Ila kwakweli miradi mikubwa jamaa anaizindua kila siku, halafu anajinasibu tunatumia pesa zetu za ndani, hivi hizo pesa za ndani wanazitoa wapi, kama kwenye kulipa kodi mbona biashara zinafungwa kila siku sababu wanunuzi hawana pesa mifukoni, sasa hii kodi tunayoambiwa na TRA kila mwezi imeongezeka inatoka wapi?
Binafsi naona bora waseme tu ukweli, tunakopa toka sehemu tofauti kwa ajili ya kuendeleza hiyo miradi, na kwanini tunajenga vipya vya gharama kila siku wakati hali yetu ya uchumi hairuhusu, si bora ujenge kwa mpangilio, kimoja baada ya kingine, hata Roma haikujengwa kwa siku moja, mnawaumiza wenye vipato vya chini, mishahara hampandishi mwaka wa nne watu wanateseka tu.