KIBE unawahukumu madaktari kana kwamba wanachodai ni pesa peke yake. Je, unayajua madai yao yote?
Mojawapo ya madai yao ni kuwapo kwa vifaa tiba na madawa kwenye hospitali, pamoja na vitanda vya kutosha na nyenzo nyingine muhimu.
Hapo wanadai pesa kwa ajili yao? Kama umesahau, kuna daktari wa Hospitali ya Wilaya ya Temeke alinukuliwa na vyombo vya habari kwamba alilazimika kumwacha mgonjwa kwenye chumba cha upasuaji na kutoka nje kukimbilia hadi kwenye duka la dawa ambalo kulikuwa na kifaa tiba kilichogharimu SHILINGI ELFU MOJA TU!
Alitumia pesa yake mwenyewe kuokoa maisha ya mgonjwa. Labda wewe hujawahi kuumwa hadi kulazwa na kufanyiwa upasuaji. Waheshimu sana madaktari. Hakuna kazi ngumu kama ya kumtibu binadam, MUUJIZA wa Mwenyezi Mungu.
KUJAFA HUJAUMBIKA
KIBE!