Habari za leo Wanajamvi?
Leo najaribu kuvuta picha ya uchaguzi wa 2020. Nakumbuka kwa umri wangu, na kwa chaguzi nilizoshiriki so far uchaguzi wa 2015 ulikuwa mgumu sana, pengine hata mara kadhaa zaidi ya ugumu wa uchaguzi wa mwaka 1995. Yawezekana ukawa ni uchaguzi wa kwanza mgumu ambao CCM iliona kuna kila dalili za kuondolewa madarakani na kuwa kambi ya upinzani.
Uchaguzi wa 2015 ulihubiri mabadiliko. Ilikuwa ni mabadiliko katika mfumo mzima wa serikali na sekta/idara zake, na katika mfumo wa uchumi ambao ungeleta mabadiliko hata kwa sekta binafsi. Kiufupi yalihubiriwa mabadiliko katika mfumo mzima wa maisha ya wananchi. UKAWA na upinzani wengine nje ya UKAWA walihubiri mabadiliko. CCM baada ya kuona haja hiyo ya wananchi, waliahidi kwamba mabadiliko yaliyotarajiwa na wananchi hao yangeweza kupatikana ndani yake pia. Ilikuwa ni ngumu kuwaamini pengine na kile kilichodaiwa kuwa ni ahadi zisizotekelezeka, lakini mgombea wa CCM Mh. JPM aliwahakikishia wananchi kwamba angewaletea mabadiliko waliyokuwa wakiyatarajia.
Tangu Rais JPM aingie madarakani tumeona mapinduzi makubwa katika maeneo mbalimbali, kuanzia katika nidhamu kwa watumishi wa umma hadi katika mfumo wa uchumi. Tumeona elimu ya msingi ikitolewa bure, uwezo ndani wa ndani wa kugharamia miradi ukiongezeka, rasilimali zikilindwa kwa nguvu zote, na sekta ya uchumi kwa ujumla ikiboreshwa (umeme wa uhakika, usafiri wa reli, barabara, maboresho bandarini, airport, ukusanyaji kodi nk).
JPM anajitahidi sana kwenda beyond expectation, hali inayonifanya nione kwamba wapinzani watakuwa na kibarua kizito cha kuhubiri aina ya “mabadiliko” watakayoyataka, iwapo wataendelea na kauli mbiu hiyo hapo 2020; kwani mabadiliko yamekwisha patikana na yanaendelea kupatikana chini ya serikali ya awamu ya tano.
Iwapo upinzani watahubiri mabadiliko, Je ni mabadiliko gani hayo?
Benmpo
Leo najaribu kuvuta picha ya uchaguzi wa 2020. Nakumbuka kwa umri wangu, na kwa chaguzi nilizoshiriki so far uchaguzi wa 2015 ulikuwa mgumu sana, pengine hata mara kadhaa zaidi ya ugumu wa uchaguzi wa mwaka 1995. Yawezekana ukawa ni uchaguzi wa kwanza mgumu ambao CCM iliona kuna kila dalili za kuondolewa madarakani na kuwa kambi ya upinzani.
Uchaguzi wa 2015 ulihubiri mabadiliko. Ilikuwa ni mabadiliko katika mfumo mzima wa serikali na sekta/idara zake, na katika mfumo wa uchumi ambao ungeleta mabadiliko hata kwa sekta binafsi. Kiufupi yalihubiriwa mabadiliko katika mfumo mzima wa maisha ya wananchi. UKAWA na upinzani wengine nje ya UKAWA walihubiri mabadiliko. CCM baada ya kuona haja hiyo ya wananchi, waliahidi kwamba mabadiliko yaliyotarajiwa na wananchi hao yangeweza kupatikana ndani yake pia. Ilikuwa ni ngumu kuwaamini pengine na kile kilichodaiwa kuwa ni ahadi zisizotekelezeka, lakini mgombea wa CCM Mh. JPM aliwahakikishia wananchi kwamba angewaletea mabadiliko waliyokuwa wakiyatarajia.
Tangu Rais JPM aingie madarakani tumeona mapinduzi makubwa katika maeneo mbalimbali, kuanzia katika nidhamu kwa watumishi wa umma hadi katika mfumo wa uchumi. Tumeona elimu ya msingi ikitolewa bure, uwezo ndani wa ndani wa kugharamia miradi ukiongezeka, rasilimali zikilindwa kwa nguvu zote, na sekta ya uchumi kwa ujumla ikiboreshwa (umeme wa uhakika, usafiri wa reli, barabara, maboresho bandarini, airport, ukusanyaji kodi nk).
JPM anajitahidi sana kwenda beyond expectation, hali inayonifanya nione kwamba wapinzani watakuwa na kibarua kizito cha kuhubiri aina ya “mabadiliko” watakayoyataka, iwapo wataendelea na kauli mbiu hiyo hapo 2020; kwani mabadiliko yamekwisha patikana na yanaendelea kupatikana chini ya serikali ya awamu ya tano.
Iwapo upinzani watahubiri mabadiliko, Je ni mabadiliko gani hayo?
Benmpo