Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,630
- 25,586
Huyu kamanda aliwahi kuingizwa kwenye kinyang'anyiro cha wale waliotajwa kuwa angeteuliwa kuwa IGP kwenye utawala wa hayati John Magufuli. Hiyo ni kwasababu huko nyuma tayari alikuwa Naibu wa Ernest Mangu aliyekuwa IGP tangu Mwaka 2013.
Baadaye baada ya kufanyiwa figisu aliendelea na cheo cha Unaibu IGP akipitwa na Kamanda Sirro ambaye aliteuliwa kuwa IGP na hayati Magufuli cheo ambacho kiufundi kilimfanya akae ofisini akisoma magazeti kutwa kucha.
Lakini baada ya hapo zengwe likaendelea cheo cha Unaibu IGP kikafutwa na kwa namna fulani Mwaka 2017 akapewa Ubalozi na akateuliwa na hayati Magufuli akaenda kuiwakilisha Tanzania huko Zambia.
Lakini katika kuangalia makamanda wasomi ndani ya Jeshi la Polisi nimeona huyu kamanda Kaniki anafaa hata kupewa kazi ya mkataba ili asaidie kulirekebisha Jeshi la Polisi kiutendaji na kimtazamo.
Ni msomi mzuri tu wa masuala ya usalama nchini na chapisho la kupata Shahada yake ya Uzamili katika Chuo cha Mafuzo ya Usalama cha "Transnational Crime and National Security: Issues and Options for Tanzania".
Kamanda mstaafu Kaniki ana Shahada ya Kwanza ya Sheria na Shahada ya Uzamili zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shahada ingine ya Uzamili inahusu usalama na Stadi za Kistratejia na pia ana Shahada ya Udaktari wa Falsafa (Phd) kutoka Chuo cha Ulinzi Tanzania.
Mtu kama huyu ni wa kumtumia uzuri kutengeneza Jeshi letu la Polisi kwa kutumia ujuzi wake wa miaka mingi ndani Jeshi hilo na utaalam alionao kutoka darasani.
Kunaweza kufanywa ni kumpatia ajira ya mkataba wa miaka mitatu mitatu huku akiwepo aliye chini yake akijifunza kazi ambaye atachukua nafasi pindi afande mkuu atapomaliza mikataba yake rasmi.
Kwa hali ya sasa kiusalama wa raia na mali zao nchini na matishio ya watu kutekwa na kupotezwa sidhani kama IGP aliepo afaa kuendelea na kazi hiyo.
Baadaye baada ya kufanyiwa figisu aliendelea na cheo cha Unaibu IGP akipitwa na Kamanda Sirro ambaye aliteuliwa kuwa IGP na hayati Magufuli cheo ambacho kiufundi kilimfanya akae ofisini akisoma magazeti kutwa kucha.
Lakini baada ya hapo zengwe likaendelea cheo cha Unaibu IGP kikafutwa na kwa namna fulani Mwaka 2017 akapewa Ubalozi na akateuliwa na hayati Magufuli akaenda kuiwakilisha Tanzania huko Zambia.
Lakini katika kuangalia makamanda wasomi ndani ya Jeshi la Polisi nimeona huyu kamanda Kaniki anafaa hata kupewa kazi ya mkataba ili asaidie kulirekebisha Jeshi la Polisi kiutendaji na kimtazamo.
Ni msomi mzuri tu wa masuala ya usalama nchini na chapisho la kupata Shahada yake ya Uzamili katika Chuo cha Mafuzo ya Usalama cha "Transnational Crime and National Security: Issues and Options for Tanzania".
Kamanda mstaafu Kaniki ana Shahada ya Kwanza ya Sheria na Shahada ya Uzamili zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shahada ingine ya Uzamili inahusu usalama na Stadi za Kistratejia na pia ana Shahada ya Udaktari wa Falsafa (Phd) kutoka Chuo cha Ulinzi Tanzania.
Mtu kama huyu ni wa kumtumia uzuri kutengeneza Jeshi letu la Polisi kwa kutumia ujuzi wake wa miaka mingi ndani Jeshi hilo na utaalam alionao kutoka darasani.
Kunaweza kufanywa ni kumpatia ajira ya mkataba wa miaka mitatu mitatu huku akiwepo aliye chini yake akijifunza kazi ambaye atachukua nafasi pindi afande mkuu atapomaliza mikataba yake rasmi.
Kwa hali ya sasa kiusalama wa raia na mali zao nchini na matishio ya watu kutekwa na kupotezwa sidhani kama IGP aliepo afaa kuendelea na kazi hiyo.