2016 Nenda Baba !!!

Kikarara78

JF-Expert Member
Nov 18, 2010
1,495
901
2016 NENDA BABA, TUNASHUKURU KWA YOTE.

1. Yametumbuliwa majipu mpaka chunusi nenda Baba.
2. Umefanya Kabeji iwe nyingi kuliko nyama siku ya Christmas nenda Baba.
3. Umefanya tujue kulikuwa Faru John na Faru Hadija yatosha Baba.
4. Ajira imezidi kuota mbawa, Baba wasalimie, mwambie 2017 akija anisajili kuwa mwanasiasa huenda nikapata dili.
5. Tumeshuhudia homa ya Zika ikileta kizaazaa nenda Baba.
6. Tumeshuhudia wimbo mpya wa Taifa Muziki - Darasa, acha maneno nenda 2016.
7. Tumeshuhudia watu wa dar wakitamani kurudi mikoani wasijue kote namba zinasomeka nenda Baba.
8. Baba kugombania rimoti na watoto, utaenda wapi pesa hakuna acha atulie kama daktari wa zamu nenda Baba.
9. Tumeshuhudia ufunguzi wa daraja jipya na watu tunakesha kufanyia shooting na kupiga picha, tuliliona wapi asante Baba.
10. Tetemeko likawatesa ndugu zetu wa kagera na watu wakataka kupiga pesa kupitia mgongo wake, 2017 usifanye kama mwenzako Baba.
11. Mvua za masika nazo zimekuwa adimu sijui nazo zinahakikiwa? nenda Baba.
12. Sijasahau bomberdier zikanunuliwa Baba wakaziita panga boy asante Baba.
13. Simba wakaongoza ligi ,kaa nao Baba wamekuwa wagumba muda mrefu.

EMBU ONGEZA NA ZAKO HAPO CHINI
 
Back
Top Bottom