ACT Wazalendo mlishiriki kubariki dhuluma ya uchaguzi uliopita; mshirika wenu anawaonesha rangi yake sasa, vumilieni

ACT Wazalendo mlishiriki kubariki dhuluma ya uchaguzi uliopita; mshirika wenu anawaonesha rangi yake sasa, vumilieni

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,009
Reaction score
6,763
Maandiko yalikuwa ukutani, wakayapuuza.

Mazingira ya kisiasa , Vyombo vya dola, tume ya uchaguzi, sheria n.k vyote vilikuwa si rafiki sawa na hapo awtu ali lakini ACT Wazalendo walichagua kushiriki kubariki uchaguzi uliyopita na kuwapa CCM uhalali ambao waliuhitaji sana,wakati ACT wote wakitarajia matokeo tofauti. Mlifuata tamaa ya madaraka ya Maalim Seif, mkashindwa kuchagua rafiki.

Nyie Kila siku mnapigwa, MNAVUNJWA NYONGA bado mnang'ang'ania SERIKAKI YA UMOJA hampo serious au mnataka wawauwe yawatokee tena kamaya Pemba 2020 au 2000 ndio mjue CCM ni Ile ile but hatuwashangai kwakuwa mlikubali kujiunga SERIAKLI YA UMOJA wakati mgumu wa Shujaa aliyeapa kuumaliza Upinzani ikifika 2020.

Eti walihakikishiwa kuwa "maridhiano yameanza". sasa sijui process hiyo ya kuridhiana inaendelea vipi. Watuambie Mtu anakuvunjia uhuru na haki zako,anakunyanyasa katika nchi yako mwenyewe wakati unaugulia anakuita anakwambia "turidhiane" na wewe unaamini. MAAJABU.

Leo Mgombea wenu huko Konde ametoka nje baada ya majumuisho akilalamika kudhulumiwa.

#TumeHuru
Huko Mbagala jana mawakala wenu na viongozi wamekamatwa kisa kusanyiko. Leo Mgombea wenu Mbagala amejeruhiwa na mnadai ni vyombo vya dola.

#Vyombovyadola
Majuzi katibu wa uenezi wa CCM Bwana Shaka kamvaa Makamu wa kwanza wa Rais na kumshambulia, kumkejeli na kumshurutisha asipowaunga mkono ajiuzulu. Yaani kwa Level ya makamu wa Rais kiprotokali hakuna hata Kiongozi mmoja wa kitaifa aliyekemea.

Kwa kweli hii ni maana ya wendawazimu.






 
ACT wana uhuru wa kushirki uchaguzi kama nyie CDM mlivyokuwa ana uhuru wa kukataa kushiriki
 
Huko Konde wamedhulumiwaje? ungetuweka wazi kulikokuzungumzia udhahania
 
Huko Konde wamedhulumiwaje? ungetuweka wazi kulikokuzungumzia udhahania


Mkuu halafu sikusema wamedhulumiwa bali wamelalamika kuwa wamedhu...
 
Ndoa na iheshimiwe na pande zote, vipigo toka kwa mume isiwe sababu ya kumrudisha mke nyumbani.
 
Back
Top Bottom