Kuna misemo mingi sana inayotuasa au kutuonya tusifanye jambo kabla ya kutafakari. Ni nani aliye mkamilifu kati ya wanadamu? Hakuna! Msemo "Learning Through Mistakes" au kujifunza kutokana na makosa unatoa picha kamili ya kuwa mwanadamu kama mwanafunzi,hujifunza kutokana na makosa yanayomkabili katika maisha yake ya kila siku!
Wa Kusoma,hata wewe uzi wako una makosa katika baadhi ya maneno uliyoandika! Kwa mfano badala ya kuandika taarifa umeandika yaarifa, badala ya kuandika taarifa ya umeandika taarifa ha! Panapotakiwa kuwekwa herufi kubwa umeweka herufi ndogo! Nafikiri ulitakiwa kuandika The Guardian na siyo the guardian,kitu ambacho ni kosa japo maana ni ile ile!
Hata wadau wengine waliochangia uzi huu wamefanya makosa yale yale yanayotokea na kufanywa na watu mara nyingi tu katika uandishi! Kuna maneno ambayo yakikosewa kidogo tu wakati wa kuyaandika huleta maana mbaya kwa msomaji au wasomaji. Hivyo basi ni vyema na haki tukaelimishana na siyo kukashifiana.