Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,829
MTUNZI: SHAABAN ROBERT.
WACHAPISHAJI : Tanzania Publishing House. Dar es Salaam.
SURA YA 1
Mfalme Rai
Rai, mfalme wa Ughaibu , alikuwa mfalme namna ya peke yake duniani. Alikuwa na tabia iliyohitilafiana kabisa na tabia za watu wengine wa zamani zake. Tabia yake ilijigawa katika theluthi tatu mbalimbali kama rangi ya ngozi ya punda milia. Kwa theluthi ya kwanza alikuwa msuluhifu akapendwa na watu, Kwa theluthi ya pili alifanana na Daud akaheshimiwa kama mtunzaji mkuu wa wanyama, na kwa theluthi ya tatu alikuwa kama Suleiman akatiiwa na majini. Kutawala suluhu na mapenzi ya wanadam, utunzaji wa wanyama, na utii juu ya viumbe wasioonekana kama majini hutaka uwezo mkubwa sana. Kwa hivi, fikiri wewe mwenyewe jinsi Rai alivyojipambanua mwenyewe na wafalme wengine.
Katika miliki ya mfalme huyu kodi ilitozwa juu ya mifugo ya wanyama. Kodi hii ilihalalishwa kwa sababu Ughaibu ilikuwa nchi ya mifugo. Ughaibu ilipokuwa juu ya kilele cha usitawi mifugo yake ilikuwa hailingani kwa ubora na mifugo ya nchi yoyote nyingine ulimwenguni. Fahari yake ya mifugo ilikuwa kubwa kabisa. Fahari hiyo haikuwezekana kukadaika ikatazamwa kwa wivu katika dunia nzima.
Malipo ya kodi hii yalifanywa kwa wanyama waliozaliwa pacha. Kila zizi lilitozwa pacha moja kila mwaka. Mazizi yaliyokuwa hayana wanyama waliozaliwa pacha katika mwaka uliodaiwa kodi yalisamehewa. Zizi lililoshindwa kulipa kodi lilitokea kwa nadra sana kwa sababu mifugo yote ilikuwa mizazi ya ajabu. Zilipatikana pacha katika mbuzi, kondoo, ng'ombe, farasi, na wanyama wengine.
Masurufu ya serikali ya Ughaibu yalitegemea katika juu ya wanyama wake. Kwa sababu hiyo kila zizi katika nchi lilihesabiwa kama hazina maalum, na kila mnyama katika zizi hilo alikuwa kama johari hasa. Mazizi yaliyopotelewa na mifugo yake kwa maradhi yalijazwa tena wanyama wapya. Masikini waliotaka mifugo, lakini waliokuwa hawana njia ya kuipata, walikidhiwa haja zao na serikali bila malipo yoyote. Basi mifugo ilienea katika nchi yote ya Ughaibu.
Kwa masurufu haya na misaada kama hii uangalifu wa mfalme juu ya wanyama wa mifugo ulikuwa hauna kiasi wala kadiri, na huruma yake juu ya wanyama wasiokuwa wa mifugo ilishawishika sana.
Rai alikuwa kiongozi muadilifu na mfalme mwema sana. Hakusita kufanya kazi ndogo wala kubwa kwa mikono yake mwenyewe. Kazi nyingi za ufalme alizitenda yeye mwenyewe. Zile ambazo hakuwahi kuzitenda yeye mwenyewe alipenda kuziona kwa macho yake zilivyofanywa. Kwa bidii zake kubwa aliweza kushiriki katika mambo mengi ya maisha akasaidia maendeleo makubwa ya nchi yake.
Hakulazimisha mtu yeyote kutenda tendo fulani, lakini alishawishi kila moyo wa mtu kuiga alivyotenda kwa hiyari yake mwenyewe. Alikuwa na mvuto mkubwa juu ya mioyo ya watu. Alitumia mvuto huu juu ya watu mpaka nchi yake ilikuwa haina mvivu, goigoi wala mwoga.
Kuondoa uvivu , ugoigoi na woga katika nchi ni kazi ngumu. Mambo haya yanapendwa sana na watu ingawa yana madhara makubwa kwao. Kwa hivi, kufaulu kwa Rai kulistahili sifa kubwa sana. Sifa yake ilifurahiwa na viumbe wote. Malaika mbinguni waliitungia mashairi; ndege hewani waliimba kwa sauti zao nzuri; wanadamu duniani waliisimulia kwa hadithi; majini na mashetani waliikariri kwa tenzi. Rai alikuwa mtu mmoja katika watu bora waliopata kutoka tumboni mwa mwanamke. Alifanya urafiki na viumbe mbalimbali kwa sababu aliwajali wote.
Ilikuwa si desturi ya Rai kusema maneno na kuacha watu wengine watende matendo, lakini alitenda matendo akaacha watu wengine waseme maneno. Tendo hukidhi haja maridhawa kuliko neno. Haja ikishughulikiwa kwa matendo hupatikana upesi, lakini ikishughulikiwa kwa maneno huchelewa kama sadaka. Rai alifaham haya lakini watu wake hawakufaham. Hawa walipaswa kuamshwa katika usingizi wao kwa matendo, sio kwa maneno. Maisha ya Rai yalipita katika matendo mbalimbali.
Katika hukumu alikuwa imara sana. Hakupendelea mkubwa wala hakudhulumu mdogo. Watu wote walikuwa sawasawa mbele ya sheria. Hakuuza haki za watu kwa rushwa. Wanadamu na wanyama walioata haki zao katika baraza lake. Hili ndilo tendo moja katika matendo yake ambalo limetia jina lake katika makumbusho yasiyosahaulika katika wakati wake, sasa na baadae katika wakati ujao duniani. Kila mtu alipoiga matendo ya mfalme yabisi katika nchi alifukuzwa.
Rutuba ilienea kila mahali. Kwa rutuba hii ardhi ya Ughaibu ilikuwa na rangi ya kahawia. Juu ya ardhi hii paliota mimea iliyofanana za zabarijudiwa uzuri. Mimea hii ilie eza neema ya vyakula kwa watu na malisho ya wanyama. Hewa ya nchi nzima ilinukia manukato kwa naua mazuri ya mimea mbalimbali.
Siku moja Rai alipokuwa akitazama hesabu za wanyama waliokusanywa kwa kodi, aliona karibu mazizi yote katika miliki yake yamekwisha lipa kodi zake ila mazizi ya Janibu. Ugunduzi huu uliamsha wasiwasi mkubwa uliokuwa ukingojea mguso mdogo tu katika moyo wake. Moyo wake ulipokuwa ukiliwa kwa wasiwasi, mawazo mbali mbali yalipita katika akili yake. Alidhani kuwa labda Janibu imepatwa na mwaka wa kiu, na kuwa malisho ya wanyama yameharibika.
Labda sotoka imeshambulia mazizi katika nchi, na kuwa vifo vingi vimetokea katika mifugo. Kwa kuwa wanadamu na wanyama wana shirika moja katika maisha, Rai alihamasika sana. Aliona dhahiri kuwa madhara ya wanyama ni hatari kwa watu vile vile. Rai alikuwa na akili tambuzi iliyopenya katika mashaka mengi ya maisha. Walakini, hizi zilikuwa dhana tu. Dhana zenyewe zilikuwa haziwezi kusaidia kujibu ugunduzi wake. Palikuwa hapana kitu kilichoweza kuzithibitisha.
Ughaibu na Janibu ilikuwa miji miwili mbalimbali chini ya miliki moja. Miji hii ilitengwa na umbali mkubwa. Ugunduzi wa Rai katika hesabu ya kodi ulifasiri upungufu ambao haukutazamiwa. Sababu ya upungufu ule haikujulikana kwa sababu habari za Janibu zilikosekana. Pasipo shaka, hukubalika bila ya swali kuwa miji miwili ina ina ndoto mbili zenye maana mbalimbali.
Rai aliweza kujua tafsiri ya ndoto ya Ughaibu kuwa jumla ya kodi ilikuwa na kasoro, lakini hakuweza kujua maana ya ndoto ya Janibu, yaani sababu ya kasoro ile. Mambo katika maisha yamo katika mwendo huu siku zote. hmHayajulikani mpaka yamechunguzwa na kuthibitishwa kwanza. Rai alikuwa mtu arifu wa mwendo huu. kwa hivi, shauri hili liliachwa kwa Maarifa, Waziri Mkuu, kuchunguzwa.
WACHAPISHAJI : Tanzania Publishing House. Dar es Salaam.
SURA YA 1
Mfalme Rai
Rai, mfalme wa Ughaibu , alikuwa mfalme namna ya peke yake duniani. Alikuwa na tabia iliyohitilafiana kabisa na tabia za watu wengine wa zamani zake. Tabia yake ilijigawa katika theluthi tatu mbalimbali kama rangi ya ngozi ya punda milia. Kwa theluthi ya kwanza alikuwa msuluhifu akapendwa na watu, Kwa theluthi ya pili alifanana na Daud akaheshimiwa kama mtunzaji mkuu wa wanyama, na kwa theluthi ya tatu alikuwa kama Suleiman akatiiwa na majini. Kutawala suluhu na mapenzi ya wanadam, utunzaji wa wanyama, na utii juu ya viumbe wasioonekana kama majini hutaka uwezo mkubwa sana. Kwa hivi, fikiri wewe mwenyewe jinsi Rai alivyojipambanua mwenyewe na wafalme wengine.
Katika miliki ya mfalme huyu kodi ilitozwa juu ya mifugo ya wanyama. Kodi hii ilihalalishwa kwa sababu Ughaibu ilikuwa nchi ya mifugo. Ughaibu ilipokuwa juu ya kilele cha usitawi mifugo yake ilikuwa hailingani kwa ubora na mifugo ya nchi yoyote nyingine ulimwenguni. Fahari yake ya mifugo ilikuwa kubwa kabisa. Fahari hiyo haikuwezekana kukadaika ikatazamwa kwa wivu katika dunia nzima.
Malipo ya kodi hii yalifanywa kwa wanyama waliozaliwa pacha. Kila zizi lilitozwa pacha moja kila mwaka. Mazizi yaliyokuwa hayana wanyama waliozaliwa pacha katika mwaka uliodaiwa kodi yalisamehewa. Zizi lililoshindwa kulipa kodi lilitokea kwa nadra sana kwa sababu mifugo yote ilikuwa mizazi ya ajabu. Zilipatikana pacha katika mbuzi, kondoo, ng'ombe, farasi, na wanyama wengine.
Masurufu ya serikali ya Ughaibu yalitegemea katika juu ya wanyama wake. Kwa sababu hiyo kila zizi katika nchi lilihesabiwa kama hazina maalum, na kila mnyama katika zizi hilo alikuwa kama johari hasa. Mazizi yaliyopotelewa na mifugo yake kwa maradhi yalijazwa tena wanyama wapya. Masikini waliotaka mifugo, lakini waliokuwa hawana njia ya kuipata, walikidhiwa haja zao na serikali bila malipo yoyote. Basi mifugo ilienea katika nchi yote ya Ughaibu.
Kwa masurufu haya na misaada kama hii uangalifu wa mfalme juu ya wanyama wa mifugo ulikuwa hauna kiasi wala kadiri, na huruma yake juu ya wanyama wasiokuwa wa mifugo ilishawishika sana.
Rai alikuwa kiongozi muadilifu na mfalme mwema sana. Hakusita kufanya kazi ndogo wala kubwa kwa mikono yake mwenyewe. Kazi nyingi za ufalme alizitenda yeye mwenyewe. Zile ambazo hakuwahi kuzitenda yeye mwenyewe alipenda kuziona kwa macho yake zilivyofanywa. Kwa bidii zake kubwa aliweza kushiriki katika mambo mengi ya maisha akasaidia maendeleo makubwa ya nchi yake.
Hakulazimisha mtu yeyote kutenda tendo fulani, lakini alishawishi kila moyo wa mtu kuiga alivyotenda kwa hiyari yake mwenyewe. Alikuwa na mvuto mkubwa juu ya mioyo ya watu. Alitumia mvuto huu juu ya watu mpaka nchi yake ilikuwa haina mvivu, goigoi wala mwoga.
Kuondoa uvivu , ugoigoi na woga katika nchi ni kazi ngumu. Mambo haya yanapendwa sana na watu ingawa yana madhara makubwa kwao. Kwa hivi, kufaulu kwa Rai kulistahili sifa kubwa sana. Sifa yake ilifurahiwa na viumbe wote. Malaika mbinguni waliitungia mashairi; ndege hewani waliimba kwa sauti zao nzuri; wanadamu duniani waliisimulia kwa hadithi; majini na mashetani waliikariri kwa tenzi. Rai alikuwa mtu mmoja katika watu bora waliopata kutoka tumboni mwa mwanamke. Alifanya urafiki na viumbe mbalimbali kwa sababu aliwajali wote.
Ilikuwa si desturi ya Rai kusema maneno na kuacha watu wengine watende matendo, lakini alitenda matendo akaacha watu wengine waseme maneno. Tendo hukidhi haja maridhawa kuliko neno. Haja ikishughulikiwa kwa matendo hupatikana upesi, lakini ikishughulikiwa kwa maneno huchelewa kama sadaka. Rai alifaham haya lakini watu wake hawakufaham. Hawa walipaswa kuamshwa katika usingizi wao kwa matendo, sio kwa maneno. Maisha ya Rai yalipita katika matendo mbalimbali.
Katika hukumu alikuwa imara sana. Hakupendelea mkubwa wala hakudhulumu mdogo. Watu wote walikuwa sawasawa mbele ya sheria. Hakuuza haki za watu kwa rushwa. Wanadamu na wanyama walioata haki zao katika baraza lake. Hili ndilo tendo moja katika matendo yake ambalo limetia jina lake katika makumbusho yasiyosahaulika katika wakati wake, sasa na baadae katika wakati ujao duniani. Kila mtu alipoiga matendo ya mfalme yabisi katika nchi alifukuzwa.
Rutuba ilienea kila mahali. Kwa rutuba hii ardhi ya Ughaibu ilikuwa na rangi ya kahawia. Juu ya ardhi hii paliota mimea iliyofanana za zabarijudiwa uzuri. Mimea hii ilie eza neema ya vyakula kwa watu na malisho ya wanyama. Hewa ya nchi nzima ilinukia manukato kwa naua mazuri ya mimea mbalimbali.
Siku moja Rai alipokuwa akitazama hesabu za wanyama waliokusanywa kwa kodi, aliona karibu mazizi yote katika miliki yake yamekwisha lipa kodi zake ila mazizi ya Janibu. Ugunduzi huu uliamsha wasiwasi mkubwa uliokuwa ukingojea mguso mdogo tu katika moyo wake. Moyo wake ulipokuwa ukiliwa kwa wasiwasi, mawazo mbali mbali yalipita katika akili yake. Alidhani kuwa labda Janibu imepatwa na mwaka wa kiu, na kuwa malisho ya wanyama yameharibika.
Labda sotoka imeshambulia mazizi katika nchi, na kuwa vifo vingi vimetokea katika mifugo. Kwa kuwa wanadamu na wanyama wana shirika moja katika maisha, Rai alihamasika sana. Aliona dhahiri kuwa madhara ya wanyama ni hatari kwa watu vile vile. Rai alikuwa na akili tambuzi iliyopenya katika mashaka mengi ya maisha. Walakini, hizi zilikuwa dhana tu. Dhana zenyewe zilikuwa haziwezi kusaidia kujibu ugunduzi wake. Palikuwa hapana kitu kilichoweza kuzithibitisha.
Ughaibu na Janibu ilikuwa miji miwili mbalimbali chini ya miliki moja. Miji hii ilitengwa na umbali mkubwa. Ugunduzi wa Rai katika hesabu ya kodi ulifasiri upungufu ambao haukutazamiwa. Sababu ya upungufu ule haikujulikana kwa sababu habari za Janibu zilikosekana. Pasipo shaka, hukubalika bila ya swali kuwa miji miwili ina ina ndoto mbili zenye maana mbalimbali.
Rai aliweza kujua tafsiri ya ndoto ya Ughaibu kuwa jumla ya kodi ilikuwa na kasoro, lakini hakuweza kujua maana ya ndoto ya Janibu, yaani sababu ya kasoro ile. Mambo katika maisha yamo katika mwendo huu siku zote. hmHayajulikani mpaka yamechunguzwa na kuthibitishwa kwanza. Rai alikuwa mtu arifu wa mwendo huu. kwa hivi, shauri hili liliachwa kwa Maarifa, Waziri Mkuu, kuchunguzwa.