Abarikiwe aliyemleta Rais Samia Duniani

Abarikiwe aliyemleta Rais Samia Duniani

Ndugu zangu watanzania,

Kwa hakika libarikiwe sana tumbo lililombeba mama Samia, lilibeba mtoto aliyekuja kuwa kiongozi wa Tanzania, kiongozi mwenye upendo, hekima, busara, ukarimu, huruma, unyenyekevu na usikivu.

Kiongozi asiye na makuu wala makidai, kiongozi mwenye kujishusha na kujua kuwa pamoja na madaraka yake makubwa kiuongozi lakini bado anabaki kuwa mwanadamu aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu.

Kiongozi ambaye pamoja na uwezo wake mkubwa kimamlaka lakini anatambua kuwa yupo Mungu ambaye ndiye anayepaswa kuabudiwa na kupewa sifa na utukufu, kiongozi ambaye wakati wote madaraka yamemfuata yeye kutokana na kupewa kibali na Mwenyezi Mungu.

Kiongozi ambaye mikono yake ameinyoosha katika kuwafuta machozi na kuwapatia haki wenye kuonewa, kiongozi ambaye ulimi wake umewaponya na kuwafariji wenye majeraha na makovu.

Ni kiongozi ambaye hajawahi kufurahi wala kuwa tayari kuongoza taifa la watu wanaolia na kububujikwa machozi kwa kuonewa, hajawahi kuwa tayari kimaneno na hata kimatendo kuhubiri uonevu, ukatili, ubaguzi na hata chuki kwa watu.

Ni kiongozi ambaye ulimi wake muda wote ni wenye kutoa maneno ya upendo mshikamano na kujenga umoja wa taifa.

Ndio sababu ya kuungwa mkono na Watanzania wote, ndio sababu ya kupendwa na kuombewa afya njema na nguvu za kuendelea kututumikia Watanzania, ndio sababu ya kusikilizwa na kufuatiliwa sana kwa hotuba zake, ndio sababu ya kuteka hisia na mioyo ya Watanzania, ndio sababu ya kukubalika kwake na makundi yote, ndio sababu ya umaarufu na ushawishi wake kuwa mkubwa sana Tanzania na nje ya mipaka ya Tanzania.

Rais samia ni nuru katikati ya giza, ni tumaini katikati ya waliokata tamaa, ni faraja kwa waliao, ni mpatanishi wa kweli, mpenda haki na mtenda haki, ni Nyota ya alfajiri iletayo matumaini ya pambazuko lililojema.

Ndio sababu ya kila Mtanzania kuwa na matumiani ya pambazuko katika maisha yao na ndoto zao, kila mmoja anao uhakika wa kutimiza ndoto zake na kufikia mafanikio anayoyataka.

Serikali yake imekuwa kwa ajili ya kuwasaidia watu, kuwawezesha na kuwashika mkono katika kufikia malengo yake. Serikali yake haipo kwa ajili ya kumuonea mtu, kumdhuru mtu, kumtesa mtu, kumliza mtu.

Ni serikali safi ya haki yenye matendo mema na hatua njema, ni serikali yenye dhamira ya kuwatumikia watu kwa upendo na uzalendo mkubwa.

Ndio sababu ya kuona mioyo ya Watanzania ikiwa haina hofu wala wasiwasi, kila mmoja anayo amani moyoni mwake, kila mmoja anayo imani na serikali hii, kila mmoja anaridhishwa na utendaji kazi wa serikali ya Rais Samia.

Viongozi aina ya Rais Samia hawazaliwi kila siku wala hawapatikani kila mahali, maana wenye moyo kama wake wa kuweza kumsikiliza kila mtu, kumvumilia kila mtu mwenye kutofautiana nao, wenye kifua kama chake, wenye kusikiliza sauti zote hata zikwaluzazo kwa lugha za ukakasi, kukaa mezani na yeyote, kujumuika na yeyote ni wachache sana.

Viongozi aina yake huja kama mitume kwa ajili ya kuwatumikia watu kwa haki na upendo. Huja wakiwa wameandaliwa na Mwenyezi Mungu, hawaandaliwi na wanadamu wala kwa mipango ya wanadamu, huja wakiwa wamepewa maaarifa na njia za kuongaza.

Mwenyezi Mungu huwapa kila kitu kama ilivyokuwa kwa Musa, huja wakiwa na kibali mkononi cha Mwenyezi Mungu katika ulimwengu wa kiroho. Huja kwa makusudi maalumu, huja kama nyota katikati ya giza, hung'aa na mwanga wao huwa tumaini la watu waitazamayo nyota hiyo, huja wakiwa na majibu ya maswali.

Ndio sababu ya kuona Rais Samia akiwa kipenzi cha Watanzania, ndio sababu ukiona Rais Samia hakauki midomoni mwa Watanzania kwa mema. Amejiandikia ukurasa wake na anaendelea kuandika kitabu chake kitakachosimuliwa vizazi na vizazi kwa mema mengi na makubwa aliyolifanyia Taifa letu yanayobaki kama alama katika mioyo ya watu.

Rais Samia kwake haki ndio kipaombele kwa kuwa anatambua ya kuwa haki huinua taifa. Ni heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi na ufahari wa kidunia.

Rais samia amechagua jina jema kwa kutenda mema kwa Watanzania, yanayomfanya kuwa chaguo la Watanzania kwa muhula wa pili, yanayomfanya apendwe na kuzungumzwa vyema na watu wa makundi yote, rika zote, jinsia zote na vyama vyote.

Rais Samia pamoja na madaraka yake makubwa, ukubwa wa kimamlaka alionao mikononi mwake na katika ulimi wake kikatiba na kisheria, lakini bado anatambua ya kuwa yeye ni mwanadamu na kwamba anayestahili kuabudiwa na kupewa sifa na utukufu ni Mwenyezi Mungu pekee na siyo mwanadamu.

Ndio sababu ya kuwa mnyenyekevu muda wote, mwenye kujishusha na kuwasikiliza watu wote pasipo ubaguzi wala kuwagawa kwa misingi ya ukabila, udini na ukanda, ndio sababu ya kuongoza taifa kwa haki na upendo.

Libarikiwe tumbo lililombeba Rais Samia, maana matumbo mengine yanaleta watu Duniani wanaokuja kuleta mateso kwa watu, uchungu katika maisha ya watu, simanzi kwa watu, machozi kwa watu, maumivu kwa watu, giza katika mioyo ya watu, majeraha na uvuli katika mioyo ya watu, kumwaga damu za watu, kunyonga watu, kuua watu, kukatisha na kuzima ndoto za watu, kushindana na Mwenyezi Mungu anayewapa watu pumzi ya kuishi.

Tujitahidi kutenda mema tukiwa hai kwa kadri tuwezavyo ili matendo yetu yasimame kututetea tukiwa hatuna uwezo wa kujitetea wala kufungua vinywa vyetu. Ya Duniani ni ya kupita tu, yanini kuumizana, kutesana, kukatishana ndoto, kujengeana chuki, kuuwana kwa sababu ya mali au madaraka au vyeo?, nani anazikwa navyo?

Kazi iendelee, Mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Ukiona mtu mzima analamba matako ujue hakuna anachoshindwa kufanya hata kuinamishwa, njaa yako imehama imefika kichwani.
Mkuu hiyo namba ya simu toka umeanza kuiandika mama hajawahi hata kukubip nasikia anapita pita humu au hajaiona uanze kuwa unaiweka juu kabisa
 
Aisee umefika mbali sanaa ankolii.

Inatosha sasa, mvua zimeanza nenda kapande njugu mawe zitakusitiri msimu wa kiangazi haya mambo ya uteuzi yamebuma kubali yaishe, move one.
Ndugu yangu mchambuzi napenda kukwambia kuwa Mimi naishi na kula kwa jasho langu ,kwa kutumia mikono yangu na nguvu zangu, Mimi Ni mkulima ninayejion fahari na heshima kuwa mkulima na kuwaa sehemu ya watanzania wazalendo waliojitolea na kujitoa kulilisha Taifa letu kwa kuhakikisha kuwa chakula kinapatikana kwa wingi na kuwafanya watanzania washibe na Kuendelea na shughuli zao za kiuzalishaji.

Lakini pia kupitia ukulima wangu nashiriki katika kutunza amani na utulivu wa Taifa letu maana huwezi ukamuongoza wala kusikilizwa na mtu mwenye njaa ya chakula,ndio maana unaona watu wakiwa na njaa wapo tayari kuandamana hata mbele ya polisi wenye mitutu ya bunduki,lakini huwezi ukawasikia watu wanaandamana na kuhatarisha maisha Yao kwa ajili ya kudai katiba mpya,hii ndio sababu hata chama chako kimekosa uungwaji mkono katika hoja hii ya katiba mpya katika kuwashawishi watanzania kuwaunga mkono.

Kazi iendeleee,mama yetu Rais Samia Tunamwamini na Tumeamua kuwa Naye Kama Rais wetu mpaka 2030
 
Ukiona mtu mzima analamba matako ujue hakuna anachoshindwa kufanya hata kuinamishwa, njaa yako imehama imefika kichwani.
Mkuu hiyo namba ya simu toka umeanza kuiandika mama hajawahi hata kukubip nasikia anapita pita humu au hajaiona uanze kuwa unaiweka juu kabisa
Sina njaa maana Mimi Ni mkulima ninayejitosheleza kwa Mahitaji ya chakula,mimi Ni mzalendo ndio maana naandika ukweli japo Ni mchungu kwa watu Aina yako wasiopenda kuona au kuusoma ukweli
 
Ndugu yangu mchambuzi napenda kukwambia kuwa Mimi naishi na kula kwa jasho langu ,kwa kutumia mikono yangu na nguvu zangu, Mimi Ni mkulima ninayejion fahari na heshima kuwa mkulima na kuwaa sehemu ya watanzania wazalendo waliojitolea na kujitoa kulilisha Taifa letu kwa kuhakikisha kuwa chakula kinapatikana kwa wingi na kuwafanya watanzania washibe na Kuendelea na shughuli zao za kiuzalishaji.

Lakini pia kupitia ukulima wangu nashiriki katika kutunza amani na utulivu wa Taifa letu maana huwezi ukamuongoza wala kusikilizwa na mtu mwenye njaa ya chakula,ndio maana unaona watu wakiwa na njaa wapo tayari kuandamana hata mbele ya polisi wenye mitutu ya bunduki,lakini huwezi ukawasikia watu wanaandamana na kuhatarisha maisha Yao kwa ajili ya kudai katiba mpya,hii ndio sababu hata chama chako kimekosa uungwaji mkono katika hoja hii ya katiba mpya katika kuwashawishi watanzania kuwaunga mkono.

Kazi iendeleee,mama yetu Rais Samia Tunamwamini na Tumeamua kuwa Naye Kama Rais wetu mpaka 2030
Tulishakataza kujielezea sana.
Move on ankolii.
 
Sina njaa maana Mimi Ni mkulima ninayejitosheleza kwa Mahitaji ya chakula,mimi Ni mzalendo ndio maana naandika ukweli japo Ni mchungu kwa watu Aina yako wasiopenda kuona au kuusoma ukweli
Namba yako ya simu inauhusiano gani na ukweli!!?
Mkulima uache kuwaza mvua, pembejeo na soko uwe busy kutafta buk7 ya Lumumba ambayo NATO sidhani kama unapata
 
Namba yako ya simu inauhusiano gani na ukweli!!?
Mkulima uache kuwaza mvua, pembejeo na soko uwe busy kutafta buk7 ya Lumumba ambayo NATO sidhani kama unapata
Silipwi ili kuandika hapa labda Kama wewe ndio unalipwa Kuja hapa jukwaani kupotosha ukweli
 
Unamsifia hadi unayemsifia anaona kero njaa yako ni Kali sana
Hapana ndugu yangu Mimi Sina njaa maana mkulima wa kweli Kama Mimi huwezi ukafa kwa njaa Wala kulia kwa njaa,pia nayoandika hapa Ni ya kweli mtupu juu ya Rais wetu mama Samia,ndio maana unaona hata viongozi mbalimbali bila kujali itikadi za vyama vyao Wanampongeza Sana Rais Samia kila wapandapo katika majukwaa ya kisiasa
 
Mkuu utateuliwa si kwa sababu umeomba Ila umeonekana
Uongozi unatoka kwa Mwenyezi MUNGU,Usimfanye vitu ili ionekane kwa ajili ya kupewa uongozi maana kwa kufanya hivyo unaweza umwa na kupata msongo wa mawazo ukiona huteuliwi ,fanya vitu kwa moyo wa uzalendo na kwa kuusema Ukweli hata Kama Ni mchungu kwa baadhi ya watu,ndio maana Mimi nawaambia ukweli watanzania ya kuwa Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania tunayopaswa kujivunia na kuiheshimu Sana maana viongozi aina yake hawazaliwi kila Siku na hawapatikani kila mahali,kwetu watanzania Ni bahati kuwa na mama Samia Kama Rais wetu ambapo hata majirani zetu wanatamani angekwenda kuwaongoza hata kwa mwaka mmoja tu
 
Mkuu utateuliwa si kwa sababu umeomba Ila umeonekana
Uongozi unatoka kwa Mwenyezi MUNGU,Usimfanye vitu ili ionekane kwa ajili ya kupewa uongozi maana kwa kufanya hivyo unaweza umwa na kupata msongo wa mawazo ukiona huteuliwi ,fanya vitu kwa moyo wa uzalendo na kwa kuusema Ukweli hata Kama Ni mchungu kwa baadhi ya watu,ndio maana Mimi nawaambia ukweli watanzania ya kuwa Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania tunayopaswa kujivunia na kuiheshimu Sana maana viongozi aina yake hawazaliwi kila Siku na hawapatikani kila mahali,kwetu watanzania Ni bahati kuwa na mama Samia Kama Rais wetu ambapo hata
 
Ndugu zangu watanzania,

Kwa hakika libarikiwe sana tumbo lililombeba mama Samia, lilibeba mtoto aliyekuja kuwa kiongozi wa Tanzania, kiongozi mwenye upendo, hekima, busara, ukarimu, huruma, unyenyekevu na usikivu.

Kiongozi asiye na makuu wala makidai, kiongozi mwenye kujishusha na kujua kuwa pamoja na madaraka yake makubwa kiuongozi lakini bado anabaki kuwa mwanadamu aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu.

Kiongozi ambaye pamoja na uwezo wake mkubwa kimamlaka lakini anatambua kuwa yupo Mungu ambaye ndiye anayepaswa kuabudiwa na kupewa sifa na utukufu, kiongozi ambaye wakati wote madaraka yamemfuata yeye kutokana na kupewa kibali na Mwenyezi Mungu.

Kiongozi ambaye mikono yake ameinyoosha katika kuwafuta machozi na kuwapatia haki wenye kuonewa, kiongozi ambaye ulimi wake umewaponya na kuwafariji wenye majeraha na makovu.

Ni kiongozi ambaye hajawahi kufurahi wala kuwa tayari kuongoza taifa la watu wanaolia na kububujikwa machozi kwa kuonewa, hajawahi kuwa tayari kimaneno na hata kimatendo kuhubiri uonevu, ukatili, ubaguzi na hata chuki kwa watu.

Ni kiongozi ambaye ulimi wake muda wote ni wenye kutoa maneno ya upendo mshikamano na kujenga umoja wa taifa.

Ndio sababu ya kuungwa mkono na Watanzania wote, ndio sababu ya kupendwa na kuombewa afya njema na nguvu za kuendelea kututumikia Watanzania, ndio sababu ya kusikilizwa na kufuatiliwa sana kwa hotuba zake, ndio sababu ya kuteka hisia na mioyo ya Watanzania, ndio sababu ya kukubalika kwake na makundi yote, ndio sababu ya umaarufu na ushawishi wake kuwa mkubwa sana Tanzania na nje ya mipaka ya Tanzania.

Rais samia ni nuru katikati ya giza, ni tumaini katikati ya waliokata tamaa, ni faraja kwa waliao, ni mpatanishi wa kweli, mpenda haki na mtenda haki, ni Nyota ya alfajiri iletayo matumaini ya pambazuko lililojema.

Ndio sababu ya kila Mtanzania kuwa na matumiani ya pambazuko katika maisha yao na ndoto zao, kila mmoja anao uhakika wa kutimiza ndoto zake na kufikia mafanikio anayoyataka.

Serikali yake imekuwa kwa ajili ya kuwasaidia watu, kuwawezesha na kuwashika mkono katika kufikia malengo yake. Serikali yake haipo kwa ajili ya kumuonea mtu, kumdhuru mtu, kumtesa mtu, kumliza mtu.

Ni serikali safi ya haki yenye matendo mema na hatua njema, ni serikali yenye dhamira ya kuwatumikia watu kwa upendo na uzalendo mkubwa.

Ndio sababu ya kuona mioyo ya Watanzania ikiwa haina hofu wala wasiwasi, kila mmoja anayo amani moyoni mwake, kila mmoja anayo imani na serikali hii, kila mmoja anaridhishwa na utendaji kazi wa serikali ya Rais Samia.

Viongozi aina ya Rais Samia hawazaliwi kila siku wala hawapatikani kila mahali, maana wenye moyo kama wake wa kuweza kumsikiliza kila mtu, kumvumilia kila mtu mwenye kutofautiana nao, wenye kifua kama chake, wenye kusikiliza sauti zote hata zikwaluzazo kwa lugha za ukakasi, kukaa mezani na yeyote, kujumuika na yeyote ni wachache sana.

Viongozi aina yake huja kama mitume kwa ajili ya kuwatumikia watu kwa haki na upendo. Huja wakiwa wameandaliwa na Mwenyezi Mungu, hawaandaliwi na wanadamu wala kwa mipango ya wanadamu, huja wakiwa wamepewa maaarifa na njia za kuongaza.

Mwenyezi Mungu huwapa kila kitu kama ilivyokuwa kwa Musa, huja wakiwa na kibali mkononi cha Mwenyezi Mungu katika ulimwengu wa kiroho. Huja kwa makusudi maalumu, huja kama nyota katikati ya giza, hung'aa na mwanga wao huwa tumaini la watu waitazamayo nyota hiyo, huja wakiwa na majibu ya maswali.

Ndio sababu ya kuona Rais Samia akiwa kipenzi cha Watanzania, ndio sababu ukiona Rais Samia hakauki midomoni mwa Watanzania kwa mema. Amejiandikia ukurasa wake na anaendelea kuandika kitabu chake kitakachosimuliwa vizazi na vizazi kwa mema mengi na makubwa aliyolifanyia Taifa letu yanayobaki kama alama katika mioyo ya watu.

Rais Samia kwake haki ndio kipaombele kwa kuwa anatambua ya kuwa haki huinua taifa. Ni heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi na ufahari wa kidunia.

Rais samia amechagua jina jema kwa kutenda mema kwa Watanzania, yanayomfanya kuwa chaguo la Watanzania kwa muhula wa pili, yanayomfanya apendwe na kuzungumzwa vyema na watu wa makundi yote, rika zote, jinsia zote na vyama vyote.

Rais Samia pamoja na madaraka yake makubwa, ukubwa wa kimamlaka alionao mikononi mwake na katika ulimi wake kikatiba na kisheria, lakini bado anatambua ya kuwa yeye ni mwanadamu na kwamba anayestahili kuabudiwa na kupewa sifa na utukufu ni Mwenyezi Mungu pekee na siyo mwanadamu.

Ndio sababu ya kuwa mnyenyekevu muda wote, mwenye kujishusha na kuwasikiliza watu wote pasipo ubaguzi wala kuwagawa kwa misingi ya ukabila, udini na ukanda, ndio sababu ya kuongoza taifa kwa haki na upendo.

Libarikiwe tumbo lililombeba Rais Samia, maana matumbo mengine yanaleta watu Duniani wanaokuja kuleta mateso kwa watu, uchungu katika maisha ya watu, simanzi kwa watu, machozi kwa watu, maumivu kwa watu, giza katika mioyo ya watu, majeraha na uvuli katika mioyo ya watu, kumwaga damu za watu, kunyonga watu, kuua watu, kukatisha na kuzima ndoto za watu, kushindana na Mwenyezi Mungu anayewapa watu pumzi ya kuishi.

Tujitahidi kutenda mema tukiwa hai kwa kadri tuwezavyo ili matendo yetu yasimame kututetea tukiwa hatuna uwezo wa kujitetea wala kufungua vinywa vyetu. Ya Duniani ni ya kupita tu, yanini kuumizana, kutesana, kukatishana ndoto, kujengeana chuki, kuuwana kwa sababu ya mali au madaraka au vyeo?, nani anazikwa navyo?

Kazi iendelee, Mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Hiyo namba ya simu ya nini sasa wewe kifaduro? Aliyemleta ni Corona

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom