A crazy story wakati nipo chuo SUA

A crazy story wakati nipo chuo SUA

Cvez

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2018
Posts
4,471
Reaction score
13,626
Mwaka 2015 wakati nipo chuo SUA Mazimbu Campus ilikua majira ya jioni around saa moja siku moja kabla ya UE. Maeneo ya Dark City, Mauki kituo cha daladala kuna sehemu tunakaa kunywa kahawa au tangawizi na karanga. Nimeshakunywa kahawa yangu hapo najiandaa kwenda kupiga msuli wa zima moto. Kuna vijana wanauza kuku pale nikchukua kipaja kimoja pale kisha nikaenda kwa Mangi mmoja hivi anakaanga chipsi nikachukua sahani moja.

Enzi hizo ile mifuko ya plastic bado haijapigwa marufuku. Mangi akanifungia chipsi then nikachukua kile kipande cha kuku nikatumbukiza ndani ya mfuko wa chips. Nikachukua barabara ya kuelekea ghetto kwangu eneo la Makaburini hukohuko Dark City. Mara ghafla naona bodaboda inakuja upande wangu kwa kasi, nikajaribu kuikwepa lakini bahati mbaya ikanigonga kwenye mguu eneo la paja. Bodaboda akaanguka nami nikaanguka. Nashukuru Mungu sikuumia sana zaidi ya maumivu kiasi kwenye mguu na uvimbe baadae, yule dereva nae aliumia kiasi kulikua na wanachuo wengi pale wakataka kumpiga ila akaomba msamaha yakaisha.

Kumbuka mwanzoni nilisema nilikua nimebeba mfuko wa chips ndani yake kuna mfuko wenye kipande cha kuku. Kitu ambacho mpaka leo sielewi ilikuaje wakati naamka kutoka chini nilipoanguka mkononi nilikua nimeshika mfuko wenye kipande cha kuku ule wa chips ulianguka chini. Mpaka leo natafakari ilikuaje nikaweza kudaka mfuko uliokua ndani hali ya kua mfuko ulio nje nilishindwa kuuzuia?​
 
mkuu umunikumbusha mbali hiyo mitaa, dark city full vibaka, mauki, Kabla ya reli, kwa mama K, unit 1 Hadi 6, kule tabora, plus workers house

Mazimbu turifurahia maisha enzi hizo yupo mc Frans siku ya Pepa au UE
France alishawahi nichimba biti pale Freedom Square nilikua napiga paper la MTH nikajua mtu wa maana kumbe fala tu.
 
Hivi kuanzia miaka ya 1985 wasomi wanaomaliza SUA kozi kama hoticulture, agric. general, forest, agro economiy, home economics n. k huwa wanaenda kufanya kazi gani kwenye soko la ajira? Kwenye sekta za kilimo au wengine benki kama nmb?
 
Hivi kuanzia miaka ya 1985 wasomi wanaomaliza SUA kozi kama hoticulture, agric. general, forest, agro economiy, home economics n. k huwa wanaenda kufanya kazi gani kwenye soko la ajira? Kwenye sekta za kilimo au wengine benki kama nmb?
Toka zamani watu hao wapo wizara mbalimbali, mashirika ya umma Kama TFDA, TBS,
Mamlaka mbalimbali ikiwemo wilayani, mikoani, n.k
Ajira zipo, tatizo miaka hii ya 2010+ mfumo umeyumba na kuumiza watu
 
kwa hiyo wanalima nyanya sio vijijini au?
Hizo coarse mzee Zina Mambo mengi Sana,
Mfano. Pale SUA ipo coarse ya Mazingira,humo ndani Kuna mengi yanafundisha

Chemical issues, biological issues, physical issues, geographical issues hivyo usikariri
 
Mwaka 2015 wakati nipo chuo SUA Mazimbu Campus ilikua majira ya jioni around saa moja siku moja kabla ya UE. Maeneo ya Dark City, Mauki kituo cha daladala kuna sehemu tunakaa kunywa kahawa au tangawizi na karanga. Nimeshakunywa kahawa yangu hapo najiandaa kwenda kupiga msuli wa zima moto. Kuna vijana wanauza kuku pale nikchukua kipaja kimoja pale kisha nikaenda kwa Mangi mmoja hivi anakaanga chipsi nikachukua sahani moja.

Enzi hizo ile mifuko ya plastic bado haijapigwa marufuku. Mangi akanifungia chipsi then nikachukua kile kipande cha kuku nikatumbukiza ndani ya mfuko wa chips. Nikachukua barabara ya kuelekea ghetto kwangu eneo la Makaburini hukohuko Dark City. Mara ghafla naona bodaboda inakuja upande wangu kwa kasi, nikajaribu kuikwepa lakini bahati mbaya ikanigonga kwenye mguu eneo la paja. Bodaboda akaanguka nami nikaanguka. Nashukuru Mungu sikuumia sana zaidi ya maumivu kiasi kwenye mguu na uvimbe baadae, yule dereva nae aliumia kiasi kulikua na wanachuo wengi pale wakataka kumpiga ila akaomba msamaha yakaisha.

Kumbuka mwanzoni nilisema nilikua nimebeba mfuko wa chips ndani yake kuna mfuko wenye kipande cha kuku. Kitu ambacho mpaka leo sielewi ilikuaje wakati naamka kutoka chini nilipoanguka mkononi nilikua nimeshika mfuko wenye kipande cha kuku ule wa chips ulianguka chini. Mpaka leo natafakari ilikuaje nikaweza kudaka mfuko uliokua ndani hali ya kua mfuko ulio nje nilishindwa kuuzuia?​
Wewe ulibeba spea ya paja na uliumia kidogo paja, endapo ungeumia sana ile spea uliyokuwa umeing'ania mkononi ndiyo ungeitumia.
 
Hizo coarse mzee Zina Mambo mengi Sana,
Mfano. Pale SUA ipo coarse ya Mazingira,humo ndani Kuna mengi yanafundisha

Chemical issues, biological issues, physical issues, geographical issues hivyo usikariri
Nasikia siku hizi imeanzishwa kozi ya elimu/education.
 
Tajiri mmoja Mbeya.
Alikuwa mpiga Maji sana(konyagi kubwa).
Alikuwa na nyumba kubwa. Alikuwa hapiti getini anaruka ukuta.
Siku hiyo pombe zilikolea. Alivyoruka, akapoteza balance na kuanguka. Mbaya sana aliangukia kidogo, kikapiga jiwe. Asubuhi walimkuta amekufa huku mkono wa kulia ameunyoosha juu ukiwa umekamata chupa ya konyagi shingoni.
 
Solomon Mahlangu Campus (SMC) Mazimbu. Dah long time sana
 
Back
Top Bottom