana pacha katika mbuzi, kondoo, ng'ombe, farasi, na wanyama wengine.

Masurufu ya serikali ya Ughaibu yalitegemea katika juu ya wanyama wake. Kwa sababu hiyo kila zizi katika nchi lilihesabiwa kama hazina maalum, na kila mnyama katika zizi hilo alikuwa kama johari hasa. Mazizi yaliyopotelewa na mifugo yake kwa maradhi yalijazwa tena wanyama wapya. Masikini waliotaka mifugo, lakini waliokuwa hawana njia ya kuipata, walikidhiwa haja zao na serikali bila malipo yoyote. Basi mifugo ilienea katika nchi yote ya Ughaibu.

Kwa masurufu haya na misaada kama hii uangalifu wa mfalme juu ya wanyama wa mifugo ulikuwa hauna kiasi wala kadiri, na huruma yake juu ya wanyama wasiokuwa wa mifugo ilishawishika sana.

Rai alikuwa kiongozi muadilifu na mfalme mwema sana. Hakusita kufanya kazi ndogo wala kubwa kwa mikono yake mwenyewe. Kazi nyingi za ufalme alizitenda yeye mwenyewe. Zile ambazo hakuwahi kuzitenda yeye mwenyewe alipenda kuziona kwa macho yake zilivyofanywa. Kwa bidii zake kubwa aliweza kushiriki katika mambo mengi ya maisha akasaidia maendeleo makubwa ya nchi yake.

Hakulazimisha mtu yeyote kutenda tendo fulani, lakini alishawishi kila moyo wa mtu kuiga alivyotenda kwa hiyari yake mwenyewe. Alikuwa na mvuto mkubwa juu ya mioyo ya watu. Alitumia mvuto huu juu ya watu mpaka nchi yake ilikuwa haina mvivu, goigoi wala mwoga.

Kuondoa uvivu , ugoigoi na woga katika nchi ni kazi ngumu. Mambo haya yanapendwa sana na watu ingawa yana madhara makubwa kwao. Kwa hivi, kufaulu kwa Rai kulistahili sifa kubwa sana. Sifa yake ilifurahiwa na viumbe wote. Malaika mbinguni waliitungia mashairi; ndege hewani waliimba kwa sauti zao nzuri; wanadamu duniani waliisimulia kwa hadithi; majini na mashetani waliikariri kwa tenzi. Rai alikuwa mtu mmoja katika watu bora waliopata kutoka tumboni mwa mwanamke. Alifanya urafiki na viumbe mbalimbali kwa sababu aliwajali wote.

Ilikuwa si desturi ya Rai kusema maneno na kuacha watu wengine watende matendo, lakini alitenda matendo akaacha watu wengine waseme maneno. Tendo hukidhi haja maridhawa kuliko neno. Haja ikishughulikiwa kwa matendo hupatikana upesi, lakini ikishughulikiwa kwa maneno huchelewa kama sadaka. Rai alifaham haya lakini watu wake hawakufaham. Hawa walipaswa kuamshwa katika usingizi wao kwa matendo, sio kwa maneno. Maisha ya Rai yalipita katika matendo mbalimbali.

Katika hukumu alikuwa imara sana. Hakupendelea mkubwa wala hakudhulumu mdogo. Watu wote walikuwa sawasawa mbele ya sheria. Hakuuza haki za watu kwa rushwa. Wanadamu na wanyama walioata haki zao katika baraza lake. Hili ndilo tendo moja katika matendo yake ambalo limetia jina lake katika makumbusho yasiyosahaulika katika wakati wake, sasa na baadae katika wakati ujao duniani. Kila mtu alipoiga matendo ya mfalme yabisi katika nchi alifukuzwa.

Rutuba ilienea kila mahali. Kwa rutuba hii ardhi ya Ughaibu ilikuwa na rangi ya kahawia. Juu ya ardhi hii paliota mimea iliyofanana za zabarijudiwa uzuri. Mimea hii ilie eza neema ya vyakula kwa watu na malisho ya wanyama. Hewa ya nchi nzima ilinukia manukato kwa naua mazuri ya mimea mbalimbali.

Siku moja Rai alipokuwa akitazama hesabu za wanyama waliokusanywa kwa kodi, aliona karibu mazizi yote katika miliki yake yamekwisha lipa kodi zake ila mazizi ya Janibu. Ugunduzi huu uliamsha wasiwasi mkubwa uliokuwa ukingojea mguso mdogo tu katika moyo wake. Moyo wake ulipokuwa ukiliwa kwa wasiwasi, mawazo mbali mbali yalipita katika akili yake. Alidhani kuwa labda Janibu imepatwa na mwaka wa kiu, na kuwa malisho ya wanyama yameharibika.

Labda sotoka imeshambulia mazizi katika nchi, na kuwa vifo vingi vimetokea katika mifugo. Kwa kuwa wanadamu na wanyama wana shirika moja katika maisha, Rai alihamasika sana. Aliona dhahiri kuwa madhara ya wanyama ni hatari kwa watu vile vile. Rai alikuwa na akili tambuzi iliyopenya katika mashaka mengi ya maisha. Walakini, hizi zilikuwa dhana tu. Dhana zenyewe zilikuwa haziwezi kusaidia kujibu ugunduzi wake. Palikuwa hapana kitu kilichoweza kuzithibitisha.

Ughaibu na Janibu ilikuwa miji miwili mbalimbali chini ya miliki moja. Miji hii ilitengwa na umbali mkubwa. Ugunduzi wa Rai katika hesabu ya kodi ulifasiri upungufu ambao haukutazamiwa. Sababu ya upungufu ule haikujulikana kwa sababu habari za Janibu zilikosekana. Pasipo shaka, hukubalika bila ya swali kuwa miji miwili ina ina ndoto mbili zenye maana mbalimbali.

Rai aliweza kujua tafsiri ya ndoto ya Ughaibu kuwa jumla ya kodi ilikuwa na kasoro, lakini hakuweza kujua maana ya ndoto ya Janibu, yaani sababu ya kasoro ile. Mambo katika maisha yamo katika mwendo huu siku zote. hmHayajulikani mpaka yamechunguzwa na kuthibitishwa kwanza. Rai alikuwa mtu arifu wa mwendo huu. kwa hivi, shauri hili liliachwa kwa Maarifa, Waziri Mkuu, kuchunguzwa.
 
SURA YA 2

Siri inafichuka

Ikibali alitakiwa na Maarifa kwenda Janibu kuchunguza kodi. Ikibali alikuwa mshauri katika halmashauri ya Ughaibu na mshairi wa mfalme. Alichaguliwa kwa kazi hii kwa sababu alikuwa na maarifa ya kuchukuana na watu. Kwa maarifa haya aliweza kupata mradi wake siku zote bila ya kuamsha uadui wa watu juu yake. Ughaibu ilikuwa teuzi katika wasimamizi wake na katika madaraka yao. Uteuzi wake ulikuwa na maana kwa sababu ukamilifu wa mtu duniani ni tabia njema. Mbali ya sifa nyingine, kila mtu bora alitakiwa kuonyesha ubora wake kwa kuchukuana na watu. Ikibali alikuwa mkamilifu wa tabia akaaminiwa na Rai, Maarifa, halmashauri na watu wadogo.

Siku ya pili, saa moja asubuhi, Ikibali alikwenda janibu. Mwendo wa saa sita kwa farasi ulikuwa kati ya Ughaibu na Janibu. Adhuhuri ilipokaribia Ikibali alikuwa amefika katika viunga vya mji aliokusudia. Huko alitua akapeleka taarifa kwa Adili, Liwali wa janibu kuwa amewasili. Adili alipopata habari alikwenda akamlaki mgeni wake nje ya mji kwa furaha. Baada ya kumlaki aliingia naye mjini. Saa saba mchana Ikibali alifika nyumbani kwa mwenyeji wake akapokewa kwa taadhima. Alikula chakula cha mchana na mudir wa Janibu, na saa nane akazuru idara zao. Hulka ya ikibali ilipendeza watu waliopata kukutana naye. Kicheko kilikuwa midomoni mwake na shukrani katika pumzo zake. Hulka njema sawa na mali. Fundisho hili linakwenda duniani mpaka sasa.

Jioni Ikibali na Adili walipokuwa peke yao mazungumzo juu ya kodi yalianza. Hapakuonekana upungufu wowote. Hesabu haikuwa kamili tu, lakini ilionyesha ziada vile vile. Ikibali alihakikishwa kuonyeshwa ziada hii asubuhi. Sababu ya kuchelewa ilihusiana na makusanyo ya ziada. Kama Adili hakutanguliwa na Ikibali siku moja, Adili alikusudia kupeleka hesabu yake Ughaibu siku ya pili. Ikibali alifikiri habari hizi njema zilitosha kutuliza wasiwasi wa mfalme. Kwa hivi, aliazimu kurudi Ughaibu kesho yake. Adili alitaka kutajamali na Ikibali. Hamu yake ilikuwa kubwa sana. Kama haja hii haikumkalifu Ikibali, Adili aliomba sana jamala ya kutafaraji naye kwa muda wa siku tatu. Kwa kuwa waungwana hawanyimani neno lisilokalifu Ikibali alikubali kuahirisha marejeo yake.

Sasa Adili na mgeni wake waliingia sebuleni. Sebule hiyo ilikuwa imesakifiwa na marmar za rangi tatu, yaani, nyeupe, nyekundu na samawati. Dari yake iliikizwa vizuri sana. Ilisaki sawasawa juu ya kuta nne zilizopakwa sherezi ya manjano. Katikati ya dari hii ilining'inia chini karabai moja iliyozungukwa na matovu ya almasi. Kuta mbili katika hizi nne zilikuwa na madirisha mazuri. Katikati ya sakafu palitandikwa mazulia ya thamani kubwa. Juu ya mazulia hayo palikuwa na meza moja ya mkangazi na viti viwili vya henzirani. Vyakula na vinywaji mbalimbali viliandaliwa juu ya meza. Walikaa kitako hapo kwa kuelekeana wakala chakula cha usiku. Baada ya kula na kunywa walizungumza mpaka wakati wa kulala.

Malazi ya Ikibali yalifanywa katika chumba kilichokuwa na sakafu ya marmar nyeupe tupu. Dari ilipakwa sherezi ya samawati na kuta zilikuwa na sherezi ya zari. Kila ukuta ulikuwa na dirisha la kioo kilichosimama juu ya mihimili ya johari. Vitanda viwili vya pembe vilivyokuwa na viwambo vya ngozi na matandiko ya pamba vilitandikwa humo.. Mihimili ya vyandarua ilikuwa ya dhahabu. Siku ile Adili alilala katika chumba kimoja na mgeni wake. Baada ya kupanda vitandani wote wawili walinyamaza kimya. Kila mtu alidhani mwenzake amelala, lakini wote wawili walikuwa macho. Ikibali alikuwa akisanifu mashairi, kama ilivyokwisha semwa kuwa alikuwa mshairi mashuhuri. Alipoendelea hivyo mpaka usiku wa manane alimwona Adili ameondoka ghafula kitandani. Chumbani lilikuwamo bweta. Adili aliokwisha vaa nguo zake aliliendwa bweta akalifungua. Alitoa mjeledi na mshumaa. Mshumaa ulipowashwa nuru kubwa sana ilitokea. Sasa Adili alifungua mlango wa chumbani akatoka nje. Hakujua kama Ikibali alikuwa macho.

Ikibali alishangaa usanifu wake ukachafula. Hakujua Adili alikusudia kwenda wapi na mjeledi usiku ule. Alijua kwamba ilikuwa si murua kunyemelea mambo ya watu, lakini alijua pia kwamba ilikuwa wajibu kujiweka tayari kusaidia katika haki. Kwa sababu ya msaada aliona haifai kulala kama mvivu nafasi ya kutenda wajibu wake ilipotokea. Wazo hili lilimwondoa kitandani akatoka nje.. Alimfuata Adili nyuma polepole. Karibu ya nyumba moja ndogo Ikibali alisimama kando. Adili alifululiza mpaka mlangoni. Aliufungua akaingia ndani. Alipotoka nje alikuwa na sinia moja. Siniani mlikuwa na sahani za chakula na birika la maji. Alijibandika begani sinia akaenda zake. Ikibali alimfuata nyuma vile vile.

Adili alipofika nyimba nyingine, kubwa kuliko ya kwanza, alifungua mlango akaingia ndani. Nyuma yake mlango ulifungwa kwa nguvu. Ikibali alinyata mpaka mlangoni akasimama kimya. Alichungulia ndani katika ufa wa mlango akaona ukumbi. Katikati ya ukumbi palikuwa na kitanda kizuri na meza moja. Manyani mawili yaliyofungwa viunoni minyororo ya dhahabu yalikuwa yamelala kitandani. Adili aliweka sinia juu ya meza. Nyani moja lilipofunguliwa lilirukaruka likalialia kinyonge. Adili alilikamata akalifunga miguu ya mbele na ya nyuma kwa kamba. Alipolitupa chini alishika mjeledi kwa mkono wa kulia akalipiga mpaka likazirai. Nyani jingine lilipigwa likazirai vile vile. Manyani yalipizinduka yalinasihiwa. Adili aliapa kuwa hakufurahi kuyaadhibu, na kwamba alitazamia faraja yao kutokea karibu.

Sasa manyani yalichukuliwa mezani kula chakula kwa vijiko na nyuma. Yaliposhiba yalinyweshwa maji. Midomo yao ilifutwa kwa leso za hariri. Kisha yalifungwa minyororo kama yalivyokuwa. Mambo haya yalipotendeka Ikibali alikuwa amesimama kimya anachungulia. Adili Alipokusanya vyombo ili atoke nje, Ikibali alitangulia kuondoka mlangoni. Alikwenda mpaka kitandani pake akajilaza kimya kama aliyekuwa hajui lililotokea. Kitambo kidogo Adili alirudi akaweka mjeledi na mshumaa bwetani. Hakushuku neno, na baada ya kuvua nguo zake alilala tena. Lakini tangu wakati ule mpaka asubuhi, Ikibali hakupata usingizi kwa mawazo mbalimbali. Kila njia ya fikra aliyokwenda haikumfikisha katika tafsiri ya mwujiza ule. Adili Alikuwa mtu wa maana. Hakutazamiwa kufanya ukatili kwa wanyama.

Mwenyeji na mgeni waliondoka vitandani. Baada ya kuoga na kuvaa walikwenda sebuleni kustaftahi. Walipokwisha walikwenda mazizini kutazama wanyama waliokusanywa. Siku ile moyo wa Ikibali ulikuwa mzito kwa mawazo, lakini hakuuliza neno juu ya siri aliyogundua. Ilikaa moyoni mwake mwenyewe. Siku ya pili , usiku wa manane vile vile, Adili alifanya tena mambo aliyofanya jana. Siku ya tatu mambo yalikuwa yaleyale. Katika muda huu wote Ikibali hakuacha siku hata moja kumfuata na kutazama matendo yake. Siku ya nne alipewa hesabu aliyojia akarudi ughaibu. Kwa kesha ya siku tatu hakuweza kuongoza vema farasi kwa usingizi. Laiti asingalikuwa mzoefu wa kupanda farasi angalitupwa chini njiani amelala.

Alipofika Ughaibu alitoa habari za ujumbe wake. Alitaka sana kuficha siri ya manyani ya Adili na adhabu yao, lakini hakuweza. Alifikiri kama Adili aliyaadhibu kwa ukatili tu asingalijisumbua kuyafuga, kuyalisha na kuyanasihi. Mtu hawezi kutunza kitu asichokijali. Zaidi ya umahiri, werevu na usuluhifu, Ikibali aliweza kufahami upandw wa pili wa neno. Aliona dhahiri kuwa Adili hakupenda adhabu ile kuendelea. Kama aliitenda kwa kulazimishwa alikuwa na haki ya kusaidiwa. Yamkini mfalme aliweza kumsaidia. Kwa sababu hii alitoa siri aliyokuwa nayo. Rai aliposikia nywele zake zilisimama kichwani, na damu yake ikasisimka mwilini. Ikibali alitumwa tena Janibu kumleta Adili pamoja na manyani yake mbele ya mfalme.
 
SURA YA 3.

Adili Mbele ya Rai

Uso wa Ikibali ulikuwa na haya na moyo wake ulijaa hisani. Alikuwa tayari kutumika kama alivyotakiwa na mfalme, lakini alichelea kuwa haini kama siri aliyotoa ilikuwa maangamizi ya Adili. Alijuta ulimi wake haukuwa na nadhari. Hapana roho mbinguni wala duniani isiyopatwa na majuto. Tuna busara nyingi sana baada kuliko kabla ya neno kufanyika. Kama taratibu ya msaada haikufaulu, Ikibali hakupenda kumkabili Adili. Wakati ule ule hakuweza kughairi dhima yake. Ugomvi baina ya hiari na dhima ulianza moyoni mwake. Mambo haya mawili hayatimiziki mara moja. Hapana mtu awezaye kwenda njia mbili wakati mmoja. Kwa hivi, Ikibali alitii mahitaji ya dhima yake akaenda janibu.

Adili alipoona Ikibali amerudi alishtuka. Alisema moyoni mwake ataokolewa katika uovu aliolazimishwa lakini hakuupenda kuutenda. Baada ya hayo alimuuliza Ikibali neno lililomrudisha ghafla Janibu. Ikibali alijibu asingalirudi ghafla vile, lakini katika jitihada yake ya kutenda wema ametenda nuksani. Alikuwa hana udhuru wa kujitetea katika lawama lake. Ulimi wake mwenyewe umemponza. Aliungama alipofika Janibu mara ya kwanza alishawishika kumpeleleza Adili siku tatu. Kila usiku alipokwenda kuadhibu manyani, yeye alimfuata nyuma. Aliporudi nyumbani kulala, yeye alitangulia mbele. Mambo aliyotenda kwa manyani yalikuwa ajabu kwake. Hakupata kuuliza sababu yake. Aliporejea Ughaibu alizungumza habari zile kwa mfalme. Mfalme aliposikia alimrudisha janibu kumchukua Adili na manyani yake.

Adili alikuwa mwema na msamehevu. Alibaini kama Ikibali alilaumika kwa kufichua siri, kadhalika yeye mwenyewe alilaumika kwa ukatili. Tafakuri ilimwonyesha Adili kuwa ukali wa mbwa huyokana na msasi. Mbwa wa msasi mkali ni wakali pia. Rai alikuwa mfalme mwadilifu. Ilijuzu Ikibali, mjumbe wake, kuwa mchunguzi hodari. Mambo yaliyogunduliwa yalikuwa kweli. Mambo yenyewe hayakumpendeza Adili mwenyewe, licha ya mfalme na mjumbe wake. Kipawa kimoja katika vipawa bora kwa mwanadamu ni ujuzi wa maovu. Adili alibarikiwa kipawa hiki. Alishukuru kuwa siri iliyogunduliwa imefika katika masikio ya mfalme. Adili mwenyewe alitaka ijulikane, lakini alichelea kuwa haini kwa mfadhili wake. Madhali imefichuka alikuwa tayari kuithibitisha.

Adili alijiandaa kwa safari ya kuitika mwito wa mfalme. Farasi watatu walitandikwa matandiko mazuri. Yeye alipanda farasi mmoja na mmoja kwa kila nyani. Ikibali alipanda farasi wake mwenyewe. Farasi wa Adili na yule wa Ikibali walikwenda sambamba njiani. Nyuma yao yaliandama manyani juu ya farasi. Kila mtu aliyeona manyani yamepanda farasi alistaajabu. Mnyama kupandwa na mnyama ilikuwa upeo wa miujiza kwa watu. Vinywa vya umati wa watu vilikuwa wazi kwa kivumo cha Lo salala! Wakati umefika wa mawe kusema, miti kujibu na wanyama kuwa watu! Ikibali aligeuza uso wake kwa Adili akasema kwa ucheshi. "Mbwa wanatubwekea kama walionusa mtara wa windo." Adili alikubali kwa kuinamisha kichwa akatabasamu, walisafiri hivi mpaka Ughaibu. Baada ya kutua Adili alipelekwa mbele ya mfalme na manyani yale.

Manyani yalipomwona mfalme yalifanya ishara mbili. Kwanza yaliinua juu mikono yao kama yaliyokuwa yakiomba, pili yalilialia kama yaliyodhurumiwa. Ishara ya kwanza ilionyesha ombi la msaada, na ile ya pili ilionyesha mashtaka. Licha ya Rai, hata mimi na wewe tungalifasiri hivi kama tungalikuwa katika baraza hiyo. Mfalme alipoona vile alitaka kujua kwa Adili sababu ya kuadhibiwa, kulishwa na kunasihiwa manyani yale kila usiku. Katika sababu zake alionywa kusema kweli tu. Adili alijibu kuwa waungwana hawasemi uongo. Atasema kweli, na manyanai yatakuwa mashahidi. Maneno yake yakiwa uongo, yatakanushwa na manyani kwa mguno, lakini yakiwa kweli, manyani yatayathibitisha kwa kuziba nyuso kwa viganja vya mikono yao. Sasa kisa baada ya kisa juu ya manyani kilisimuliwa
 
SURA YA 4

Ndugu Zake

Katika kisa cha kwanza Adili alisema manyani yale mawili yalikuwa ndugu zake. Baba yao alikuwa mmoja na mama yao mmoja. Baba yao aliitwa Faraja. Faraja alikuwa mtoto wa pacha. Wakati wa kuzaliwa pacha huyo mtoto mmoja alikufa pakabaki mmoja. Huyu aliyebaki aliitwa faraja kwa sababu aliwafariji wazazi wake katika msiba wa ndugu yake. Alipokuwa wazazi wake walimwoza mke, yaani mama yao. Mama yao alichukua mimba ya kwanza akazaa mwana aliyeitwa Hasidi. Alichukua mimba ya pili akazaa mwana vile vile aliyeitwa Mwivu. Alichukua mimba ya tatu akazaa mwana tena aliyeiywa Adili. Walilelelewa mpaka wakawa watu wazima wenye vichwa vilivyofunzwa lakimi mioyo iliyosahauliwa. Busara kubwa kichwani haina faida kama moyoni hamna chembe ya wema.

Baba yao alipokufa aliacha shamba zuri, duka kubwa, mifugo mbalimbali na nakidi shilingi hamsini elfu. Walimzika kama desturi wakafanya matanga. Siku arobaini zilipopita, Adili alikaribisha matajiri na watu maarufu wa janibu karamuni. Karamu ilipokwisha Adili alitamka kuwa maisha ni safari, na dunia ni matembezi kwa wanadamu. Maskani yao ya milele yako peponi. Hapana mtu ambaye atabaki duniani. Baba yake amekufa akiacha mali nyingi. Alichelea kuwa walikuwako watu waliomdai au walioweka amana kwake. Alitaka kila mtu apate kulipwa ili aindoe lawama la baba yake ulimwenguni. Baada ya kusema hivyo kimya kikubwa kilitokea. Watu walinyamaza kama waliokuwa wamenyang'anywa ndimi zao.

Halafu walijibu kwa umoja kuwa hawakuweza kuuza pepo kwa dunia. Walikuwa wacha Mungu na wafuasi wa haki. Walifahamu halali na haramu. Jambo moja katika mambo waliyokimbia kabisa lilikuwa mali ya yatima. Walimfahamisha Adili kuwa mali ya baba yake ilikuwa imebaki mikononi mwa watu. Bila shaka watu hao watamlipa. Hapakuwa na mtu hata mmoja miongoni mwao aliyedai kitu kwa marehemu. Walithibitisha kuwa walimsikia mara nyingi baba yake Adili akisema kuwa alichelea sana deni. Katika uhai wake alizoea kuomba asife na deni. Tabia ya baba yake ilikuwa kamili. Kila karadha aliyochukua alilipa kabla ya kudaiwa. Alipokopesha kitu kwa mtu hakudai kwa fadhaa. Wadeni wake walimlipa pole pole. Mtu aliyekuwa hana njia ya kulipia alisamehewa.

Adili aliwashukuru kwa kuhudhuria karamuni na kwa kumpa hakika ya ukamilifu wa baba yake. Wageni walipokuwa wanakwenda zao waliambiana njiani, "Mwana wa mhunzi asiposana huvukuta. Adili atakuwa mwema kama baba yake."

Sasa Adili aliwaambia ndugu zake kuwa kwa ushahidi uliotolewa alitosheka kuwa baba yao alikuwa hadaiwi na mtu. Urithi walioachiwa ulikuwa mkubwa sana. Warithi walikuwa watoto watatu tu. Aliuliza kama ndugu zake walipenda urithi ule ugawiwe kila mtu achukue sehemu yake, au uachwe kama ulivyokuwa ili watumie shirika. Ndugu zake walitaka urithi ugawiwe kati yao.

Adili alikwenda kumwita kadhi. Kadhi alipokuja aligawa urithi wao katika mafungu matatu. Mafungu yote yalikuwa sawasawa kwa thamani. Kila mmoja alipata fungu lake. Adili alichukua shamba na duka. Mali nyingine walioewa ndugu zake.

Basi Adili alifungua duka lake. Alinunua bidhaa akatia dukani mpaka likajaa tele. Alikaa kitako akafanya biashara. Ndugu zake walinunua marobota ya ngozi na bidhaa nyingine wakafanya safari ya kwenda nchi ngeni kufanya biashara. Siku ya kuagana nao, Adili aliomba Mungu awabariki ndugu zakw ugenini, naye ampe riziki yake kwao. Alifanya biashara kwa muda wa mwaka mmoja. Hakuacha kuhesabu kitu alichonunua wala alichouza. Vitu vyote, kilichoingia ndani na kilichotoka nje , vilitiwa daftarini kwa uangalifu. Mali bila ya daftari hupotea bila habari. Adili alikuwa macho sana juu ya neno hili. Aliweka hesabu ya kila siku na ya kila mwezi. Mwisho wa mwaka alipolinganisha faida na hasara aliona amepata mali kama ile iliyoachwa na baba yake. Hakika mtu anayehesabu mapato na matumizi yake hafi maskini.

Siku moja Adili alikuwa amekaka dukani pake. Ulikuwa wakati wa baridi. Alikuwa amejifunika mablanketi mawili. Moja lilikuwa la sufu na jingine la pamba. Aliona ghafla watu wawili wanakuja dukani. Walikuwa hawana kitu. Kila mmoja alivaa kanzu mbovu bila ya nguo nyingine ndani. Midomo yao ilibabuka kwa baridi. Alipotambua kuwa walikuwa ndugu zake, moyo wake uliwaka moto kwa huzuni. Watu aliowapenda walikuwa katika hali mbaya sana. Aliondoka kitini akaenda kuwakumbatia. Mitiririko ya machozi ya moto ilitoka machoni mwake. Hakuweza kujizuia kulia kwa sababu ya mapenzi makubwa aliyokuwa nayo juu ya ndugu zake. Mapenzi yakw yalitoneshwa na hali mbaya waliyokuwa nayo.

Adili Alikuwa tayari siku zote kugawana na mtu yeyote tonge moja la chakula lililokuwa mikononi mwake. Alipoona ndugu zake katika matambaa hakuweza kuhimili. Uchi wao ulikuwa uchi wake. Alivua mablanketi yake mwenyewe akampa kila mmoja lake.

Maji ya moto yalitengenezwa akawapeleka msalani kuoga. Kisha alitoa sandukuni vikoi viwili, fulana mbili, kanzu mbili, jozi mbili za viatu na kofia mbili akawapa. Vitu hivyo vilikuwa vizuri na thamani yake ilikuwa kubwa sana. Baada ya kuvaa nguo walikaribishwa sebuleni. Wakati ule hali yao ilikuwa bado dhaifu sana kwa uchovu na njaa. Chakula kililetwa katika sinia moja ya dhahabu iliyonakshiwa kwa fususi. Walitafadhalishwa kula chakula wakala mpaka wakashiba.

Adili aliyageukia manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea. Manyani yaliziba nyuso kwa viganja vyq mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 5

Mgawo Mwingine

Katika kueleza msiba wao, ndugu zake Adili walisema walipoondoka Janibu walikwenda Gube. Walianza kuuza bidhaa zao huko. Ngozi iliyonunuliwa Janibu kwa shilingi moja iliuzwa kwa shilingi kumi, na ile ya shilingi mbili kwa shilingi ishirini. Walipata faida kubwa sana. Baadaye walinunua viatu kwa bei ya shilingi kumi jozi moja. Viatu hivyo vingalifika Janibu vingaliuzwa kwa shilingi arobaini kila jozi. Walipotoka Gube walikwenda mji wa Gharibu wakafanya biashara kubwa kuliko ya mara ya kwanza. Walishindwa kujua hesabu ya fedha waliyoipata, walisifu uzuri wa miji waliyokwenda, usitawi wa biashara na fauda iliyopatikana huko.

Mtu kushindwa kujua pato lake mwenyewe huonyesha uchache wa uangalifu. Lakini Adili hakusema neno juu ya hili. Ulikuwa si wakati wa kusema makosa. Ndugu zake walitaka huruma wakati ule siyo kulaumiwa.

Kisha waliendelea kusema kuwa msiba wao ulikuwa hausemeki. Walipoona wamepata mali nyingi hawakufurahi kukaa ugenini tena. Iliwatokea dhahiri kuwa mtu huchuma juani akala kivulini. Kwa kila mtu kwao ni kivulini na ugenini ni juani. Fikira hii ilipowatopea walifanya safari ya kurudi kwao. Basi walijipakia chomboni. Kwa muda wa siku tatu safari yao ilikuwa njema, lakini siku ya nne bahari ilichafuka. Mvua ilianza na giza lisilopenywa na nuru lilifunika bahari. Mchana ulikuwa kama usiku. Palitokea radi na umeme. Dhoruba kali iliandama nyuma. Mawimbi makubwa kama milima katika bahari isiyopimika kina yaliwakabili. Jahazi yao ilipeperushwa kama jani mwambani ikavunjika. Shehena ya mali ilikuwa chomboni ilitota. Fikira ya mali yao haikuwajia. Waliomba wokovu wa maisha yao tu. Kwa msaada wa mbao chache zilizopatikana katika chombo kilichovunjika, walielea baharini mchana na usiku kwa muda wa siku sita.

Siku ya saba, walipokuwa karibu kukata tamaa, jahazi ilipita karibu yao. Mabaharia wa jahazi hiyo waliwaokoa. Jahazi iliyowaokoa ilikuwa na safari ya kwenda nchi nyingine. Iliwapasa kuwa katika safari zile na kufanya kazi bila ijara chomboni. Waliposhuka katika kila bandari waliyofika waliomba chakula katika baadhi ya miji walipewa chakula, lakini katika miji mingine hawakupata kitu. Kwa hivi, waliuza nguo walizovaa wapate fedha ya kununulia chakula. Uchi wao uliweza kungojea nguo, lakini njaa yao haikuweza kungoja chakula. Waliapata robo tatu za mashaka ya dunia toka siku waliyokufa maji mpaka siku waliyofika kwao. Laiti waaingalipatwa ma bahati mbaya wangalirusi Janibu na utajiri mkubwa.

Ndugu zake walikuwa masogoro katika kusema. Walijifunza sana kutumia ulimi na midomo. Adili alivutwa na maneno yao siku zote. Hakujua kama tumaini lake juu ya ndugu zake lilikuwa kazi bure. Walikuwa waovu katika kila inchi ya miili yao. Baada ya kuwasikiliza aliwapa pole. Alisema kuwa mali hufidia roho lakini roho haifidiwi na kitu. Salama ya maisha yao ilikuwa bora kuliko faida iliyopotea. Umaskini umetengana hatua moja tu na utajiri. Kwa kuwa vitu vile vimekaribiana sana, wako watu katika dunia waliopata kuonja uchungu wa umaskini na ladha ya utajiri. Madhali ndugu zake wameonja uchungu wa umaskini, aliwakuza moyo kutazamia ladha ya utajiri wakati ujao.

Siku ya pili Adili aliwachukua ndugu zake kwa kadhi. Alipofika aliomba mali yake igawanywe mafungu matatu sawasawa kati yao. Alifanya hivyo kwa kuwaambia mali ile pia ilitokana na baba yao. Kila mtu alichukua fungu lake akafungua duka. Adili aliomba dua kuwa ndugu zake na yeye wote wabarikiwe. Aliwaonya wenziwe hatari ya uvivu na hasara ya ulevi. Aliwapa chakula na haja nyingine za lazima bure siku zote. Walikaa nyumbani mwake raha mustarehe. Mara kwa mara walipokuwa pamoja, Adili aliambiwa sifa za nchi ngeni. Ndugu zake walikumbuka mali yao na usitawi wa biashara walioona. Walimvuta Adili kusafiri pamoja nao tena kwa sababu faida za safari, yaani kufarijika katika hamu, kujua namna ya kuendesha maisha, kupata elimu mpya, kuelewa tabia za watu mbalimbali, kukutana na marafiki wa kweli kushinda ndugu, na mtu mwenye bahati mbaya kwao huweza kupata bahati njema ugenini.
Adili aliyageukia manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea. Manyani yaliziba nyuso kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 6

Tandu na Nyoka

Moyo hauhimili mshawasha wa mfululizo. Hasa mshawasha wenyewe ukitokana na mtu unayempenda au tamaa ya utajiri. Moyo wa Adili ulikuwa na mapenzi makubwa juu ya ndugu zake. Aliwapenda kama pumzi ya maisha yake mwenyewe. Aliposikia maneno yao alisema haikuwezekana katika maisha yake kukataa haja iliyotakiwa na ndugu zake. Alikubali kusafiri pamoja nao walikopenda.

Fedha ya kuchanga kwa ajili ya safari iliyokusudiwa ilikisiwa. Mafungu matatu sawasawa yalitakiwa. Fungu la kila mtu lilipokusanywa jumla kubwa sana ya fedha ilipatikana. Walinunua ngozi na bidhaa nyingine. Halafu walikwenda bandarini wakaajiri jahazi kubwa. Walipakia mali yao na vyakula mbalimbali. Siku ya pili walipakia chomboni wakasafiri.

Adili alisumbuka safarini kwa sababu ilikuwa mara yake ya kwanza kusafiri baharini. Baada ya safari ya siku tatu walifika bandarini. Bandari yenyewe ilikuwa ya kwanza katika bandari walizokusudia kwenda. Walishuka wakafanya biashara. Kwa faida iliyopatikana pale, Adili alisadiki maneno yaliyosemwa na ndugu zake. Waliondoka pale wakaenda mji wa pili. Huko walifanya biashara vile vile wakapata tija kubwa kuliko ya kwanza. Walikwenda mji wa tatu wakauza bidhaa zao kwa faida kubwa pia. Kabla ya kufika miji yote waliyokusudia kwenda, waliona wamekwisha rudisha thamani ya mali yao, na faida iliyopatikana ilikuwa kubwa sana. Nusu moja ya mali waliyokuwa nayo ilikuwa imeuzwa. Palibaki nusu ya pili kuuzwa. Walikwenda miji mingine.

Baada ya safari siku moja walifika jabalini. Nahodha aliamuru kutua tanga na kutia nanga. Kisha mabaharia walitakiwa washuke jabalini kutafuta maji kwa sababu jahazini mlikuwa hamna maji hata tone moja. Pipa la maji jahazini lililotosha kwa mwezi mmoja lilitoboka. Maji yake yalivuja bila ya kujulikana na mtu. Mabaharia wote walishuka wakatafuta maji chini ya jabali. Adili alipanda juu ya jabali. Huko aliona tandu linakimbia. Rangi yake ilipendeza sana. Iling'ara kama kioo. Nyuma yake lilifuatwa mbio na nyoka aliyetisha kabisa. Nyoka alipolifikia aliliuma kichwani. Kisha alilibana jiweni. Tandu lilitoa mlio wa kusikitisha. Kwa mlio ule Adili alijua kuwa tandu lilikuwa hatarini. Mara ile moyo wake uliingiwa na huruma. Hakuweza kuvumilia. Aliokota jiwe liliokaribia uzito wa ratili moja akamtupia nyoka. Jiwe lilimpiga nyoka kichwani. Ilikuwa shabaha nzuri sana. Kichwa chote kilipondeka kwa pigo moja akafa mara ile.

Ghafula tandu lilijigeuza mwanadamu, yaani, msichana mzuri. Uso wake ulivuta macho ya Adili kwa haiba yake kubwa. Mbele ya wanawake mia moja wazuri, msichana huyo angalitokea, wote wangalijichukia wenyewe kwa kujiona hawakulingana nae kwa uzuri. Tazamo la mwanamume yeyote lingalivutwa kama angalitokewa na msichana huyo. Alikwenda kwa Adili akampa mkono. Alimshukuru kwa wema aliomtendea. Adili aliombewa dua na msichana apate himaya mbili. Himaya ya dunia na himaya ya ahera. Ya kwanza imfae katika maisha yake, na ya pili imwokoe siku ambayo mtu hatafaliwa na kitu kingine ila wema aliotenda. Kama alivyookolewa msichana aliahidi kutenda neno lolote jema kwa Adili katika wakati ujao.

Baada ya hayo msichana alielekeza kidole chake cha shahada chini. Mara moja ardhi ilipasuka akaingia ndani yake. alipokwisha jitia ndani ardhi ilijifunga sawia. Msichana hakuonekana tena. Adili alifahamu kuwa alikuwa si mwanadamu ila jini. Kitambo kidogo aliona nyoka aliyemwua anawaka moto. Mara moja alikuwa majivu matupu. Kufumba kope na kufumbua mahali palipokuwa na majivu palitokea chemchemi ya maji safi. Mambo haya yalikuwa mwujiza mkubwa sana kwa Adili. Alirudi kwa wenziwe na habari za ugunduzi wa maji. Adili alishangiliwa sana kwa ugunduzi wake. Walipkwisha chota maji ya kutosha walilala. Asubuhi walitweka wakasafiri baharini mchana na usiku kwa muda wa siku thelathini. Walikuwa hawaoni bara wala kisiwa. Maji yao yalikwisha tena.

Nahodha alipotangaza chomboni kuwa maji yamekwisha mabaharia waliomba chombo kielekezwe upande wa bara. Lakini nahodha aliapa kuwa hakujua upi ulikuwa upande wa bara toka mahali walikokuwako. Aliposema hivyo mioyo yao ilihuzunika machozi yakawatoka machoni njia mbili mbili. Walikuwa hawana neno la kutenda ila kuomba hifadhi ya Mungu. Siku ile walilala na kihoro. Kulipokucha waliona jabali refu sana baharini. Walianza kufurahi tena.

Tanga liligeuzwa wakaenda jabalini. Walipolikaribia walitua. Kisha walishuka chomboni wakapanda jabalini kutafuta maji. Hali zao zilikuwa dhaifu kwa kiu. Walitafuta hiku na huko lakini hawakuona maji. Adili alipanda juu zaidi. Huko alitazama upande wa pili wa jabali akaona kwa mbali sana akaona ukuta umezunguka. Ilipata mwendo wa robo saa toka jabalini mpaka ulikokuwa ukuta. Aliwaita wenziwe waliokuwa chini ya jabali.

Walipokuja aliwaonyesha ukuta alioona. Alidhani ndani yake ulikuwako mji mkubwa ambako maji na vitu vingine viliweza kupatikana. Basi aliwashauri wenziwe kwenda kule. Wenziwe wote walikataa kwenda. Walichelea kuwa mji wenyewe usije kuwa wa watu wabaya. Wakikamatwa utakuwa mwisho wa maisha yao. Kwa vile walivyokuwa katika hatari ya kiu, hawakuweza kujasiri katika hatari nyingine kwa tamaa ya maji. Walikataa kwenda wakajitolea wenyewe kufa kwa kiu, Lakini Adili hakukubali. Moyo wake ulikuwa imara sana. Alitaka kujaribu kujiokoa kwanza kabla ya kujitolea kushindwa. Ilikuwa idhilali kwake kujilegeza mbele ya shida iliyowezekana kushindwa. Kwa hivi, alisema kuwa hakua na mamlaka juu ya mabaharia wote, lakini alitaka kwenda na ndugu zake. Lo, ndugu zake waliruka wakakataa kufuatana naye. Walionywa na Adili kuwa mwanadamu ameumbwa kwa heri na shari, na hasa kwa heri.

Ilikuwa hasara iliyoje kutazamia shari tu katika maisha! Juu ya onyo hili ndugu zake hawakuwa tayari kwenda naye. Basi aliwaomba wamngoje jabalini. Walipokubali kufanya hivyo alikwenda zake peke yake kujaribu bahati yake.

Adili aliyageukia manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea. Manyani yaliziba nyuso kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 7

Mji wa mawe

Adili alikwenda mpaka ulikokuwa ukuta alioona. Kimo cha ukuta wenyewe kilikaribia futi arobaini. Juu ulikuwa na upana wa futi kama ishirini. Wote ulikuwa wa mawe yaliyowekwa kwa imara na ustadi. Mivule , mikangazi, mibuyu na miti mingine ya magogo manene iliota juu yake. Miti yote iligeuka mawe, lakini rangi ya majani yake ilikuwa ya kijani. Maki ya ukuta wote ilikuwa futi ishirini. Duara kubwa sana ilikuwa katikati ya ukuta huo. Katika duara hiyo ulikuwako mji uliokuwa na majengo mazuri sana . Milango mia moja ilikuwa ukutani, na kila mlango ulitengana na mwingine kwa umbali wa maili hamsini. Milango yote ilikuwa ya chuma kilichokuwa na maki ya futi saba. Ulikuwa mji mzuri na wenye ngome bora duniani.

Milango yake ilikuwa wazi. Adili alipotaka kuingia ndani aliona mtu amesimama mlangoni. Kichaka kikubwa sana cha funguo kilikuwa mkononi mwake. Adili alidhani mtu yule alikuwa bawabu. Alikwenda karibubyake akamwamkia. Hakujibu neno. Alimwamkia mara ya pili na ya tatu lakini hakujibu hata kidogo. Adili alishangazwa na adabu ya mtu aliyemwamkia.

Alidhani hakuelewa lugha yake. Lugha ni pingamizi kubwa kwa watu duniani. Kwa hivi alimwamkia kwa ishara. Hili liliposhindwa kufaulu alimsogelea akamshika begani. "Bwana umelala nini?" Hakujibu wala hakutikisika. Alizidi kumtazama na kumshika mwilini. Alipofanya hivyo aliona kwamba alikuwa si mtu ila jiwe lililokuwa halina maisha. Ugunduzi huu ulitia mzizimo wa hofu katika moyo wa Adili lakini alijikaza. Adili alikuwa si mtu wa kukata tamaa. Tamaa kwake ilikuwa gurudumu la maisha naye alijua namna yakuitawala. Mzizimo wa hofu iliyotambaa moyoni mwake uliyeyushwa na udadisi wake mkubwa.

Aliondoka aliposimama akaingia ndani kidogo. Huko aliona mtu mwingine amesimama barabarani. Alimkaribia akamtazama. Lilikuwa jiwe vilevile. Alizungukazunguka barabarani. Kila alipokwenda alitazama huku na huko. Mabarabara yote yalikuwa yamejaa watu waliosimama, Lakini wote walikuwa mawe matupu. Alipofika sokoni aliona umati mkubwa wa watu. Baadhi yao walikuwa wamekaa kitako na wengine walikuwa wamesimama wima. Mbele ya watu waliokaa palikuwa na vikapu vya nafaka iliyogeuka chngarawe, unga uliokuwa vumbi, matunda yaliyobadilikia komango, na vitu vinginw vya biashara vilivyogeuzwa mawe. Vyote vilikuwa katika hali iliyokuwa haifai kwa chakula. Sababu iliyoweza kueleza mabadiliko yale ilikuwa bado kuonekana. Kwa hivi, Adili aliazimu kuitafuta kwa kila hali. Adili alikuwa na uchunguzo uliomwongoza katika ugunduzi mkubwa.

Alipoondoka sokoni aliona nyumba moja kubwa barabarani . Milango yake ilikuwa wazi. Hili lilikuwa duka la tajiri mkubwa. Alipoingia ndani aliona mwenyewe amelala juu ya kitanda cha dhahabu. Kitanda chenyewe kilitandikwa nguo nzuri na matakia ya zari teule. Mbele yake palikuwa na kabati lililokuwa na kimo cha futi kumi na upana wa futi tano. Tajiri mwenyewe alikuwa mgumu na baridi kama jiwe; na vitu vyake vyote kadhalika. Adili alitazama kabatini akaona mifuko imepangwa safu. Alishika mfuko mmoja lakini kitambaa chake chote kilikuwa vumbi. Vitu vilivyokuwa katika mifuko hiyo ilikuwa sarafu ya dhahabu tupu. Hii haikubadilika mawe wala vumbi. Alijaribu kuchukua dhahabu, lakini hakuweza kama alivyopenda. Moyo wake uliingiwa na fikira kwamba kama angalikuja na ndugu zake wangaliweza kuchukua dhahabu ya kutosha.

Alipotaka kutoka nje aliona makabati yaliyotiwa nguo za hariri na sufu. Nguo hizo zilikuwa za rangi mbalimbali na za almaria bora. Aliponyoosha mkono wake kuzishika zilikuwa vumbi kama vitambaa vya mifuko ya dhahabu. Alitoka akaingia duka jingine. Huko aliona mali nyingi sana kuliko alizoona katika duka la kwanza. Ah, maskini! Mali ilipatikana lakini haikuwa na wachukuzi. Watu waliokuwa na njaa na jahazi yao iliyotaka shehena walikuwa wamesimama kando kwa zembe. Jahazi ilifika nchi ya dafina ya ajabu, lakini mabaharia wake hawakushuka pwani kuipakia. Kula uhondo kwataka matendo. Asiye matendo hula uvundo.

Adili alikuwa kama chura kilichofurahia mvua lakini kilikuwa hakina mtungi wa kuwekea maji. Alitamani kuwa na nguvu za ndovu ili achukue dhahabu ya kutosha lakini haikuwezekana. Basi aliingia hapa akatoka. Alikwenda pale akaondoka na fikira ya mwujiza alioona.

Kila barabara aliyopita ilikuwa na watu, ng'ombe , farasi, nyumbu, punda na mbwa , lakini wote walikuwa mawe matupu. Hofu kubwa ilitambaa moyoni mwake kuwa naye asijegeuzwa jiwe. Lakini alijifariji kuwa labda ilikuwako sababu ya mji ule, wanyama na vitu vyake kuwa mawe, na kuwa lile lilikuwa fundisho kwake. Wazo hili lilimpa nguvu akaendelea kupeleleza. Alipoingia katika maduka ya masonara aliona wenyewe wamegeuka mawe. Mikono yao ilikuwa imeshika vito vilivyokwisha tengenezwa. Vito vingine vilikuwa ndani ya mikebe. Alipoona vile alitupa mbali dhahabu aliyokuwanayo kwanza akarukia vito kwa pupa . Lakini mara moja alisimama kwa mshangao. Alijiona amekaliwa na uzito wa vitu alivyopapia. Juu ya uzito huo hakuweza kuongeza hata pini moja ya shaba. Vitu vilivyobaki vilimtazama kama vilivyokuwa vikimsimanga kwa choyo yake. Tamaa ya mali ni kubwa. Mioyo mingi haitoshwi na mali. Walakini, kwa kweli fikira ya mali isiyo kadiri ni mzigo usiochukulika.

Alipotoka pale aliingia katika maduka ya majohari. Huko aliona wenyewe wamekaa vitini. Mbele ya kila tajiri lilikowako bweta. Mabweta hayo yalijaa yakuti, almasi, fususu, lulu, feruzi na majohari mengine. Matajiribwote walikuwa mawe. Alitupa chini vito vilivyotengenezwa akachagua yakuti; aliacha yakuti akashika almasi; alikataa almasi akatwaa fususi; alitaka lulu badala ya fususi na feruzi kwa majohari mengine.

Alikuwa hana nguvu ya kuchukulia majohari yote. Kiasi cha majohari aliyoweza kuchukua hakikupunguza wingi alioukuta. Majonzi yalimjia akasikitika juu ya ndugu zake kwa kukosa kufuatana naye. Ndugu zake walikuwa na miguu ya kwendea bali hawakuitumia; walikuwa na nguvu za kuchukulia tunu zilizotosha kwa utajiri wao lakini hawakuwapo. Hili lilimwonyesha Adili kuwa maumbile yalikuwa si bahili. Yalikuwa karimu katika kugawa vipawa. Lakini zaidi ya nusu ya hasara za wanadamu hutokea kwa sababu wenyewe hawataki kutumia vipawa vyote walivyopewa. Basi alichukua alichoweza akaendelea mbele. Moyo wake ulijaa majuto juu ya ndugu zake aliopenda kushiriki nao furaha ya ugunduzi, fahari ya usitawi wa utukufu wa matendo bora.

Alipozunguka nyuma ya maduka alitokea kulikokuwa na nyumba moja kubwa kabisa. Nyumba yenyewe ilikuwa na milango mingi. Miongoni mwa milango hiyo mmoja ulikuwa mkubwa sana. Kwanza hakufaham kwa nini mwenyewe alipata gharama kubwa juu ya milango mingi kama ile. Kisha aliona kuwa gharama yake ilikuwa na maana kwa mtu mwenye akili. Si nyumbani tu lakini hata katika jambo lolote hadhari hukataza mtu kujitia ndani yake kama halina milango ya kuingilia na kutokea. Milango ya nyumba ile ilitosha kwa salama. Baada ya kuwaza hivyo alipita kwa mlango mkubwa uliokuwa wazi akaona mabawabu na askari waliokuwa na sura za kuogofya. Lakini walikuwa mawe.

Ndani kulikuwa na uwanja mkubwa uliozungukwa na viti pande zote. Aliendelea mbele kidogo akatokea katika halmashauri kuu. Juu ya nusu ya halmashauri hiyo palijengwa ulingo. Ulingo wenyewe ulikuwa umejengwa kwa ustadi mwingi. Juu yake palizunguka watu aliodhania kuwa mawaziri, makadhi, mashehe, wanajimu, washauri na madiwani wengine. Kati yao palikuwa na kiti cha dhahabu kilichotonewa kwa majohari mbalimbali. Juu ya kiti hicho alikaa mfalme aliyevaa lebasi za fua zilizokuwa hazitamaniki kwa kumetameta. Kichwani mwake alivaa taji. Taji hilo lilipangiliwa kwa majohari ali ali. Kwa mng'ao mkubwa wa majohari mfalme mwenyeww alikuwa hatazamiki. Alipopanda juu ya ulingo kutazama aliona kuwa hadhara yote ilikuwa mawe matupu.

Alishuka chini akaingia katika halmashauri nyingine. Hiyo kadhalika ilikuwa sawasawa na ile ya mfalme ila ilikuwa na madiwani wanawake watupu. Baadhi ya madiwani walikuwa wamesimama mbele ya malkia na mikono yao vifuani, na wengine walikuwa wamepiga magoti chini yake kwa unyenyekevu. Walakini halmashauri hiyo ilikuwa na mapambo bora kuliko ile ya kwanza. Ilikuwa na meza ya pembe na viti vya mpingo. Juu ya meza palikuwa na bilauli za johari memetevu. Halmashauri nzima ilikuwa imejaa wanawake waliokuwa na uzuri wa sifa kubwa sana. Malkia mwenyewe alikuwa amekaa kitako kati yao. Mabibi wote walikuwa mawe matupu. Utulivu wa akili ya Adili ulichafuka. Alitupa chini majohari yote yaliyokuwa katika miliki yake. Moyo wake ulisimama juu ya bilauli zilizokuwa mezani. Alichukua zilizotosha kuwa mzigo wake akaondoka pale kabla moyo haujarogwa na uzuri wa mabibi waliogeuka mawe.
 
SURA YA 8.

Mrithi wa Mji wa Mawe

Baada ya kwenda mbele hatua chache Adili aliona mlango mdogo. Kizingitini pake palikuwa na ngazi iliyoongoza juu. Alipopanda vidato vichache aliona dalili za mtu au watu walioishi mle. Kwanza alikuwa akipanda kwa kusitasita, lakini sasa dalili zile zilimvuta akafululiza kupanda. Aliendelea mpaka orofani. Alifuata zilikoongoza dalili mpaka akafika kulikokuwa na chumba kidogo. Mlango wake ulikuwa wazi, kwa hivi aliingia ndani. Huko aliona pazia la hariri lililotariziwa kwa vito vya dhahabu, lulu na yakuti linaning'inia mbele yake. Fusuai hizo zilimeremeta kama nyota. Dalili alizoona ziliendelea nyuma ya pazia hilo. Alijipa moyo mkuu akafunua pazia. Alipofanya hivyo macho yake yaliona mlango wa tarabe.

Mlango huo ulikuwa mzuri sana. Mbao zake zilikuwa za mpingo, nazo zilinakshiwa kwa johari na pembe. Mtu yoyote angaliona mlango huo angalistaajabu sana. Adili alibisha hodi akaingia katika chumba kikubwa. Chumba chenyewe kilikuwa kimepambwa vizuri sana. Katikati yake palikuwa na meza na kiti. Msichana wa fahari alikuwa amekaa kitako pale juu ya kiti. Usonwake ulikuwa umetukuka. Kwa uzuro uliokuwa haumithiliki. Bila shaka yeye alikuwa malkia wa wazuri katika dunia nzima. Libasi alizovaa zilikuwa nzuri na za thamani kubwa sana. Katika miji yote mingine aliyopata kufika katika safari zake, Adili alikuwa bado kukutana na mtu yeyote mwingine aliyevaa libasi nzuri kama zile.

Kama uzuri ulio peponi wamejaaliwa malaika; karibu uzuri wote ulio duniani alijaaliwa msichana huyo. Uzuri wake ulikuwa haulingani kwa uzuri na mwanamke mwingine yeyote aliyesifiwa kuwa mzuri katika zamani zake. Msichana mwenyeww alikuwa anasoma kitabu kitakatifu. Matamko yake yalikuwa kama mafuatano ya muziki. Moyo wa Adili ulitekwa na mapenzi ya tamasha hiyo. Akili yake ilipotea na nuru ya macho yake ilizimika kitambo. Ile ilikuwa mara ya kwanza mshale wa mapenzi kupenya moyoni mwake. Ulipenya katikati ya moyo wake. Haukuacha nafasi ya mapenzi ya mwanamke mwingine. Licha ya Adili hata mtu mwingine aliyekuwa hajui mapenzi angalikutana na mwanamke huyo moyo wake ungalitekwa pia.

Akili ya Adili iliporudi alimwamkia mwenyeji wake. Mwenyeji aliyeamkiwa hakuitikia tu, lakini alitaja jina la aliyemwamkia vile vile akamkaribisha kwa furaha. Adili alimwuliza alilijuaje kina lake, yeye alikuwa nani na miujiza gani iliyopita pale hata viumbe wa mji mzima wakageuka mawe. Bila ya kusema neno msichana aliondoka akaenda kuchukua kiti. Alikiweka karibu yake akamwomba Adili kukaa kitako. Mwendo aliotumia katika kwenda na kurudi wakati wa kuchukua kiti ulichukua pumzi zoye za Adili. Alikwenda kwa hatua za kupendeza , na mikono yake ilipunga kama upepo. Uzuri wake wa fahari ulikuwa na madaha makubwa. Chumba chake kilikuwa kama mahali pa faraja panapotafutwa na wanadamu.

Miguu ya msichana

Na mwendo aliokwenda,

Adili alipoona

Moyowe ulimshinda.

Alikuwa na miguu

Mfano wa charahani,

Wala ulimwengu huu

Hajatokea kifani.

Alipendeza hatua

Wakati alipokwenda,

Chini viatu vyalia

Mithali kama kinanda.

Alikwenda kwa madaha

Mwanamke mwenye enzi,

Yaliyompa furaha

Kila mwenye kubarizi.
 
SURA YA 9

Mji Ulivyogeuka Mawe

Sasa msichana alieleza kwamba yeye alikuwa binti mfalme, na jina lake lilikuwa Mwelekevu. Baba yake, Mfalme Tukufu alikuwa yule aliyeonekana kitini katika halmashauri ya madiwani wanaume. Mama yake, malkia Enzi, alikuwa yule aliyeonekana katika halmashauri iliyohudhuriwa na madiwani wanawake. Ufalme wao ulikuwa na utukufu na nguvu nyingi. Labda dola yao ilikuwa ya kwanza duniani iliyokuwa na miji laki moja. Isipokuwa, Fahari, mji uliogeuka mawe, miji mingine ilizama baharini. Raia chini ya bendera yao walikuwa lukuki. Mawaziri walikuwa laki tano. Kila waziri alikuwa na umati wa watu. Amirijeshi mmoja alikuwa na majemedari elfu moja na sufufu ya majeshi. Hazina za nchi zilikuwa na mali zisizohesabika kama machimbo ya Tanganyika.

Ulimwengu uliajabia dola yao kwa ushujaa wa askari na kwa busara ya mawaziri wao. Walakini, juu ya sifa hizo, mfalme, malkia na raia walikuwa waabudu mizimu. Mizimu yao ilikuwa miti. Miti yenyewe ni ile iliyogeuka mawe ukutani. Kabwere, Mganga na imamu wa mizimu hiyo alivuta mioyo ya watu wote. Siku moja asubuhi mfalme na malkia walikwenda katika halmashauri zao, kila mmoja akakaa juu ya kiti chake. Madiwani walikuwa wamewazunguka kabla ya kuanza kazi zao za desturi; mtu mmoja ambaye hakujulikana alikotoka alisimama ghafula mbele ya mfalme akajitangaza kuwa aliitwa Mrefu.

Mrefu alikuwa mwujiza katika viumbe. Alikuwa na miguu mikubwa na mapaja manene, kiuno cha utambo na kifua kipana na shingo yake ndefu ilichukua kichwa kikubwa. Mabega yake ya mraba yalining'iniza chini mikono iliyokuwa na nguvu kama manjanika. Kwa kimo cha kukithiri alitembea baharini bila ya kuguswa na maji magotini, akafikia vilele vya milima kwa mikono yake. Aliweza kukamata ndovu chini au nyangumi baharini akamwoka kwa jua mbinguni. Sauti yake ilikuwa kama radi kwa wepesi wake wa ajabu wa kuzunguka dunia nzima kwa sekunde moja, alionekana kama kiumbe kilichoumbwa maalum kuokoa kitu motoni, baharini au katika hatari nyingine.

Mrefu alimwambia Tukufu kuwa mfalme ni naibu wa Mungu duniani. Kwa hiyo , ufalme ni amana kubwa. Amna hiyo ilitaka uangalifu mkubwa kwa sababu ni dhima bora iliyowekwa mikononi mwa wanadamu. Wajibu wa kwanza wa mfalme ni kuwa mwadilifu katika matendo yake. Kila tendo, jema au baya , ni mfano kwa raia wake. Kwa sababu ya maisha ya milele ibada ya mizimu ilikuwa maangamizi , na uimamu wa kabwere ujinga mtupu.

Tukufu alimtazama msemaji akasema kwa ukali, "Nini kilichokujusurisha kusema upuuzi, Mrefu? Kama kwa sababu ya urefu ubongo wako umeyeyuka kwa jua, kaa kitako chini ya kivuli cha mizimu yetu utaburudika. Kama umerogwa, Kabwere atawakomesha waliokuroga. Riziki ya wanadamu hutoka mimeani. Kwa sababu hiyo, mimi na kaumu hii twaabudu miti. Funga ulimi wako, bwana. Usipofunga hasira ya mizimu itakuwa juu yako. Tafadhari jiokoe."

Mrefu alionya , "Hapana haja ya jibu la haraka. Tumia wakati upendao wa kufikiri. Nimesema neno la Mungu. Mungu hachelei tisho la mwanadamu, kazi ya mikono yake mwenyewe. Neno takatifu gumu kufahamika, lakini lina tija kwa wajisumbuao kulifasiri. Kila msaada nitakupa wa kulifasiri."

Tukufu hakujali onyo hili akaamrisha kushikwa kwa Mrefu aliyekuwa hasogeleki wala hashikiki. Uwezo usio hadhari ni kileo kibaya sana. Siku ile ilikuwa ya tisho na msiba, ole na maangamizi makubwa. Kwa laana iliyotamkwa na Mrefu, miji mingine yotw ya dola hii iligharika, na kila kiumbe kilichokuwa na maisha katika Fahari kiligeuka jiwe.

Hili lilipotokea Mwelekevu alikuwa darini anachungulia nje kwa dirishani. Toka pale aliweza kumwona Mrefu na kusikia maneno yake. Hakupendelea kushindwa kwa baba yake. Hapana mtoto apendeleaye hili . Walakini, mapendeleo yakiachwa mbali, nuru ya fikira humulika mno siku zote juu ya kweli kuliko uongo, na juu ya haki kuliko dhuluma. Nuru hii ndiyo iliyomwokoa Mwelekevu katika maangamizi yale ya kutisha. Na tangu siku ile aliamini kuwa onyo la bure likikataliwa huleta majuto ya milele.

Hayo yalipokwisha jiri Mrefu alimpa binti mfalme chuo kitakatifu alichomsifia kuwa bora kuliko vitabu vyote vya duniani vikichanganywa pamoja. Kwa matumizi mengine, Mrefu aliomba mkomamanga uote. Mkomamanga huo ulizaa komamanga moja kila siku. Kila chembe katika komamanga hilo ilikuwa chakula na kinywaji mbalimbali. Kwa mti ule wa ajabu binti mfalme aliweza kuishi maisha ya faraja. Mwisho alionywa kuwa siku ya kuona mti ule umezaa matunda mawili ajue Adili, mwokozi wake amefika. Hilo ndilo lililomjulisha siku ile kuwa mgeni wake alikuwa si mtu mwingine ila Adili.

Usemi wa binti mfalme ulimwonyesha Adili kuwa turufu huenda kwa mchezaji siku zote. Laiti asingalikwenda wenziwe walikoogopa akatafuta tafuta asingalikutana na bahati ambayo hakutazamia kuja katika ndoto zake . Alishukuru akamchukua binti mfalme pamoja na tunu bora alizoweza . Katika tunu zake yalikuwemo pia makomamanga mawili ya ajabu. Hayo yalikomesha kiu na njaa katika merikebu yao kwa muda wa siku kadha wa kadha.

Adili aliyageukia manyani akayauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea. Manyani yaliziba nyuso zao kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 10

Kutoswa kwa Adili

Nahodha na mabaharia walimshangilia Adili kama mtu wa bahati ya peke yake, na kuwa mtu mwingine yeyote kati yao angalifuatana naye kwenda walikoogopa , asingalikutana na bahati ile kubwa. Adili aliwashukuru wote akisema kwa furaha mkulima alikuwa mmoja siku zote, lakini walaji wengi. Pato lake lilikuwa pato lao vile vile.

Aligawa tunu zake katika mafungu manne yaliyokuwa sawasaw. Fungu la kwanza alimpa nahodha, na kila ndugu yake akapata fungu moja. Fungu lililobaki lilikuwa lake mwenyewe. Hili aliligawa tena katika mafungu mengi, kila baharia akapata sehemu yake. Isipokuwa ndugu zake, watu wote chomboni walishukuru wakamwombea heri. Nyuso za ndugu zake zilionekana zimekunjamana na macho yao yaliiva. Alifahamu hawakuridhika kwa sababu ya choyo chap kikubwa.

Aliwataka radhi akawaambia kuwa ingawa mafungu yao yalikuwa madogo, lakini wao walikuwa ndugu zake. Mali yake ilikuwa mali yao katika maisha na mauti. Palikuwa hapana sababu ya kukasirika.

Wakati alipokuwa akisema na ndugu zake stahani, Mwelekevu alikuwa amekaa ngamani na jahazi inakwenda moto mmoja.

Sasa Hasidi na Mwivu walimwuliza Adili nia aliyokuwa nayo juu ya bibi yule mzuri aliyempata katika mji wa Mawe.

Aliwajibu kuwa wakifika salama janibu nia yake ilikuwa kumwoa.

Hasidi aliomba kuwa angalifurahi kama angalimwoa yeye bibi yule.

Mwivu kadhalika alinasihi kuwa angalipenda kumwoa yeye.

Kwa kusikitika, lakini kwa imara kabisa, Adili alijibu kuwa kama walitaka neno jingine lolote katika miliki yake angaliwapa, ila hakufikiri kuacha mkono wa bibi yule kuguswa na mru mwingine katika ndoa ila yeye mwenyewe. Wao walimtaka lakini yeye alimpenda zaidi. Walakini wakirudi Janibu atawatafutia mabibi wawili wazuri. Gharama yote itakuwa juu yake. Arusi zao na yake zitakuwa siku moja , fungate na furaha yao itakuwa moja.

Ndugu zake walihoji kama mume mmoja katika Afrika aliweza kuoa wake wengi, na mke mmoja katika Asia alipata kuolewa na waume kadhaa, isingalikuwa vema kama ndugu watatu wa Janibu wangalishiriki uzuri wa mke mmoja?

Adili alibisha kuwa kulikuwa na mambo yaliyofaa na yaliyokuwa hayafai kushiriki. Ndoa ilikuwa jambo moja katika yale yaliyokataa ushirika. Ushirika katika ndoa ulipasa wanyama na ndege. Mtu alitukuzwa mno kuliko mnyama. Huchukiza akiishi katika maisha duni. Ilipasa watu wa wakati ujao katika Afrika, Asia na Janibu kuishi katika maisha bora ya utu, na kuifanya dunia mahali pa kiasi, sio ulafi na uchafu. Mwanamume hakukusudiwa kuwa fahali wa kila mtamba, wala mwanamke kuwa tembe la kila jogoo.

Ushirika wa ndoa ulipofanikisha na uvundo wa kuchukiza duniani, ndugu zake walinyamaza kimya kama walioridhika, lakini moto ulikuwa ukiwaka mioyoni mwao. Usiku Adili alipokuwa amelala na jahazi inakwenda mbio kwa pepo za omo, ndugu zake walikuwa macho. Mawazo mabaya hurusha usingizi. Kuzinduka kwake usingizini Adili alijiona amechukuliwa hangahanga. Kufumbua macho aliona ndugu zake wamemfunga kifati. Mmoja alimshika kichwani na mwingine miguuni. Koo yake ilisongwa sana. Aliwauliza kwa pumzi nyembamba aliyoweza kuvuta neno walilotaka kumtendea.

Alijibiwa , "Huss, fedhuli wee! Wauliza neno ulijualo. Koma sasa! Tumesalitika na mapenzi ya mwanamke aliyeko chomboni. Tumekushauri kumwoa shirika. Umekataa. Huna budi kufa."

Alitoswa baharini kama kitu kilichokuwa hakifai.

Adili aliyageukia manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea. Manyani yaliziba nyuso kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 11

Wokovu wa Adili

Adili alipotupwa alizama kama jiwe katika kilindi cha bahari ambacho urefu wake haukutambulikana. Viwambo vya masikio yake vililia akadhani maji yalipenya sikio hata sikio, na mianzi ya pua yake ilijaa maji yaliyozuia pumzi. Macho yake yalipofumbuka vimemeta kama nyota mbinguni vilionekana katika maji, vimemeta hivyo vilifanywa na mtikiso wa mwili wake. Kutumbukia baharini usiku wa giza ni hatari ya kutisha sana.

Kasi ya kutupwa ilipokoma alijitatamua akakata vifungo vya kamba iliyotatizwa mwilini mwake. Sasa mikono na miguu yake ilianza kufanya kazi. Nusu ya nguvu yake ilikuwa imetumika, lakini matumaini yake yalikuwa kamili. Adili alikuwa si mkata tamaa, na kabla pumzi yake haijakwisha alikusudia kuebuka. Jaribu lake lilikutana na fanaka, maana kabla moyo wale haujakoma alijiona anaelea juu ya bahari. Aliinua kichwa juu ya maji akahema kwa nguvu kama gari moshi. Kulipopambazuka alikuwa katika bahari iliyoghadhibika kwa dhoruba kali, na halibyake ilikuwa taabani. Kutazama hatari usoni kunavunja moyo wa mtu lakini alijikaza kiume.

Mara ile palikuja ndege aliyekuwa na umbo la kutisha akamwopoa Adili majini. Kama koleo, miguu ya ndege ilimshika kwapani akaruka naye. Fikiri wewe mwenyewe hofu aliyokuwa nayo Adili. Binafsi yake alijiona ameokoka kuliwa na papa akawa chakula cha tai. Ndege mwenyewe alipaa juu mpaka Adili alipotelewa na fahamu. Fahamu yake ilipomrudia alijiona katika nyumba kubwa sana iliyokuwa nzuri ajabu. Wasichana warembo na walio changamka walikuwa watumishi katika nyumba hiyo . Miongoni mwao palikuwa na bibi mmoja aliyejipambanua kama malkia, huyo alikaa juu ya kiti cha enzi kilichopambwa na majohari mbalimbali. Rangi ya mavazi yake ilikuwa fua, na kichwani alivaa taji lililopigisha moyo mshindo kwa uzuri.Yule ndege alikuwapo, lakini mara ile alijigeuza msichana wa utanashati mkubwa. Msichana mwenyewe alikuwa yule aliyezama ardhini, baada ya kuokolewa na Adili, alipokuwa katika umbo la tandu na kushambuliwa na nyoka jabalini.

Malkia alimwuliza msichana mtu aliyemwokoa baharini alikuwa nani, na kwa nini aliletwa mbele yake.

Msichana alieleza kuwa mtu yule alikuwa mfadhili wake mkubwa. Zamani maisha yake yalipokuwa katika hatari ya nyoka alipata wokovu kwake. Alimwokoa na kumleta mbele yake kwa sababu aliahidi kulipa fadhili yake.

Kusikia vile, Malkia alisimama akampa mkono Adili aliyeupokea huku amepiga magoti chini. Malkia alimwinua akamkaribisha kuketi kitini akisema, "Starehe, mwanangu. Hali yako ni hali yetu".

Kisha msichana alimwuliza Adili kama aliweza kumtambua yeye alikuwa nani. Adili alijibu kuwa hakuweza.

Msichana alieleza kuwa yeye alikuwa tandu katika jabali fulani zamani akakaribia kuuwawa na nyoka, lakini aliokolewa.

Adili alikubali kuwa alikumbuka kuona tandu jeupe, nyoka mweusi, na msichana aliyezama ardhini.

Tandu lilikuwa yule msichana. Naye alikuwa Huria binti Kisasi. Kisasi alikuwa mfalme wa Majini. Aliyekaa kitini alikuwa mama yake. Jina lake lilikuwa Mjeledi, Malkia wa Majini. Nyoka aliyepigana naye Huria alikuwa waziri wa Ngazi. Alijulikana kwa jina la Hunde. Hunde alikuwa kiumbe cha mwisho katika wanaume waliokuwa na sura mbaya. Siju moja katika matembezi Huria alikutana na Hunde. Alikuwa hatazamiki kwa ubaya, licha ya yeye kumtazama mtu. Pale pale Hunde aliingiwa na shauku kubwa juu ya Huria. Wanawake hukutana na mikasa mingi mibaya duniani. Mioyo yao hulemewa na haja zisizokubalika; masikio yao hutiwa uziwi kwa maombi ya haraka; na miili yao ni mawindo ya jeuri daima.

Hunde alikwenda kwa Kisasi kumposa Huria. Kisasi alijibu Hunde alikuwa ni sufu kwa binti yake ijapokuwa alikuwa waziri wa Ngazi, na kwamba asingalithubutu mbele yake haja kama ile. Tangu siku ile alikomeshwa tamaa ya kuposa mabinti wafalme. Aliudhika akatisha kumwonyesha Huria uwezo wake. Na tangu alipotisha hivyo hakumpa nafasi hata ya uzi kupenya tundu la sindano.

Kila mahali Huria alipopita , Hunde alifuata nyayo zake mpaka aligundua alikokuwa. Iliendelea hivyo mpaka Kisasi akapigana naye. Alishindwa akakimbia. Huria alipotaka kutembea alijigeuza umbo la mnyama. Kila alipojigeuza na yeye alijigeuza vile vile akanusa harufu yake kama mbwa. Alipojigeuza panya, yeye alikuwa paka, alipojifanya paka, yeye alijigeuza chui; na alipokuwa chui, yeye akawa simba. Kila alipoingia yeye alipajua kwa kufuata nyayo zake. Wanaume wana inda mbaya ufisadi unapowapofusha.

Siku aliyojigeuza tandu , yeye alikuwa nyoka akamfukuza. Alipochoka kukimbia alimkamata. Kabla hajamhasiri, Adili alimpiga jiwe akafa. Alijigeuza mtu akaonekana na Adili kwa macho yake. Kabla ya kujizamisha chini aliahidi kulipa wema kwa Adili.

Huria aliomba dua siku zoye ya kuweza kutimiza ahadi yake kwa Adili. Siku aliyotoswa baharini na ndugu zake alikuja upesi kumwokoa katika hatari. Ilipasa wazazi wake, Mfalme na Malkia wa Majini kumkirimu mfadhili wake.

Alimwambia mama yake kwa deni alilowiwa na Adili lilikuwa kubwa sana. Hakudai lilipwe lote lakini lipunguzwe kama lilivyowezekana.

Mjeledi alimwambia Adili kuwa wema wake haukuoza. Kwa kumwokoa Huria aliwatendea wazazi wake fadhili na heshima kubwa nchi ya Majini. Ilikuwa zamu yao kumkirimu walivyoweza sasa.

Adili aliyenyamaza kwa muda mrefu alijibu, "Deni langu limekwisha lipwa lote. Niliokoa maisha ya binti yako, naye ameokoa yangu. Hapana deni tena kati yetu."

Malkia wa Majini alitabasamu akasema, "Usiseme kikembe mwanangu. Wema wako ulikuwa asilia, nawe ulitangulia kuutenda; wa binti yangu ulikuwa wa kuigiza, naye ameutenda nyuma. Asili na uigaji ni vitu mbalimbali. Havilinganiki wala havitalinganika milele."

Adili alipelekwa katika hazina ya majini iliyokusanya utajiri wote wa ulimwengu. Johari ndogo katika hazina hiyo ilikuwa na uzito usiochukulika kwa Adili. Alipochaguzwa kuchukua alichopenda hakuweza kuchagua kitu chochote.

Malkia alisikitika akasema, "Haidhuru!" Alishika simu akauliza" Naweza kusema na mfalme wa majini?"

Jibu lilikuja , " Naam, Kisasi huyu! Nani mwenzangu?" " Mjeledi , Malkia wa majini ndiye asemaye. Adili amechaguzwa apendacho katika hazina yetu, lakini ameshindwa kuchukua hata kitu cha uzito wa sindano moja. Wanadamu hawajaweza kutumia uwezo waliopewa kama Majini. Nataka msaada wako."

" Vema. Mlete hapa," kengele iliishilia.

Adili alikwenda katika halmashauri ya Majini. Alipofika mfalme alikuwa amekaa kitini kwa juu kuelekea hadhara kubwa ya mawaziri. Joho la mfalme lilikuwa la rangi ya fua, na kichwani alivaa taji la zari. Mawaziri walivaa majoho meusi, na vichwa vyao vilikuwa wazi. Hadhara nzima ilisimama Adili alipotokeza . Ilipokaa kitako tena alipewa kitabu cha hawala ya hazina ya majini. Kwa kila hawala iliyoandikwa na kutiwa sahihi ilipochomwa Adili aliweza kupata alichotaka katika hazina ya majini. Alifurahi kwa zawadi ile. Ilikuwa nyepesi kuwekeka, rahisi kutumika, nayo si nzito kuchukulika. Alimshukuru mfalme wa majini akarudi kwa Huria.

Adili aliyageukia Manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea . Manyani yaliziba nyuso zao kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 12

Nduguze kuwa Manyani

Baada ya Adili kutoswa, nahodha alishtuka akauliza nini kilichotumbukia baharini kwa kishindo kikubwa. Kusikia vile ndugu zake walianza kujiliza uongo kuwa ndugu yao amepotea. Nahodha alikwenda kutazama akaona Adili hayuko. Aliamuru kutua tanga na kuteremsha mashua. Lakini sasa dhoruba kali ilianza, na chombi kilichokuwa katika mrama mkubwa, kwa mawimbi makubwa ya upepo na umande, kilipakia maji, omo na tezi, na kulia ja kushoto. Giza kuu lilinyemelea roho za mabaharia. Palikuwa hapatiliki nanga. Kwa hivi tamaa ya kumuokoa Adili ilikatika.

Nahodha alipotaka kujua Adili alivyopotea, ndugu zake walimwambia kuwa ndugu yao aliamka akaenda msalani. Ghafula walisikia anguko kubwa majini. Watu wote jahazini walisikitika kupotelewa na Adili. Ndugu zake walilizana kitambo wakanyamaza. Kilio cha kujisingizia hakina machozi wala matanga.

Hasidi na Mwivu walichukua sanduku la Adili wakalifungua. Walitoa majohari yote wakagawana mafungu mawili usiku ule ule. Sasa ugomvi kati yao ulianza juu ya yule msichana mzuri aliyekuwa chomboni. Hasidi alitaka kumwoa, na Mwivu kadhalika alitaka kumwoa. Asiyefurahia heri ya mwenziwe, shari yake kumghadhibikia. Walimsahau ndugu yao aliyepotea dakika chache zilizopita kama aliyekufa miaka kumi iliyopita. Walikuwa na mioyo migumu iliyoje!

Mwelekevu, yule msichana mzuri, alikuwa hana tabasamu. Uzuri wake ulisawazika kwa machozi ya njia mbili usoni. Huzuni ilimshika vibaya, lakini alikuwa imara kutetea heshima yake. Aliwaambia wale ndugu wawili wasigombane bure. Hakuwa tayari kuolewa na yeyote kati yao. Na kabla ya sauti ya maneno aliyosema haijaishilia masikioni mwao, alijitosa baharini akatoweka vile vile.

Hasidi na Mwivu hawakujua la kutenda. Atakaye makaa ya mgomba hapati kitu ila jivu tupu. Ndugu hawa wawili walimtosa ndugu yao kwa tamaa ya kupata msichana , lakini walipata aibu tupu. Walikaa kitako wamefedheheka, walipokuwa katika hali hiyo na jahazi inakwenda mbio, Huria na Adili walitua ghafula kama ndege chomboni.

Marejeo ya Adili yalishangaza watu chomboni. Macho ya ndugu zake yalisutana. Kwa kutahamaki walimkumbatia wakajifanya kumfariji. Walisema hatari yake ilitisha, na msiba wao ulikuwa mkubwa. Watu wengine wote chomboni waligeuza macho yap kando waliposikia uongo wa ndugu zake. Walakini Adili aliwashukuru akisema bahari haiweki amana ya kitu kieleacho, kwa kuwa alielea aliokoka.

Kwa hasira kubwa Huria alinena, "kama mngalijua hatari ya kumtosa mtu baharini, au mngalikuwa na fikira za msiba, msingalijaribu kumtumbukiza ndugu yenu baharini alipolala. Wauaji ninyi hamstahili kuishi," aliwashika shingoni pamoja na mkono wa kushoto akawabana kwa nguvu ya ajabu. Mkono wake wa kulia uliinua ngumi juu tayari kuwaangukia kwa uzito mwingi. Ndimi vinywani na mboni machoni mwao zilitoka kwa hofu wakataka kuombewa.

Damu nzito kuliko maji. Hasidi na Mwivu walikuwa damu kwa Adili . Hakuvumilia kuona hilaki yao akamwomba Huria kuwasamehe. Walimtosa tu, hawakumwua. Huria alibisha kuwa walistahili kifo. Jaribu la jinai lilitosha kuhalalisha adhabu ha kifo ujinini. Adili alitaradhia kuwa jaribu la jinai halikutosha kuhalalisha kifo duniani. Kama walikufa kwa sababu yake angalikuwa mnyama wa mwitu mbele ya macho ya watu. Huria aliposikia maneno hayo alinena sheria ya wanadamu ilitatiza. Kwa sababu hiyo walikuwa hatarini milele. Walakini alikubali kuwasamehe kwa sharti ya kuwageuza wanyama. Aliwalaani watoke katika umbo la uanadamu. Mara ile ndugu zake walikuwa manyani.

Kisha Huria aliwakabili watu waliokuwa chomboni akasema. Adili alikuwa rafiki yake mkubwa. Alimjali na kumheshimu juu ya marafiki zake wote. Alipata upendo wake kwa sababu alikuwa salihi na mstahiki wa kuajabiwa na dunia nzima. Ataonana naye mara kwa mara. Mtu yeyote akifitini ataona nguvu ya mkono na uwezo wa ulimi wake. Atampatiliza kama alivyofanya kwa waovu wale wawili. Wajihadhari wapatw kujiokoa kwa sababu alikusdia kutimiza alivyosema. Aliwaonya pia watakapofika kwao wasisemw habari ile. Mtu yeyote atakayejaribu kunong'ona habari ile atakoma kusema milele.

Aliagana na Adili akasema, "Funga manyani haya kwa kamba . Ukifika Jannibu utayafunga kwa minyororo viunoni mbalimbali. Utayatia chumbani na kila moja lifungwe peke yake. Kila usiku wa manane utachukua kiboko ukafungue kila nyani ulipige mpaka lizimie. Utayapa posho na kuyaadhibu hivi daima. Kama amri hii haikutiiwa utaadhibiwa wewe." Alipokuwa akitoa amri hii alijibadilisha sura za ajabu kila dakika moja. Watu wote jahazini walishikwa na mshangao mkubwa kwa mabadiliko yake ya mfululizo, wakatosheka kuwa aliweza kubadili kitu chochote katika umbo alilotaka.

Adili aliyageukia manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea. Manyani yaliziba nyuso kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
SURA YA 3.


Adili Mbele ya Rai


Uso wa Ikibali ulikuwa na haya na moyo wake ulijaa hisani. Alikuwa tayari kutumika kama alivyotakiwa na mfalme, lakini alichelea kuwa haini kama siri aliyotoa ilikuwa maangamizi ya Adili. Alijuta ulimi wake haukuwa na nadhari. Hapana roho mbinguni wala duniani isiyopatwa na majuto. Tuna busara nyingi sana baada kuliko kabla ya neno kufanyika. Kama taratibu ya msaada haikufaulu, Ikibali hakupenda kumkabili Adili. Wakati ule ule hakuweza kughairi dhima yake. Ugomvi baina ya hiari na dhima ulianza moyoni mwake. Mambo haya mawili hayatimiziki mara moja. Hapana mtu awezaye kwenda njia mbili wakati mmoja. Kwa hivi, Ikibali alitii mahitaji ya dhima yake akaenda janibu.


Adili alipoona Ikibali amerudi alishtuka. Alisema moyoni mwake ataokolewa katika uovu aliolazimishwa lakini hakuupenda kuutenda. Baada ya hayo alimuuliza Ikibali neno lililomrudisha ghafla Janibu. Ikibali alijibu asingalirudi ghafla vile, lakini katika jitihada yake ya kutenda wema ametenda nuksani. Alikuwa hana udhuru wa kujitetea katika lawama lake. Ulimi wake mwenyewe umemponza. Aliungama alipofika Janibu mara ya kwanza alishawishika kumpeleleza Adili siku tatu. Kila usiku alipokwenda kuadhibu manyani, yeye alimfuata nyuma. Aliporudi nyumbani kulala, yeye alitangulia mbele. Mambo aliyotenda kwa manyani yalikuwa ajabu kwake. Hakupata kuuliza sababu yake. Aliporejea Ughaibu alizungumza habari zile kwa mfalme. Mfalme aliposikia alimrudisha janibu kumchukua Adili na manyani yake.


Adili alikuwa mwema na msamehevu. Alibaini kama Ikibali alilaumika kwa kufichua siri, kadhalika yeye mwenyewe alilaumika kwa ukatili. Tafakuri ilimwonyesha Adili kuwa ukali wa mbwa huyokana na msasi. Mbwa wa msasi mkali ni wakali pia. Rai alikuwa mfalme mwadilifu. Ilijuzu Ikibali, mjumbe wake, kuwa mchunguzi hodari. Mambo yaliyogunduliwa yalikuwa kweli. Mambo yenyewe hayakumpendeza Adili mwenyewe, licha ya mfalme na mjumbe wake. Kipawa kimoja katika vipawa bora kwa mwanadamu ni ujuzi wa maovu. Adili alibarikiwa kipawa hiki. Alishukuru kuwa siri iliyogunduliwa imefika katika masikio ya mfalme. Adili mwenyewe alitaka ijulikane, lakini alichelea kuwa haini kwa mfadhili wake. Madhali imefichuka alikuwa tayari kuithibitisha.


Adili alijiandaa kwa safari ya kuitika mwito wa mfalme. Farasi watatu walitandikwa matandiko mazuri. Yeye alipanda farasi mmoja na mmoja kwa kila nyani. Ikibali alipanda farasi wake mwenyewe. Farasi wa Adili na yule wa Ikibali walikwenda sambamba njiani. Nyuma yao yaliandama manyani juu ya farasi. Kila mtu aliyeona manyani yamepanda farasi alistaajabu. Mnyama kupandwa na mnyama ilikuwa upeo wa miujiza kwa watu. Vinywa vya umati wa watu vilikuwa wazi kwa kivumo cha Lo salala! Wakati umefika wa mawe kusema, miti kujibu na wanyama kuwa watu! Ikibali aligeuza uso wake kwa Adili akasema kwa ucheshi. "Mbwa wanatubwekea kama walionusa mtara wa windo." Adili alikubali kwa kuinamisha kichwa akatabasamu, walisafiri hivi mpaka Ughaibu. Baada ya kutua Adili alipelekwa mbele ya mfalme na manyani yale.


Manyani yalipomwona mfalme yalifanya ishara mbili. Kwanza yaliinua juu mikono yao kama yaliyokuwa yakiomba, pili yalilialia kama yaliyodhurumiwa. Ishara ya kwanza ilionyesha ombi la msaada, na ile ya pili ilionyesha mashtaka. Licha ya Rai, hata mimi na wewe tungalifasiri hivi kama tungalikuwa katika baraza hiyo. Mfalme alipoona vile alitaka kujua kwa Adili sababu ya kuadhibiwa, kulishwa na kunasihiwa manyani yale kila usiku. Katika sababu zake alionywa kusema kweli tu. Adili alijibu kuwa waungwana hawasemi uongo. Atasema kweli, na manyanai yatakuwa mashahidi. Maneno yake yakiwa uongo, yatakanushwa na manyani kwa mguno, lakini yakiwa kweli, manyani yatayathibitisha kwa kuziba nyuso kwa viganja vya mikono yao. Sasa kisa baada ya kisa juu ya manyani kilisimuliwa
Utamu njoo uongo kolea
 
SURA YA 13.

Adhabu ya Kwanza.

Baada ya kutoweka kwa Huria. Adili alikwenda ngamani kumtazama Mwerekevu. Hakiona mtu. Alipouliza aliambiwa alijitosa baharini ndugu zake walipomkalifu kumuoa. Adili hakuweza kujizuia, akaanguka chini kwa huzuni. Moyo wake ulifumwa kwa msiba akalia kama mtoto mdogo.

Uzuri aliotetea kwa thamani ya maisha yake ulipotea. Aliona wokovu wake haukumfaidia. Bahati ilikuwa mbaya na katili sana kwake. Alifikiri kwamba yeye peke yake ndiye aliyepatwa na ajali mbaya kama ile tangu kuumbwa kwa dunia. Adili aliwaza hivyo, haijulikani mtu mwingine angewazaje.

Kulipokucha chombo chao kilitia nanga Janibu. Matajiri walipanda chomboni wakaamkiana na Adili. Walizungumza mambo mengi, lakini hapakuwa na mtu hata mmoja aliyeuliza habari za ndugu zake. Hili lilimshangaza akamaizi kuwa walio aili walikuwa hawana nafasi katika kumbukumbu za dunia.

Alishuka pamoja na manyani yake akaenda zake nyumbani kwake. Baada ya kuyaweka chumbani alijishughulisha na kupakuwa mali yake. Hakuwahi kutafuta minyororo ya manyani siku ile, na usiku alisahau kuyapiga akalala. Saa saba usiku Huria alitokea na hasira imemjaa tele. Alisema kuwa alikuwa jini. Neno la jini halirudi. Kwa kukosa kutii amri yake adhabu ya kwanza ilimpasa Adili.

Kabla Adili hajajibu neno, mikono yake miwili ilikuwa katika mkono wa kushoto wa Huria. Hakuweza kuponyoka. Kwa mkono wa kulia Huria alimpiga Adili kibao mpaka akazimia. Ndipo alipokwenda yalipokuwa manyani akiyapiga kiboko vile vile mpaka yakakaribia kufa.

Alimrudia Adili aliyekuwa anaanza kupata fahamu akasema, “Twaa kiboko hiki, utayapiga manyani haya kesho usiku kama nilivyofanya. Siku moja ikipita bila kuyapiga, kiboko hiki kitaishia mwilini mwako.” Macheche ya moto yaliyoka kinywani mwake alipokuwa akiamuru hili, na mara neno la mwisho lilipotamkwa alitoweka.

Siku iliyofuata Adili alikwenda kwa sonara akatengeneza minyororo miwili ya dhahabu. Aliileta nyumbani mwaka akaifunga viunoni mwa manyani yake. Usiku alipokwenda kuyapiga na kuyaposha machozi yalimlengalenga machoni.

Katika ini alifumwa na mshale, na moyoni mwake michomo ya maumivu makali. Hakupendelea kuadhibu wanyama waliokuwa kwanza ndugu zake. Huruma yake ilikuwa lakini ilikalifiwa na amri.

Huria alijua huruma ya Adili na kuwa alimkalifu sana. Lakini ndugu zake walikuwa waovu, katili, hiani na wauwaji wa kutisha. Walikosa fikra wakawa duni Kama wanyama wa porini. Adhabu kali kwa waovu ilikuwa ndiyo ulinzi peke yake ya wema. Jini ililiona hivyo, haijulikani mtu angalionaje.

Siku nyingi zilipita, Adili alidhani labda adhabu ya Huria ilikwisha. Siku moja hakuyapiga manyani yake. Loh salale! Dhahama gani? Alijuta kuzaliwa akatamani ardhi ipasuke ajitie ndani yake. Alipigwa kiboko siku hiyo kuliko siku ya kwanza. Mwili wote ulienea makato ya kiboko akavuja damu mpaka akazirai.

Aliteremsha mavazi aliyovaa mpaka kiunoni akaonesha makovu ya mapigo ya Huria. Wepesi wa maumbile wa kuondoa alama haukuweza kufuta makovu ya Adili. Yalijionyesha wazi wazi mwilini mwake.

Toka siku ile na baadaye, hakusahau maumivu ya mapigo yale. Kwa muda wa miaka kumi hapakupita tena hata siku moja aliyoacha kuyapiga manyani yake. Kwa huruma yake kila baada ya kuyapiga aliyanasihi akilia:-

“Nala sumu ndugu zangu
msambe naona tamu,
Takalifu kubwa kwangu,
Kuadhibu yangu damu,
Sina raha ndugu zangu,
Neno hili kwangu gumu.”


Mwisho wa ushahidi, Adili aliyageukia manyani akauliza kama yaliyosemwa yalitokea au hayakutokea.
Manyani yalijiziba nyuso kwa viganja vya mikono yao kwa aibu.
 
Kipindi cha mama na mwana RTD! Simulizi hii niliisikia hapo kwa mara ya kwanza.
 
SURA YA 14.

HARUSI

Adili alipolala mtingisho mkubwa ulitokea chumbani mwake sakafu ikapasuka. Kuzinduka uso wake ulikutana na uso wa Huria. Wa kwanza ulijaa matumaini, wa pili ulituna kwa hasira. Nyuso zao zilisomana. Kila uso ulijaribu kuzua mzungu wake.

Adili alivunja amri aliyopewa mara tatu. Alionekana alizoea kuhalifu. Kukomeshwa mazoea yake alipasa kugeuzwa nyani kama ndugu zake. Walakini, kabla ya hili kuwa Huria alitaka kusikia kama Adili alikuwa na udhuru wa kujitetea.

Adili hakusema, lakini tabasamu ya mvuto mwingi ilikuwa ikicheza usoni mwake. Alichukua barua ya Rai akampa Huria. Huria aliposoma barua hakuweza kufanya alilokusudia. Alitoweka akaenda ujinini kumshauri baba yake.

Barua ya Rai ilipowekwa mbele ya Kisasi, kuopolewa kwa ndugu zake Adili kuliridhiwa. Huria alimwuliza Mfalme wa majini labda haja ya Mfalme wa wanadamu isingakubaliwa ingalikuwaje. Baba alieleza.

Mfalme wa wanadamu aliweza kufanya dhara aliyotaka kwa majini. Alikuwa mwanadamu. Mwanadamu alikuwa bora kuliko jini. Majini katika Jua, Mwezi, Mushtara, Zebaki, Zuhura, Mirihi, Sumbla, Zohali, Sarateni, Kausi na Utaridi hayakuweza kushindana na watu katika ardhi.

Majini yaliweza kugeuza watu watu katika umbo lolote, lakini watu waliweza kufunga majini yote katika chupa moja. Magereza yao yalikuwa mabaya sana. Kama mtu asingalikuwa mzembe mwenyewe, busara ya jini ingalikuwa busara yake. Alipasa kuheshimiwa kama alitaradhia heshima yake.

Mara ile Huria alirudi kwa Adili akatangaza kuwa haja ya Rai ilifaulu. Mfalme wa majini alikubali ndugu zake kuwa watu tena.

Aliyabadili manyani akasema, “Tokeni katika uhayawani mrudi katika utu.” Walikuwa watu tena, wakajiangusha miguuni mwa ndugu yao kuomba radhi. Adili alimshukuru Huria, na punde wakaagana.

Asubuhi watumishi walimwona bwana wao na watu wawili. Waliwatambua kuwa walikuwa ndugu zake. Walipouliza kuwa walikuwa wapi kwa muda mrefu, bwana alijibu kuwa walikuwa manyani yaliyoonekana jana yakila naye. Walifurahi kumuona bwana wao si mkichaa, wakamwombea azidishiwe furaha katika maisha yake.

Baada ya kustaftahi aliwavika ndugu zake nguo ali ali, akapanda nao farasi kwenda Ughaibuni. Liwali Adili alipofika Ughaibu na habari kuwa manyani yake yalikuwa watu tena palikuwa na furaha kubwa sana. Jitihadi na kufaulu kwa Rai kuliandikwa katika kumbukumbu za dunia. Hasidi na Mvivu walipoletwa barazani kila mtu aliajabia sura zao. Walikuwa wazuri ajabu.

Mfalme wa Ughaibu alimsifu Adili kuwa alikuwa sababu kubwa ya wokovu kwa ndugu zake katika dhima ya wanyama.

Mateso yaliyompata yalishinda uvumilivu wa mtu. Alivumilia mateso mengi kwa ajili yao. Alikuwa mwanamume barabara na fahari ya Ughaibu. Nchi yake ilimsifu hivi, haijulikani nchi yangu au yako ingalimsifiaje mtu wa namna ile.

Alipogeuka kwa ndugu zake Adili, Rai alionya kama wavivu wajitahidi kuwa hodari, ilikuwa kinyume hodari kuwa mvivu. Kama waovu walitaka kuwa wema, ilichukiza wema kuwa waovu. Kama masikini walitafuta utajiri, ilikuwa ujinga matajiri kufuja walichokuwa nacho. Kama mbegu kidogo iliongezwa mchanga, ilikuwa uharabu mtu kuua ndugu yake. Pia ilikuwa aibu kubwa sana kwa wazuri kutenda maovu.

Wakamilifu walikuwa na nafasi kubwa duniani kuliko wapungufu. Maonyo ya Mfalme yalikuwa mwanana, lakini yalishinda mioyo ya watu waliokusudiwa kuonywa.

Walimshukuru wakaahidi kuwa walikoma kutenda dhara kwa ndugu yao, na kwa kitu chochote kilichokuwa na maisha. Ahadi hii haikuvunjwa.

Mawe huwa dhahabu,
au johari na chuma.
Na mtu anapotubu,
dhambi yake kukoma.
Nidhani zake thawabu,
na heshima ya daima.


Adili alipanda farasi akarudi Janibu na ndugu zake. Njiani alikutana na mabibi watatu waliopanda farasi vile vile.

Mabibi wenyewe walikuwa wazuri na watanashati sana. Wa kwanza alikuwa Mwelekevu aliyeokolewa na Mrefu. Macho ya Adili na ya Mwelekevu yalipokutana mioyo ya giza ilijaa nuru tena. Wote wawili walishuka chini wakaamkiana.

Aha, ilikuwa furaha kubwa iliyoje! Mioyo miwili ya mapenzi iliyopoteana ilikutana tena. Neno halikuwezekana kusemeka. Walitazamana wakachekana. Walishikana mikono wakabusiana. Walikuwa katika siku bora ya maisha yao.

Adili alipomwambia Mwelekevu kuwa wavulana wawili watanashati aliokuwa nao walikuwa ndugu zake, Mwelekevu kadhalika alisema kuwa wasichana wawili warembo aliofuatana nao walikuwa marafiki zake.

Watu wote wanne walishuka chini wakaamkiana vile vile. Kisha wote walipanda farasi wao wakashika njia kuelekea Janibu.

Walipofika palifanywa harusi tatu siku moja. Siku hiyo ilikuwa kubwa kuliko yoyote iliyopita Janibu.
 
Back
Top Bottom