MNDEE,
Shukran kwa video hiyo
Hapa najiuliza sasa eti JK anaenda kumuambia Mugabe ashughulikie mambo ya wananchi wake..........i mean what a joke........
Kinachonishangaza zaidi ni kuona wananchi wa mameneo hayo hayo wanzidi kukpigia kura Chama Kilichowaletea maafa ya kila aina.............safari ni ndefu sana
Tatizo uelewa na ujasiri wa kuthubutu watanzania wa sasa ni waoga sana na hawajali ni sawa na watoto hudanganywa kiurahisi kwa kupewa kofia na kanga,ukiangalia angalau kidogo mijini kuna muamuko wa kujua mazuri na mabaya,huko vijijini ndiko kuna ukosefu mkubwa wa huduma na ndiko kuna watu wengi lakini unapowaambia CCM ndio imewafikisha hapo na angalieni upande mwingine hawakuelewi wanakuona mhuni sasa watu wavijijini mpira ndo huo uko kwenu,chagueni kusuka au kunyoa
Hakuna mabadiliko lakini mwaka nenda mwaka rudi viongozi wale wale wanarudi kuomba kura na wanachaguliwa. Tatizo linaanzia kwenye chombo kinachopitisha wagombea, wenye nazo na 'wenzetu' ndio wanapitishwa. Pia kukosekana kwa upinzani serious nako ni tatizo, wananchi wakitupiwa pilau, fulana na doti ya kanga mchezo umekwisha.
Bado Vyama vya ushindani havijafanya kazi nzuri huko vijijini. wao hufika huko wakati wa uchaguzi zaidi kulik nyakati za kawaida........hili ni tatizo na wasipoli-address CCM wataendelea kushinda....kwani wao wanaonekana sana kuwa wako karibu na wananchi.....