89% of Tanzanians do not pay income tax - Don

BabuK

JF-Expert Member
Jul 30, 2008
1,845
329
Since the current income tax system mainly focus on the formal sector with little to no account of informal sector, about 89 per cent of Tanzanians do not pay tax revealed Mzumbe University Senior Lecturer Dr Prosper Ngowi yesterday.

He was addressing journalists during a workshop organised by ‘Action Aid International in Tanzania' to discuss the country's current taxation system.

The Norwegian Church Aid funded the research earlier this year, and the results show that the current taxation system focuses more on the formal sector hence takes to account but a spec of the productive masses leaving a majority of the informal sector unchecked and untaxed.

"There are 15 million people who can pay tax in the country, but only 1.5 million people are paying taxes…" Dr Ngowi said, adding that the system has a lot of loopholes that allow tax evasion.

Action Aid Resident Director, Aida Kianga highlighted the need for more discussions to table new tax collection methodology to expand the scope and in turn increase government revenue and allow for more community service programmes and other forms of government expenditure to provide better social services and jobs.

SOURCE: THE GUARDIAN
 
The Hypothesis test done is not correct. If you say 89% of Tanzanians do no pay taxes, do students, unemployed graduates, subsistence farmers, children have taxable income i.e. earn more than TShs. 2,040,000 a year.

The test should first establish among Tanzanians, how many are in employment self employed in business then the test should have done on this group. He has to go further and clarify what he mean by informal secter because currently you will find some business with huge wholesale shop and when comes to taxes, they are assessed under the small business with turnover of less than 20 million i.e. they dont produce audited accounts are required by the Income Tax Act 2004
 
Thanks Ndachuwa, there are many remaining questions regarding the news.
Even FDI's such as mobile companies, mining companies etc 'enjoy' the loopholes of such taxation system, they evade from paying tax.
 
ukifanya watu waanze kulipa kodo hata kesho hapa katika kila kitu kinachotakiwa kulipiwa kodo, wataandamana ajabu....si maisha yatakuwa magumu zaidi kwa watu na walikuwa wamezoea vya dezo? ajabu yake sasa, kama tukilipa kodi kwa uaminifu bila kuwepo mianya ya rushwa na katika kila kinachotakiwa, tutakusanya hela nyingi sana na haingekuwa lazima tutegemee misaada ya cameroon. ndo maana bongo unaweza kuishi kwa magumashi ukatajirika kwa haraka sana kama una akili....ALL IN ALL, IKI NI KITU KIBAYA SANA NDO MAANA WABONGO WANASHINDWA KUISHI NCHI ZINAZOFUATA MFUMO MZURI WA KODI.
 
ni watu 1.5 million nchini wanaolipa kodi kati ya 15millioni wanaoweza kulipa kodi

still we have long journey na ndio maana ukiimport kitu kidogo you have to pay alot.

 
  • Thanks
Reactions: SMU
Importers na wafanyakazi tu!

Sisi wafanyakazi ndio tunaipata kweli joto ya jiwe. Hao 89% nao wakianza kulipa kodi si nchi inakuwa tajiri.
 
na hizo VAT wanazoweka kwenye products zote sio kodi?

Embu kuwa more specific ni aina gani ya kodi unaongelea hapa.....all Tanzanians pay tax na haikwepeki....ukiongelea PAYE tax wafanyakazi ndo wanahusika,pamoja na import taxes....hapo nakubali inaweza ikawa iyp 11% ya watanzania......

Kodi inakusanywa nyingi sana,kupitia bidhaa,na wafanyakazi,,,zinatafunwa na wachache......huyo Dr. ngowi haja-specify,,,,so,,,kwa upande mwingine sikubaliani na hoja....my take ambayo naona inapunguza ukusanyaji wa kodi,ni kutotoza kodi kwenye mazao.

Regarding 80% ya watanzania kuwa wakulima....the remaining 8% tuseme ni hawa majamaa wa black market na vijana wa mjini kama tupendavyo kuwaita....system irekebishwe


cc.Harry Kitilya-TRA E.O
-minister of finance
-wanaJF woote
 
Waache kutuzingua bana,Inamaana hizo soda na bia tunazokumywa hatukatwi vat ambayo ndio kodi?
 
bora tu wasilipe, mana hatuoni kodi kinachosaidia zaidi ya kufadhili makundi ya wahuni tu hapa nchini, na zingine kuhifadhiwa nchi za nje tu, na kusamee kodi kwa wawekezaji wasio stahiki kusamehewa kodi, na kuridhika na wizi wa kodi unaoendelea waweezaji wageni tu.
 
na hizo VAT wanazoweka kwenye products zote sio kodi?.....embu kuwa more specific ni aina gani ya kodi unaongelea hapa.....all Tanzanians pay tax na haikwepeki....

Ungetaka awe specific kwa kiasi gani zaidi ya kusema income tax/kodi ya mapato?

..Since the current income tax system mainly focus on the formal sector with little to no account of informal sector, about 89 per cent of Tanzanians do not pay tax revealed Mzumbe University Senior Lecturer Dr Prosper Ngowi yesterday....
 
Ni utafiti mzuri and i support bse ela nyingi za serikali zaishia kwa watu
 
Hakuna mtanzania asiyelipa kodi,tena hii ni nchi ambayo haina huruma kwa wananchi wake hasa upande wa kodi,nenda kiwanda chochote cha sukari halafu ulia tozo za serikali kwenye kilo moja ya sukari kabla haijatoka kiwandani.
 
The Hypothesis test done is not correct. If you say 89% of Tanzanians do no pay taxes, do students, unemployed graduates, subsistence farmers, children have taxable income i.e. earn more than TShs. 2,040,000 a year.

The test should first establish among Tanzanians, how many are in employment self employed in business then the test should have done on this group. He has to go further and clarify what he mean by informal secter because currently you will find some business with huge wholesale shop and when comes to taxes, they are assessed under the small business with turnover of less than 20 million i.e. they dont produce audited accounts are required by the Income Tax Act 2004

Nakubaliana na wewe Nachuwa, kuna items nyingi ambazo zimepungua kwenye hii study, but at least focus ingekuwa income tax, maana kuna VAT na kodi za mazao au za masokoni etc
 
income tax is unconstitutional and it is a pre colonial idea. The truth is that there is no basis for income tax in the tz constitution : just think of it - why should the government think that what you get from your salary for instance is 100% profit.
 
wasiolipa kodi ni makampuni makubwa likiwemo la Norway waliofadhili huo utafiti kwani mpaka sasa hivi bado hawajalipa kodi ya gesi,makampuni ya simu na madini kwa uchache.Mwananchi wa Tanzania analipa kodi kiasi kikubwa kwani hata makampuni ya bia na sigara yanayoongoza kulipa kodi walipaji wakubwa ni wananchi wa kawaida,lakini viongozi wetu wakiwemo wabunge ndio wanaoongoza kutolipa kodi
Nini kifanyike?
Tuondoe misamaha yote ya kijinga ya kutolipa kodi.
Sifa ya kupata uongozi iwe pamoja na kuonyesha alivyolipa kodi kwa kipindi cha miaka 5 iliyopita kwani uzoefu umeonyesha wakwepaji wakubwa wa kodi ndio baadae wanaingia kwenye siasa ili waendelee kukwepa vizuri.
Tuwe na matumizi(tuheshimu walipa kodi) sahihi ya kodi za wananchi wakati wananchi wa kawaida ndio walipaji kodi wakubwa wanasiasa na viongozi wa umma wamekuwa wakijiongezea marupurupu bila kumjali mlipa kodi pia kama mnakumbuka kauli ya aliyekuwa waziri wa fedha Mramba wakati wa mchakato wa kununua ndege ya rais alisema lazima inunuliwe hata kama wananchi watakula nyasi kauli hii si tu ni dharau bali inaonyesha haiwajali walipa kodi
Ufisadi wa fedha za umma ukomeshwe kama baadhi ya mambo na mengine mengi yakitekelezwa na wananchi wakaelimishwa kutakuwa na msukumo mkubwa wa kulipa kodi
 
[h=2][/h] Jumamosi, Septemba 08, 2012 08:42 Maximilian Lukos, Dar es Salaam

IMEELEZWA kuwa zaidi ya asilimia 89 ya Watanzania wanaofanya biashara, hawalipi kodi kutokana na mfumo mbovu wa ukusanyaji kodi uliopo. Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam juzi na Mtaalamu wa Masuala ya Uchumi, Dk. Prosper Ngowi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya mfumo wa ukusanyaji kodi iliyoandaliwa na Taasisi ya Kimataifa ya Action Aid.
Dk. Ngowi ambaye pia ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Morogoro, alisema kutokana na utafiti alioufanya nchini kwa kufadhiliwa na Mfuko wa Misaada ya Makanisa ya Norway mwaka huu, aligundua mfumo huo wa ukusanyaji kodi, umelenga zaidi kwenye sekta rasmi kuliko sekta zisizo rasmi.

Alisema kwamba, kitendo cha kutojali sekta zisizo rasmi, kimesababisha upungufu mkubwa katika ukusanyaji wa kodi, kwa kuwa huhusisha watu wachache badala ya watu wengi.

"Kulingana na utafiti nilioufanya, nimebaini kuwa licha ya ukweli kwamba katika nchi yetu kuna watu milioni 15 ambao wanatakiwa kulipa kodi ambao asilimia kubwa wanatoka katika sekta rasmi na isiyo rasmi, lakini kati yao, watu milioni 1.5 ndio wanaolipa kodi kutoka sekta rasmi na kuacha watu milioni 13.5 ambao ni sawa na asilimia 89 bila kulipa kodi.

“Mfumo huo umesababisha Serikali kujitumbukiza katika kitanzi kwa kushindwa kukusanya kodi hiyo, hususani katika makampuni mbalimbali ya madini, ambayo kwa mwaka 2010 yalikwepa kulipa kodi yenye thamani ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 700,” alisema Dk. Ngowi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Action Aid hapa nchini, Aida Kianga, alisema Serikali inatakiwa kuandaa mikakati imara na kufanya majadiliano zaidi ili kugundua mbinu mpya za kukusanya na kupanua ukusanyaji wa kodi na kuongeza mapato ya Serikali.

"Suala hapa siyo kulipa kodi zaidi, kinachotakiwa hapa ni kutafuta njia stahiki ya kupanua wigo wa kukusanya kodi kwa ajili ya maendeleo yetu, vinginevyo hali itazidi kuwa mbaya,'' alisema Kianga.

Kwa upande wake, Mshauri Mwelekezi wa Masuala ya Demokrasia, Martha Jerome, kutoka katika taasisi hiyo, alisema Serikali inatakiwa kutengeneza mbinu za kuvutia watu ili waweze kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa.

[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
 
Safi kabisa.

Serikali ya kihuni inayoendeshwa na wahuni ukilipa kodi sio ndio jeuri na maauaji yangeongezeka.
Mpaka sasa hicho kiwango "kidogo" kilichokusanywa umeridhika na utumikaji wake? JK kila siku yuko angani na misafara ya kifahari akitalii duniani, ungempa hela zaidi angefanya nini kama sio kufuru?

Serikali hii haistahili zaidi ya inachopata. Huyo mtafiti naye sijui alifika mbali kiasi gani ktk utafiti wake; maana kila siku tunajiuliza makampuni makubwa kama simu na madini pamoja na biashara kubwa kubwa za vigogo na jamaa zao huwa hazilipi kodi. Ni vema angetafiti aina za walipa kodi ktk hiyo 11% ya walipaji. Tujue watu waliofaidi kwa ufisadi rasilimali zetu kama JK, EL, Mkapa, Mramba, Ridhiwani nk ndio wawe mfano kwa walipa kodi sio kwenda kuwakamua mama/dada zetu pale Manzese sokoni kwa kuweka chungu cha samaki na meza ya vitumbua.
 
Back
Top Bottom