Nilidhani hili jambo ni serious na halina utani. Mbona unajibu hivo ndugu yangu? Maana yake kila wanawake 10 walio na ajira karibu watano walipata hizo ajiri kwa kutoa mwili wao kama rushwa. Hii inaweza kuhusisha dada yako, mke wako, shemeji yako, au mchumba wako ambaye unataraji kumuuoa hivi karibuni atakapokuwa confirmed pale kazini kwao.
Huu ni udhaifu wa wanaume, tukiri tu wazi. Mzaha unaoufanya kwenye jambo nyeti kijamii linaonyesha kwa namna fulani au unafurahishwa na vitendo hivyo au ni mdau. Tuwalinde wanaweke, kama tukitaka ngono tusitumie advantage zetu na shida zao. Hii imezidi na inaudhi sana wanaume kujidai wana nguvu kumbe ni dhaifu wa kutupwa.