Rutunga M
JF-Expert Member
- Mar 16, 2009
- 1,769
- 1,382
Basi la kampuni ya BATCO lililokuwa lilitokea Tarime mkoani Mara kwenda Jijini Mwanza limepata ajali mbaya katika eneo la Pida Kyakabakari mjini Musoma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Philip Kalagi, ameithibitishia JamiiForums kutokea kwa ajali katika eneo la hilo na kwamba basi la kampuni hiyo limepinduka na kuacha njia na kuwa taarifa za awali zimeonyesha wapo majeruhi 17 ambao wamekwisha ondolewa katika eneo la ajali na kupelekwa Hospitalini.
Amesema majeruhi hao wamepelekwa katika Hospitali za Wilaya ya Bunda na Musoma kwa matibabu, na hivyo taarifa kamili juu ya tukio hilo zitatolewa baadae.