2010; World Cup ya kiwango cha chini katika historia ya miaka ya karibuni...

Wakuu napingana na nyie mlio wengi - kiwango cha Ujerumani, Mexico, Urugway, Ghana, Brazil, Spain na Agentina ni kizuri sana. Mfano game ya jana kati ya Argentina na Mexico ilikuwa ya kiwango cha juu mno ni kati ya game nzuri so far.

Tutaona viwango safi hasa kwa hizi timu za America ya kusini wanacheza mpira wa kasi sana. angalia magoli ya jana lile moja na mexico na lile la mbali la Tevez - angalia movements wanapokuwa na mpira utapenda.

Still to come jamani - timu zilozotoka ndiyo zilikuwa zinadororesha mashindano haya zimeshatoka - timu kama uingereza jamani? hata kama wangepewa goli la Lampard lakini sijaona kitu wamefanya, kweli soka ya uingereza ina tatizo kubwa, something has to be done faster. kuna mdau amesema anamkosa Gaucho - mi nafikiri gaucho alikuwepo kwenye timu ya Mexico yule kijana machachari sana jina limenitoka ila wadau mtamkumbuka tu ana kasi mjanja sana. tutamkosa sababu timu yake bora imetolewa na timu bora zaidi.


Kuna watu timu zao zikiboronga tu basi wanasema mashindano hayana kiwango....Uingereza nje, tuacheni wanaume wa Argentina ya Maradona na Messi tukamue....Huu ni mwaka wa Amerika ya Kusini kutwaa ubingwa.

Historia inaonyesha kwamba timu za Ulaya na Amerika Kusini huwa zinapokezana ubingwa...

1986 - Argentina
1990 - West Germany
1994 - Brazil
1998 - France
2002 - Brazil
2006 - Italy

If you know what I mean!
 
Uhondo mtupu.. Hii ndo raha ya WOZA maoni, ubishi ndoto za mchana na usiku yaani almuradi ni raha tu.
 
Kwa wafuatiliaji wa WC ya mwaka huu watakubaliana na wachambuzi mbalimbali wa soka duniani kuwa haya ndiyo mashindano yaliyotia fora kwa kiwango duni kati ya mashindano matano (au zaidi), ya miaka ya karibuni. Ndiyo mashindano ambayo waamuzi ama kwa makusudi au kwa ufinyu wa ujuzi wameboronga zaiai, na ndiyo mashindano yaliyoongoza kwa kuwa na warusha maonyesho ya TV wenye viwango duni zaidi hata ikilinganishwa na ligi za mataifa kadhaa... It is so sad!!!!!!!!!!

nilivyojua hamna watu kama pato,gaucho,bent,totti na mafundi wengine wa kabumbu hili nililitegemea...hapohapo kuna marobot kama heskey na baptista.unategemea nini!hapohapo TBC ndo warusha matangazo.....
 
Tatizo la watu wamezoea kuona italia, england, france, brazil, argentina.sasa zinapotolewa watu wanaona hamna viwango.
 
hii ni the best worldcup, wanaosema ni mbaya ni kwamba timu zao zimetolewa baaasi, mexico super, ghana wako juu ukiondoa matatizo ya umaliziaji, ureno kamwonyesha brazil kuwa ukikaa vibaya na kombe huchukui, argentina safi zaidi ya mexico, uingereza pumba za mwaka ndo maana wakachezea kichapo cha mbwa mwizi toka kwa wajeru,tatizo watu wanapenda kuendeshwa na historia, kwamba uingereza hajafungwa na ujerumani since 1966, mara oohh france ndo sijui nn, those things are outter control these days, matatizo yaliyopo ukiondoa maamuzi mabovu ambalo ni tatizo la fifa the rest ni matatizo ya kawaida ambayo hutokea kila mara kutegemea na mahali world cup ilipofanyika...SA wamejitahidi sana na naamini some of the wazungu walokuwa siku zote wanaona Afrika kwa ujumla wake ni nothing watakuwa mpaka sasa wanashangazwa na everything they see down in mzansi!!lets be realistic guys..

Kaka hapo kwenye Blue umepigilia msumari ni ukweli kabisa na mimi nakupa tano 100%. Siyo wale mataa tunaowacheki kwenye Runinga wakati wa Champion Ligi - Terry, Johnson, Upson, Ashley cole mnapitwa na kufugwa magoli ya aibu kama yale? Holding midfilder Garry Barry vipi mzee kulikoni? Gerald, Lampard mnashindwa kweli kuchezesha kiungo watoto wadogo wanawadharirisha? siyo ninyi mnaolipwa zaidi duniani mbona mnawaangusha washabiki wenu hadi wananuna? Rooney vipi miguu mizito baada ya kutua Bondeni? si ni wewe unaitwa mzee wa kufumania nyavu na wapenzi wa Man U?

Wakuu kikosi cha Uingeleza kimesheheni wachezaji wanaolipwa zaidi duniani tena mastaa, tatizo ukiwakusanya pamoja unapata hayo mzee bob giza anaita Pumba za msimu. Inabidi wawaombe radhi waingeleza wenzao na sisi washabiki wa soka duniani kwa kutegemea watakula pilau kumbe tunapata mihogo tena isiyo na chumvi.
 
The wc is steel sweet......Dont u enjoy it????? I do...I really do......
 
makocha wengi wenye asili ya italy wanapenda sana chelsea,na england capello alichagu wachezaji ambao kwa kiasi kikubwa wametoka chelsea :biggrin1:,no arsenal player,france ilikuwa arsenal wengi wao japo kaachwa nasri kiasi wapenzi ambao mimi nawafahamu ni arsenal walichukizwa sana na hata diaby ktk mechi za majaribio kutocheza walikuwa wanalaumu sana,spain ni barca ni wazuri nawakubali,germany ni bayern munich.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom