Abarikiwe aliyemleta Rais Samia Duniani

Abarikiwe aliyemleta Rais Samia Duniani

Uongozi unatoka kwa Mwenyezi MUNGU,Usimfanye vitu ili ionekane kwa ajili ya kupewa uongozi maana kwa kufanya hivyo unaweza umwa na kupata msongo wa mawazo ukiona huteuliwi ,fanya vitu kwa moyo wa uzalendo na kwa kuusema Ukweli hata Kama Ni mchungu kwa baadhi ya watu,ndio maana Mimi nawaambia ukweli watanzania ya kuwa Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania tunayopaswa kujivunia na kuiheshimu Sana maana viongozi aina yake hawazaliwi kila Siku na hawapatikani kila mahali,kwetu watanzania Ni bahati kuwa na mama Samia Kama Rais wetu ambapo hata majirani zetu wanatamani angekwenda kuwaongoza hata kwa mwaka mmoja tu
Ndio maana nikasema wewe umeonekana utateuliwa,
 
Uongozi unatoka kwa Mwenyezi MUNGU,Usimfanye vitu ili ionekane kwa ajili ya kupewa uongozi maana kwa kufanya hivyo unaweza umwa na kupata msongo wa mawazo ukiona huteuliwi ,fanya vitu kwa moyo wa uzalendo na kwa kuusema Ukweli hata Kama Ni mchungu kwa baadhi ya watu,ndio maana Mimi nawaambia ukweli watanzania ya kuwa Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania tunayopaswa kujivunia na kuiheshimu Sana maana viongozi aina yake hawazaliwi kila Siku na hawapatikani kila mahali,kwetu watanzania Ni bahati kuwa na mama Samia Kama Rais wetu ambapo hata
Umerudia
 
Hapana Mimi Sina njaa maana ninajilimia chakula kwa mikono yangu na siyo kwenda kupima unga madukani
Yaani ukimkubali Kiongozi alie madarakani unaambiwa una njaa.. Tanzania hiyo njaa ipo wapi mahindi ya kuchoma yanauzwa Tsh 500 nyanya wanauza kwa Sado hizo Samaki zinauzwa kwa mafungu hapo soko la Kilombero ,Arusha...
 
Yaani ukimkubali Kiongozi alie madarakani unaambiwa una njaa.. Tanzania hiyo njaa ipo wapi mahindi ya kuchoma yanauzwa Tsh 500 nyanya wanauza kwa Sado hizo Samaki zinauzwa kwa mafungu hapo soko la Kilombero ,Arusha...
Wameshapagawa na kuchanganyikiwa na upepo mkali wa Rais Samia unao endelea kuvuma kila Kona ambapo watanzania wanaendelea kumuunga mkono mh Rais wetu
 
Ndugu yangu na rafiki yangu Dolphin T napenda kukuhakikishia kuwa siwezi kukufuru Wala kufanya dhihaka kwa Mwenyezi MUNGU maana huyu hafananishwi na yeyote Wala na chochote ,huyo Ni alfa na Omega, ndio maana hata katika andiko langu nimeandika Hilo juu ya uweza wa MWENYEZI MUNGU
Mjinga wewe ashakumu sio matusi! Kasome tena kichwa Cha Uzi wako na ulichoandika na uangalie nilichoandika!

Unaposema abarikiwe aliyemleta Samia Duniani moja kwa moja unamrejea Mungu muumba wa vitu vyote ikiwemo wewe na ujinga wako uliokithiri!

Ilikushinda Nini kuandika abarikiwe aliyemzaa Samia?

Mwenye uwezo wa kumleta mtu duniani Ni Mungu Tu na sio vinginevyo! Uwe unajishauri Mara nyingi unapoandika hizi ngonjera zako ambazo zimejaa nadharia tu na hakuna practical Wala tangible issues.

Vinginevyo utakua unakufuru Mungu. Na Mungu wetu Ni Mungu mwenye wivu Sana! Hakuna kiumbe chochote juu ya nchi au Mbingu kinachoweza kumbariki Mungu Mana yeye ndiye atiaye baraka zake!

Usisahau Kuna watu walimtaka Mungu amshukuru Jiwe kwa kuiondoa Korona Tanzania (Afande Shana) unajua aliko Sasa na wengi wanaofanana na hayo!

Kama wewe Ni Mkristo kasome biblia hata Yesu alionekana champion lakini Kuna watu waliogopa kukufuru kupitia yeye;
Kasome:

Lk 11:27 SUV​

Ikawa alipokuwa akisema maneno hayo, mwanamke mmoja katika mkutano alipaza sauti yake, akamwambia, Heri tumbo lililokuzaa, na matiti uliyonyonya.

Yesu akamjibu heri yao wanaosikia neno langu na kulishika

Sasa wewe kilaza unaona kabisa umekosea bado unashupaza shingo!
Eti abarikiwe aliyemleta Samia Duniani! Serious?
 
Ndugu zangu watanzania,

Kwa hakika libarikiwe sana tumbo lililombeba mama Samia, lilibeba mtoto aliyekuja kuwa kiongozi wa Tanzania, kiongozi mwenye upendo, hekima, busara, ukarimu, huruma, unyenyekevu na usikivu.

Kiongozi asiye na makuu wala makidai, kiongozi mwenye kujishusha na kujua kuwa pamoja na madaraka yake makubwa kiuongozi lakini bado anabaki kuwa mwanadamu aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu.

Kiongozi ambaye pamoja na uwezo wake mkubwa kimamlaka lakini anatambua kuwa yupo Mungu ambaye ndiye anayepaswa kuabudiwa na kupewa sifa na utukufu, kiongozi ambaye wakati wote madaraka yamemfuata yeye kutokana na kupewa kibali na Mwenyezi Mungu.

Kiongozi ambaye mikono yake ameinyoosha katika kuwafuta machozi na kuwapatia haki wenye kuonewa, kiongozi ambaye ulimi wake umewaponya na kuwafariji wenye majeraha na makovu.

Ni kiongozi ambaye hajawahi kufurahi wala kuwa tayari kuongoza taifa la watu wanaolia na kububujikwa machozi kwa kuonewa, hajawahi kuwa tayari kimaneno na hata kimatendo kuhubiri uonevu, ukatili, ubaguzi na hata chuki kwa watu.

Ni kiongozi ambaye ulimi wake muda wote ni wenye kutoa maneno ya upendo mshikamano na kujenga umoja wa taifa.

Ndio sababu ya kuungwa mkono na Watanzania wote, ndio sababu ya kupendwa na kuombewa afya njema na nguvu za kuendelea kututumikia Watanzania, ndio sababu ya kusikilizwa na kufuatiliwa sana kwa hotuba zake, ndio sababu ya kuteka hisia na mioyo ya Watanzania, ndio sababu ya kukubalika kwake na makundi yote, ndio sababu ya umaarufu na ushawishi wake kuwa mkubwa sana Tanzania na nje ya mipaka ya Tanzania.

Rais samia ni nuru katikati ya giza, ni tumaini katikati ya waliokata tamaa, ni faraja kwa waliao, ni mpatanishi wa kweli, mpenda haki na mtenda haki, ni Nyota ya alfajiri iletayo matumaini ya pambazuko lililojema.

Ndio sababu ya kila Mtanzania kuwa na matumiani ya pambazuko katika maisha yao na ndoto zao, kila mmoja anao uhakika wa kutimiza ndoto zake na kufikia mafanikio anayoyataka.

Serikali yake imekuwa kwa ajili ya kuwasaidia watu, kuwawezesha na kuwashika mkono katika kufikia malengo yake. Serikali yake haipo kwa ajili ya kumuonea mtu, kumdhuru mtu, kumtesa mtu, kumliza mtu.

Ni serikali safi ya haki yenye matendo mema na hatua njema, ni serikali yenye dhamira ya kuwatumikia watu kwa upendo na uzalendo mkubwa.

Ndio sababu ya kuona mioyo ya Watanzania ikiwa haina hofu wala wasiwasi, kila mmoja anayo amani moyoni mwake, kila mmoja anayo imani na serikali hii, kila mmoja anaridhishwa na utendaji kazi wa serikali ya Rais Samia.

Viongozi aina ya Rais Samia hawazaliwi kila siku wala hawapatikani kila mahali, maana wenye moyo kama wake wa kuweza kumsikiliza kila mtu, kumvumilia kila mtu mwenye kutofautiana nao, wenye kifua kama chake, wenye kusikiliza sauti zote hata zikwaluzazo kwa lugha za ukakasi, kukaa mezani na yeyote, kujumuika na yeyote ni wachache sana.

Viongozi aina yake huja kama mitume kwa ajili ya kuwatumikia watu kwa haki na upendo. Huja wakiwa wameandaliwa na Mwenyezi Mungu, hawaandaliwi na wanadamu wala kwa mipango ya wanadamu, huja wakiwa wamepewa maaarifa na njia za kuongaza.

Mwenyezi Mungu huwapa kila kitu kama ilivyokuwa kwa Musa, huja wakiwa na kibali mkononi cha Mwenyezi Mungu katika ulimwengu wa kiroho. Huja kwa makusudi maalumu, huja kama nyota katikati ya giza, hung'aa na mwanga wao huwa tumaini la watu waitazamayo nyota hiyo, huja wakiwa na majibu ya maswali.

Ndio sababu ya kuona Rais Samia akiwa kipenzi cha Watanzania, ndio sababu ukiona Rais Samia hakauki midomoni mwa Watanzania kwa mema. Amejiandikia ukurasa wake na anaendelea kuandika kitabu chake kitakachosimuliwa vizazi na vizazi kwa mema mengi na makubwa aliyolifanyia Taifa letu yanayobaki kama alama katika mioyo ya watu.

Rais Samia kwake haki ndio kipaombele kwa kuwa anatambua ya kuwa haki huinua taifa. Ni heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi na ufahari wa kidunia.

Rais samia amechagua jina jema kwa kutenda mema kwa Watanzania, yanayomfanya kuwa chaguo la Watanzania kwa muhula wa pili, yanayomfanya apendwe na kuzungumzwa vyema na watu wa makundi yote, rika zote, jinsia zote na vyama vyote.

Rais Samia pamoja na madaraka yake makubwa, ukubwa wa kimamlaka alionao mikononi mwake na katika ulimi wake kikatiba na kisheria, lakini bado anatambua ya kuwa yeye ni mwanadamu na kwamba anayestahili kuabudiwa na kupewa sifa na utukufu ni Mwenyezi Mungu pekee na siyo mwanadamu.

Ndio sababu ya kuwa mnyenyekevu muda wote, mwenye kujishusha na kuwasikiliza watu wote pasipo ubaguzi wala kuwagawa kwa misingi ya ukabila, udini na ukanda, ndio sababu ya kuongoza taifa kwa haki na upendo.

Libarikiwe tumbo lililombeba Rais Samia, maana matumbo mengine yanaleta watu Duniani wanaokuja kuleta mateso kwa watu, uchungu katika maisha ya watu, simanzi kwa watu, machozi kwa watu, maumivu kwa watu, giza katika mioyo ya watu, majeraha na uvuli katika mioyo ya watu, kumwaga damu za watu, kunyonga watu, kuua watu, kukatisha na kuzima ndoto za watu, kushindana na Mwenyezi Mungu anayewapa watu pumzi ya kuishi.

Tujitahidi kutenda mema tukiwa hai kwa kadri tuwezavyo ili matendo yetu yasimame kututetea tukiwa hatuna uwezo wa kujitetea wala kufungua vinywa vyetu. Ya Duniani ni ya kupita tu, yanini kuumizana, kutesana, kukatishana ndoto, kujengeana chuki, kuuwana kwa sababu ya mali au madaraka au vyeo?, nani anazikwa navyo?

Kazi iendelee, Mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Ongezea na email address
 
Bwashee umemsahau aliyemteua kuwa makamu wake, bila huyo hayo yote uliyoyasema asingeyafanya.
Central committee ya CCM ndio inayoteau mgombea mwenza.
Mgombea Urais anapewa jukumu la kutangaza tu hana utashi. Na kama kumbukumbu zangu ziko vizuri ile 2015 hata hilo jukumu la kutangaza hakupewa, walimuona chizi maarifa na ilivyokuwa Kanda anayotokea wasivyo wathamini wanawake wakaona anaweza kumtangaza mtu mwengine kabisa.
 
Sijamaliza kusoma, ila niseme una hoja USIKILIZWE na ULIPWE kabisa. Hili Pambio sijawahi kuliona tangu dunia iumbwe.
 
Back
Top Bottom