Abdullah Kassim Hanga: Kutoka Kiongozi hadi adui wa mapinduzi ya Zanzibar

kunawakati nakuwa mzito sana kuwatukuza na kywaheshimu hawa wana muungano wawili mzee Karume na Mwl Nyerere kunamambo ya kinyama sana waliyatenda kwa wenzao tena walio wapigania kupata madaraka

Mabaya waliyofanya Hawa Wawili waliyafanya kipindi ambacho habari ilikuwa bidhaa adimu sana!

Unyama wa Hawa Viumbe Wawili ni Mkubwa kuliko wa kina Yahya Jammeh tofauti ni kuwa walimiliki mifereji yote ya habari na kuchuja kila wasichotaka kuwafikia Raia na kweli hakikuwafikia!

Ulikuwa ukiandamwa unauawa na hata Mali chache ulizoacha zinataifishwa kumkomoa Wajane na Mayatima ulioacha! Oscar Kambona alivyokoswa koswa kuzimwa kwa kukimbilia Uingereza basi kuanzia Majumba mpaka Kandambili alizoacha Tanzania zilitaifishwa na mpaka Leo hatujawahi kuambiwa alikuwa na kosa gani?

Kuna Wazee wetu Mungu awarehemu ulikuwa ukiwatajia Hawa watu kwa kukuheshimu basi watakaa kimya wasitie neno kutuudhi lakini unaona wanakaza meno kwa chuki na hasira

Ilitakiwa ikifika April 7 na October 14 kila Mwaka Familia zao ziwe zinatuomba Radhi kwa dhulma zilizofanyiwa Wazee wetu na Hawa watu
 
This is best
Asante sana
RIP
Dr Khasim Hanga
Abdulaziz Twala
Dr Othman Sharif
Saleh Sadaalah
Inaonekana ukiwa msomi ZNZ ya zamani ya Karume ni kujitafutia tiketi ya kifo!Sielewi ilikuaje Mzee Jumbe na Prof Babu wakawa hai hadi wakafa natural cause
 
Jmn jmn hizi siasa hizi! Unau mtu kisa ukae wewe. Je utakaa milele? Ndio maana wakati mwinfine watu wanakufa vifo vya taabu na mateso au watoto wanakuwa mawenge kisa cha mambo wanayotenda. Karume alikufaje? Wengine wanakufa midomo wazi!!!! Wengine macho kaa?????
angalia watoto wa nyerere, sio kosa lao ni laana iliyosababishwa na aliyoyafanya baba/babu yao
 
Mwandishi wa hii makala naweza kumuita mnafiki mno. Kama mtu ukisoma sehemu ya pili ya makala.

Mwandishi, sehemu ya pili, eti anamlaumu hanga kwa kuongoza mapinduzi na anasema pengine alikua anajuta baada ya kusalitiwa, huu ni mtazamo wa kipuuzi sana.

Mwandishi, hanga alifanya mapinduzi ya haki, mapinduzi yaliyofuta ugandamizwaji wa waunguja uliokua Ukifanywa na sultan akishirikiana na vibaraka washenzi ambao ni wapemba.

Usaliti na uroho wa madaraka wa karume ndio uliochukua maisha ya hanga, na wala sio kingine. Karume ni mtu ambaye alikua hajiamini, na kisaikolojia mtu ambaye hajiamini ni rahisi mno kua katili.

Mwandishi, tunajua fika kua mapinduzi ya zanzibar yaliathiri watu wengi, hasa waliokua wananufaika na utawala wa kisultani, ambao bila shaka ni wapemba. Kwahiyo kama wewe ni mwathirika jitahidi upime madhila waliokua wanayapata waunguja(ambao wengi wao walikua weusi), ambao walikua wanalimishwa karafuu kama ng'ombe na kuuwawa hovyo cha kigezo cha utumwa.

Kwa dhana hii ifahamike kua mapinduzi yalikua hayazuiliki!

Mwisho kbsa utaelewa kua mapinduzi yalikua na nia njema, ila viongozi baada ya mapinduzi walikua wana kasoro.
 
Hizo historia tulikuwa hatufundishwi mashuleni. Nimesoma history mpaka A Level, lakini hakufundishwa kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar na wasisi wake. Tulikuwa tunafundishwa zaidi kuhusu uhuru wa Tanganyika.

Ukicheki hata past exams papers, nadra kukuta swali kuhusu mapinduzi ya Zanzibar, maybe just in case, mtu asije akafunguka huko wakati anashuka mapoints. Labda historia ya Mapinduzi ya Zanzibar iliachwa kufundishwa kwenye somo husika ili tujifanyie "homework" wenyewe?
EMT;

Shukrani. Nilimsoma Kassimu Hanga baada ya kununua kitabu cha mtoto wake aliye Urusi. Katika historia ya Tanzania hayumo lakini ni mtu mashuhuri. Mtoto wake alikuja Tanzania, anasema hali aliyokuta bibi yake ilikuwa pathetic.

Kuhusiana na historia ya Tanzania, kulikuwa hakuna uhuru wa kujieleza. Hivyo waandishi wengi wameandika kufuata mistari ya watawala.
 
Huyo mtoto hajutii yaliyomkuta baba bali kaweka pesa mbele
Sijaona juha kama huyo mtoto wa Hanga asemaye babake alikufa ki kawaida. Tena huyo anaweza muua nduguye aliyezaliwa Urusi. Huyo ni wa kuogopwa kama zica.
 
Bora ungeandika kitabu ukauza ukapata pesa maana reeeeeeeeeeeeeefu kati ya watu 10 wawil tu ndo wanaweza kulisoma!!
Wasioipenda hii habari ni wale wasioitaka 'kweli' ya yale mapinduzi ya kinyama, ambayo walioyafanya walijaribu sana kuficha ukweli wake.
 
Asalam Aleikum sheikh Mohamed Said
Nimeku tag hapa kuomba u share na kidago chetu mada uloongelea leo kuhusu mchango wa wanawake katika harakati za kudai uhuru.
Ikiwezekana tuwekee video
Shukran
 
Back
Top Bottom