Polisi kwa mara nyingine wamempiga na kumjeruhi mwandishi wa habari aliyekuwa akifuatilia kampeni za mgombea urais wa chama cha National Unity Platform, Robert Kyagulanyi, katika Wilaya ya Kween, eneo la Sebei.
Chanzo cha ukatili huo wa polisi dhidi ya mwandishi huyo asiye na silaha bado...
Aliyekuwa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Makini, Coaster Jimmy Kibonde ameomba Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kumpatia Gari ambalo alipewa kama mmoja wa wagombea wa nafasi ya Urais Tanzania kwakuwa amelitendea haki kwa Kufanya kampeni karibu mikoa yote...
Majalio Kyara aliyekuwa Mgombea Urais kupitia Chama cha Sauti ya Umma (SAU) amesema mchakato wa uchaguzi umeisha, na sasa jambo ambalo linatakiwa kufanyika ili kutuweka pamoja ni mazungumzo ili kumaliza tofauti zilizojitokeza.
Amesema Watanzania wanapaswa kuacha vurugu, badala yake watafute...
Mgombea urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Hussein Mwinyi tayari amepiga kura katika kituo cha kupigia kura Kariakoo viwanja vya michezo ya watoto Jimbo la Kwahani.
Dk Mwinyi amefika katika kituo hicho saa 2:10 asubuhi ya leo Jumatano, Oktoba 29, 2025 akiwa ameongozana na...
Mgombea urais wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Wilson Elias amesema endapo chama chake kitapata ridhaa ya kuongoza nchi, kitaweka satelaiti angani ili kudhibiti uhalifu unaofanyika katika maziwa ya Victoria na Tanganyika pamoja na mipaka ya nchi kwa ujumla.
Ahadi hiyo ameitoa...
Selemani Said Bungara 'Bwege' amesema alikuwa anashiriki katika uchaguzi na kukiuza chama chake cha ACT Wazalendo, lakini tokea Mgombea wa Urais kupitia Chama chake, Luhaga Mpina aenguliwe ameona ni kama wagombea wote wa udiwani na ubunge kupitia chama ACT Wazalendo wameenguliwa kwasababu...
08 October 202
Zanzibar, Tanzania
KESI YA CUF DHIDI YA TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR YAENDELEA KUSOTA MAHAKAMANI
Wakili wa Bw. Hamad Masoud anayewania kiti cha urais wa serikali ya Zanzibar azungumza, hata ya mwanzo ya mapingamizi kuwa mahakama haiwezi kusikiliza kesi hiyo yaliyoletwa mahakamani...
Wakuu,
Kwa picha hizi mwaka hakuna Uchaguzi kabisa yaani ni maigizo tu.
Mgombea wa urais kupitia Chama cha ADC, Wilson Elias akinadi sera zake katika mkutano wa chama hicho uliofanyika leo Jumamosi, Septemba 27, 2025 katika viwanja vya Tanganyika Peckars jijini Dar es Salaam. Picha na Michael...
Mgombea urais kupitia Chama cha ADA TADEA, George Bussungu, amesema iwapo atachaguliwa, serikali yake itajenga mji maalum wa teknolojia unaoitwa Bongo Technological City, ambapo vijana wenye vipaji kutoka mikoa yote watapelekwa kwenda kuvumbua na kuendeleza miradi mbalimbali ya kiteknolojia...
Mgombea urais kupitia Chama cha Wakulima (AAFP), Kunje Ngombale Mwiru, amesema dhamira yake ya kufuga mamba Ikulu kwa ajili ya kuwala mafisadi si mzaha, bali ni mkakati mahsusi wa kupambana na ufisadi nchini.
Mwiru amesema wapo waliodhani kauli hiyo ni masihara ya kisiasa au porojo za kampeni...
Wenye ndoto za kuoa na Mahali ni kipengele baasi tumsikilize huyu mgombea wa CCK
==
CHAMA cha Kijamii (CCK) kimewataka Watanzania, hususan vijana, kukiamini na kukipa ridhaa ya kuongoza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Ubunge na Udiwani unaotarajiwa...
Chama cha Alliance for African Farmers Party (AAFP) kimesema endapo kitapata ridhaa ya kuongoza nchi, kitaanzisha hatua kali dhidi ya vitendo vya ufisadi, ikiwamo kujenga bwawa maalumu lenye mamba Ikulu kwa ajili ya kuwachukulia hatua mafisadi.
Kauli hiyo imetolewa leo, Jumatano Septemba 17...
Aliyekuwa Mbunge wa Simanjiro na mwanasiasa mkongwe, Christopher Olesendeka, amesema wagombea wa Urais wa Tanzania kutoka vyama vya upinzani hawawezi kulinganishwa na mgombea wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Akizungumza katika kampeni za ubunge jimbo la Mbulu Mjini mkoani Manyara hivi karibuni...
Tume imekubali pingamizi lililowasilishwa na Ndugu Hamza Saidi Johari Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya uteuzi wa Ndugu Luhaga Joelson Mpina kuwa mgombea wa kiti cha Rais kupitia Chama cha ACT-Wazalendo.
Hivyo, jina la Ndugu Luhaga Joelson Mpina, mgombea wa kiti cha Rais kupitia Chama cha...
Mgombea wa CUF Gombo Samandito Gombo ameahidi endapo atashinda atahakikisha kila mtoto atakayezaliwa nchini kabla hata ya kupewa jina na wazazi wake atapewa kitambulisho cha taifa cha Nida ili kumuondolea usumbufu pindi atakapokuwa mtu mzima
Gombo Samandito Gombo ameyasema hayo leo Septemba 14...
Wakuu,
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha African Democratic Alliance (ADA - TADEA) George Gabriel Bussugu amesema kuwa endapo atapewa ridhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, atahakikisha Tanzania inamiliki Satellite yake.
Akizungumza leo katika...
Mgombea wa Kiti cha Urais Zanzibar kupitia chama AAFP, Said Soud alisema hayo tarehe 3/09/2025 wakati anamjibu Mgombea wa Urais Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia tiketi ya Chama Cha ACT wa Wazalendo Othman Masoud Othman anayedaiwa kutoa kauli za kichochezi na kukejeli sheria za uchaguzi...
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Wakulima (AAFP) Kunje Ngombale Mwiru ameahidi kugawa trekta 2 kwa kila kaya kumi katika kata ya Ifakara Mkoani Morogoro.
Pia ameahidi kuwapatia Vijana wenye umri kuanzia miaka 18 mashine aina ya power tiller kwa kila kijana ili...
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA), Hassan Almas, ameahidi kuwa iwapo chama chake kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi, serikali yake itatungua sheria kali dhidi ya mapenzi ya jinsi moja ndani ya siku 30 baada ya kuundwa kwa...
Mgombea wa Kiti cha Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wa Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA) Hassan Almas, amesema ndani ya siku thelethini baada ya kupewa ridhaa ya kuwa Rais wa Tanzania atafanya maboresho makubwa kwenye sekta mbalimbali hapa nchini ikiwa ni pamoja na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.