Abdulhalim
Platinum Member
- Jul 20, 2007
- 17,199
- 3,016
Hilo ni suala jengine, la INCOME DISTRIBUTION.
Hio kikawaida ni changamoto, tena haipo kwenye Nchi za Ulimwengu wa tatu tu, bali hata huko kwenye maendeleo.
HOJA YA MSINGI.
1. Uchumi unakuwa.
2. Shilingi haijashuka thamani kwa asilimia hamsini tangu 2005; JK alipopata Urais.
3. kushuka kwa thamani ya shilingi sio lazima kiwe ni kiashiria cha kudorora kwa uchumi.
4. Kuwa na Currency Note ya Tshs sio jambo la kubezwa. kwani wangapi wanaenda sehemu mbali mbali na kutakiwa kulipa hela zaidi ya Tshs 50000 kununulia bidhaa au huduma?
Baada ya HOJA hio, tunaweza kufungua mjadala wa Income Distribution, ambao utakuwa mrefu mno.
Nawasilisha
Kama ni kweli basi ndo uje thamani ya tsh inavyoshuka. Wenzete Kenya note kubwa ni buku!
Umeyasikia wapi hayo?yap mniwieradhi kwahilo ni elfu hamsini (50,000)
Siwezi kushangaa Mawaziri na maofisa wakubwa wa Tanzania wana account wameweka hela zao kwenye USD.- Hii Ina maaana hata mawaziri na wachumi hawana imani na Noti ya nchi yao. Ni vipi watatunga policy za kuimarisha Tsh????
Nchi kama south africa Kiongozi kuwa na account ya USD ni kashfa kama wanzo ni kwa kificho ficho Nchi kama south africa unaweza kuhangaika kupata huduma kama huna rand lakini si kwa tanzania. Watunga sera na policy maker wametengeza mazingira hata sisi raia na wao tunakosa imani na fedha yetu kwa kisingizo cha soko huria.
Wadau, being critical is acceptable, but not over critical.
Siku zote mnapaswa kutumia vielelezo kujenga hoja, na sio kubwabwaja tu; na iwe vielelezo makini; sio UCHAKACHUZI.
mwaka 2005 JK alipoingia Madarakani Exchange rate ya Tshs against USD ilikue Tshs 1235 - 1260/ USD; sasa exchange rate ni Tshs 1475 - 1505/USD.
Hio devaluation ya Tshs against the USD haijaawahi kufikia hio ASILIMIA HAMSINI. Jamani, jamani, msichakachue data zisizokuwa zenyewe.
Likewise, kuna sababu kadhaa zinazoweza kupelekea Tsh kushuka thamani kulinganishwa na USD za kiuchumi ambazo sio viashiria vya Uchumi kuzorota. Ningewashauri huu uwanja musiuingie kwani utahitaji Darasa refu kidogo.
All in all, Economy ya Tanzania inakua.
Pili, kule Ulaya kuna noti ya Euro 1000, ambapo Euro moja ni Tshs 2000, hivyo kuna noti ya Tshs 2,000,000. Kama Benki kuu itaona umuhimu wa kutoa Currency ya 50,000/= hakuna mushkeli, sema itazunguka zaidi mijini.
Suala la Currency Substitution huchangiwa kwa kiasi kikubwa na INFLATION; ningeshauri mupitie Econimic Reviews za BoT
Wadau, being critical is acceptable, but not over critical.
Siku zote mnapaswa kutumia vielelezo kujenga hoja, na sio kubwabwaja tu; na iwe vielelezo makini; sio UCHAKACHUZI.
mwaka 2005 JK alipoingia Madarakani Exchange rate ya Tshs against USD ilikue Tshs 1235 - 1260/ USD; sasa exchange rate ni Tshs 1475 - 1505/USD.
Makame!
Absolutely you are wrong!
Uchumi haukui kwa kuchapisha minoti,for what i know and believe ..the more paper money a country prints for its own purpose the less currency will be worth!so kuprint minoti ya elfu50 ndiko kutapeleka nchi shimoni!you can't deal with inflationary trends by manipulating currency!
Hivi wachumi wa wizara ya fedha na central bank wamelala usingizi au ni huko kusoma kwa kukariri???Am sure hata interest rate and inflation rate hawajui ni kiasi gani kwa sasa!wajiulize tuna export kiasia gani na tuna import kiasia gani!
Nadhani ulikuwa una maanisha noti ya 100Pili, kule Ulaya kuna noti ya Euro 1000, ambapo Euro moja ni Tshs 2000, hivyo kuna noti ya Tshs 2,000,000. Kama Benki kuu itaona umuhimu wa kutoa Currency ya 50,000/= hakuna mushkeli, sema itazunguka zaidi mijini.
Uchumi upi unaokua? Kama wa mafisadi kweli unakua na utaendelea kukua ..at least kwa miaka mingine 5..lakini kwa wananchi wa kawaida uchumi unarejea nyuma..na mifano michache iliyotolewa na wadau ni kielelezo tosha..Mathalan..
--Kushuka kwa thamani ya TSh dhidi ya USD.
--Bidhaa muhimu kupanda bei wakati kwa kasi kisichoendana na kuongezeka kwa kipato.
Halafu labda niongezee hapo kwenye pengo la maskini na tajiri, pamoja na kwamba lipo hata kwene dunia ya kwanza, huwezi ukalinganisha paka wa NYC na paka wa Tandale..ingawa wote ni paka..hivi ni vitu viwili tafauti kabisa, sawa na mchana na usiku.
hata chumvi bei juu, dagaa, sembe, mkaa, nini dola? huku kwetu kijijini.
ACHA KUDANGANYA WATU WEWE!!!, HIYO NOTI YA EURO 1000 ULIIONA NCHI IPI YA ULAYA?. INAONEKANA WEWE NI MBAMBAISHAJI TU AU UNAPASIKIA TU ULAYA.SISI TUNAOISHI HUKU NOTI KUBWA KABISA NI EURO 500, HIYO 1000 UMEIBUNI WEWE MWENYEWE. Kwa taarifa yako hiyo noti ya 500 ni kwa matumizi makubwa sana. vitu vya kawaida kama nguo huwezi kukuta ikiuzwa Euro 500, tofauti na madafu yako hayo unayosema. Huku kuna hata sent za Euro zinatumika.Sasa fananisha na nchi yako hata sh 10 tu haina kazi.
Nadhani Makame hujajibu hoja za baadhi ya watu humu ndani kwanza naomba nikuulize maswali haya:-
a. Je noti 50,000 ina faida gani kwa watanzania? Huoni kama wakiprint hiyo ni dalili ya kwamba shilingi yetu imeshuka thamani mno kiasi serikali inaona umuhimu wa kutoa sarafu nyengine ili itumike katika uchumi?
b. Unasema uchumi umekuwa kwa mtazamo upi? An increase in the dollarization in Tanzania? Figures za kwenye kitabu tu ambazo hazireflect hali halisi ya mtanzania au umekuwa katika mifuko ya watu wachache?
c. Tatu tupambanulie hoja zako vizuri tupate kuelewa.
Sasa huoni kama jamii imeloose confidence na Tshs kutumika kama medium of exchange?
:tape::tape::tape:Atakuwa kashauriwa na Mugabe tu na hivi raisi wetu anavyoogopa wazee, na ije tu hiyo noti ilikuprove weakness ya TZ monetary system