Account in Dollars

Habari wakuu!
1.Nini tofaauti ya current account na Saving account?
2.Je hyo USD account napewa ATM card? Kama ndio ATM kuna $ pia?
3.Nikiwa na $ account kwenye bank naweza nikarusha hela(TT) kununua gari japan? Je cost zake zipo vp? Maana bank nyingine kutuma TT ni 60$
4.Nini faida ya kua na $ acc vs TZS acc?

Mkuu majibu ya maswali yako hivi:
1. Current akaunti ni akaunti ya kibiashara (hufunguliwa na makampuni makubwa na madogo) wakati savings ni akaunti ya mtu binafsi ya kutunza pesa zake. Masharti ya transactions ya pesa yanatofautiana na hapa ni maelezo marefu

2.Kwa uzoefu wangu mdogo, mabenki yetu hayatoi ATM kwa Forex accounts wanakupa kadi tu za kawaida ambapo ni lazima uende kaunta pale unapotaka kuchukua au kuweka pesa

3. Jibu ni ndiyo waweza kurusha USD kutoka akaunti yako moja kwa moja kwenda Japan kununua gari. Gharama zinatofautina kutoka benki moja kwenda benki nyingine, the cheapest ni Bank of India wanaotoza USD 12, CRDB na NMB ni USD 50

4. Faida ya kuwa na USD account Vs Ths account ni kuwa, thamani ya pesa yako inazidi kuongezeka dhidi ya shilingi inayoporomoka kila wakati
 
asante kwa taarifa hii nilikuwa nafikiria kufungua a/c axim bank nimedili mawazo na endelea kutupa feedback zaidi kuhusu hiyo acces bank

Dada Nakshi, bado Exim Bank are better kwenye USD account. Wao kwa mwezi hawa-charge chochote kwenye savings account wakati AcessBank wanacharge USD 1.00. Gharama za kuchukua pesa Exim ni 1% ya kiasi unachochukua na AccessBank wamepandisha kwa sasa ni 1% na si 0.5% kama ilivyokuwa hapo awali. Vilevile Exim Bank kama unalipwa kwa check hawana charges zozote kwenye clearance ya check wakati benki zingine wanalipisha.
 
burudani kabisa
nimefurahia sana darasa hili......surely sikufanya research yangu ya kutosha kabila sijaamua kufungua $$ account. Ngoja nikafunge zangu za NBC na CRDB kumbe wananiibia aisee.......

I must admit nimevutika na Exim Bank, only that naona kila wakati bank hubadili sera zao ambazo sisi wateja inabidi kukubaliana nao no matter what...

But EXIM is good!
 
burudani kabisa
nimefurahia sana darasa hili......surely sikufanya research yangu ya kutosha kabila sijaamua kufungua $$ account. Ngoja nikafunge zangu za NBC na CRDB kumbe wananiibia aisee.......

I must admit nimevutika na Exim Bank, only that naona kila wakati bank hubadili sera zao ambazo sisi wateja inabidi kukubaliana nao no matter what...

But EXIM is good!

Mkuu mimi ilibidi nizunguke mabenki kadhaa kabla ya kufungua akaunti yangu Exim. NBC ndo balaa mkuu kahame fasta. Ukitaka kuwa nazo mbili basi nyingine fungua Bank of India kama uko DAR. Pamoja na kubadilikabadilika kwa gharama za mabenki nimegundua kuwa benki za wahindi are cheaper to operate an account there na hawabadilishi sana charges zao. Nilifunga yangu CRDB miaka 6 iliyopita wakati wanancharge USD 2 kwa mwezi na sasa wamefikisha 5 wakati Exim bado ni sifuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom