MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Habari zenu ndugu zangu. Ni muda mrefu sana sija post kitu wala kuanzisha thread humu ndani bali nimekua nikipitia tu maneno ya wengine. Wahenga walisema ni bora zaidi kusikiliza kuliko kuongea. Kwa leo nimeona nitupie senti mbili zangu kwenye hali ya kisiasa nchini hasa kuelekea 2015.
Kwanza kabisa niseme nina amini kwa asilimia 100 kwamba 2015 ndiyo utakua uchaguzi muhimu kuliko yote katika historia ya Tanzania, hata kushinda ule wa 1995 ambao ndiyo ulikua uchaguzi wa kwanza kushirikisha vyama vingi. Pia niseme kwamba huu siyo utabiri wa kishehe Yahya bali ni jinsi tu ninavyo ona mambo yanavyo kwenda. 2015 bado ni mbali na tunayo yaona leo yanaweza yakawa tofauti ndani ya miaka mitatu. Sasa nitaje sababu za mimi kuhifikia hivi.
1. Umaarufu ya upinzani na wapinzani:
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Upinzani (haswa Chadema) umepiga hatua kubwa sana hii miaka saba. Ni nani ambae 2005 ange dhani kura za Kikwete zingine pungua toka asilimia themanini na kitu mpaka asilimia sitini na kitu? Ni nani 2005 angeamini leo hii Chadema ingekua na wabunge zaidi ya arobaini? Upinzani umekomaa Tanzania, vyama vya upinzani vimeanza kukua wakati CCM imekua ikizeeka.
Zama za CCM kumsimamisha mgombea yoyote yule na kutegemea atashinda kwa sababu tu ni mwanaCCM zimepita. 2015 CCM lazima iwe makini ya watu watakao wapa dhamani ya kupeperusha bendera ya chama kuanzia ubunge mpaka uraisi. Wakidhani wanaweza mpachika yoyote na kumpromote kwa vile tu ni mwana CCM wataumia. Mfano vizuri ni uchaguzi uliopita ambao ulimpa kijana mdogo tena asiye na uzoefu wa kisiasa Nassari ushindi. Mbombea wa CCM kwenye uchaguzi huo alikua bwana Sioi na aliwekwa kwa vile tu ni mtoto wa marehemu mbunge mteule wa jimbo hilo na mkwe wa Lowasa.
2. Viongozi wa CCM sasa wanaweza kosoana wenyewe kwa wenyewe:
Japo bado kuna nidhamu ya woga, tumeona baadhi ya viongozi wa CCM ambao wapo tayari kutofautiana na chama chao kwenye maswla fulani. Mfano mzuri ni Bunge lililo pita na zile sign 75 alizo kusanya zito. Kipole pole nidhamu hii ya woga inapungua na tutarajie mengi zaidi huko mbeleni.
3. CCM haitaki kukubali hali halisi:
CCM bado haijakubali kuwa upepo unabadilika. Hakuna kitu kibaya kama mgonjwa kuogopa kwenda hospitali kwa kuhofia majibu. Matokeo yake ni kufuga ugonjwa mpaka unakuua. CCM is in DENIAL. Kama CCM inataka kujiokoa ikubali kuwa ina dalili ya maradhi, ikubali kujipima na kuanza kutafuta tiba mapema. Ikisubiri 2015 ugonjwa unaweza ukawa mbaya kiasi cha kuto kutibika.
4. Wananchi wamebadilika:
Sasa hivi Watanzania wameinuka. Japo mbali kuna safari ndefu ya Watanzania kuanza kujitambua na kutambua haki yao bado tunaona ongezeko la watu ambao sasa wanajua viongozi ni watumishi wao na si mabosi wao. Jinsi watanzania watakavyo endelea kutambua hili ndiyo itakapo zidi kuwawia vigumu CCM kutumia ubabe.
5. Vyombo vya dola vinaundwa na walalahoi:
Tumeona serikali mara kadhaa ikitumia nguvu ya dola kulinda utawala wake. Ila serikali inasahau kuwa asilimia kubwa ya vyombo hivi vinaundwa na wananchi walalahoi. Leo hii polisi wa kawaida anaetumwa kwenda kupiga wananchi wenzake hana tofauti ya kimaslahi wala kimaisha ya hao watu anaoenda kupiga. Itafika kipindi nacho hawa walalahoi wanaounda dola watachoka kuburuzwa na serikali. Je wakuu wa vyombo hivi wataingia wenyewe barabarani?
Hali ya kisiasa Tanzania sasa hivi ni onyo kwa CCM na changamoto kwa upinzani. Tutaona mengi kuelekea 2015. Mwenyezi Mungu atujalie tu uzima na afya.
Kwanza kabisa niseme nina amini kwa asilimia 100 kwamba 2015 ndiyo utakua uchaguzi muhimu kuliko yote katika historia ya Tanzania, hata kushinda ule wa 1995 ambao ndiyo ulikua uchaguzi wa kwanza kushirikisha vyama vingi. Pia niseme kwamba huu siyo utabiri wa kishehe Yahya bali ni jinsi tu ninavyo ona mambo yanavyo kwenda. 2015 bado ni mbali na tunayo yaona leo yanaweza yakawa tofauti ndani ya miaka mitatu. Sasa nitaje sababu za mimi kuhifikia hivi.
1. Umaarufu ya upinzani na wapinzani:
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Upinzani (haswa Chadema) umepiga hatua kubwa sana hii miaka saba. Ni nani ambae 2005 ange dhani kura za Kikwete zingine pungua toka asilimia themanini na kitu mpaka asilimia sitini na kitu? Ni nani 2005 angeamini leo hii Chadema ingekua na wabunge zaidi ya arobaini? Upinzani umekomaa Tanzania, vyama vya upinzani vimeanza kukua wakati CCM imekua ikizeeka.
Zama za CCM kumsimamisha mgombea yoyote yule na kutegemea atashinda kwa sababu tu ni mwanaCCM zimepita. 2015 CCM lazima iwe makini ya watu watakao wapa dhamani ya kupeperusha bendera ya chama kuanzia ubunge mpaka uraisi. Wakidhani wanaweza mpachika yoyote na kumpromote kwa vile tu ni mwana CCM wataumia. Mfano vizuri ni uchaguzi uliopita ambao ulimpa kijana mdogo tena asiye na uzoefu wa kisiasa Nassari ushindi. Mbombea wa CCM kwenye uchaguzi huo alikua bwana Sioi na aliwekwa kwa vile tu ni mtoto wa marehemu mbunge mteule wa jimbo hilo na mkwe wa Lowasa.
2. Viongozi wa CCM sasa wanaweza kosoana wenyewe kwa wenyewe:
Japo bado kuna nidhamu ya woga, tumeona baadhi ya viongozi wa CCM ambao wapo tayari kutofautiana na chama chao kwenye maswla fulani. Mfano mzuri ni Bunge lililo pita na zile sign 75 alizo kusanya zito. Kipole pole nidhamu hii ya woga inapungua na tutarajie mengi zaidi huko mbeleni.
3. CCM haitaki kukubali hali halisi:
CCM bado haijakubali kuwa upepo unabadilika. Hakuna kitu kibaya kama mgonjwa kuogopa kwenda hospitali kwa kuhofia majibu. Matokeo yake ni kufuga ugonjwa mpaka unakuua. CCM is in DENIAL. Kama CCM inataka kujiokoa ikubali kuwa ina dalili ya maradhi, ikubali kujipima na kuanza kutafuta tiba mapema. Ikisubiri 2015 ugonjwa unaweza ukawa mbaya kiasi cha kuto kutibika.
4. Wananchi wamebadilika:
Sasa hivi Watanzania wameinuka. Japo mbali kuna safari ndefu ya Watanzania kuanza kujitambua na kutambua haki yao bado tunaona ongezeko la watu ambao sasa wanajua viongozi ni watumishi wao na si mabosi wao. Jinsi watanzania watakavyo endelea kutambua hili ndiyo itakapo zidi kuwawia vigumu CCM kutumia ubabe.
5. Vyombo vya dola vinaundwa na walalahoi:
Tumeona serikali mara kadhaa ikitumia nguvu ya dola kulinda utawala wake. Ila serikali inasahau kuwa asilimia kubwa ya vyombo hivi vinaundwa na wananchi walalahoi. Leo hii polisi wa kawaida anaetumwa kwenda kupiga wananchi wenzake hana tofauti ya kimaslahi wala kimaisha ya hao watu anaoenda kupiga. Itafika kipindi nacho hawa walalahoi wanaounda dola watachoka kuburuzwa na serikali. Je wakuu wa vyombo hivi wataingia wenyewe barabarani?
Hali ya kisiasa Tanzania sasa hivi ni onyo kwa CCM na changamoto kwa upinzani. Tutaona mengi kuelekea 2015. Mwenyezi Mungu atujalie tu uzima na afya.