Adhabu kubwa ya mpenzi anayekusaliti

kuchangumu

JF-Expert Member
Apr 2, 2014
724
290
Wanaume wengi wanapobaini kuwa wapenzi wao wanawasaliti, hutunisha misuli kuonesha umwamba kwa kuwatwanga makonde wapenzi wao au kuwafanyia mbaya wale waliowanasa.

Lakini uchunguzi niliofanya unaonesha kuwa ubabe haukomeshi tabia ya usaliti.Kuna wengi ambao waliwafumania wake zao, wakawapiga na kuwajeruhi, lakini wakajikuta hawakukomesha tatizo,

zaidi ya kuwapa usugu wapenzi wao wa kuendeleza wizi tena kwa dharau na kejeli huku wakibembelezana kwa maneno haya: "mzushi kaenda kazini njoo sasa hivi Wapendanao Gesti" au "vipi yule bwegge alikuuliza jana ulipochelewa kurudi" Jamaa anaweza kumuuliza hivyo mke au mpenzi wa mtu.

Adhabu nzuri ya mpenzi anayekusaliti ni kumnasa live kwenye usaliti wake kisha kumpuuza huku wewe ukiendelea na mambo yako kama kawaida, ukifanya hivyo utakuwa unamtibu ugonjwa wake wa kupenda penda hovyo na hii ndiyo dawa hasa ya kumponya msaliti, lakini pia inasaidia kupunguza maumivu ya penzi. Kumchunga na kumlilia machozi hakusaidii.
Karibuni!
 
Hata mie nimewahi mkuta demu wng live saa saba usiku,na kondomu iliyotumika ipo kama hapo.Daaa nilitoa somo kwa kuwaeleza maisha yapo vipi na matokeo yake pia.

Then nikasepa,alipata tabu sn yuke demu,alikuwa akiwaza nilivokuwa naishi naye anapoteza fahamu.Mama yake akaniita but nilimficha kabisa,ili kuokoa maisha yake nilijifanya kumsamehe but badaye alijiongeza.
 
hii adhabu ni mbaya sana kuna mama mmoja jirani yangu alikimbia ndoa yake ya miaka 10 baada ya kufumaniwa na mumewe hakuuliza chochote sanasana akazidi kumpenda aliondoka mwenyewe mpaka leo hajarudi

Naww unadhan utafanyiwa hivyo?
 
Adhabu nzuri ya mpenzi anayekusaliti ni kumnasa live kwenye usaliti wake kisha kumpuuza huku wewe ukiendelea na mambo yako kama kawaida, ukifanya hivyo utakuwa unamtibu ugonjwa wake wa kupenda penda hovyo na hii ndiyo dawa hasa ya kumponya msaliti, lakini pia inasaidia kupunguza maumivu ya penzi. Kumchunga na kumlilia machozi hakusaidii.
Karibuni!

Mkuu ukitangaza msimamo huo utachapiwa monday to monday. Binadamu wa siku hizi dhamira zao zimefilia mbali!!
Unamfumania macho makavu kama mwizi aliyekabwa na msosi kooni. Utabaki ukiimba "ukiwa mjanja kuchapiwa ni siri ya ndani" huku ukijiona booonge la mjanja

Kama hasimami kwenye misingi ya ndoa piga chini
 
adhabu ni kumuonesha upendo zaidi, haina haja ya kupiga wala kufukuza hautatatua tatizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom