mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Kuna mambo mengi yamejificha juu ya Mavoko kuondoka wasafi, tuachane na propaganda za udini kama wengi walivyokuwa wanaaminishwa.
Mtakumbuka wakati Mavoko anasaini WCB alikuwa katika ubora wake kiasi cha kuanza kushindanishwa na Diamond Platnumz. Hilo suala lilikuwa likimnyima usingizi Diamond na kuhofia kushushwa. Ili kuweza kummaliza Mavoko ilitakiwa asainiwe WCB, kweli waliweza kumshawishi na kumpa mkataba wa miaka 10.
Kimbembe kikaanza pale Wasafi Rich Mavoko hakuwa tena yule wa 'Pacha wangu' bali kila alichotaka kufanya alikuwa anabanwa na mkataba, akabaki kuwa mpenzi mtazamaji.
Kila mmoja anamjua Mavoko kuwa ni mtunzi mzuri sana, ana nyimbo kibao za kutoa lakini ataanzia wapi masikini kutoa! Mkataba ulikuwa mchungu sana kwake, hata kolabo nazo zikawa shida na kukatishwa tamaa.
Diamond ni mbaya ndio lakini wabaya zaidi ni Babu Talent(Babu Tale) na Sallam. Hawa wanamnyenyekea sana Diamond wapate kula yao. Ilifika wakati mpaka Mavoko alivyowasikilizisha nyimbo zake, kama waliipenda nyimbo hawa wanyonyaji walitoa uamuzi kuwa hapa akikaa Diamond hii ngoma itakuwa noma. Wimbo kama Baila kapokwa mtoto wa Moro.
Nyimbo ambazo wasanii wa WCB walipeleka kwenye menejimenti na hawa wanyonyaji kujua kuwa zitakuwa hit songs lazima walishinikiza Diamond awepo. Wimbo kama Kokoro ilibid iwe Mavoko na Davido, Kwang'waru ilibidi asimame Konde Boy na Davido ila menejimenti ikasema hapa piga ua lazima akae Mond.
Mavoko alikuwa na jina kubwa Wasafi lakini mifukoni hana mavumba goto limekata, asilimia kubwa ilikuwa inaingia WCB. Kaondoka mnyonge hana kitu huku Babu Talent na Sallam wakitokwa mashavu.
Pale mwenye sauti kidogo kati ya wasanii ni Konde Boy kipenzi cha Mond, wengine hawana namna ndio maana unaona kama Vany Boy kajenga kastudio kake, huyu alishapigwa biti ukizingua tunakurudisha Tip Top connection.
Kichekesho ni Mbosso, huyu pesa yake inaenda kwa Fella mnyonyaji kwa makubaliano kwamba Fella ilitakiwa aue kundi la Mkubwa na wanae maana walishaanza kuwa tishio na likivunjika basi WCB wamtwae Baba Moza, ila akawachomolea ndio wakadondokea kwa Mbosso.
Mavoko soon atakuwa juu kama yote, subiri Boss Ruge apone muone, NASEMA subiri Boss Ruge afanikiwe kupona muone kampeni za kumkabidhi Mavoko kiti cha ufalme zitakavyo-damshi.
Nimewapa habari kama yote.
Mtakumbuka wakati Mavoko anasaini WCB alikuwa katika ubora wake kiasi cha kuanza kushindanishwa na Diamond Platnumz. Hilo suala lilikuwa likimnyima usingizi Diamond na kuhofia kushushwa. Ili kuweza kummaliza Mavoko ilitakiwa asainiwe WCB, kweli waliweza kumshawishi na kumpa mkataba wa miaka 10.
Kimbembe kikaanza pale Wasafi Rich Mavoko hakuwa tena yule wa 'Pacha wangu' bali kila alichotaka kufanya alikuwa anabanwa na mkataba, akabaki kuwa mpenzi mtazamaji.
Kila mmoja anamjua Mavoko kuwa ni mtunzi mzuri sana, ana nyimbo kibao za kutoa lakini ataanzia wapi masikini kutoa! Mkataba ulikuwa mchungu sana kwake, hata kolabo nazo zikawa shida na kukatishwa tamaa.
Diamond ni mbaya ndio lakini wabaya zaidi ni Babu Talent(Babu Tale) na Sallam. Hawa wanamnyenyekea sana Diamond wapate kula yao. Ilifika wakati mpaka Mavoko alivyowasikilizisha nyimbo zake, kama waliipenda nyimbo hawa wanyonyaji walitoa uamuzi kuwa hapa akikaa Diamond hii ngoma itakuwa noma. Wimbo kama Baila kapokwa mtoto wa Moro.
Nyimbo ambazo wasanii wa WCB walipeleka kwenye menejimenti na hawa wanyonyaji kujua kuwa zitakuwa hit songs lazima walishinikiza Diamond awepo. Wimbo kama Kokoro ilibid iwe Mavoko na Davido, Kwang'waru ilibidi asimame Konde Boy na Davido ila menejimenti ikasema hapa piga ua lazima akae Mond.
Mavoko alikuwa na jina kubwa Wasafi lakini mifukoni hana mavumba goto limekata, asilimia kubwa ilikuwa inaingia WCB. Kaondoka mnyonge hana kitu huku Babu Talent na Sallam wakitokwa mashavu.
Pale mwenye sauti kidogo kati ya wasanii ni Konde Boy kipenzi cha Mond, wengine hawana namna ndio maana unaona kama Vany Boy kajenga kastudio kake, huyu alishapigwa biti ukizingua tunakurudisha Tip Top connection.
Kichekesho ni Mbosso, huyu pesa yake inaenda kwa Fella mnyonyaji kwa makubaliano kwamba Fella ilitakiwa aue kundi la Mkubwa na wanae maana walishaanza kuwa tishio na likivunjika basi WCB wamtwae Baba Moza, ila akawachomolea ndio wakadondokea kwa Mbosso.
Mavoko soon atakuwa juu kama yote, subiri Boss Ruge apone muone, NASEMA subiri Boss Ruge afanikiwe kupona muone kampeni za kumkabidhi Mavoko kiti cha ufalme zitakavyo-damshi.
Nimewapa habari kama yote.