vifo maandamano tanzania

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. Waufukweni

    PostGE2025 Rais Samia: Mmenipa heshima kubwa mno! Ulimwengu unauliza, “Kwanini asilimia 97?” Nasema natamani mngekuwepo, mkaona

    Wakuu, Kwani nyinyi mliokuwepo mliona nini? 🤕 == Rais Samia amewashukuru wananchi wa Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kwa imani kubwa waliyompatia katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akiahidi kurejea tena Mkoani Arusha kutoa shukrani zake kwa wananchi. Samia amesema hayo Ijumaa Novemba...
  2. Waufukweni

    PostGE2025 Andrew Nyerere: Maiti ziliokotwa barabarani, majeruhi walipelekwa Mochwari kumaliziwa

    Andrew Nyerere, mtoto wa kwanza wa Hayati Mwalimu Nyerere amesema "Maiti ziliokotwa barabarani, majeruhi walipelekwa mochwari kumaliziwa Serikali ikiri kwamba ilifanya makosa"
  3. je parle

    PostGE2025 Aliyeshauri Watu kuuliwa bila sababu za kueleweka ni nani?

    Tangu internet imeachiwa sijapata hisia za mwanamke kabisa yani Kila nikiona hizo videos mtandaoni watu wamekufa kama mbuzi yan Sikudhani kama ingefika siku watanzania tukafanyiana vitendo vya kinyama kiasi hiki.? Unaua tu hata kama umetumwa lakin pia askari muwe mnatumia hata akili za kawaida...
  4. DuaZaMama

    PostGE2025 CNN: Mwanamke huyu aliyepigwa risasi alikuwa na ujauzito wa miezi 3

    Vyanzo vya karibu na familia yake viliiambia CNN kuwa mwanamke huyo alikuwa na ujauzito wa miezi mitatu, na ameacha nyuma mume na watoto wawili. CNN
  5. Waufukweni

    PostGE2025 Rais Samia: Tumeambiwa vijana walioingia barabarani kudai haki walilipwa fedha kwanza

    Rais Samia amesema "Tunaambiwa kwamba vijana wale walioingia kudai haki walilipwa fedha kwanza ndiyo wakaingia barabarani, na wengi wao waliingia barabarani kutokana na hizo fedha walizopewa. Je, fedha hizo zilitoka wapi?" wakati akizindua Tume huru ya uchunguzi wa Matukio ya uvunjifu wa Amani...
  6. Waufukweni

    PostGE2025 Prof. Wangwe: Polisi nao wachunguzwe kutokana na kuhusishwa na vitendo vya mauaji

    Mtaalamu wa uchumi, Prof. Samuel Wangwe, amesema Tume ya Rais ya kuchunguza chanzo cha machafuko ya Oktoba 29, 2025 inapaswa kuangalia pande zote, ikiwemo Jeshi la Polisi, kutokana na tetesi kwamba nao walihusika katika vitendo visivyo vya kiungwana. Akizungumza kwenye kipindi cha Mizani...
  7. Waufukweni

    PostGE2025 Prof. Chijoriga: Lazima tusameheane ili Taifa lisonge mbele

    Hivi kwanini wanataka raia tuwasamehe na siyo kuwataka watu wao wawajibike kwa uovu wao? Kwahiyo sheria zilitungwa kwa ajili gani ikiwa wahalifu hawashughulikiwi? == Mkuu wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Prof. Marcelinna Chijoriga, amesema kutokana na hali ilivyo nchini kwa...
  8. kimsboy

    PostGE2025 Ushahidi wa mauaji ya Mo29 wafika ICC. Mmoja akiri kuua watu 300

    Wakuu, hii ni breaking news na habari kubwa mno, Ushahidi wa mauaji ya Mo29 yamefika ICC.Nimeattach hii voice notes.Kweli nimeamini Ogopa Mungu na Teknolojia kwa huu ushahidi Hachomoi nawaambia ndugu zangu, siku za mwizi ni arobaini. 1.Ushahidi wa Video 2.Ushahidi wa picha za Satellite...
  9. Mtu Alie Nyikani

    PostGE2025 Habil wa TikTok aibua tuhuma nzito kwa Haji Kheir juu ya Oktoba 29. adai polisi waliojaribu kuwatetea vijana waliuawa

    Wakuu habari za mda huu. Kuna kijana mmoja huko TikTok anaitwa Habil & Kabil ukifuatilia video zake na tuhuma anazo toa juu ya Haji Kheir ni nzito sana na za kuogepesha mno. Pia soma: Haji Omar Kheir - Mshauri wa Rais Ikulu, ana uhusika na mauaji Uchaguzi 2025?
  10. DuaZaMama

    PostGE2025 Rais Samia: Yaliyotokea yametutia DOA tuna kazi ya kutafuta fedha wenyewe

    Rais Samia Suluhu amesema hali iliyotokea nchini wakati wa uchaguzi mkuu imeitia doa nchi, na kwamba huenda ikapunguza sifa ya kupata mikopo kirahisi, hivyo ameagiza viongozi kutafuta zaidi fedha za ndani ili kutekeleza miradi. Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza baada ya kuwaapisha Mawaziri...
  11. PAYE

    PostGE2025 Kesi ya watuhumiwa 11 wa maandamano ya uchaguzi yaahirishwa, upelelezi bado haujakamilika

    Kesi inayowakabili watuhumiwa 11 kati ya 172 wanaodaiwa kuhusika na matukio ya uhalifu yaliyotokea baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imeahirishwa hadi Novemba 26 mwaka huu baada ya upande wa mashitaka kudai kuwa upelelezi bado haujakamilika. Watuhumiwa hao upande wa Wilaya ya...
  12. Just Pray

    PostGE2025 Sheikh Mziwanda: Nimesikitika TEC kuita ‘Vurugu’ za Oktoba 29 kuwa ‘Maandamano’

    Kiongozi wa Taasisi ya Asaalam Islamic Foundation Sheikh Muharram Mziwanda ameeleza kushangazwa na Kauli ya Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) kuwa kilichofanyika Oktoba 29, 2025 ilikuwa maandamano na si vurugu, uharibifu na wizi kama ilivyoshuhudiwa katika maeneo mbalimbali...
  13. Heparin

    PostGE2025 Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC): Mauaji ya Oktoba 29 yachunguzwe na Taasisi huru zisizoegemea upande wowote, ikiwemo za Kimataifa

    Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetaka kufanyika uchunguzi wa mauaji ya Oktoba 29 kupitia Taasisi huru, uchunguzi ambao utashirikisha wadau wa ndani na nje ya nchi na kuongozwa na vyombo visivyoegemea upande wowote ikiwemo taasisi za dini na taasisi huru za kimataifa ili ukweli...
  14. Waufukweni

    PostGE2025 Heche: Nimesikitika hajatamka Watu wangapi wamekufa, idadi ya majeruhi. Waliohusika kufanya mauaji wachukuliwe

    Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche amezungumza kupitia BBC baada ya hotuba ya Rais Samia akifungua Bunge la 13.
  15. Cute Wife

    PostGE2025 Rais Samia aliongoza Bunge kusimama kwa dakika 1 kuwaombea waliofariki kwenye vurugu siku ya uchaguzi

    Rais Samia awaambia wabungge na waliohudhuria bunggeni kusimama kwa dk 1 kuwaombea wote waliopeta maisha, waliojeruhiwa wapone haraka, na pole kwa wale wote waliopoteza mali zao kipindi hiko. Akisema yeye binafsi ameumia sana. Amessma serikali imeunda tume kuchunguza kilichofanyika, akisema...
  16. Waufukweni

    PostGE2025 Mchungaji: Zipo athari za walioshuhudia vifo, serikali izungumze na wananchi kuliponya taifa

    Mchungaji Rose Shaboka ameiambia DW kuwa serikali pia lazima ijitoe ili kuzungumza wazi na wananchi katika kuliponya taifa, Lazima Wantanzania wakubali kilichotekea, na kutafuta suluhu kwa siku zijazo.
  17. DuaZaMama

    PostGE2025 Godlisten Malisa: Utu ni zaidi ya mali, CRDB msisahau kutoa pole kwa waliopoteza uhai

    Anaandika Mwanasiasa na mwanaharakati Godlisten Malisa....... "CRDB Bank imetoa maua na tuzo ya pole kwa The Voice Bar Kinyerezi, inayodaiwa kuharibiwa kutokana na ghasia za Oktoba 29. Ni jambo jema kuwajali wateja wenu kwa kiwango hiki, na kwa hilo nawapongeza. Lakini je, vipi kuhusu mamia ya...
  18. Waufukweni

    PostGE2025 Video: Wananchi wazika nguo na viatu mara baada ya mwili wa marehemu aliyeuawa na polisi kutopatikana

    Wananchi, wakiwa na huzuni na mshikamano, walizika nguo za marehemu aliyeuawa na polisi baada ya mwili wake kutokupatikana ishara ya kuenzi utu na kupaza sauti ya haki.
  19. Waufukweni

    Mwananchi aliyepigwa Risasi ya Tumbo: Wamedhamilia kutuua wanatupiga Risasi za moto, Risasi hii hapa ninayo

    Mwananchi mmoja aliyepigwa risasi tumboni wakati wa maandamano amesema kuwa "Wamedhamilia kutuua wanatupiga Risasi za moto, Risasi hii hapa ninayo"
  20. PAYE

    Ubalozi wa Norway waomboleza na Watanzania kwa kuwapoteza wapendwa wao

    Ubalozi wa Norway unatoa pole za dhati kwa wote walioathirika na matukio ya hivi karibuni nchini Tanzania. Tunaungana na familia na jamii zilizopoteza wapendwa wao na pia na wale wote wanaokabiliana na changamoto za kipindi hiki kigumu. Fikra zetu ziko pamoja nanyi, na tunaheshimu kumbukumbu za...
Back
Top Bottom