Machafuko ya uchaguzi wa Oktoba 2025 nchini Tanzania yalifunikwa na giza zito la kuzimwa kwa intaneti, baada ya mrindimo wa bunduki kunyamaza ghafla. Sasa, ushahidi mpya unafichua kile ambacho hakikusimuliwa - vifo vya watu ambao idadi yao bado haijulikani, miili iliyotoweka, na tuhuma za...
Aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Dkt. Hellen Kijo Bisimba amesema "Kwa uzoefu wa Tanzania, serikali huwa na hofu kubwa dhidi ya maandamano na maandamano ndiyo njia pekee iliyobaki kuishinikiza serikali"
Mwanamitandao Clemence Mwandambo amesema amekuwa akitumia video anazochapisha mtandaoni katika kuwashauri wanasiasa na kuwasilisha mawazo yake, lakini mara nyingine wanasiasa wamekuwa hawataki kuambiwa mawazao tofauti na wakiambiwa hivyo wanaona kama wanaowaambia wana kiburi.
"Kwa bahati mbaya...
Mfanyabiashara na mdau maarufu wa maendeleo nchini, Azim Dewji, amewatahadharisha Watanzania kuwa makini na viashiria vya vurugu ambavyo vinaweza kutoa mwanya kwa mataifa ya nje kuvamia na kupora rasilimali za nchi, akitolea mfano wa matukio ya hivi karibuni nchini Venezuela.
Akizungumza kuhusu...
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne, Mizengo Pinda, amesema maandamano yaliyotokea Oktoba 29 hayakuwa ya amani, akieleza kuwa baadhi ya Vijana walishiriki bila kupata maelekezo sahihi, hali iliyosababisha mipango ya kuharibu mali na miundombinu ya umma pamoja na...
Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa mwanzoni mwa mwaka 2026 Serikali imejipanga kujenga umoja wa kitaifa ambapo mchakato wa kuunda Tume ya Maridhiano tayari umeanza na Serikali itashirikiana na wadau wote ili kukubaliana muundo wa Tume hiyo.
Katika hotuba yake ya kuaga mwaka 2025 na...
Tume ya Uchunguzi imetoa wito kwa wananchi kupuuza ushawishi wowote unaolenga kuwazuia kushirikiana na tume hiyo na badala yake watoe maoni na ushauri kwa tume.
Wito huo umetolewa Desemba 26 kupitia taarifa ya tume kwa umma iliyobainisha kuwepo kwa watu au makundi ya watu yanayotekeleza...
Leo nimewasikiliza hawa Wamachinga wa Dar na mmoja wao anasema ni bora tupoteze uhai lakini tulitibu taifa. Naona hata hawa tujumuishwe kwenye kundi la Wasanii, kususia biashara zao, twende kuwaunga mkono wale ambao wana Utu na hawajitokezi kuzungumza ujinga bila kujali watu waliopoteza maisha...
Kwenye mahojiano na Jamhuri TV, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema kwenye Vita ya Kagera, vijana wengi waliuawa na adui. Aidha, ukilinganisha na takwimu zinazozungumziwa sasa, idadi ya waliokufa ni kubwa zaidi kuliko ile ya vita. Tofauti ni kwamba, wakati ule tuliuawa na adui, lakini sasa...
Wanadai kuna Polisi waliouwawa katika vurugu za Oct 29. Kitu cha ajabu hatujaona wala kusikia serikali na CCM wakitoa mkono wa pole kwa marehemu hao.
Pia kuna wananchi kibao wamefariki katika vurugu za Oct 29. Baadhi yao walikuwa mashabiki wakubwa wa Rais Samia na CCM. Mfano mzuri ni Sharifu...
Ukitoa bomu la Hiroshima lililoua watu 70,000 instantly, vifo vilivyotokea Tanzania siku ya uchaguzi 2025 vimeingia kwenye historia ya dunia kwa watu wengi kuuawa na polisi kwa kipindi kifupi.
Inakadiliwa tarehe 29/10/2025 watu 10,000 waliuawa ndani ya siku 3 (masaa 72), sawa na watu 3,300 kwa...
Ujumbe ambao inadaiwa umetumwa na aliyekuwa kada wa CCM, Dkt Godfrey Malisa ambaye aliripotiwa kutekwa usiku wa Novemba 20, akiwa nyumbani kwake maeneo ya msamaria majengo au malenga, siku chache baada ya kutoa maazimio ya Kamati ya Kitaifa ya Kurejesha Haki na Amani katika Nchi Yetu (Tanzania)...
Kanisa Katoliki la Baltimore, Maryland, Marekani (eneo la DMV) siku ya Jumapili, Desemba 14, 2025, limefanya ibada maalum ya kuwaombea mashujaa waliouawa wakati na baada ya uchaguzi Oktoba 29 wakipigania haki, ambapo waumini walikusanyika kuwakumbuka na kuwaombea marehemu hao.
Katika ibada...
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imesema ina wasiwasi kuhusu taarifa za vifo, majeruhi, watu kupotea na kukamatwa katika muktadha wa uchaguzi wa tarehe 29 Oktoba nchini Tanzania.
Hayo ni kwa mujibu wa Kamishna Mkuu wa Ofisi hiyo, Volker Turk, ambaye ametoa wito wa familia kupata...
Leo, Jumatano Desemba 10.2025 kesi Na. 30210/2025 iliyofunguliwa na Mwanaharakati Rosemary Mwakitwange na wenzake wawili (2) ambao ni Mawakili Deogratias Mahinyila na Edward Heche dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Wajumbe Nane wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa amani...
Mama mmoja amehudhuria mahafali ya chuo kikuu kwa niaba ya mwanawe aliyefariki baada ya kuuawa na jeshi la polisi siku ya tarehe 29 Oktoba, wakati wa mauaji ya vijana waliodai mabadiliko nchini.
Kijana huyo aliuawa akiwa anarudi nyumbani, siku chache kabla ya kuhitimu masomo yake.
Katika...
Ni jambo la fedheha kuwa si Rais Mstaafu Kikwete wala CCM hawajalaani mauaji ya vijana wa Tanganyika.
Hili limekaaje wadau?
NYONGEZA.
Hapa karibuni, Msukuma ameliongelea hili.
CCM imedoroa.
Dereva wa bajaji anaeleza kuwa baada ya kumpeleka abiria wake aliyepigwa risasi na kuvunjika niguu yote, alikamatwa, akapigwa sana kisha kuingizwa mahabusu. Ndani ya mahabusu, alikuta watu waliojeruhiwa vibaya—waliovunjika miguu, viuno na viungo vingine kwa risasi—wengine wakifariki wakiwa humo...
Muna Love ame-share screenshot ya moja ya ndugu wa aliyekuwa amepewa kesi ya uhaini baada ya maandamano ya Oktoba 29 akidai kuwa walitumika kubeba miili ya waliuawa kwenda kuwazika kwenye makaburi ya pamoja huko Kondo ambako hata ripoti ya uchunguzi ya CNN ilieleza uwepo wa makaburi hayo.
"Dada...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.