PreGE2025 ACT Wazalendo yamtaka Msajili wa Vyama vya Siasa kumchukulia hatua Makalla kauli ya CHADEMA kutaka kupandikiza M-Pox na Ebola nchini

PreGE2025 ACT Wazalendo yamtaka Msajili wa Vyama vya Siasa kumchukulia hatua Makalla kauli ya CHADEMA kutaka kupandikiza M-Pox na Ebola nchini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,410
Reaction score
4,988
Chama cha ACT Wazalendo kimemwandikia rasmi Msajili wa Vyama vya Siasa malalamiko dhidi ya Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amosi Makalla kutokana na matamshi yake ya madai kuwa CHADEMA kinaendesha harambee ya kununua virusi vya M-pox na Ebola kwa lengo la kuzuia uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Katika barua rasmi ya tarehe 24 Machi 2025 iliyotumwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ambayo Jambo TV tumepata kuiona, Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu, ameeleza kuwa kauli ya Makalla ni "ya kizembe, isiyo na msingi na inayoweza kuzua taharuki kwa jamii."

"Kauli hii haitakiwi kutafsiriwa kuwa ni hujuma dhidi ya CHADEMA pekee, bali ni kauli inayohujumu nchi kitaswira na kiuchumi," amesema Ado Shaibu katika barua hiyo.

Kwa mujibu wa ACT Wazalendo, kauli kama hiyo inaweza kuwa na athari kubwa kwa sekta ya utalii na uwekezaji nchini kwa kuwa inajenga hofu kuhusu usalama wa kiafya wa Tanzania kimataifa.

Katika maombi yao kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, ACT Wazalendo wanapendekeza Makalla ajieleze kuhusu kauli hiyo, kufuta kauli hiyo hadharani, kuomba radhi kwa umma na hatua nyingine za ziada zinazoweza kuchukuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa.

Pia soma
 
Back
Top Bottom