Mkuu wala hujafanya kosa kutoa dukuduku lako, japo kuwa ingekuwa na nguvu zaidi kama ungelitoa duku duku lako kabla ujaacha kazi.Hapa wengine wanaweza kuona kwamba umeamua kuyasema yote kama kuwa komoa kwa vile walikataa kusikiliza ombi lako la mapumziko ya dharula.
Sema hoja ya matokeo mabovu imeweza kuzipa nguvu mambo uliyosema. Itasaidia wazazi kupata kujua hali halisi kabla wajaamua kwenda kutupa hela kwenye shule ambayo haina misingi bora ya kufundisha watoto wao.
Wakitoka hapo wanasoma copies za Nyangwine na kuangalia TV!Najua wanafunzi siku hizi wao na simu, wao na bongo fleva wao na mapenzi baasi!
mkuu,dukuduku langu nimelitoa nimeshatoka kwani nilishafikia wakati nikaona mimi ni profesional kama mourinho alivyoprofessional hvyo kuingiliwa kazi na bepari ambaye hajui miiko ya hii kazi ni kosa kubwa sana.Kwa hyo mimi niliona sitapoteza chochote kwa kuachana na dharau alizonazo huyu bepari.Nakukumbusha hayakuwa mapumziko ya dharura bali ni family problem ambayo nilikuwa nikaishughulikie mikoani.
Nimekuwepo pale nafanya kazi pale kama mwalimu.Kuwepo kwangu pale kwa miezi mitatu lilikuwa darasa ambalo sikutegemea kulipata.Sifanyi umbeya wala simhalibii bepari anayemilki shule wala siwahalibii walimu na wafanyakazi waliopo pale,wala siwaharibii wanafunzi na wazazi wao.Nimejifunza yafuatayo:1 sababu zilizotolewa na haki elimu na Ndarichako kuwa wanafunzi walifeli kwa sababu hawako makini,ni za ukweli wanafunzi hawasomi mpaka walazimishwe kwa kusimamiwa 2.Nimetambua kwa nini walimu wana badilisha shule kila uchao.Kwa bepari yule,walimu wanaoweza kufanya naye kazi ni wale ambao wamekosa sehemu nyingine,wamestaafu,wanaegesha au wanafki ambao wanajipendekeza kwa bepari.Kuwa mwl pale hauna tofauti na mbwa hauthaminiwi, unatumiwa tu kama box na wakati wowote waweza kutupwa kama takataka.3 Kazi ya ualimu inadharauliwa kuliko nilivyokuwa nafahamu.Bepari ambaye hata hajasomea ualimu anajifanya ndo anafahamu kuliko walimu waliosomea eti anawafundisha walimu.Usitarajie kiwango cha elimu kipande.4.Hakuna mkataba kwa kazi ya ualimu kwenye shule za private.Wakati wowote bepari akijisikia kukutimua anakutimua na wewe ukijisikia kusepa unasepa tu.5 Usipate na tatizo litakalokuchukua wiki mbilg hvi,utaambiwa uchague moja kati ya kazi au matatizo yako (ndicho kilichonitoa pale).6 Hakuna kodi ya serikali inayochukuliwa kwa sababu wafanyakazi wanachukulia mishahara dirishani.7 Hakuna hela inayopelekwa nssf.HAYO NDIO NILIYOJIFUNZA KWA SIKU 90 NILIPOKUWA PALE GREEN ACRES MABEZI
Mkuu wenger,wangekubali maombi yangu ningelalamikia mambo mengine kwa sababu nimetaja mambo kadhaa ambayo hayaendi sawa.Kwa great thnkers lazima nije kupata ushauri na maoni mbalimbali,mi inaniuma kuona taaluma niliyosomea inadhalilishwaNimekupata mkuu, nilijaribu kuangalia upande wa pili wa shillingi,je kama wangekubalimaombi yako ungekuja kutoa malalamiko?
Umetusaidia sana mkuu kwa habari na tunashukuru sana kwa kucheza "Mourhino" style lol.
Hivi wewe Mwalim kweli? au uliingilia tu kazi za watu? Tazama ulivyoandika, spellings unakosea, hujui pa kuweka "coma" wala "full-stop", uandishi wenyewe hohehahe! ama kweli, shule zimeingiliwa. Ni aibu wewe kusema kuwa u Mwalim.
Hivi wewe Mwalim kweli? au uliingilia tu kazi za watu? Tazama ulivyoandika, spellings unakosea, hujui pa kuweka "coma" wala "full-stop", uandishi wenyewe hohehahe! ama kweli, shule zimeingiliwa. Ni aibu wewe kusema kuwa u Mwalim.