2019
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 2,982
- 4,457
Kwa kweli nisiwe mnafiki. Niliacha kupenda siasa toka baadhi ya wapinzani kuanza kuunga mkono juhudi za JPM. Marufuku ya siasa ikachangia pia. Utendaji wa hayati nao nikaupenda.
Kilichonifanya nisimpende Magufuli baadae ni hali ya mgawanyiko uliokuwa unaendelea nchini.
Haya ni Rais wetu JPM katangulia wapo waliofurahi na wapo waliosikitika pia.
Baada ya serikali ya awamu ya sita kuchukua hatamu na kuanza kufungulia mambo mengi yalifungwa na kurekebisha uhusiano na majirani, wapinzani, wafanyabishara na wafanyakazi kuongezewa mishahara,nchi ilikuwa kama umepata uhuru toka kwa mkoloni mweusi. Mama akapendwa na watu wote bila kuangalia itikadi yao.
Mara baada ya siku 100 kufika kauli yake kuhusu wapinzani na katiba mpya ikawatisha baadhi ya wananchi. Lakini bado hakupoteza mvuto.
BAJETI MPYA YA 2021-2022 YAMWARIBIA
Hapa ni lazima Hayati Magufuli akumbukwe na wote sababu alidaiwa kuwajali wanyonge zaidi kuliko matajiri. Bajeti iliyopitishwa na waziri wa fedha Mwigulu Lameck Nchemba ndio mtihani wa pili kwa Rais SSH baada ya dai la katiba mpya.
Huenda akaponzwa na waziri wa fedha lakini atabeba lawama yeye sababu yeye ndie alimteua na anaweza pia kumuwajibisha.
Je, kwa mabadiliko haya 2025 atatoboa?
USHAURI WANGU KWAKE
Pamoja na miradi mikubwa aliyokuwa amefanya mtangulizi wake haya maisha hayakuepo? Je kweli serikali imekosa chanzo kingine cha kuongeza mapata badala ya huduma zinazotumiwa zaidi na wananchi wa kawaida? Kwanini wasingebana kwenye vitu vya anasa kama alivyofanya Magufuli?
Je, ni Serikali kukamua wananchi kama njia ya kujiongezea mapato? Hakuna rasilimali zinazoweza kutumiwa kuiongezea serikali mapato?
Kilichonifanya nisimpende Magufuli baadae ni hali ya mgawanyiko uliokuwa unaendelea nchini.
Haya ni Rais wetu JPM katangulia wapo waliofurahi na wapo waliosikitika pia.
Baada ya serikali ya awamu ya sita kuchukua hatamu na kuanza kufungulia mambo mengi yalifungwa na kurekebisha uhusiano na majirani, wapinzani, wafanyabishara na wafanyakazi kuongezewa mishahara,nchi ilikuwa kama umepata uhuru toka kwa mkoloni mweusi. Mama akapendwa na watu wote bila kuangalia itikadi yao.
Mara baada ya siku 100 kufika kauli yake kuhusu wapinzani na katiba mpya ikawatisha baadhi ya wananchi. Lakini bado hakupoteza mvuto.
BAJETI MPYA YA 2021-2022 YAMWARIBIA
Hapa ni lazima Hayati Magufuli akumbukwe na wote sababu alidaiwa kuwajali wanyonge zaidi kuliko matajiri. Bajeti iliyopitishwa na waziri wa fedha Mwigulu Lameck Nchemba ndio mtihani wa pili kwa Rais SSH baada ya dai la katiba mpya.
Huenda akaponzwa na waziri wa fedha lakini atabeba lawama yeye sababu yeye ndie alimteua na anaweza pia kumuwajibisha.
Je, kwa mabadiliko haya 2025 atatoboa?
USHAURI WANGU KWAKE
Pamoja na miradi mikubwa aliyokuwa amefanya mtangulizi wake haya maisha hayakuepo? Je kweli serikali imekosa chanzo kingine cha kuongeza mapata badala ya huduma zinazotumiwa zaidi na wananchi wa kawaida? Kwanini wasingebana kwenye vitu vya anasa kama alivyofanya Magufuli?
Je, ni Serikali kukamua wananchi kama njia ya kujiongezea mapato? Hakuna rasilimali zinazoweza kutumiwa kuiongezea serikali mapato?