A vivid metaphor on the war on corruption (Picha)

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
mtoni.jpg


Mkazi wa Mtoni Kijichi akishiriki kuzima moto uliotekeza makazi ya mama mmoja hivi. Nilipoiangala picha hiyo nilibakia kujiuliza kama juhudi zetu katika mapambano haya zinalingana na uzito wa kazi iliyopo mbele yetu au we are fighting the proverbial "losing battle"? Kweli tunaweza au tuache magari makubwa kufanya kazi hii (assuming the get there on time na wana maji ya kutosha!)
 
Picha inatia huruma mno. Tatizo hata wakija huwa wanakuwa eti hawana maji, ila siku hizi huwa hawaji kabisa, manake wakija wakisema hawana maji ni mawe mtindo mmoja. Sielewi kikosi cha zimamoto kiko kwa kazi gani?, WIZI MTUPU.
 
Mkazi wa Mtoni Kijichi akishiriki kuzima moto uliotekeza makazi ya mama mmoja hivi. Nilipoiangala picha hiyo nilibakia kujiuliza kama juhudi zetu katika mapambano haya zinalingana na uzito wa kazi iliyopo mbele yetu au we are fighting the proverbial "losing battle"? Kweli tunaweza au tuache magari makubwa kufanya kazi hii (assuming the get there on time na wana maji ya kutosha!)

Mzee Mwanakijiji,
Ukiona Chiligati na Kikwete wanatishia watu 'Nyau', ujue kuwa ingawa uzimaji wetu moto umetegemea ka-kikombe, usichoona ni huko juu angani ambako kuna wingu limesheheni kumwaga mvua ya enzi za Noah.

Ndio maana ule moto wa akina Kikwete, Lowassa, Rostam n.k, unaanza kuwewesuka kupitia akina Chiligati n.k.
 
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/

......nilibakia kujiuliza kama juhudi zetu katika mapambano haya zinalingana na uzito wa kazi iliyopo mbele yetu au we are fighting the proverbial "losing battle"? ........ [/quote]

[SIZE="4"]Vita iliyopo mebele yetu ni kubwa, na pana, maadui wana kila siraha, kuanzia mizinga, ndege ziendazo kasi kama zile za Tonardo, mitambo ya kutungulia maroketi kama Patriot, wana kila kitu. Lakini kibaya zaidi wanamtandao kuanzia juu mpaka chini wako well organized, wana comanding post, wana nidhamu, wanawataalam kuanzia wa protocol mpaka Itifaki, halipindi Jambo. Wana Pesa, wanamedia, wanweza kuchapa Propaganda.

Sisi Tunawatu wanaolala hoi, wanaosubiri Masiha ashuke kuwakomboa, Sisi tunamawazo lakini hatuwezi kuingia barabarani kuwaambia sasa inatosha waondoke, kwani nikifanya hivyo mwanangu hatasoma tena, nitapigwa risasi na kikosi cha Fanya Fujo Uone, sisi hatuwezi kuwaondoa kwenye karatasi, kwani tunaogopa kuwachagua wengine tutauza nchi, tumeambiwa tutakaribisha Vita.

Nia Tunayo mzee, sababu Tunayo, lakini Uwezo wetu ni mdogo sana kama unavyotuona kwenye Picha.[/SIZE]
 
Japokuwa chanzo cha 'MOTO' huu wa kutisha ni mchanaganyiko wa Nishati ya 'ememe,gesi,mafuta' in-shallah Mi-naelekea kufikiri tutauzima tu,swali ni je moto huu umedhoofisha kiasi gani Paa,kuta au hata msingi wa nyumba yenyewe??kama hatuja chelewa sana twaweza anza 'nyumba mpya 2010??'
 
Hii picha inaonesha jinsi viongozi wetu wasivy juu Priority za wananchi wao na hili ndiyo tatizo ya hata kutotusikiliza sisi
 
Kuna hii ya Michuzi pia ni kule Bagamoyo, eti gari ya zimamoto imetumwa kutoka Dar!! Imefika hakuna cha kuzima.
acxveu.jpg
 
Vita iliyopo mebele yetu ni kubwa, na pana, maadui wana kila siraha, kuanzia mizinga, ndege ziendazo kasi kama zile za Tonardo, mitambo ya kutungulia maroketi kama Patriot, wana kila kitu. Lakini kibaya zaidi wanamtandao kuanzia juu mpaka chini wako well organized, wana comanding post, wana nidhamu, wanawataalam kuanzia wa protocol mpaka Itifaki, halipindi Jambo. Wana Pesa, wanamedia, wanweza kuchapa Propaganda.

Sisi Tunawatu wanaolala hoi, wanaosubiri Masiha ashuke kuwakomboa, Sisi tunamawazo lakini hatuwezi kuingia barabarani kuwaambia sasa inatosha waondoke, kwani nikifanya hivyo mwanangu hatasoma tena, nitapigwa risasi na kikosi cha Fanya Fujo Uone, sisi hatuwezi kuwaondoa kwenye karatasi, kwani tunaogopa kuwachagua wengine tutauza nchi, tumeambiwa tutakaribisha Vita.

Nia Tunayo mzee, sababu Tunayo, lakini Uwezo wetu ni mdogo sana kama unavyotuona kwenye Picha.

Mbogela mkuu salam;
Kwa hali hii uliyofafanua tutegemee USHIDI WA DAVID (DAUDI) dhidi ya GOLIATH eeeeeeeMUNGU TUSAIDIE>
 
Hii picha inaonesha jinsi viongozi wetu wasivy juu Priority za wananchi wao na hili ndiyo tatizo ya hata kutotusikiliza sisi

Gembe,

Nilisoma kwenye thread moja jamaa kuna jamaa amesema kuwa unasomeshwa na fisadi mmoja masters SA (sijui ya tatu maana ulishawahikutamba humu kuwa unayo). Sijaona ukikanusha wala kukubali sasa hapa unauliza kuhusu priority kama hizo tuhuma ni za kweli jibu si unalo? Nikikusaidia mafisadi wanaiba hela na priority zao ni kujenga mahekalu, magari ya kifahari pamoja na kuwachukua watoto wa maskini wachache na kuwasomesha ili waje walinde mali zao kwenye jeshi letu la polisi, takukuru na waandishi wa habari yes waandishi wa habari.
 
Kwa hali hii uliyofafanua tutegemee USHIDI WA DAVID (DAUDI) dhidi ya GOLIATH eeeeeeeMUNGU TUSAIDIE>

Nakubaliana na wewe kabisa, lakini ndhani hatuwezi kukaa kusubiri Mungu ashushe baraka zake kuja kuamulia ugomvi huu na kumpa mwenye haki haki ya kumiliki nchi. Nadhani Tunahitaji Moyo wa yule Mama Ross Park wa miaka ya 60 huko marekani iliyozaa movement kubwa ya civil rights na baadaye martin Luther King Jr kuonekna kinara. Tunataka akina Ross Park Tanzania, Madagascar leo imekombolewa na mcheza disco, angalia historia ya Ulaya Mashariki inaonyesh kuwa watu simple ndio wakuwategemea kila siku, hawana conflict of interest, hawana cha kupoteza, tuingie huko waliko tuwaamshe waje kusima moto, hawaogopi nguo zao za thamni kunuka moshi wala kuchafuka, wana nguo simple hata zikungua hapo hakuna shida.
 
Mwanakijiji,

Huko nyuma niliwahi kusema tatizo letu kubwa ni kuwa wengi wetu watanzania, baada ya kuzoea maisha ndani ya hili bonde la kashfa na uchafu, sasa tunaanza kuliona kama makao yetu ya kudumu. Wengine, baada ya kuathirika na uvundo kwenye hili bonde, wamepoteza kabisa uwezo wao wa kunusa, kusikia wala kuona na hivi sasa wanachapa usingizi humo bila wasiwasi - thubutu ufikirie kuwaondoa humo !!

Kosa kubwa wanalofanya wachache ambao hawajaathirika ni kule kuwa na imani potofu eti wako mashujaa ambao pamoja na kuogelea kwenye uvundo huo, hawanuki kwa sababu wanaweza kujipaka manukato ya muda. Kwa kuendelea kuwakumbatia watu kama hao na kuwapa sifa wasizostahili, tunazidi kulipalilia na kuliwekea mbolea hili shamba ambalo zao lake kuu ni ufisadi - sasa hili zao lingine latoka wapi ?

Je kuwaita wasafi tukijua wazi wanaishi ndani ya dampo kwenye uchafu, tutakuwa kweli hatuhalalishi maisha ndani ya dampo ? Mafisadi tumewashika pabaya lakini kuwakumbatia washiriki wao kwenye maamuzi mbalimbali yanayoididimiza nchi na kuwaita mashujaa, ni ujinga. Sasa inabidi tubadilishe mbinu ya mapambano na kama hatuwezi kuwatenganisha kwa sababu wameshikamana, lazima tuwaangamize wote.

Kama unaoga mtoni, ukitaka kukauka ni lazima utoke kwenye maji. Hivyo hivyo tuwakatae kwa nguvu zote wanaooga kwenye tope halafu wanajiita wasafi huku wanaendelea kubaki kwenye tope. Hizi ni mbinu za danganya toto na koleo tuwe tayari kuliita kwa jina lake halisi - hakuna cha Sita. Kilango, Mwakyembe - wote ni hao hao Mkapa, Lowassa, Rostam, Serukamba wakiongozwa na kamanda wao mkuu,
Jakaya Mrisho Kikwete.​
 
Gembe,

Nilisoma kwenye thread moja jamaa kuna jamaa amesema kuwa unasomeshwa na fisadi mmoja masters SA (sijui ya tatu maana ulishawahikutamba humu kuwa unayo). Sijaona ukikanusha wala kukubali sasa hapa unauliza kuhusu priority kama hizo tuhuma ni za kweli jibu si unalo? Nikikusaidia mafisadi wanaiba hela na priority zao ni kujenga mahekalu, magari ya kifahari pamoja na kuwachukua watoto wa maskini wachache na kuwasomesha ili waje walinde mali zao kwenye jeshi letu la polisi, takukuru na waandishi wa habari yes waandishi wa habari.

mkuu solomon salam.
Mkuu unamaana MAFIA stail (MAFIOSO) basi kazi ipo ya kupambana na watoto wa MAGOD FATHERS kwanza. si mchezo mkuu................!!!!
 
Mkjj,

Wewe ni Kamanda acha kuonyesha dalili zozote za kuingiwa na wasiwasi! Kumbuka vita za Majimaji na za akina Mkwawa! Starling hauawi - labda ajinyonge mwenyewe. Tutashinda ila tukaze buti maana hawa mafisadi wamesambaza agents wao sehemu nyingi sana ili kujaribu ku -dilute nguvu zetu! Aluta continua Kamanda na tutashinda tu, kwa sababu hakuna option ya pili!
 
It won't be easy, lakini tusikate tamaa, sasa ndio tunahitaji ushirikiano wa viungo vyote vya mwili, ubongo ukichukua nafasi kubwa, huenda kikombe ndio silaha kubwa sana ya kuuzima moto kuliko magari ya hawa jamaa wa fire, lakini kama wote tutashika hicho kikombe na kuumwagia moto kwa wakati mmoja kwa uwingi wetu moto utazimika. Tatizo letu wengi tunapenda kuwa watazamaji, huku tukitamani kuwa na nchi ya asali na maziwa waliyoitengeneza watu wengine, we do not want to be part of the picture in the making, happy to enjoy the cake!! Kama huu uchungu tulionao hapa ungekuwa contagious huko mitaani na vijijini, hatungehitaji gharama kuuzima huu, huenda pumzi zingetosha!!
Dk.Slaa alivyoanza kuuwasha pale Mwembeyanga, wengi walimwona kachanganyikiwa, lakini mpaka leo facts zinaeleweka, huenda tunahitaji kuonekana kama tumechanganyikiwa watz wote, wakija na pumba zao washangae.
 


Sisi Tunawatu wanaolala hoi, wanaosubiri Masiha ashuke kuwakomboa, Sisi tunamawazo lakini hatuwezi kuingia barabarani kuwaambia sasa inatosha waondoke, kwani nikifanya hivyo mwanangu hatasoma tena, nitapigwa risasi na kikosi cha Fanya Fujo Uone, sisi hatuwezi kuwaondoa kwenye karatasi, kwani tunaogopa kuwachagua wengine tutauza nchi, tumeambiwa tutakaribisha Vita.

Nia Tunayo mzee, sababu Tunayo, lakini Uwezo wetu ni mdogo sana kama unavyotuona kwenye Picha.

Sikubaliani na wewe, wananchi kwenye nafasi zao wanajitahidi. Vijana wamanzeshe wemepurukushana na mapolisi. Wananchi vijijini wanalia ardhi, wanafunzi vyuoni wanalia cost sharing. Walimu wanataka kugoma kila leo. Tatizo sio wananchi, wananchi wapo tayari kama simba. Tatizo sisi watu wa katikati, ambacho tunachokidogo, ndio tunahofu ya kupoteza. Lakini sio walalahoi hata kidogo. Kwanza, wao wapo vijijini wanaendelea kulima na kutulisha, wapo kariakoo wanabeba magunia, wapo majumbani ni wasafisha nyumba. wapo mitaani hawana kazi - kila siku wanaongea matatizo waliyonayo. Ni sisi wa katikati, ambao hatujui tunataka kutetea haki za walalahoi ama kuendealea kutembea na walionacho! Tupo njiani panda, basi hofu imetutanda! msukumo wa maisha unatukimbiza, mwaka unapita! unahofu oh! sina kibanda, gari, hadhi na mambo kibao. Basi fikira zimejazwa mahitaji ya nyakati. Ndio sisi, tujitizame sisi!
 
Last edited:
Back
Top Bottom