ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,592
Habarini wanajamvi wenzangu
Ni matumaini yetu kuwa tu wazima na tunaendelea na pilikapilika za
sikukuu ya Pasaka ,na mambo mengine kiujumla,
Leo nimependa kusema nanyi hususani ndugu zetu hawa na jamaa
zetu, wengine ni marafiki zetu wa karibu sana katika maisha yetu.
Jambo la leo ambalo nimeonelea nizungumze nanyi ni kutokana na
mfumo au niseme desturi na mila za baadhi ya kabila zetu hapa TZ
Mila zetu zimetufanya tuwe na mfumo mbovu wa maisha hususani
kuendekeza kuzifuata hata kama hizo mila na desturi zinapotosha
imekuwa ni desturi ya maisha yetu kwa ujumla, Jambo ambalo
nataka kuliongelea hapa ni TOHARA kwa WANAUME. Mila nyingi
hususani katika mikoa mingi hawatahiriwi eti ni kuenzi mila na
tamaduni zao. Mila nyingi zimekuwa potofu hasa zile za kusema
mtoto wa kike anatahiriwa, hii ni mila potofu ambayo huleta mau-
aji na maangamizi kwa watoto wetu wa kike. Nilikuwa sitaki
kuongelea wanawake zaidi hapa ila nimejikuta kuongea tu kutokana
na hii mada hapa.
Leo nimependa kuwafunda wanaume kutokana na mila hizi ambazo
wamezilea na kuzipenda na kuzitelekeleza, mila nyingine kama hizi ni
uchafu uliokithiri. jamani wewe uliona wapi mwanaume hatahiriwi.
si kuleteana uchafu mnamo faragha.
Mila zingine ni upotofu na uchafutu, wewe kwa akili zako unathubute
kutokutahiriwa kwa ajili ya usafiwako na mwenzako pia, huoni
unamuambukiza magonjwa mwenziowakati wa faragha jamani.
Sijafurahishwa na mila na tamaduni hizindo mana nimeonelea
leo niwafunde wanaume hasa vijana ambao hamjaingia katika
NDOA mjifunze na kuondoikana na upotofu huu.
na dhana hii ya kutokutahiriwa. Wewe kijana kama hujaenda
kutahiriwa nenda hospitali kashughulikiwe ili uwe msafi. Jamani onen
i ni aibu kwa kutokutahiriwa, na ni ashamed pia kaka zangu, vijana na
ndugu zangu sio busara kabisa kutokufanya jambo hilo.
Lady nimependa leo niwafunde kidogo kuhusu jambo hili kwani ni
hatari kwa afya zetu na ni uchafu kutokutahiriwa.
NAWATAKIA MAANDALIZI MEMA YA SIKUKUU YA PASAKA
NAWAPENDA NA MSINICHUKIE KWANI MM NI MSAIKOLOGIST
POKEENI ZAWADI HII YA PASAKA KWENU
View attachment 88337View attachment 88338View attachment 88339
Seconded.Agreed, medically here are some of the benefits of male circumcision:
1. Hygiene - simpler or easier to wash the penis
2. Cosmetic appearance of the penis
3. Decreased risk of UTI
4. Decreased risk of sexually transmitted infections, including HIV/AIDS by approx 60%. However, safe sexual practices remain essential.
5. Prevention of the penile problems/complications like Phimosis.
6. Decreased risk of penile cancer
7. Decreased risk of carcinoma of the cervix of your female partner!
If you are a man and you are not yet circumcised please go to the hospital to be circumcised!
NATIONALLY:
Percentage of men age 15-49 who reported having been circumcised shows that Practically all men in Zanzibar (99 percent) are circumcised compared with 66 percent in Mainland Tanzania. The prevalence of circumcision is lowest in Shinyanga (21 percent), Rukwa (24 percent), and Iringa (29 percent). Source: THMIS 2007-8.
However the figures may change as today THMIS have released the new findings for the THMIS 2011/12.
Kwa kila jamii lazima iwe na Desturi, mila na utamaduni wake. Kila Desturi, mila na utamaduni ni bora kwa mila husika, na utamadumi huohuo, ukiupeleka katika jamii nyingine, unaweza usiwe bora. Kutokana na mwingiliano wa sasa kijamii, kumetokea mvutano wa tabia, mila, desturi na tamaduni. Hata hivyo, kila jamii hujitahidi kulinda mila zake ili zitawale, wakati jamii nyingine ikijaribu kudhoofisha mila za jamii kinzani. Jamii itakayoshinda, ndiyo hutawala.
Ukija kwenye mada, Sisi huku kwetu, wanaume huwa hawatahiri. Believe it or not, ukipata mwanaume ambaye hakutahiriwa, hutatamani mwanaume kilema (aliyepunguzwa viungo vya mwili). Hii ni kwa sababu, kale ka kofia, hufanya kale ka kichwa kaendelee kuwa sensitive kila kanapoguswa, na pale ndipo ngoma inaponoga. Swala la magonjwa, ni katika zile mila ambazo wanawake kumi huchangia mme mmoja, tabia ambayo huku kwetu ni mwiko. Kwetu hatuna tabia za kuchangia mswaki, wala tabia za mafiga matatu hatuna.
Kwa wale ambao mama hufunda mwana kwa kumwelekeza kuwa figa moja haliinjiki chungu, na vijana husifiwa kwa wingi wa wanawake anaogegeda nje ya ndoa, Hakika kutahiri ni lazima ili kupunguza risk za magonjwa, Ingawa takwimu vilevile zinaonesha kuwa kule wanakotahiri sana, ndiko kwenye maambukizo mengi ya magonjwa.
Dawa ya dhambi ni damu ya yesu na siyo tohara. Naomba utamaduni wenu wa kuwafanya wanaume kuwa vilema kwa kuwapunguzia viungo vya mwili, uishie huko kwenu, na huku kwetu tuendelee kuenzi mila na utamaduni wetu mzuri wa kuwafanya wanaume wetu waishi kama Mungu alivyowaumba. Mungu atujalie tusiingiliwe na utamaduni wa mafiga matatu, wala tusije kuchangia miswaki. Kila mtu awe na mswaki wake, na kila chungu kiinjikwe kwa figa moja.
"WALE WA UTAMADUNI USIOKUBALI UKILEMA, TUJITETEE"
kwa kila jamii lazima iwe na desturi, mila na utamaduni wake. Kila desturi, mila na utamaduni ni bora kwa mila husika, na utamadumi huohuo, ukiupeleka katika jamii nyingine, unaweza usiwe bora. Kutokana na mwingiliano wa sasa kijamii, kumetokea mvutano wa tabia, mila, desturi na tamaduni. Hata hivyo, kila jamii hujitahidi kulinda mila zake ili zitawale, wakati jamii nyingine ikijaribu kudhoofisha mila za jamii kinzani. Jamii itakayoshinda, ndiyo hutawala.
Ukija kwenye mada, sisi huku kwetu, wanaume huwa hawatahiri. Believe it or not, ukipata mwanaume ambaye hakutahiriwa, hutatamani mwanaume kilema (aliyepunguzwa viungo vya mwili). Hii ni kwa sababu, kale ka kofia, hufanya kale ka kichwa kaendelee kuwa sensitive kila kanapoguswa, na pale ndipo ngoma inaponoga. Swala la magonjwa, ni katika zile mila ambazo wanawake kumi huchangia mme mmoja, tabia ambayo huku kwetu ni mwiko. Kwetu hatuna tabia za kuchangia mswaki, wala tabia za mafiga matatu hatuna.
Kwa wale ambao mama hufunda mwana kwa kumwelekeza kuwa figa moja haliinjiki chungu, na vijana husifiwa kwa wingi wa wanawake anaogegeda nje ya ndoa, hakika kutahiri ni lazima ili kupunguza risk za magonjwa, ingawa takwimu vilevile zinaonesha kuwa kule wanakotahiri sana, ndiko kwenye maambukizo mengi ya magonjwa.
Dawa ya dhambi ni damu ya yesu na siyo tohara. Naomba utamaduni wenu wa kuwafanya wanaume kuwa vilema kwa kuwapunguzia viungo vya mwili, uishie huko kwenu, na huku kwetu tuendelee kuenzi mila na utamaduni wetu mzuri wa kuwafanya wanaume wetu waishi kama mungu alivyowaumba. Mungu atujalie tusiingiliwe na utamaduni wa mafiga matatu, wala tusije kuchangia miswaki. Kila mtu awe na mswaki wake, na kila chungu kiinjikwe kwa figa moja.
"wale wa utamaduni usiokubali ukilema, tujitetee"
Dada umeanza kwa ukali sana na imekuwa hivo hadi mwisho, kumbuka unashauri tu na kitu unashauri ni sehemu ya maishaya watu kwa miaka mingi(utamaduni). Watu wanabadirika lakini jua inachukua muda kwa sababu c wote wana access ya kujua hiyo elimu uliyo nayo wewe.
unasema maranyingi MILA ZIMEKUWA POTOFU je zimekuwa potofu kuanzia lini hadi lini? tunatahiri kwa sababu ni mila potofu ama kwa sababu ya ya vitu fulani fulani ambavyo tunadhani tukitahiri tunaweza kujiprotect?
Je kuzaliwa na GOMVI ni mila ama?
Je ni kwanini tunazaliwa na MAGOMVI?
Tatizo la wasomi wa siku hizi na hasa WATANZANIA ni kupokea mambo pasipo kufanya utafiti wa kina kuhusu jambo hilo.
Fuatilia matokeo ya utafiti wa ukimwi na malaria aliyoyazindua Kikwete leo
Ndugu zangu kazi ya mola haina makosa.
hayana ukweli wowote maana hata robo ya popolation hawajapimwaFuatilia matokeo ya utafiti wa ukimwi na malaria aliyoyazindua Kikwete leo