wilchuma
JF-Expert Member
- May 16, 2013
- 1,102
- 333
Wamefukuzwa tar 31/12/2015, Bandiko limetoka 01/01/2015.
Haya ni maajabu.
ila hii naona ka ilipangwa ila hapa kuna namna ngoja tuone
POWER TO THE PEOPLE
Wamefukuzwa tar 31/12/2015, Bandiko limetoka 01/01/2015.
Haya ni maajabu.
ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPARENCY
ACT- TANZANIA.
MAKAO MAKUU OFSI YA UENEZI NA MAHUSIANO YA JAMII
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT-Tanzania, Kadawi Lucas Limbu, kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya ACT-Tanzania, ametengeua uteuzi wa Thomas Matatizo, kuwa mwanasheria wa chama kuanzia leo, tarehe 1 Januari 2015.
Mwenyekiti wa ACT-Taifa, amefuta uteuzi huo kwa kutumia ibara ya 37(w) (vi) ya Katiba ya ACT-Tanzania.
Bw.Thomas Matatizo ametenguliwa uteuzi wake kutokana na kujipa mamlaka ya kufanya kazi asizotumwa na chama, kushirikiana na wanaokidhoofisha chama na kudhihaki maamuzi halali ya kikao yaliyofanyika jana tarehe 31 Desemba 2015 lakini atabaki kuwa mwanachama na mjumbe wa kamati.
Katika kikao hicho, Kamati ya watu 11 iliyopewa mamlaka ya kuongoza chama kwa mujibu wa sheria Na. 5 ya vyama vya siasa ya mwaka 1992, iliamua kumvua uwanachama, aliyekuwa Katibu Mkuu wa ACT, Samson Mwigamba, Mshauri wa chama Prof. Kitila Mkumbo na wanachama wengine kutenguliwa nafasi walizokabidhiwa kwa nia ya kukieneza chama lakini badala yake wanatumia nafasi hizo vibaya kukigawa na kukihujumu chama
Kwa taarifa hii, tunawaomba umma wa Watanzania kokote waliko, kutosikiliza kauli na vijineno vitakavyotolewa na Bw. Matatizo au Mwigamba. Kauli halali na thabiti ya chama itatolewa na mwenyekiti au yule ambaye amempa mamlaka.
Aidha chama chetu hakijampa mamlaka ya kuthibitisha wala kubatilisha maamuzi ya vikao mtu yeyote, bali sheria mama ya chama yaani katiba ndiyo inaelekeza mamlaka yenye uwezo wa kufanya hivyo.
Grayson Nyakarungu,
Katibu Mwenezi - ACT, Tanzania.
0755 023 503
Nimeanza kuamini katika majina sasa, kama ilivyo kwa Hawa 'Ghasia', na Kitila 'Mkumbo' na sasa huyu bwana Thomas 'Matatizo'. Sidhani kama hawajakaribisha matatizo.
Ova
At least umekuja na argument tofauti segwanga ZZK ni mjanja sana na anajua kucheza na karata zake ameona sasa majeraha yake ya kisiasa yanapona na anaanza tena kukubalika CDM/UKAWA ameamua kukiua ACT na kuwatosa wale wote aliokuwa nao tangu mwanzo
Amesoma upepo na ameona yeye kung'ara nje ya CHADEMA ni ngumu kaamua kutengeneza mazingira ya kikiua chama na afanye patano na chama CHADEMA for his future political life
Siasa za Tanzania ni ngumu sana
Ha ha ha ha!Nashukuru mimeshaitika wito nipo.Mkuu.... Nguruvi3..nilitaka kukuuita bahati....nzuri umefika karibu sana...Naukumbuka mjadala uliouongoza kule kwenye JUKWAA LA GT wachache tulikuelewa lkn kuna watu watoa Povu nyingi natamani utupie Link tujikumbueshe....!!
Hawa ACT hawana tofauti na wajomba zao Chadema.
Kuna kirusi kinasafishwa, hii ni baada ya failed plan A, then kinaletwa UKAWA, huku kwa kushirikiana na mmoja wa mhimili mkuu wa UKAWA, kazi imekwisha October,2015.
Wamefukuzwa tar 31/12/2015, Bandiko limetoka 01/01/2015.
Haya ni maajabu.
Tafadhali Zito rudi zako chadema