Aden Rage:Mpango wa kujenga uwanja umeishia wapi/

Aden Rage:Mpango wa kujenga uwanja umeishia wapi/

Nakapanya

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2012
Posts
2,096
Reaction score
709
Mwenyekiti wa klabu ya simba Ndg Rage aliahidi wana msimbazi kuwa watajenga uwanja kwa ajili ya klabu ya simba,akasema kwamba Waturuki bdio watakaojenga uwanja na wakati huo walikua wakifanya upembuzi yakinifu.
Ninchojiuliza je huo upembuzi yakinifu ulishafanyika?kama tayari mnasubiri nini kuanza kujenga uwanja?na kama bado je huoni umetudanganya wana msimbazi?

NB;Ndugu wana jamvi kwa jinsi mambo yanavyoenda katika klabu kuna uwezekano kweli wa uwanja kujengwa?
Pongezi za dhati kwa watani zetu wa jangwani kwa hatua waliyofikia na nina waombea nia yao itimie na isjekuwa porojo kama za Bwana Rage. indoor.jpg
 
Nilishasema mara nyingi kuwa huyu ndugu ni mwongo. hakuna cha uwanja wala nini. Nenda Bunju kama utakuta uwanja wanaosema upo kwa ajili ya uwanja wa kisasa wa Simba
 
Huyu ndugu mamneno mengi sana,analeta siasa kwenye mpira,bora angeondoka tupate wtu makini watakaoipeleka mbele klabu yetu.
 
ahadi aliyoitoa bwana Rage ni kwamba upembuzi ungekuwa umekamilika tangu mwaka jana,sasa ninchouliza je huo ipembuzi yakinifu bado unaendelea au ndo Utopian kama kawa?
 
pongezi kwa yanga kwani wameshaanza kujenga? Wote ni wale wale
 
Rage aache kutengeneza uwanja wake wa kujifunzia shabaha za bastola awajengee simba uwanja?
 
Hivi ile mall aliyosema kuwa ataijenga tabora kabla ya 2015 imeanza kujengwa??
 
Huyo rage ni mwizi tu na mwanasiasa mpuuzi.
 
ahadi aliyoitoa bwana Rage ni kwamba upembuzi ungekuwa umekamilika tangu mwaka jana,sasa ninchouliza je huo ipembuzi yakinifu bado unaendelea au ndo Utopian kama kawa?

Wadau wangekuwa siriaz wangehoji kuhusu pesa aliyotumia Rage na Kaburu kwenda Uturuki kusaini mkataba wa upembuzi yakinifu.
 
Tanzania kila kitu kimejaa Siasa sababu viongozi wa mpira ndio wale wale wanasiasa, ukienda kwenye Elimu the Same sasa mnategemea nini na hawataki kuwa achia wengine!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom