2015 ipigie kura CCM

2015 ipigie kura CCM

293169_110242569123705_1446482124_n.jpg
Hahahhahahaaaaaaaaaaahahaaa!!!!!!liwalo na liwe wakti anajimaliza mwenyewe!!!!!!
 
Mvamiziardhi.jpg

An elderly man of Madale village on the outskirts of Dar es Salaam ponders what to do next after his hut was bulldozed in an operation conducted by Kinondoni municipality under CCM government.

Tatizo wazee kama hao inakuwa huna la kuwambia kuhusu CCM, wanasema CCM ndio baba ndio mama na wale waliohamishiwa kule mabwepande na kujengewa mahema ndio kabisa ,wao na CCM ni kama Paka na Samaki .

Tusiwape CDM nchi hata kidogo .kwani watatuzamisha na kupora mali zetu na kulipa kwa wafadhili wao huko ulaya.

muda mfupi baada ya bomoa bomoa sura ya eneo hilo huko tegeta/mabwepande itakuwa hivi
DarEsSalaam25.jpg
 
lakini serikali ya nyinyiem hivi mnakuwa wapi HAWA WATU WANAPOJENGA HIZI NYUMBA..??

mnasubiri wajenge halafu mkavunje..! SERIKALI MAKINI INAMZUIA MTU ANAPOANZA TU KUCHIMBA MSINGI..! KWA KIPINDI HICHO TAYARI HUWA ANAKUWA NA MAHALI PA KULALA LAZIMA..!this is not fair! GROW UP!

Serekali yenyewe hata haijui ina watu wangapi na wanakaa wapi itawezaje kuwazuia wakati wao wanajua wanaongoza wanyama maana wanajua kila sehemu ni pori sasa inapotaka kuwauzia wawekezaji ndio inakuta watu walishafika huko siku nyingi inaanza kwa kuwavunjia.

kama serekali ingekuwa inawapenda na kuwajali watu wake haya yasingetokea maana mzee kama huyu alienda kujenga huko kwa kujisitiri kutikana na ukata na shida za maisha sasa serekali inapovunja na kumwacha hapo inategemea nini? kwamba huyu ataenda kujitafutia msitu mwingine na kufweka na kuweka kakibanda cha matope na nyasi na watazalia na kualikana ndugu jamaa na marafiki wakimaliza kufyeka pori panakuwa mji serekali inauhitaji inaenda inawabomolea tena.

Ni lazima serekal;i ifikie mahali ijaribu kutafuta njia za kuzuia ujenzi wanaoita haramu. kwa mfano kipindi cha nyuma ilikuwa ni kawaida kabisa kukuta kiwanja kimoja kikiwa na hati ya umiliki kwa watu wawili aua zaidi na ilikuwa inapekelekea kuwa na migogoro mingi sana ya Ardhi na watu wa wizara walikuwa wanhusika sana kwa hil, serekali imeamua kwasasa kabla hujapata hati ya kumiliki kiwanja lazima lazima kuwe na idhini ya mtendaji kuthibitisha kuwa wewe ndiye mmiliki wa sehemu hiyo pia kunatolewa fomu maalumu ambazo zitajazwa na kusainiwa na majirani wanaokuzunguka kwa pande zote za mipaka ya eneo lako hii inasaidia sana kwani inawezekana kumwonga mtendaji na akakusainia pengine ukiwaonga na majirani lakini mwisho wa siku mgogoro wa ardi ukitokea walau kuna mtu ambaye ni mtendaji anaweza kuwajibishwa.

Sasa kwa swala la ujunzi holela serekali ifanyaje walau uwekwe utaratibu kwasababu serekali kuu yote iko Dar haitaweza kusimamia kutoa dar na kujua mtu aliyeko mkoa mwingine anayeanza ujenzi basi kutungwe sheria itakayosimamimiwa na serekali za mikoa na serekali za mitaa yaani ikikutwa na mtu asijenge bila kupatiwa kibali walau cha serekali ya mtaa hata kama ni banda la kuku na serekali ya mtaa ifanye tathimi ishirikishe wataala mpaka wa mkoa kutoa vibali vya ujenzi na kuwe na mtu wa mwisho ambaye atawajibishwa ikiwa kutatokea ujenzi haramu au holela.
Najua tatizo kubwa la nchi yetu ni rushwa lakini kukiwa naserekali makini itaweza mbona serekali nyingine duniani zinaweza utashanaa hata maafisa mipango miji wapo lakini miji inajengwa holela tu. na tusipobadili sasa basi kila siku tutakiwa tukishuhudiwa bomoa bomoa zinazoendelea kuwati watu umaskini maana kuanza makazi mapya ni gharama kubwa sana hata kama ni nyumba ya udongo.

Tatizo la kwanza ni rushwa na tatizo la pili ni kuwa na serekali dhaifu.
 
Mnasahau jinsi magufuli anavyojifia kwa kuvunja nyumba za watu? Kufuta makandarasi?
 
Tatizo wazee kama hao inakuwa huna la kuwambia kuhusu CCM, wanasema CCM ndio baba ndio mama na wale waliohamishiwa kule mabwepande na kujengewa mahema ndio kabisa ,wao na CCM ni kama Paka na Samaki .

What to do next; is already did, dont you know? Kalaghabao
Tuwapeni CDM tuangalie kwa muda wa miaka mitano .kama wakituzamisha tugomee uchaguzi na kuwepo serikali ya mseto kila mmoja yumo.

Ni kwa sababu hakuna kama sisiemu. Hawawezi kumnyanganya paka nyama na kumwachia fisi. CDM ni mafisi yatakula hata mizogz achilia mbali mifupa amabayo paka atabakiza na fisi huyo huyo akaambuliwa. Hakuna wa kuzugwa hapa.. Chama mbadala bado.
 
Nitachukua rushwa ccm nitaichangia chadema,nitakula ccm nitalal chadema
 


Ndo maana nasema wao kua Arusha or Moshi hakusaidii maana hiyo mikoa ni ya CHADEMA no doubt so waweke efforts zao kwenye maeneo ambayo ni full CCM na wajaribu kubadilisha mawazo na fikra za wananchi wa huko now that's their greatest challenge
......[/QUOTE]

Mkuu, hujawahi kuisikia M4C na Oparesheni Sangara? Ziko Arusha na Moshi tu?
 
Kwenye red ya kwanza: Nadhani yuko sawa anatumia kitu kinaitwa kejeli, then ukisoma content unaelewa exactly alichomaanisha. na kwenye red ya pili: I think that is what CDM is doing, na si rahisi kukamilisha kazi hiyo kwa siku moja, it needs time and tolerancy.

Tolerance now that's the key word....cdm would need to be patient careful and skilful...coz ccm aint gonna sit back and watch the rest do their thing....
 
naunga mkono hojaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
sipigii ccm kura hata iweje na lolote liwe.kura yangu bora nikae nayo ndani nitazme tv au kutembelea ndugu na jamaa kama itashindikana siku hiyo kuipa chama nitakachoridhika nacho kuwa kinastahili japo kupewa nafasi ya kuongoza.
kuliko kuipa ccm nasema sitaki ccm tenaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Tatizo wazee kama hao inakuwa huna la kuwambia kuhusu CCM, wanasema CCM ndio baba ndio mama na wale waliohamishiwa kule mabwepande na kujengewa mahema ndio kabisa ,wao na CCM ni kama Paka na Samaki .

.

Tatizo lipo hapo kwenye bold. Inabidi kwanza kuwaelimisha kuwa CCM siyo baba wala mama. Waafrika tuna amini wazazi hawakosei. Wakikosea tuna wajibu wa kuwasamehe kwani watabaki kuwa ni wazazi wako. Hivyo watu wanadhani CCM kama ilivyo wazazi ina haki ya kusamehewa hata pale inapotenda kinyume kabisa na matarajio ya wapiga kura wake.
 
sipigii ccm kura hata iweje na lolote liwe.kura yangu bora nikae nayo ndani nitazme tv au kutembelea ndugu na jamaa kama itashindikana siku hiyo kuipa chama nitakachoridhika nacho kuwa kinastahili japo kupewa nafasi ya kuongoza.
kuliko kuipa ccm nasema sitaki ccm tenaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Iron Lady kama kweli huna mpango wa kuipigia kura CCM kwa maana ya kutotaka ikutawale basi huna budi kuhakikisha kuwa siku ya kura unapiga kura dhidi ya CCM bila kukosa. CCM inashinda mara nyingi siyo kwa sababu inapigiwa kura na watu wengi bali kwa sababu wasioipenda wengi hawajitokezi kupiga kura ya kuikataa wakidhani kuwa wanaikomoa.
 
Tatizo kubwa ni Watanzania kuipa CCM "guarantee" ya kuwa madarakani kwa muda usio na kikomo. Tuelewe kuwa hata watu wanaoonekana wastaarabu wakishahakikishiwa ukuu na utukufu wa kuduma bila kujali mienendo yao huishia kuharibu. Ndio maana hatutakiwi kabisa kuwa na ushabiki kwa vyama vya siasa au kwa wanasiasa binafsi. Wanatakiwa kila wakati wajiandae kuwajibishwa (constantly kept on their toes!).

Kwa mantiki hiyo, kama uchaguzi ungekuwa unafanyika leo basi ningeshauri CHADEMA wapewe nafasi ya kuongoza nchi (sababu ziko wazi). Lakini nao wapate ujumbe mapema kwamba wakijisahau tu wajiandae kurudi upinzani. Mtu asijidanganye kufikiri CHADEMA inayoendesha M4C leo ndivyo itakavyokuwa ikiwa Magogoni. Hakuna uhakika wa aina hiyo kwa wanasiasa.

Kwa CCM dawa pekee ya kukiokoa chama hicho ni kukaa upinzani ili kitakaswe na sumu zote mbaya zilizokidhoofisha sana kiafya - hasa ufisadi uliokithiri wa mali na maadili, kibri na jeuri iliyopitiliza na kiweze kurejea tena kwa wananchi kwa unyenyekevu unaotakiwa. Wanaokipenda chama chao kwa dhati hiyo ndio njia pekee ya kurejesha sauti yao ndani ya chama - kwani mamluki wote bila shaka watahama haraka sana (dalili za kupoteza madaraka zikionekana tu) na kuelekea kuwaghilibu jamaa wa M4C. Ndivyo walivyofanya kwa Kaunda na UNIP yake na wote kumvamia Chiluba na kuanza kuimba ngonjera za MMD miaka ile.
 
Mimi sina tatizo na watu kubomolewa nyumba zao as long as taratibu zimefuatwa.hapa namaanisha kama mwenye nyumba ana haki basi awe amelipwa fidia anayostahili.hata hivyo pamoja na hayo,tatizo la msingi naloliona hapa ni kwamba serikali hii ya ccm haina mipango endelevu na ya mda mrefu.mambo kama haya yasingekua yanatokea kama tungekua na mipango.watanzania tuamke.hawa watu tukiwaweka pembeni hata kwa miaka mitano tu watajifunza.bila kuwajibishana hatutaijenga nchi.
 
Nyumba zimebomolewa madale, ... waathirika wote wamegawiwa vyumba magogoni na kupewa ajira WAMA!... Dhaifu anawapenda sana, tena hapendi watendewe hivyo!.. WASAIDIZI WAKE TU NDIYO WANAOWAONEA!!.....MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA!....
 
Problem ya Hii Nchi Kila kitu Kipo defined ila Nani wa kumfunga paka kengele? Serekali imeajiri surveyors na Town Planners na wote wapo dar!! Ila nani wa Kuwapangia Majukumu? Hayuppo!! Sasa wanaenda Mitaani Kupima Viwanja Vya watu!!

Du niliposoma kwamba 2015 ipigie ccm nimetapika,nilishajiandaa 4CDM4EVA&4EVRTHING.
 
Back
Top Bottom