Utotole
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,608
- 4,265
Wapo watu wengi wamesoma kuliko hata hao wanaolipwa milioni 50...lakini kwa kuwa hawakubahatika kujuana na mkubwa, wataishia kwenye milioni 7 tu. Na hao watu wanayo nafasi kwenye mashirika na taasisi za umma kama hao hao wanaolipwa. Ukitaka kutumia kigezo cha uzalishaji kwamba ndicho kipange nani analipwa kiasi gani unakuwa na akili kama za mkulu wetu wa zamani kidogo...ambaye ndiye huyo aliyekwenda kusomba 'rafiki zake' huko nje ya nchi eti waje wamsaidie 'kuendeleza' Tanzania kwa makubaliano ya malipo makubwa kulingana na standards za huko Ulaya na Marekani.Wenye wivu mzuri, akiona mwenzie anapata kipato kizuri kwa sababu ya kusoma na yeye anaenda kusoma!!
Si kila sekta inazalisha (directly), na hatuwezi kusema kuwa kwa kuwa huyu anashughulika na shirika au taasisi isiyozalisha basi hana umuhimu. Katika sekta ya umma, kila mtu ana mchango wake. Kama ingekuwa ni hivyo basi tungevunja shule zote maana hazizalishi. Hata hospitali tungebomoa maana ni huduma tu, na madaktari hawana umuhimu kwa mtazamo wenu maana hawazalishi, isipokuwa wafanyakazi wa shirika la nyumba ndio wana umuhimu kuliko walimu na madaktari...halafu tungeona mwisho wake. nahisi kwa mtazamo wenu tungepata maendeleo sana nchi nzima ikiwa TPDC, TRA na NHC...akili hizi zina matege.
Tusidanganyane, mtu kulipwa pesa nyingi US (kwa conversions za bongo) haimaanishi kwamba yeye ni exceptional. Ikumbukwe kwamba hata bartender au mhudumu supermarket US anaweza kuwa na kipato kikubwa kuliko hata profesa wa bongo...ni standard ya maisha ya huko. Walioko huko ughaibuni na wabaki huko huko maana malipo ya huku hayawezi kuwaridhisha kwa haki. na hata huo mchango wao si kwamba ni wa ajabu sana. nina hakika wapo wengi wenye uwezo huo. Ni nia tu na dhamira imekosekana kuiendeleza nchi hii maana kila mmoja anataka atafune tu provided meno anayo.
