PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,723
SERIKALI itatakiwa kutumia Dola za Marekani 1.1 milioni sawa na zaidi ya Sh1.5 bilioni kutekeleza mpango wake wa kufukia mashimo ya mgodi wa Buhemba ulioko Bunda mkoani Mara.
Mgodi huo ambao tayari umesitishwa uchimbaji wake, utatakiwa kugharimu kiasi hicho cha fedha kwa ajili kuyaweka mazingira yake katika hali ya usalama.
Gharama hizo pia zitatokana na ukweli kwamba baadhi ya kampuni za uchimbaji mkubwa wa madini, kutoweka dhamana kwa serikali kugharamia shughuli za kukarabati mazingira.
Ripoti ya hali ya mazingira ya mgodi huo iliyotolewa wiki hii jijini Dar es Salaam na Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, imesema mpango wa kufunga mgodi huo haukutekelezwa ipasavyo.
"TMAA ilifanya ukaguzi wa mazingira wa mgodi uliofungwa wa Buhemba na kubaini kuwa maeneo ya mgodi huo yameachwa katika hali hatarishi," ilisema sehemu ya ripoti hiyo na kuongeza;
"Hii inatokana na ukweli kwamba mpango mzima wa kufunga mgodi haukutekelezwa ipasavyo. Inakadiriwa kuwa kiasi cha Dola 1.1 milioni za Marekani, kinahitajika kutekeleza mpango wa kufukia mashimo ya mgodi huo.
TMAA imewasilisha taarifa ya ukaguzi ya mgodi huo kwa mamlaka husika kwa hatua zaidi."
Hata hivyo ripoti hiyo imebaini kuwa baadhi ya migodi pia haitekelezi ipasavyo mpango wa usimamizi na utunzaji wa mazingira uliopitishwa na serikali.
"Huu ni ukiukwaji wa masharti ya leseni. TMAA inaendelea kushirikiana na vyombo vingine vya serikali hususan Baraza la Usimamizi wa Mazingira (Nemc), kuhakikisha kasoro zilizoonekana wakati wa ukaguzi zinarekebishwa," imesema ripoti hiyo ya uchunguzi iliyofanywa kuanzia Agosti, 2007 hadi Desemba 2009 .
Katika hatua nyingine TMAA imepanga kukagua shughuli za utunzaji wa mazingira katika migodi yote mikubwa, ya kati na baadhi ya migodi ya wachimbaji wadogo katika kipindi cha mwaka 2010.
\source:http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=17366
Mgodi huo ambao tayari umesitishwa uchimbaji wake, utatakiwa kugharimu kiasi hicho cha fedha kwa ajili kuyaweka mazingira yake katika hali ya usalama.
Gharama hizo pia zitatokana na ukweli kwamba baadhi ya kampuni za uchimbaji mkubwa wa madini, kutoweka dhamana kwa serikali kugharamia shughuli za kukarabati mazingira.
Ripoti ya hali ya mazingira ya mgodi huo iliyotolewa wiki hii jijini Dar es Salaam na Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, imesema mpango wa kufunga mgodi huo haukutekelezwa ipasavyo.
"TMAA ilifanya ukaguzi wa mazingira wa mgodi uliofungwa wa Buhemba na kubaini kuwa maeneo ya mgodi huo yameachwa katika hali hatarishi," ilisema sehemu ya ripoti hiyo na kuongeza;
"Hii inatokana na ukweli kwamba mpango mzima wa kufunga mgodi haukutekelezwa ipasavyo. Inakadiriwa kuwa kiasi cha Dola 1.1 milioni za Marekani, kinahitajika kutekeleza mpango wa kufukia mashimo ya mgodi huo.
TMAA imewasilisha taarifa ya ukaguzi ya mgodi huo kwa mamlaka husika kwa hatua zaidi."
Hata hivyo ripoti hiyo imebaini kuwa baadhi ya migodi pia haitekelezi ipasavyo mpango wa usimamizi na utunzaji wa mazingira uliopitishwa na serikali.
"Huu ni ukiukwaji wa masharti ya leseni. TMAA inaendelea kushirikiana na vyombo vingine vya serikali hususan Baraza la Usimamizi wa Mazingira (Nemc), kuhakikisha kasoro zilizoonekana wakati wa ukaguzi zinarekebishwa," imesema ripoti hiyo ya uchunguzi iliyofanywa kuanzia Agosti, 2007 hadi Desemba 2009 .
Katika hatua nyingine TMAA imepanga kukagua shughuli za utunzaji wa mazingira katika migodi yote mikubwa, ya kati na baadhi ya migodi ya wachimbaji wadogo katika kipindi cha mwaka 2010.
\source:http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=17366