2015: Kiongozi Tumtakaye - MTU WA WATU...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,998
Wazo la Leo (kutoka lililopita). Sifa za huyu mtu ambaye tunataka aje na kuwa Rais wetu na nyuma yake safu nzima ya viongozi wenye uwezi nilisema ni lazima ajitofautishe kwenye mambo kadhaa. Lakini kabla hatujaangalia haya naomba niangalia sifa moja ambayo niliidokeza mara ya mwisho - MTU WA WATU.

Kwa bahati mbaya maana ya "mtu wa watu" kwa baadhi ya watu wanafikiria ni mtu "maarufu kwa watu" au "anayependwa na watu". Maana ya kuwa "mtu wa watu" ni zaidi ya hivyol. Ninapuzungumzia ni "mtu wa watu" nina mambo matatu kichwani.

a. Anayetokana na Watu: Kiongozi huyo siyo anayejipachika au kupachikwa kwa watu. Bali watu (wananchi) wanamtambua uwezo wake, vipaji vyake na ni wao ndio wanamsukuma kuwatumikia. Na yeye akitambua uzito wa utumishi huo anasita. Anasita si kwa sababu hana uwezo au nia ya kuwatumikia la hasha! Anasita kwa sababu anatambua uzito (the gravity) ya wito wa kuwatumikia watu. Kwa hiyo anakuwa ni 'the reluctant hero'. Lakini anaposhawishiwa na wananchi wake na baadaye anakubali kuwatumikia basi huyo anakuwa ni kiongozi wa 'watu'.

b. Anayeongozwa na utu wa watu wake: Mojawapo ya mambo ambayo yanatusumbua sana kwa viongozi wetu ni suala la kuangalia vitu na si utu wa watu. Tunaangalia nani ni 'mwenzetu' kwa misingi ya urafiki, udugu, udini, ukabila na hata uchama. Kiongozi wetu ajaye ni lazima awe juu ya hivi vinavyotutofautisha bali aongozwe na kitu kimoja kinachotuunganisha wote - utu wetu. Hatutaki wala kustahili kiongozi anayeongozwa na "uenzetu huu" unaoangalia dini, kabila, rangi, hali ya maisha, elimu au ujiko wa kisiasa. Mtu wa watu ni yule anayejali UTU WA WATU wote.

c. Anayewejabika kwa watu: Sasa kiongozi ajaye si yule ambaye anatoka kwa watu au anaongozwa na utu wa watu wote bali zaidi ni yule anayewajibikwa kwa wananchi wake. Hatutaki kiongozi au Rais ambaye anajiona au kujifikiria kuwa ni "juu" ya wananchi. Mojawapo ya matatizo makubwa ambayo tunayaona (angalau kwa watu wenye msimamo wangu) ni kuwa viongozi wengi wanajiona ni "juu" ya wananchi kiasi kwamba wamekuwa na mawazo ya kikoloni. Yaani, wako pale kuwafanyia watu vitu - wasiulizwe, wasipingwe, wasihojiwe na wala wasiwajibishwe na wananchi wao. Wakati wakoloni walikuwa wanajali zaidi kuwajibishwa na "Ofisi ya Makoloni" kule Uingereza watawala wetu wa sasa wanajali sana kuwajibishwa na "vyama vya siasa". Wanaogopa zaidi vyama vyao kuliko wananchi wanaowatumikia! Isipokuwa wakati wa uchaguzi tu!

Tunataka kiongozi ambaye anatambua na kukubali kuwa yeye ni mtumishi wa wananchi. Na kutokana na utumishi huo basi wananchi kwake ni watu wa juu kuwaheshimu, kuwatii na kukubali mamlaka yao. Leo hii wale waliowekwa kutawala juu yetu wanawachukulia wananchi kwa dharau iliyoki(utter contempt). Hawanyenyekei mbele ya wananchi, wanajiaminisha kuwa wao 'ni bora' na wanastahili kuwepo pale. Matokeo yake wamekuwa wakifanya lolote, vyovyote, na kwa lolote. Hatutaki viongozi kama hao.

Tunaposema "mtu wa watu" hatumaanishi mwenye sura nzuri au tabasam zuri; hatumaanishi mwenye kujichekelesha, kucheka, kucheka cheka na kuchekewa au kuchekelewa na watu. Na kwa hakika tunaposema "mtu wa watu" hatumaanishi yule mwenye kugongewa, kupongezwa au kushangiliwa na watu. Bali yule ambaye anatoka kwa watu, anajali utu wa watu wote na anatambua kuwa anawajibika kwa watu huku akiheshimu mahitaji, matamanio na mamlaka yao.

Huyu ndiye MTU WA WATU!

Lakini uwezo wa mtu tunayemtaka kuwa kiongozi unaweza kuoneshwa vipi?

Wazo hili litaendelea inshallah.
 
watawala wetu wa sasa wanajali sana kuwajibishwa na "vyama vya siasa". Wanaogopa zaidi vyama vyao kuliko wananchi wanaowatumikia! Isipokuwa wakati wa uchaguzi tu!

Tunataka kiongozi ambaye anatambua na kukubali kuwa yeye ni mtumishi wa wananchi. Na kutokana na utumishi huo basi wananchi kwake ni watu wa juu kuwaheshimu, kuwatii na kukubali mamlaka yao.
Wazo hili litaendelea inshallah.
Nimependa sana ulivo weka hapo mkuu. Asante sana.
 
Lowassa asingekuwa mwizi ni mchapa kazi hodari sana na anaogopewa sio dhaifu tatizo mwizi
 
Kiongozi tunayemtaka ni mwenye jeuri kwa maslahi ya nchi, si mwema na mtu wa watu. Tumeona wengi wanaopewa nafasi kwa wasifu huu, na wote ni hovyo hovyo tu! Utu wao ni kuuza watu na mali zao wakiwa ndani, huku wanakuchekea, *{%[#[?]*]!]?\€\
 
Hii sifa ya mtu wa watu ikitumika kwa mara nyingine tena kutupatia kiongozi wa awamu ya tano tutakuwa bado na nchi inatwa tanzania? sina hakika katika hili.
 
Suala hapa siyo limewekwaje ni litatekelezwaje? tunataka katiba itamke jinsi ya kumpata kiongozi huyu.
 
Najua unapoelekea umeanza na kigezo si umri, ukaja uzoefu which is subjective sasa unakuja spin off nyengine awe mtu wa wa watu. Ila usisahau kipengele kimoja tu ASIWE MDINI MAANA TANZANIA YA SASA NI KAA LA MAWE!!!! au TANKI LA PETROLI!!!! Tafakari
 
Wazo la Leo (kutoka lililopita). Sifa za huyu mtu ambaye tunataka aje na kuwa Rais wetu na nyuma yake safu nzima ya viongozi wenye uwezi nilisema ni lazima ajitofautishe kwenye mambo kadhaa. Lakini kabla hatujaangalia haya naomba niangalia sifa moja ambayo niliidokeza mara ya mwisho - MTU WA WATU.

Kwa bahati mbaya maana ya "mtu wa watu" kwa baadhi ya watu wanafikiria ni mtu "maarufu kwa watu" au "anayependwa na watu". Maana ya kuwa "mtu wa watu" ni zaidi ya hivyol. Ninapuzungumzia ni "mtu wa watu" nina mambo matatu kichwani.

a. Anayetokana na Watu: Kiongozi huyo siyo anayejipachika au kupachikwa kwa watu. Bali watu (wananchi) wanamtambua uwezo wake, vipaji vyake na ni wao ndio wanamsukuma kuwatumikia. Na yeye akitambua uzito wa utumishi huo anasita. Anasita si kwa sababu hana uwezo au nia ya kuwatumikia la hasha! Anasita kwa sababu anatambua uzito (the gravity) ya wito wa kuwatumikia watu. Kwa hiyo anakuwa ni 'the reluctant hero'. Lakini anaposhawishiwa na wananchi wake na baadaye anakubali kuwatumikia basi huyo anakuwa ni kiongozi wa 'watu'.

b. Anayeongozwa na utu wa watu wake: Mojawapo ya mambo ambayo yanatusumbua sana kwa viongozi wetu ni suala la kuangalia vitu na si utu wa watu. Tunaangalia nani ni 'mwenzetu' kwa misingi ya urafiki, udugu, udini, ukabila na hata uchama. Kiongozi wetu ajaye ni lazima awe juu ya hivi vinavyotutofautisha bali aongozwe na kitu kimoja kinachotuunganisha wote - utu wetu. Hatutaki wala kustahili kiongozi anayeongozwa na "uenzetu huu" unaoangalia dini, kabila, rangi, hali ya maisha, elimu au ujiko wa kisiasa. Mtu wa watu ni yule anayejali UTU WA WATU wote.

c. Anayewejabika kwa watu: Sasa kiongozi ajaye si yule ambaye anatoka kwa watu au anaongozwa na utu wa watu wote bali zaidi ni yule anayewajibikwa kwa wananchi wake. Hatutaki kiongozi au Rais ambaye anajiona au kujifikiria kuwa ni "juu" ya wananchi. Mojawapo ya matatizo makubwa ambayo tunayaona (angalau kwa watu wenye msimamo wangu) ni kuwa viongozi wengi wanajiona ni "juu" ya wananchi kiasi kwamba wamekuwa na mawazo ya kikoloni. Yaani, wako pale kuwafanyia watu vitu - wasiulizwe, wasipingwe, wasihojiwe na wala wasiwajibishwe na wananchi wao. Wakati wakoloni walikuwa wanajali zaidi kuwajibishwa na "Ofisi ya Makoloni" kule Uingereza watawala wetu wa sasa wanajali sana kuwajibishwa na "vyama vya siasa". Wanaogopa zaidi vyama vyao kuliko wananchi wanaowatumikia! Isipokuwa wakati wa uchaguzi tu!

Tunataka kiongozi ambaye anatambua na kukubali kuwa yeye ni mtumishi wa wananchi. Na kutokana na utumishi huo basi wananchi kwake ni watu wa juu kuwaheshimu, kuwatii na kukubali mamlaka yao. Leo hii wale waliowekwa kutawala juu yetu wanawachukulia wananchi kwa dharau iliyoki(utter contempt). Hawanyenyekei mbele ya wananchi, wanajiaminisha kuwa wao 'ni bora' na wanastahili kuwepo pale. Matokeo yake wamekuwa wakifanya lolote, vyovyote, na kwa lolote. Hatutaki viongozi kama hao.

Tunaposema "mtu wa watu" hatumaanishi mwenye sura nzuri au tabasam zuri; hatumaanishi mwenye kujichekelesha, kucheka, kucheka cheka na kuchekewa au kuchekelewa na watu. Na kwa hakika tunaposema "mtu wa watu" hatumaanishi yule mwenye kugongewa, kupongezwa au kushangiliwa na watu. Bali yule ambaye anatoka kwa watu, anajali utu wa watu wote na anatambua kuwa anawajibika kwa watu huku akiheshimu mahitaji, matamanio na mamlaka yao.

Huyu ndiye MTU WA WATU!

Lakini uwezo wa mtu tunayemtaka kuwa kiongozi unaweza kuoneshwa vipi?

Wazo hili litaendelea inshallah.

Hakuna kitu kama hicho na huyo mtu umemtengeneza wewe lakini kiuhalisia hayupo!

Nitakwambia kwa nini, Raisi yoyote atakayekuja iwe hapa kwetu au kwingine kokote ni lazime awe na hela aidha pesa ziwe zake au kama hana basi mtu mwingine ampe, na kwa hali jinsi ilivyo wanasiasa wengi ni maskini na ili uweze kushinda uchaguzi unahitaji vitu 3 HELA, HELA na HELA bila hivyo hata awe mtu wa Mungu achilia mbali wa watu hatoshinda kamwe na hatofika popote na kampeni zake.

Huo ndio ukweli na uhalisia mengine yote ni kujidanganya! Zito anakula rushwa kama ni kweli kuhusu shutuma hizo unafikiri kwa nini? sio kwa sababu ndani ya moyo wake ni mpenda Rushwa bali anahitaji pesa na yeye anatoka umaskinini, pesa atapata wapi? Bila pesa hawezi fanya chochote hata na yeye anajua hilo!
 
Mtu wa watu kama le mutuz?

Akiisoma hii mada yako , anaweza kujitahidi kuziba nyufa ili 2015 awe ametimiza vigezo vyako.
 
Tutaendelea inshallah wiki ijayo na wazo hili kuweza kuonesha kuwa ni lazima tuinue kiwango (raising the standard) ya viongozi tunaowataka. Tusije kuwa na viwango ambavyo vitatupa viongozi wanaostahili.
 
Tutaendelea inshallah wiki ijayo na wazo hili kuweza kuonesha kuwa ni lazima tuinue kiwango (raising the standard) ya viongozi tunaowataka. Tusije kuwa na viwango ambavyo vitatupa viongozi wanaostahili.

Dedication.
A MAN OF THE PEOPLE~by CHINUA ACHEBE
 

Attachments

  • 180px-ManOfThePeople.JPG
    180px-ManOfThePeople.JPG
    14 KB · Views: 36
Hizo zote ulizozitaja hapo juu siyo sifa za kiongozi. Au niseme labda siyo sifa ambazo mtu anayependa madaraka huwa nazo.
Ni mtu anayependa madaraka kuliko wenzake ndiyo hupata madaraka, na si vinginevyo.
Kwa hiyo mtu wa watu (kwa maana uliyoelezea) hawezi kuwa kiongozi.
Ndiyo maana kunakuwa na katiba ambayo itampunguzia mpenda madaraka (ambaye mara nyingi sana huwa kiongozi) kujifikiria kuwa yupo juu ya wananchi.
Hilo ndiyo suala la kuzungumzia iwapo utataka kiongozi mwenye sifa ulizotaja..... huwa hawaji naturally like we'd like to think.
 
Hizo zote ulizozitaja hapo juu siyo sifa za kiongozi. Au niseme labda siyo sifa ambazo mtu anayependa madaraka huwa nazo.
Ni mtu anayependa madaraka kuliko wenzake ndiyo hupata madaraka, na si vinginevyo.
Kwa hiyo mtu wa watu (kwa maana uliyoelezea) hawezi kuwa kiongozi.
Ndiyo maana kunakuwa na katiba ambayo itampunguzia mpenda madaraka (ambaye mara nyingi sana huwa kiongozi) kujifikiria kuwa yupo juu ya wananchi.
Hilo ndiyo suala la kuzungumzia iwapo utataka kiongozi mwenye sifa ulizotaja..... huwa hawaji naturally like we'd like to think.

Twende taratibu tu; hata sijazungumzia "sifa za viongozi"; wazo hili litakapoendelea utazidi kuelewa ninachozungumzi ni nini hasa.
 
- Una maana Le Biig Shoow, jamani niacheni nipumzike kidogo tu! ha! ha! ha! ha!

Wilie!


Swalama Mkuu!

Willie, kama individuals wangekuwa wana Personal Manager, ningeomba kazi kwako.

The thing is, you have some talents and certain behavior inclination which can make you a rich. Very rich in did.

The question is: How do you use that talents? If you ask me, I will tell you politics is not your line ingawa unaipenda sana.

Let us keep networked and connected . . . .
 
MKJJ, I tend to agree. It is all about Leadership:

1. Kiongozi wa watu ni yule ambaye akisema watu wanamsikiliza no matter kama ana position au hana. Mandela aliongoza akiwa gerezani.

2. Kiongozi wa watu ni yule ambaye anapigania maslahi ya watu wake no matter what. Japokuwa kuna baadhi ya sheria dhalimu, Kiongozi wa kweli ataweka mbele maslahi ya watu wake bila kujali sheria au kanuni even if it means kuitwa dictator.

3. Kiongozi wa watu ni yule ambaye analeta mabadiliko kwa ku-influence au kushawishi na watu wakakubali kwa hiari kwa moyo mkunjufu. Haitaji kutumia nguvu, sheria wala, hila au vyombo vya dola kuwashawishi watu.

4. Kiongozi wa watu ni lazima awe Muadilifu na uadilifu wake uwe wa asili unaotokana na utu wake na wala si wa woga wa yeye asije kuonekana si muadilifu (Unafiki)

5. Kiongozi wa watu anaongozwa na utashi na dhamira ya kweli ya kuwatumikia watu wake. Hana ajenda ya siri. hategemei fadhila wala malipo wala gains zozote: Mahatma Gandhi was such a leader.

6. Kiongozi wa watu lazima awe mbunifu wa kutatua matatizo ya watu wake. Awe na ndoto na maono ya nini hasa angependa awafanyie watu wake. Ni lazima aguswe na matatizo ya watu wake na ayachukulie kama ni matatizo yake binafsi.

7. Kiongozi wa watu, hana makundi kwa kuwa anaongozwa na dhamira na utashi wa kutumikia watu wake.

8. Kiongozi wa watu yuko tayari kuwasikiliza watu wake na kujirekebisha pale anapokosea kwani yeye ni sehemu ya hao watu.

9. Kiongozi wa watu atajitahidi kuwa na timu ya viongozi walio na sifa zinazofanana na zake na si viongozi wa kupewa shukrani au ambao anawafahamu kwa namna moja au nyingine.

10. Kiongozi wa watu, anaongoza watu na si taasisi, shirika, wizara nk. na hivyo anatakiwa awe na hekima katika kuwaongoza na kufanya maamuzi.
 
Back
Top Bottom